Aisee Shida Vijana Vijana Wakija Vichwa Chini,mikono Nyuma Mkishakabidhiana Maumivu Sijui Kama Mfumo Umebadilika Nlinunua Boda Moja 2015 mpya tukaenda kwa mwanasheria yeye akiwa na mdhamini wake ,service juu yake kila siku anatakiwa alete 10,000 (hapa Nlimuambia Awe Anarusha Kwa Fahari Huduma Crdb)Ikiisha Mwaka Inakuwa Yake,akizidisha Siku 5 Yaani Deni Hajaleta Tunaterminate Contract,nachukua Boda Bila Kumrudishia,ila Nlifanyia Kazi Mwezi 1 tu nikaiuza na nliyemuuzia nae akaiuza ndani ya mwezi maana pasua kichwa hiyo biashara.
kijana alikuwa haleti pesa,nkampa simu tuwasiliane simu hapatikani,kwake hayupo mke na mtoto mchanga wakawa wanalia njaa kwangu kwa kujua hela zote mume analeta kwangu,nkimsaka anajificha,nkawa mbabe nikaweka dau kijiweni atakayefanikisha nimkamate nampa 15,000 siku hiyo nlimpata akakabidhi funguo zote ila ilishaanza kuchoka no service nikauza na nliyemuuzia baada ya mda akaniambia ameuza pasua kichwa
ila kuna mdada kaifanikisha hii biashara anazo boda kama 15 hivi