Biashara ya Bodaboda

Biashara ya Bodaboda

Ndio maana tunashindwa kushindana na wahindi na wachina. Wenzetu hiyo faida ya 3000 kwa siku ni nyingi mno na kwa kuwa wana nidhamu ya biashara wanafanikiwa sana.
Wenzetu wana Pambana, kuwa na vitega uchumi vingi vyenye kuwaletea hizo 3000 tatu za kutosha
 
Binafsi niko njiani kuianza hii biashara ndani ya mwezi mmoja. Sioni faida kuiweka 2.3M banki na mitozo yote hii kuliko kuikosa 3000 ya siku, nani atanipa bure?
Mkataba kwa siku 10k wengine hadi 12k ndani ya mwezi unaingiza 300k hadi 360k

Ukiwa nazo mbili 600k hadi 720k kwa mwezi

Tuseme zote ulinunua used kwa 1.3m + 1.3m= 2.6m

Ndani ya miezi 4 umerudisha hela yako yote uliyonunulia unaanza kutengeneza faida

NB: Nidhamu ya matumizi, usimamizi mzuri wa chombo, usicheke na dereva kuwa kauzu
 
Mkataba kwa siku 10k wengine hadi 12k ndani ya mwezi unaingiza 300k hadi 360k

Ukiwa nazo mbili 600k hadi 720k kwa mwezi

Tuseme zote ulinunua used kwa 1.3m + 1.3m= 2.6m

Ndani ya miezi 4 umerudisha hela yako yote uliyonunulia unaanza kutengeneza faida

NB: Nidhamu ya matumizi, usimamizi mzuri wa chombo, usicheke na dereva kuwa kauzu
Kumbe mwanafunzi una nielewa vyema.
👉Msisahau na bajaji. Ntawapa dark secret kuhusu hivi vyombo vya moto
 
Nina mwaka mmoja sasa katika hii Biashara.

Mimi Huwa nawapa vijana Pikipiki mpya FEKON Kwa MKATABA Wa miezi 11 au 12. Mahesabu ni 100,000/= Kila baada ya siku 10 yaani Kwa Siku ni hesabu ya 10,000/=.

Vijana wengine sio waaminifu na kweli hamna mtu mkamilifu Kwa asilimia 100% changamoto zipo anaweza kupata dharula, ajali, kuumwa au matatizo binafsi tu. Ambayo Kwa hizo siku 10 anaweza kukuletea 60K au 70K au 80K etc ila Hamna shida Huwa naandika kama deni ambalo baadae Mkataba ukiishi naongea nae Tena mezanii.

Ni Biashara nzuri Kwa maana FEKON Moja inauzwa 2.3M Kwa Faida wewe Utapata sio chini ya 1M Kwa miezi 11 au 1.3M Kwa miezi 12. Ambayo ni sawa na faida ya 100,000/= Kwa Kila mwezi Kwa Pikipiki Moja.

Mwaka Huu nataka nijaribu Kwa kununua Pikipiki USED na nianze kuwapa vijana Pikipiki USED za 1.2M -1.5 Millions Kwa Mikataba ya miezi 7 mpka miezi 8. Ili nitengeneze Faida nyingi Kwa muda mchache na Kwa kutumia Hela ndogo badala ya kununua Pikipiki mpya ya 2.3M.

Changamoto zipo lakini usikate Tamaa, Kila Biashara inachangamoto zake.

Vijana wapo mtaani kwako ni swala la kupeana Mkataba mbele ya mashahidi wa pande zote mbili na Kwa kusainiwa na Mwenyekiti au Mjumbe Wa Kijiji/ mtaa husika.
"Ni Biashara nzuri Kwa maana FEKON Moja inauzwa 2.3M Kwa Faida wewe Utapata sio chini ya 1M Kwa miezi 11 au 1.3M Kwa miezi 12. Ambayo ni sawa na faida ya 100,000/= Kwa Kila mwezi Kwa Pikipiki Moja"

Miss allocation of money. Asante kwa mchanganuo, biashara hii hainifai
 
Biashara ya bodaboda ni nzuri sana na inalipa haswa endapo tu dereva utakua wewe mwenyewe, otherwise utakua unamfaidisha mtu. Imagine dereva anaingiza zaidi ya 30k then ya bosi ni 10k, tena hapo kashajaza mafuta na other expenses kasha clear.
 
Back
Top Bottom