Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

Wawekee wateja maziwa ya unga ya kupima na prestige ya kupima wakikuzoea utanikumbuka
Prestige ya kupima!
Sijawahi iona. Huona prestige za makopo sealed, hizi za kupima zinakuwa kwenye ujazo gani?
 
Tafuta fremu fungua duka....nenda TRA kaombe TIN number (siku moja tu unapata), watakupa tax clearance nenda halmashauri kaomba leseni ya biashara ndani ya siku saba unapata na gharama ni 70,000 tu. Then waulize hapo halmashauri bibi afya yuko wapi ili wakupe certificate ya afya maana wanasumbua baadae kama huna cheti cha afya. Kwangu walikuja wanataka kunipiga faini eti kwanini nauza unga na maharage sina cheti cha afya... uduanzi kabisa. Ila niliwafuata wakanipa. Then pale dukani nunua dust bin la uchafu la kuweka maganda ya pipi, chupa za maji nini nakadharika ili wasije jamaa kukupiga faini maana siku hizi pesa baba inatafutwa kama nini. Then fungua duka kula vichwa hapo....mambo ya kisheria yameishai hapo. Kitambulisho mimi sikuchukua maana mtaji wangu ni zaidi ya milioni 4 kwa mwaka na wala sitaki umasikini na kusumbuana na watu....

Ajabu juzi walikuja watu wa halmashauri ya ubungo wakawa wamejaza form eti wanasema nauza duka bila kulipa service levy. Na wakawa wamesaini kwenye karatasi eti nimekubali nilipe faini 380,0000/-. Nikawaambia kuwa kwa nini mimi nilikuja kuomba leseni pale Halmashauri hamkuniambia kuhusu mambo ya service levy? na iweje wewe usaini siani yako kwa kuandika jina langu alafu useme mimi nimekubali. Nikawaambia kuwa utaratibu ni nyie kunipa elimu alafu niende kama natakiwa kulipa service levy nilipe sio kuja na kunitisha na makaratasi mengi alafu unataka pesa on the spot 380,000/-. Tulizinguana wakaondoka hawajarudi mpaka leo na wala sijui kama natakiwa kulipa service levy au la!!! Ila acheni bana wafanyabiashara wanateswa na hawa watu wanajiita manispaa duhhhh....ila nakomaa nao tu ninapoelewa tunaenda sawa nisipoelewa mtiti kweli kweli mpaka nielewe....huwa sitoi pesa hivi hivi
Mkuu hizi kanuni ulizoeleza hapo zinawahusu hata wenye mitaji chini ya m.4?
 
Chumvi kubwa kwa huku 12000
Chumvi ndogo 5000
Ponpon 40000
Freestyle hizi ni ped ndogo nabkubwa 22000
Betri aina zote ndogo na kubwa wakati kubwa huku nilipo ni 110000
Sukari kg 50 ni 105000
Sukar kg 25 ni 54000
Ngano azam bora 25500
Kleesoft sabuni ya unga kg 15 ni 31000
GOOD
 
Mm mpk leo mume wangu ananiambia eti sijapata faida wala nisiweke hela eti ni faida najidamganya so hela zote nazirudisha kwenye kununua bidhaa i mean nanunua na pia naongezea bidhaa mpya. So mpk sasa hivi sijajua ntatoaje faida nilitamani na mm kujua hilo somo
Ni rahisi kwake kujua faida anayoipata kwani awali kabisa wakati anaanza biashara alihesabu kila bidhaa alizozileta kisha akajua bei aliyonunulia kila bidhaa na bei atakayouzia. Hivyo, aliweze kujua faida ya kila bidhaa moja moja. Kisha akawa anarekodi kila siku vitu anavyouza. Mfano kama kitu kanunua 250, ye anauza kwa 500. Hapo faida ni 250 so kama leo kauza hivyo vitu kwa siku 10 means ana faida ya 2500.

Kikubwa na cha msingi katika biashara yoyote no matter how small it is, kutunza kumbukumbu ya mauzo na matumizi yako ya biashara ni muhimu ili kujua kama mwenendo wa biashara yako.
 
You guys are fun!!! so you keep asking for my progress. By the way.... so far so good and I see the future will hold well. Please, take all the advises in this thread into action if you are real serious. Don't keep your eye on my business, it will not help you.
Very true. Shida moja kubwa binadamu tunakosa uthubutu and that's the biggest problem vijana wa sasa tunalo. We don't want to take risks. Mtu badala ya kuchukua mafunzo anataka kujua progress akiamini kufanikiwa kwako basi naye akifanya ulichofanya atafanikiwa kama wewe.
 
Uzi bora kwangu kila siku maana lazima niupitie kupata nondo mpya, asante nyote mnaochangia
 
Kujua faida kwakwel ni ngumu mno. kujua kama kuna faida n kuangalia maendeleo ya biashara, kwamba vitu vikiisha hela ya kununulia ipo na pia ukiongeza vitu biashara bado inakuwa imesimama

Just hua tunajua faida kwa kuangalia maendleo ya duka.

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuuuu sasa hiyo si ni hatari...! Matumizi yanaweza kuzidi faida
 
Kwa mtaji ulionao tafuta bidhaa moja tu uuze kwa jumla, biashara ya duka la reja reja hailipi faida zake kwenye bidhaa ni ndogo sana kama 10% maake ni kwamba ukiuza laki moja kwa siku unapata faida 10,000 bado kodi Tra, manispaa, usafi, mlinzi. Kwa pesa hiyo unaweza fanya biashara ya nafaka na ikakulipa vizuri tu mfano unatoa mchele Morogoro au mbeya unakuja kuuza Dar,
Ni ushauri tu.
Mkuu kama hujui jambo bora ukakaa kimya, mimi hizi ndio biashara zangu, hiyo kwa rejareja faida yake si chini ya 20% labda uwe unauza bei za chini ya zilizozoeleka, na hiyo jumla ndio ina faida ndogo sana, faida zake ni 7% mpaka 12%, hapo inategemea na aina ya biashara.

Reja inayolipa zaidi ni vipodozi na baadhi nyinginezo ambazo ni za kupatania bei hasa ukiwa eneo zuri ya vitu maduka vitu vidogo mtaani bei zake zinajulikana
 
Ahsante kwa ushauri mkuu. Mtaji wa nafaka upo mkuu nimeshaleta mzigo kutoka mbeya wa mchele na nina unga wa sembe na dona pia. Nataka kuweka na vitu vingine vya rejareja. Faida ya asilimia 10 inanitosha mkuu nyingi sana hiyo madam turnover ikiwa kubwa.
Kama umeshaweka hivyo vitu utakua umeelewa komenti yangu mkuu, na faida zake zilivyo...
 
Duka la rejareja faida yake ni ndogo mnooo,kwa mfano waweza uza laki tatu kwa mwezi ukapata faida 15000 tuu.Kwa mm ninavyoona fanya biashara ya kitu kimoja kingi uuze kwa jumla mfano viazi toka Mbeya to dar,au maharage na nafaka nyingine.
Sio kweli mkuu, hizi biashara nmefanya mwaka wa 10 huu sijaona faida ndogo hivyo, kwenye laki hukosi 20
 
Asante Mkuu
Tafuta fremu fungua duka....nenda TRA kaombe TIN number (siku moja tu unapata), watakupa tax clearance nenda halmashauri kaomba leseni ya biashara ndani ya siku saba unapata na gharama ni 70,000 tu. Then waulize hapo halmashauri bibi afya yuko wapi ili wakupe certificate ya afya maana wanasumbua baadae kama huna cheti cha afya. Kwangu walikuja wanataka kunipiga faini eti kwanini nauza unga na maharage sina cheti cha afya... uduanzi kabisa. Ila niliwafuata wakanipa. Then pale dukani nunua dust bin la uchafu la kuweka maganda ya pipi, chupa za maji nini nakadharika ili wasije jamaa kukupiga faini maana siku hizi pesa baba inatafutwa kama nini. Then fungua duka kula vichwa hapo....mambo ya kisheria yameishai hapo. Kitambulisho mimi sikuchukua maana mtaji wangu ni zaidi ya milioni 4 kwa mwaka na wala sitaki umasikini na kusumbuana na watu....

Ajabu juzi walikuja watu wa halmashauri ya ubungo wakawa wamejaza form eti wanasema nauza duka bila kulipa service levy. Na wakawa wamesaini kwenye karatasi eti nimekubali nilipe faini 380,0000/-. Nikawaambia kuwa kwa nini mimi nilikuja kuomba leseni pale Halmashauri hamkuniambia kuhusu mambo ya service levy? na iweje wewe usaini siani yako kwa kuandika jina langu alafu useme mimi nimekubali. Nikawaambia kuwa utaratibu ni nyie kunipa elimu alafu niende kama natakiwa kulipa service levy nilipe sio kuja na kunitisha na makaratasi mengi alafu unataka pesa on the spot 380,000/-. Tulizinguana wakaondoka hawajarudi mpaka leo na wala sijui kama natakiwa kulipa service levy au la!!! Ila acheni bana wafanyabiashara wanateswa na hawa watu wanajiita manispaa duhhhh....ila nakomaa nao tu ninapoelewa tunaenda sawa nisipoelewa mtiti kweli kweli mpaka nielewe....huwa sitoi pesa hivi hivi
 
Nilifanikiwa mkuu naendelea mdogo mdogo. Kifupi bidhaa huwa nanunulia maduka ya jumla pale Manzese Tip top na darajani na ndo nilienda kuna wauzaji waungwana sana wakanipa list zote na utaratibu wa kupanga bei.

Kuna jamaa walijitokeza humu kunisaidia ambao nilitaka niwape elfu 40,000 ila nikaona wazugaji tu. Mara tuma kwanza pesa mara njoo tuonane hii kasi sio rahisi kama unavyofikiri na wakati mimi nilitaka mtu aniandalie excel file yenye bidhaa zote na bei ya kununulia na kuuzia na wapi nikanunue alafu nampa hiyo 40,000 simple tu. Watu wagumu kweli. Baada ya kuona longo longo hizi na mimi ni mtu aisiyetaka complication na mtu wa kuyaona mambo hata magumu kuwa ni marahisi nikaachana nao nikaingia mwenyewe chimbo madukani na kwenye maduka ya akina mangi na kuulizia. Wengine walinifukuza na wengine walikataa kata kata hata kwa kuwalipa. Ila kwa vile penye nia pana njia nilifanikiwa. Na kwa vile sina hiyana na tamani watanzania wenzangu watamanio kuifanya hii biashara waifanye bila longo longo nyingi nimeweka hapa baadhi ya bidhaa ambazo nimezidowload kwenye accounting software ninayotumia dukani. So far so good nilianza na mauzo ya siku ya kwanza ya shilingi 10,200 nikala faida ya buku mbili kwa siku na kwa sasa in average mauzo ni 70,000 kwa siku with average profit ya 30% ambayo ni 21,000 kwa siku.

Nenda kafungue mkuu na niulize nikwambie ninayoyajua so far kwa hii experience ya miezi mitatu.

Karibu sana

Mkomamazu
Nashukuru na wewe uliliona kuna wadau wanakatisha tamaa sana wakati biashara hawazijui, hongera mkuu kwa kutokatishwa tamaa
 
Mm mpk leo mume wangu ananiambia eti sijapata faida wala nisiweke hela eti ni faida najidamganya so hela zote nazirudisha kwenye kununua bidhaa i mean nanunua na pia naongezea bidhaa mpya. So mpk sasa hivi sijajua ntatoaje faida nilitamani na mm kujua hilo somo
Nunua daftari chora jedwali lenye tarehe, manunuzi, mauzo, faida, na matumizi utagundua kila kitu, ukiona umenunua mzigo wa laki 1 ukaandika faida yake ikawa elfu 20 au ziadi au pungufu kidogo ujue siku ukiwa na mauzo hayo faida yake inacheza hapo kwenye elfu 20...
 
Sio kweli biashara ipo hivi ulieka mtaji wala laki 5 hiii leo mtaji unasomeka laki 9 hivyo ww biashara yako inaongezeka ila huchunguzi
Mm mpk leo mume wangu ananiambia eti sijapata faida wala nisiweke hela eti ni faida najidamganya so hela zote nazirudisha kwenye kununua bidhaa i mean nanunua na pia naongezea bidhaa mpya. So mpk sasa hivi sijajua ntatoaje faida nilitamani na mm kujua hilo somo
 
Mkuu hizi kanuni ulizoeleza hapo zinawahusu hata wenye mitaji chini ya m.4?
Na wewe fanya homework kidogo bana....si umesikia kila siku kuwa vitambulisho vya wafanyabiashara wanapewa wenye mtaji chini ya 4,000,000! sasa ukiwa nacho hicho si ndo umemaliza kila kitu au? Sina hakika ya njia wanayopitia ila nadhani haihitaji process zote hizo.
 
Nipo kwenye hii biashara (rejareja). Nimefanya kaubunifu flan ka kuongeza maziwa ya mgando ya mgando na cake tam baada ya kugundua kuna uhitaji. Nasubri laini zang za figo pesa na Mpesa. Vyote hv (maziwa, figo, m-pesa) nimefanya kwaajil ya kujiingizia pato tengefu au la pemben. Mfano maziwa kwa mwez (predictably) napata si chin ya laki na nimeanza wik 3 zilzopta Expecting to increase kwa upande wa tigo na m-pesa sijajua maana sijawahifanya na lain zang hazijatoka bado miez 2 ss hvyo mwnye uzoefu naomba kujua pato lake kwa mwezi.

Hapa pia naomba kuongezewa ubunifu mwngine wa biashara nyingine simple kama ya hyo maziwa itakayo nipa kuanzia laki (100, 000) kwenda juu.

Asanteni.

Note:
Duka lina miez 3 ss.
 
Back
Top Bottom