Biashara ipi rahisi kuiendesha hata ukiwa mbali?

Biashara ipi rahisi kuiendesha hata ukiwa mbali?

Akitaka ziwe separate ni mbili za wastani au ndogo.
Akitaka ziungane, inakua moja yenye unit 3.
Ila ahakikishe anaujua ujenzi. Maana kama hajui, hiyo hela ataburuzwa aache pagale.
Ramani za nyumba mbili napata wapi
Ah mambo ya ujenzi hapa kwake...koplin, pima maji, tofali kulala au kusimama vyote najua
 
Ramani za nyumba mbili napata wapi
Ah mambo ya ujenzi hapa kwake...koplin, pima maji, tofali kulala au kusimama vyote najua
Unahitaji zaidi ya hayo.
Ukiujua ujenzi utauza kazi kwa tofali, ila hapo utatakiwa kuelewa kila kinachofanyika na kikikosewa ujue kimekosewa na kirekebishwe vipi.

Otherwise utauza kazi yote kwa fundi mkuu ili yeye ndo auze kwa tofali au day.
Na hapo ndo anapotengeneza faida kwenye kazi yako

Material chukua kwa supplier, usichukue kwa retailer. Kuna tofauti kubwa sana
Hayo ni kwa uchache.
 
Nunua shamba kubwa mkoani huko karibu na wafugaji... weka lunch ya kununua ng'ombe bei ndogo unawanenepesha unauza! Tumia 40% tu ya hio pesa ili uive vzr kabda ujaingia mazima.
 
Biashara kuendesha ukiwa mbali inawezeakana lakini shida kuu ni kukosekana Kwa kitu kimoja tu
UAMINIFU.
kama hutoibiwa ama kudokolewa faida basi itaibiwa jumla
Utakuwa umechezea mtaji wako tu.
Biashara inahitaji uwepo wako ndipo itaenda Kwa ufanisi
Japo watu waaminifu wapo lakini namna ya kuwapata Sasa
kwa hio kwenye biashara kinacho angaliwa ni uaminifu tu? Haaa
 
Biashara kuendesha ukiwa mbali inawezeakana lakini shida kuu ni kukosekana Kwa kitu kimoja tu
UAMINIFU.
kama hutoibiwa ama kudokolewa faida basi itaibiwa jumla
Utakuwa umechezea mtaji wako tu.
Biashara inahitaji uwepo wako ndipo itaenda Kwa ufanisi
Japo watu waaminifu wapo lakini namna ya kuwapata Sasa
sikiliza Biashara sii tu kuangakia Faida haoo ndio tunapo kwama, ndio maana tunaweka either Mke au Baba au Mama kisa tunatafita waaminifu, Biashara ni zaidi ya hio uaminifu,tunakwama sana
 
Kila biashara ni rahisi sana ukisimuliwa. Ingia ufanye ndio utajua kuna mambo hukuwahi kuambiwa. Imani yangu juu ya biashara ni

1. Sio kila mtu anaweza kufanya biashara. Naamini kuwa kila kazi iliyopo chini ya jua ni wito. Ili dunia iwe na balace lazima kila kazi ifanyike. Ni lazima kuwe na mtu mwenye kufanya kazi ya chini kabisa amabayo wengine wanaidharau ili tu dunia iwe kwenye balance kwa sababu watu watahitaji huduma yake. Unaweza kuingia kwenye biashara ambayo kuna mwenzio katoboa uka copy na ku pest na usitoboe. Ninaamini kwamba ukijua kusudi la wewe kuwepo duniani itakusaidia kujua nini sahihi kwako kufanya.

Namna moja wapo ya kujua ni pamoja na msukumo wa ndani yako. Kama kuna msukumo unatoka ndani yako kufanya jambo flani, kuna uwezekano mkubwa hio ndio calling yako. Kuna mdau hapo juu kasema biashara inakuhitaji wewe uliye na maono nayo, ila kuna watu wanamwita mtu wa negativity. Niseme hivii, huyo jamaa yupo sahihi asilimia zote. Kusimamia wazo ili likue huwa inatoka ndani yako. Yaani wewe ndio uko na maono ya kile unachokifanya kitu ambacho wengine hawataona.

Mfano mdogo sana, tunakubaliana wote kuwa biashara zina changamoto si ndio, sasa namna ya ku deal na baadhi ya changamoto inahitaji wito wa ndani ulionao. Kwamba uwe na msukumo wa ndani kutatua na kuzivumilia changamoto zitakazojitokeza. Mfano una fanya biashara ya kununua na kuuza, umenunua ila mzigo hautoki, hapo unahitaji msukumo wa ndani yako ku push kwa namna yoyote mzigo utoke. Sasa kufikiri hizo strategy kama unachokifanya sio kitu ukipendacho utafika muda utaona unateseka na huo ndio huwa mwanzo wa kuuwa biashara, ila kama inatoka rohoni uta feel proud sana kutafuta solution.

2. Imani yangu ya pili ya biashara ni kwamba kila biashara ina lipa. Tofauti ni mitaji na usimamizi. Ndio maana kila biashara inaanzishwa kila leo na kila biahsra ina kufa kila leo na zingine zina miaka zinaishi na kukua zaidi.

3. Ni vizuri kuomba ushauri wa nini ufanye ila ni vizuri zaidi kufanya unachokipenda kwa kuwa ndio utakisimamia kwa umakini. Biashara ni maisha, ili uifaidi inatakiwa iingie kwenye damu iwe sehemu ya wewe. Hio bond ikikosekana mwanzoni mwa biashara kufa kwake ni kugusa tu. FANYA UNACHOKIPENDA NA NDICHO UTAKACHOKISIMAMIA.

4. Kama huna passion na biashara ila unataka kuwekeza pesa yako ili izae, basi usifanye biashara, fanya uwekezaji wa hio pesa. Wekeza kwenye BOND, wekeza kwenye viwanja, wekeza kwenye nyumba za kupangisha na vitu vingine kama hivyo. Usizungushe pesa ili hali wewe huna muda huo hasa mwazo wa biashara utalia.

ZINGATIA: Biashara ni kuzungusha pesa kwa haraka ikupe faida ndogo au kubwa kwa haraka. Kuwekeza ni kununu au kutengeneza kitega uchumi kwa gharama kubwa au ndogo, kisha kitakuingizia pesa kidogo kidogo na baada ya muda mrefu sana ndio utaanza kuingiza faida.
 
Nashukuruni kwa mawazo na michango yenu! Lakini bado najiuliza, kama ni lazima niisimamie kwa karibu sana, inawezekanaje watu wengine wakawa na biashara karibia kila mkoa? Inawezekanaje watu wengine wanamiliki biashara hata chi za nje na bado zikafanya vizuri bila uwepo wao mahali pa biashara? Au kwa vile biashara zao ni biashara kubwa?
Hakuna bishara huanza kwa kusimamia na mtu mwingine asie mwanzilishi na ikadumu. Hizo unazoziona, wenye nazo wapo nazo karibu kwelikweli haijalishi ziko mbali mbali. Na nyingi hianza kwa udogo kisha wamili huwa nazo karibu wakijifunza tabia za biashara, baadae huzitanua aakijua kabisa namna wata deal na huo utanukaji. Unamuona kijana aliyeanzisha kampuni ya kutuma pesa wingereza/usa (sina haikika) kuja tz na kenya, yeye ndio top, operator mkuu hadi sasa.

Sasa hivi anasema wanataka kutanua matawi waingie Chad na nchi zingine, hapo wataanza kugawa majumu kwa watu zaidi na kuajili zaidi ila bado kuna wakurugenzi wa body na yy akiwa ndio mkuu wao watakua wana monitor kwa karibu sana.

Unamuona vunja bei
Unamuona milladyayo
Unamuona Chris Lukos
Unamuona Nifa
Hao ni baadhi, biasha inakutaka wewe hasa mwanzo, mfumo ukiimarika itajiendesha kama biashara za akina Mo na Bahresa mwa sasa
 
Waafrica kila mwenye pesa anawaza kufanya biashara. Biashara ni Hobby, Biashara inahitaji spirt kubwa sana, Biashara inamuhitaji mwenye wazo awe intact kwenye eneo la biashara ili kuendeleleza ile wazo yake.

Sasa watu wanajidanganya kwamba anaweza muweka Mke/mme/Baba/Mama/KAka/Dada/Mjomba/Shangazi/Shemeji/Baba mkwe/Mama mkwe wasimamie wazo, hii ni kujidanganya, hao hawajui lolote sio initiator wa wazo.

Ndioa maana wakina Mengi au wakina Bagharesa walianza kusiamamia wazo lao hadi walipo fikia levo za juu kabisa za kufanya deligate.

Sasa wewe day one ya Biashara yako inaanza na kukaimisha mtu, hio biashara haitafika kokote kule

Kama huwezi/huna muda wa kusimamia wazo lako nakushauri hizo pesa nunua hata bond za Serikali tu, la sivyo utazika pesa zote na utakuja lilia chooni kilio cha kujuta.Biashara za kupiga simu sio biashara.
umenena vyema kabisa yani kile kitu cha uhalisia kwenye biashara inakuhitaji mwanzoni muhusika 100%
 
Mia Nina Entrepreneurship spirit lakini mtaji sina😬
Kila biashara ni rahisi sana ukisimuliwa. Ingia ufanye ndio utajua kuna mambo hukuwahi kuambiwa. Imani yangu juu ya biashara ni

1. Sio kila mtu anaweza kufanya biashara. Naamini kuwa kila kazi iliyopo chini ya jua ni wito. Ili dunia iwe na balace lazima kila kazi ifanyike. Ni lazima kuwe na mtu mwenye kufanya kazi ya chini kabisa amabayo wengine wanaidharau ili tu dunia iwe kwenye balance kwa sababu watu watahitaji huduma yake. Unaweza kuingia kwenye biashara ambayo kuna mwenzio katoboa uka past na usitoboe. Ninaamini kwamba ukijua kusudibla wewe kuwepo duniani itakusaidia kujua nini sahihi kwako kufanya.

Namna moja wapo ya kujua ni pamoja na msukumo wa ndani yako. Kama kuna msukumo unatoka ndani yako kufanya jambo flani, kuna uwezekano mkubwa hio mdio calling yako. Kuna mdau hapo juu kasema biashara inakuhitaji wewe uliye na maono nayo, ila kuna watu wanamwita mtu wa negativity. Niseme hivii, huyo jamaa yupo sahihi asilimia zote. Kusimamia wazo ili likue huwa inatoka ndani yako. Yaani wewe ndio uko na maono ya kile unachokifanya kitu ambacho wengine hawataona.

Mfano mdogo sana, tunakubaliana wote kuwa biashara zina changamoto si ndio, sasa namna ya ku dela na baadhi ya changamoto inahitaji wito wa ndani ulionao. Kwamba uwe na msukumo wa ndani kutatua na kuzivumilia changamoto zitakazojitokeza. Mfano una fanya biashara ya kununua na kuuza, umenunua ila mzigo hautoki, hapo unahitaji msukumo wa ndani yako ku push kwa namna yoyote mzigo utoke. Sasa kufikiri hizo strategy kama unachokifanya sio kitu ukipendacho utafika muda utaona unateseka na huo ndio huwa mwanzo wa kuuwa biashara, ila kama inatoka rohoni uta feel proud sana kutafuta solution.

2. Imani yangu ya pili ya biashara ni kwamba kila biashara ina lipa. Tofauti ni mitaji na usimamizi. Ndio maana kila biashara inaanzishwa kila leo na kila biahsra ina kufa kila leo na zingine zina miaka zinaishi na kukua zaidi.

3. Ni vizuri kuomba ushauri wa nini ufanyanye ila ni vizuri zaidi kufanya unachokipenda kwa kuwa ndio utakisimamia kwa umakini. Biashara ni maisha, ili uifaidi inatakiwa iingie kwenye dami iwe sehemu ya wewe. Hio bond ikikosekana mwanzoni mwa biashara kufa kwake ni kugusa tu. FANYA UNACHOKIPENDA NA NDICHO UTAKACHOKISIMAMIA.

4. Kama huna passion na biashara ila unataka kuwekeza pesa yako ili izae, basi usifanye biashara, fanya uwekezaji wa hio pesa. Wekeza kwenye BINDS, wekeza kwenye viwanja, wekeza kwenye nyumba za kupangisha na vitu vingine kama hivyo. Usizungushe pesa ili hali wewe huna muda huo hata hapo mwazo wa biashara utalia.

ZINGATIA: Biashara ni kuzungusha pesa kwa haraka ikupe faida ndogo au kubwa ka haraka. Kuwekeza ni kununu au kutengeneza kitega uchumi kwa gharama kubwa au ndogo, kisha kitakuingizia pesa kidogo kidogo na baada ya muda mrefu sana ndio utaanza kuingiza faida.
 
Me nadhani ni swala la mifumo lazima uhifahamu kwanza biashara unayotaka kuifanya, kisha utengeneze mifumo itakayo kusaidia kuendesha biashara yako.
 
Wekeza kwenye bond za serikali au UTT.

Kama una kiwanja sehemu inayopangishika unaweza jenga vi apartments vidogo viwili.

Kama unataka kufanya biashara deal na vitu vinavyohesabika kwa urahisi pia ujitahidi kutumia CCTV camera na upate daily report kwa whatsapp na Mara chache ufanye stock taking
 
Waafrica kila mwenye pesa anawaza kufanya biashara. Biashara ni Hobby, Biashara inahitaji spirt kubwa sana, Biashara inamuhitaji mwenye wazo awe intact kwenye eneo la biashara ili kuendeleleza ile wazo yake.

Sasa watu wanajidanganya kwamba anaweza muweka Mke/mme/Baba/Mama/KAka/Dada/Mjomba/Shangazi/Shemeji/Baba mkwe/Mama mkwe wasimamie wazo, hii ni kujidanganya, hao hawajui lolote sio initiator wa wazo.

Ndioa maana wakina Mengi au wakina Bagharesa walianza kusiamamia wazo lao hadi walipo fikia levo za juu kabisa za kufanya deligate.

Sasa wewe day one ya Biashara yako inaanza na kukaimisha mtu, hio biashara haitafika kokote kule

Kama huwezi/huna muda wa kusimamia wazo lako nakushauri hizo pesa nunua hata bond za Serikali tu, la sivyo utazika pesa zote na utakuja lilia chooni kilio cha kujuta.Biashara za kupiga simu sio biashara.
Truth kabisaaa
 
Back
Top Bottom