Biashara ya Bodaboda

Biashara ya Bodaboda

Nina mwaka mmoja sasa katika hii Biashara.

Mimi Huwa nawapa vijana Pikipiki mpya FEKON Kwa MKATABA Wa miezi 11 au 12. Mahesabu ni 100,000/= Kila baada ya siku 10 yaani Kwa Siku ni hesabu ya 10,000/=.

Vijana wengine sio waaminifu na kweli hamna mtu mkamilifu Kwa asilimia 100% changamoto zipo anaweza kupata dharula, ajali, kuumwa au matatizo binafsi tu. Ambayo Kwa hizo siku 10 anaweza kukuletea 60K au 70K au 80K etc ila Hamna shida Huwa naandika kama deni ambalo baadae Mkataba ukiishi naongea nae Tena mezanii.

Ni Biashara nzuri Kwa maana FEKON Moja inauzwa 2.3M Kwa Faida wewe Utapata sio chini ya 1M Kwa miezi 11 au 1.3M Kwa miezi 12. Ambayo ni sawa na faida ya 100,000/= Kwa Kila mwezi Kwa Pikipiki Moja.

Mwaka Huu nataka nijaribu Kwa kununua Pikipiki USED na nianze kuwapa vijana Pikipiki USED za 1.2M -1.5 Millions Kwa Mikataba ya miezi 7 mpka miezi 8. Ili nitengeneze Faida nyingi Kwa muda mchache na Kwa kutumia Hela ndogo badala ya kununua Pikipiki mpya ya 2.3M.

Changamoto zipo lakini usikate Tamaa, Kila Biashara inachangamoto zake.

Vijana wapo mtaani kwako ni swala la kupeana Mkataba mbele ya mashahidi wa pande zote mbili na Kwa kusainiwa na Mwenyekiti au Mjumbe Wa Kijiji/ mtaa husika.
Maelezo yako nayakubali kwa100% mm nlifanya ila nliacha wakati zinauzwa1.8 mil
Nafkiria kurudi ulingoni mwakani,vijana bado wananipigia kuhitaji pk pik
 
Ushauri wangu kwako ukifanikiwa kununua hizo pikipiki usije kujaribu kutoa kwa mkataba maana baada ya mkataba kuisha hiyo pikipiki inakuwa sio mali yako tena.
Nunua pikipiki mpe kijana awe anakuletea pesa kila siku kama ikatokea akishindwa makubaliano unachukua pikipiki yako.

Ipo hivi ukimpa mtu pikipiki kwa mkataba, kwa siku anatakiwa awe anakuletea elfu 10 na kwa kawaida mkataba huwa ni miezi 13.
Pikipiki mpya unanunua kwa mil 2.8,kwa siku unaletewa elfu 10.
Elfu 10000*30=300,000.
300,000*13=3,900,000
3,900,000-2,800,000=1,100,000

Faida yako kwa miezi 13 ni mil 1.1
Ina maana kwa mwezi unaingiza 84,615/=
Kwa siku unaingiza elfu 2,820/=
Na hapo pikipiki inakuwa sio yako tena.
Unatoa mil 2.8 ili upate faida ya 2,820 kwa siku??? Nakushauri kimbia.
Wengi wanofanya hii biashara ni wavivu na wana upeo mdogo kufikiri.

NB:nunua pikipiki ila usitoe kwa mkataba, tafuta kijana awe anakuletea pesa kila siku akishindwa unachukua chombo yako
Hii ya hesabu kwa siku ni Majanga zaid
 
Nyie ndo wale motivation speaker kaz yenu kubwabwaja tu Lima matikiti heka sjui nn ingieni field kwa vitendo unakuta ata boda boda hujui ata kuziba pancha
Kiongozi,Mtoa mada yupo sahihi.Hii biashara inalipa na maelezo yake ni sahihi
 
Makasiriko ya nini mkuu!!mwenye ka bucha tu ka nyama mwenye mtaji wa kg 20 tu ambazo gharama yake ni 110,000,akiuza kwa 8000 tu kwa kilo anapata 160,000 hapo faida yake 50,000 kwa siku tena mapema tu!!!eti mtaji wa 2.3 milioni kupata 3300/ =au mtaji wa milioni 34. Kupata 49,500 kwa siku ni haki sio sawa hata kidogooo!!jipeni moyo tu.
Hapo unazungumzia Active na Passive income
 
Bro Nina Kazi yangu Kila mwezi napata Mshahara.

Hii Biashara ni kuongeza mzunguko wangu Wa Hela, Biashara zipo nyingi ningeamua kuacha kazi na kwenda kufanya hizo Biashara nyingine mtaani kama kufungua duka au kuuza bidhaa tofauti.

Ila nilihitaji Biashara ambayo inaweza kujisimamia yenyewe kipindi Mimi nikiendelea na mishe zangu za Kazini.

Mimi Kwa mwaka mmoja tu pekee nimefunga Pikipiki zaidi ya 15.

Kwa Pikipiki zangu 15 tu, Kwa Siku napata 150,000/=, Kwa wiki napata 1,050,000/=, kwa mwezi Kwa hizi Pikipiki 15 napata REJESHO La zaidi ya 4,500,000/=. Kwa mahesabu ya haraka Kwa Siku napata Faida ya zaidi ya 45,000/=🟧.

Kipindi napata hizi Hela zote Mimi nipo Ofisini naendelea na mishe zangu na mshahara mwingine nausubiria mwisho Wa Mwezi.
pikipiki 15 ni sh ngapi? hazipati ajali? vp mafuta,service,kukamatwa nk,vp boda akiumwa ,akifiwa,akiwekwa ndani ,akipata dharura, vi ikiibiwa
hiyo biashara inaonekana mtaji mkubwa faida upuuzi,ni wavivu tu wa kufikiria bussienss plan na ana hela mfukoni ndio atakwenda huko,au kujionyesha tu kwa watu kwamba nayeye ana bodaboa
 
Ushauri wangu kwako ukifanikiwa kununua hizo pikipiki usije kujaribu kutoa kwa mkataba maana baada ya mkataba kuisha hiyo pikipiki inakuwa sio mali yako tena.
Nunua pikipiki mpe kijana awe anakuletea pesa kila siku kama ikatokea akishindwa makubaliano unachukua pikipiki yako.

Ipo hivi ukimpa mtu pikipiki kwa mkataba, kwa siku anatakiwa awe anakuletea elfu 10 na kwa kawaida mkataba huwa ni miezi 13.
Pikipiki mpya unanunua kwa mil 2.8,kwa siku unaletewa elfu 10.
Elfu 10000*30=300,000.
300,000*13=3,900,000
3,900,000-2,800,000=1,100,000

Faida yako kwa miezi 13 ni mil 1.1
Ina maana kwa mwezi unaingiza 84,615/=
Kwa siku unaingiza elfu 2,820/=
Na hapo pikipiki inakuwa sio yako tena.
Unatoa mil 2.8 ili upate faida ya 2,820 kwa siku??? Nakushauri kimbia.
Wengi wanofanya hii biashara ni wavivu na wana upeo mdogo kufikiri.

NB:nunua pikipiki ila usitoe kwa mkataba, tafuta kijana awe anakuletea pesa kila siku akishindwa unachukua chombo yako
safi kabisa
 
Kuna kitu hapa watu wanashindwa kuelewa Sina mtaji Wa 34.5 Millions, nimesema nilianza na mtaji Wa 9 Millions Kwa kuanza na Pikipiki 4 tu mpka kufika sasa zipo zaidi ya Pikipiki 15.

Concept hapa ni kwamba Kwa marejesho haya haya ya Pikipiki nilizonunua mwanzoni ndio nilitumia kununua Pikipiki nyingine zilizofuata huku nikiongeza 30% ya sehemu ya Mshahara wangu Kila mwezi.

Mtaji wangu ni 9 Millions + 30% ya Mshahara wangu Kila mwezi mpka kufika hatua hii Kwa muda wa miezi 13 mpka Leo hii.

Kukosoa sio jawabu nipeni ushauri Wa Biashara ambayo inatakiwa kuingiza Faida ya zaidi ya 50,000/= Kwa Siku Kwa mtaji Wa 9 - 10 Million's.

Kukosoa Kwa sababu ulisikia mtu mwingine akishindwa hiyo biashara sio jambo jema, Nina zaidi ya mwaka mmoja sasa na sijaona shida yyote katika hii Business.

Kushindwa kwako sio kwamba na mwingine asifanye hiyo Biashara, TUKOSOE Kwa kutoa USHUHUDA Wa Biashara unayofanya wewe na KIPATO/FAIDA unayopata Kwa Siku itapendeza.

🟢Mfano Mimi Kwa Siku sikosi REJESHO La 150,000/=. Katika hii Hela 50,000/= ni kama Faida yangu Kwa Siku na 100,000/= ni Hesabu ya hela inayorudi kutokana na uwekezaji wangu ndani ya siku Moja Kwa mwezi mmoja (30 days) nitarudisha 3M ya mtaji wangu.

🟡TUPEANE IDEA ZA BIASHARA ZA KUFANYA, TOA USHUHUDA KAZI/BIASHARA UNAYOFANYA NA FAIDA UNAYOPATA ILI TUPATE MOYO WA KUFANYA BIASHARA NYINGINE PIA, ILI NlWEKEZE KATIKA BUSINESS NYINGINE.
Kiongozi komaa ongeza pikipiki ziwe za kutosha , kuna kampuni inaitwa watu credit yenyewe inafany issue kama hizo na kunamshkaji aliniambia kuna kipindi walikuwa wanatoa pikipiki mia mbili kwa mwezi na zaidi , ipo pia kenya wanatoa huko pikipiki karibu elfu, naijua its a well off company , jipange endelea kuongeza mzigo
 
Kuna jamaa anapikikinzaid y 300 ila anatoa kwa mkataba mana kila mwezi lazima anunue pikipki 10+ hakuna mwezi unapita janunua mpya yule jamaa tangu nimjue
 
Yani namba B hesabu 22k??
Acha dhuluma mkuu, namba B ni bajaj yenye miaka nane maximum.

Namba B hesabu yake 10000 au 15000 kwa derava mshamba kama vipi kaaa na kipumbu chako
Basi Kaa bila kazi
 
Yani namba B hesabu 22k??
Acha dhuluma mkuu, namba B ni bajaj yenye miaka nane maximum.

Namba B hesabu yake 10000 au 15000 kwa derava mshamba kama vipi kaaa na kipumbu chako
Mkuu mbona sijakuita Wala kukutukana ndugu🤔🤔, hiyo Bajaj engine bando nzima na iko Bomba.
👉Body ndo imara kabisaaa, Afu ishapata dereva na analeta 20 per day bro.
 
Sasa kweli yaani pikipiki 15 ni sawa na milioni 34.5 unaona faida ya 49,500 kwa siku ni sawa kweli?!!Hapanaaa hiyo kwa hesabu za kibiashara ni hakuna kitu hapo!!
Nashangaa hio 49k jamaa aniita faida wakati mtaji bado haujarudi hizi hesabu hizi aiseee
 
Jiandae Kwa Hela za service za Kila mara, maana bodaboda anajua hiyo Pikipiki sio ya kwake na hawezi kuitunza Kwa umakini.

Atahakikisha anabeba chchote kile hata kama ni tofali, chuma etc Ili tu akuletee hesabu yako na Hapo Pikipiki haimalizi mwaka imechakaa na umetumia Marejesho kurekebisha Pikipiki yako.
Hapa ndipo napouona ukichaa kwenye uendeshaji wa hii biashara
Yaani dereva anakuja na masharti yake kwenye chombo cha mtu 😁
 
Mkuu mbona sijakuita Wala kukutukana ndugu[emoji848][emoji848], hiyo Bajaj engine bando nzima na iko Bomba.
[emoji117]Body ndo imara kabisaaa, Afu ishapata dereva na analeta 20 per day bro.
Injini ya miaka nane iwe full acha uongo mm nipo kwenye bajaj mwaka wa 10
 
Back
Top Bottom