Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Biashara ya mchele ukitaka inaweza fanyika kwa watu wa aina 5.
1. Unakuwa na mashamba yako au yakukodi. Ukalima.ukakoboa.ukaingiza sokoni mwenyewe. Hao ni wachache na wana maeneo makubwa.
2. Wananunua mpunga kwa jumla na wana mashine za kukoboa. Wanahifadhi bei zikipanda wanakoboa na kuingiza mchele sokoni.
3. Wananunua mpunga mashambani na kuhifadhi kwenye magodown/mashine huko maeneo kama ubaruku nk. Bei zikiimarika wanakoboa na kuingiza sokoni ama kwa kuleta wao au kuuzia huko mashine.
4. Wanaenda nunua mchele huko mashine unaokobolewa na kusafirisha kuleta sokoni kama wafanyabiashara wa jumla.
5. Unanunua huku mjini kwa wafanyabiashara wa jumla nawe unauza kwa wenzio. Jumla au rejareja.

We unaulizia na.ngapi upate undani wake na umelenga mbeya? Morogoro? Mchele wa mwanza na shinyanga una soko rwanda na burundi dar haulipi.

Mimi nilifikiria wa shinyanga lakini mchele nije kuuza reja rejana jumla. Na kwa nini wa shinyanga au Mwanza hauna soko Dar. Unatofautiana vipi na mwingine?

Natanguliza shukrani.
 
Kadri ya jinsi nilivyoelewa maswali yako juu:
Ili kujua mpunga kama ni mzuri huwa tunachukua sample na kuumenya na kisha kutathmini ubora wake-mzuri hutoa punje zilizonyooka na nyeupe wakati mbaya hutoa mpunje zilizovunjikavunjika, ama nyekundu badala ya nyeupe.

Pia ubora wa punje/mchele huweza tegemeana na mashine uliyokobolea na technician anaeseti mashine-kuna mashine zenye wataalam wa kuseti mashine kulingana na mpunga unaokobolewa kwa wakati husika na mchele wote utokao kwenye mashine hizo ni "super" au ulionyooka tu.

-Ubora wa mchele hutathmini faida utakayopiga wakati wa kuuza mchele huo.
Kwa mtaji mkubwa wa kuweza kununua tani hata 2 za mchele ni vyema ukauza mchele pale bei ya mchele inapokuwa juu zaidi sokoni wakati mashineni ukiuzwa kwa bei ya chini. Kwa mfano kama mashineni unauzwa kwa Tsh.800 kwa kilo na kuuzwa kwa Tsh. 1400 sokoni na wewe ukanunua tani 2 kwa Tsh. 1,600,000/- na kuuza kwa Tsh. 2,800,000/- wakati gharama ya usafiri ni kama 90,000/- kama utakuwa umetoa mzigo Shinyanga kuja Dar kwa mfano, hapo unakuwa umetengeneza faida ya 700,000/- kwa safari moja.

-Faida itaongezeka kutegemeana na safari unazofanya kwa wiki yaani safari moja, mbili au tatu; na hii inaonesha atakaepiga faida zaidi ni yule anaenunua mchele na kusafirisha moja kwa moja kuliko anaechukua mpunga na kupanga mstari mashineni ili akoboe ambapo anaweza koboa tani chache tu siku.

Kuna wakati pia kununua mpunga na kuuhifadhi kwa ajili ya kukoboa na kuuza baadae kunalipa sana, kwa mfano ikiwa leo gunia linauzwa kwa Tsh. 55,000/- na ukanunua na kulihifadhi hadi mwezi wa 12 (2016) au kwanza mwakani (2017) ambapo bei inaweza kuwa 85,000/- hadi 100,000/- kuna uwezokano wa kupiga faida isiyopungua 25,000/- kwa gunia kama utauza mpunga kama mpunga; ukikoboa na kuuza mchele unapiga zaidi ya hiyo (25,000/-)

Kwa ujumla ni vyema kipiga zote (mchele na mpunga) kulingana na kile kinachotoa faida zaidi kwa msimu husika, eneo unalofanyia biashara kama vyote vinapatikana kama mpunga haupatikana usione tabu kwenda maeneo ama mkoa wanakolima na nununua kisha hifadhi au koboa-ukiwa mfanyabiashara lazima uzungukie maeneo ya interest yako na utajua mikoa mingi na hata vijiji vingi nchini na umbali kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine hususani ukishakuwa na usafiri wako.

Asante kwa majibu ya kina. Barikiwa sana

Mimi nataka kununua lakini naona mpunga ni risk sana sababu nahitaji mchele ulionyooka grade 1na vile siendi kununua mwenyewe natuma mtu basi ni bora mchele kuliko mpunga.

Pia naomba ushauri,mchele grade 1 wenye kupendwa na watu unaonukia na wenye ladha ni wa mkoa upo Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Morogoro? Wapi nitapata mzuri zaidi?
 
Mkuu ni vyema kweli kujifunza hata mimi hapa najifunza kutoka kwa walionitangulia na kunishawishi niingie huku kwa kweli kuna watu wako juu kiasi kwamba wao mchele wao ni wa kimataifa simu wanazopokea ili wapeleke mzigo ni kutoka Rwanda, Kenya na wanapeleka kweli ila nasi ndo tunawapatia mzigo na tunapata faida ya kutosha.

Kizuri zaidi ni kupiga zote mchele mpunga vyote nunua kama una nafasi na una sehem nzur ya kuhifadhi kwani kuna wakati mpunga unakuwa chini sana kati ya 35 000/- na 55,000/- tu katika mikoa ya Katavi na shinyanga respectively lakini baada ya muda fulani unauza kwa 85000/- hadi 100,000/ - na ukikoboa inakuw zaidi ya hapo.

Hapa mwenzako ni kuzunguka tu mikoani kama mtalii wa ndani ila watu wanakusanya punga na hata shambani naingia.
Hakuna kitu kitamu kama hii game mkuu vigari vya M20 kwako itkuwa kawaida tu hadi natamani serikali iache amsha amsha inayofanya kwa vijana kuhimiza wajiajiri-waachwe waendelee kusubiri ajira za kuagizwa maana wao waziona hizi kazi ni kizamani. Kusema kweli namuona mbunge mmoja yuko kwenye kilimo na anapiga gunia 5, 000 na anapeleka sijui nje na ana trecta zake kwa kweli hata wananchi wakimpiga chini ubunge hana njaa kabisa.
Mkuu napenda kujua yafuatayo:

1: Msimu wa mavuno ni upi?
2: Kama nataka kuchukulia mchele kati ya Shinyanga au Mwanza halafu nisafirishe Burundi au Rwanda,itanigharimu kiasi gani kwa kuanzia na tani mbili?
3: Kuhusu vibali vya kutoa mchele hapa na kupeleka kwenye nchi nilizotaja hapo juu vikoje?
4: Kwa wastani gunia inafika kiasi gani kwa kipindi cha mavuno na soko lake kwenye nchi hizo likoje?

Naonba yeyote mwenye ufahamu wa hayo anisaidie kunijibu.
 
Hapo mpka ufanye kwanza research kwa watu wanao Fanya biashara za mikoan but mm huwa nauzia hapahapa na inanilipa, japo kuwa mda mwingi nafanya shughuli za kiserikali.
 
Asante kwa majibu ya kina..Barikiwa sana
Mimi nataka kununua lakini naona mpunga ni risk sana sababu nahitaji mchele ulionyooka grade 1..na vile siendi kununua mwenyewe natuma mtu basi ni bora mchele kuliko mpunga.

Pia naomba ushauri,mchele grade 1 wenye kupendwa na watu unaonukia na wenye ladha ni wa mkoa up? Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Morogoro? Wapi nitapata mzuri zaidi
Nitaku-PM mkuu naona umeuliuza confidential question! Hahahaaaaaah, nimefurahi sana mkuu kwa swali lako!
 
Mkuu napenda kujua yafuatayo:

1: Msimu wa mavuno ni upi?
2: Kama nataka kuchukulia mchele kati ya Shinyanga au Mwanza halafu nisafirishe Burundi au Rwanda,itanigharimu kiasi gani kwa kuanzia na tani mbili?
3: Kuhusu vibali vya kutoa mchele hapa na kupeleka kwenye nchi nilizotaja hapo juu vikoje?
4: Kwa wastani gunia inafika kiasi gani kwa kipindi cha mavuno na soko lake kwenye nchi hizo likoje?

Naonba yeyote mwenye ufahamu wa hayo anisaidie kunijibu.
Nitajibu baadae mkuu usiwaze
 
Okay, kama utakuwa poa biashara iko poa sana tena sana hususan kama utakuwa na uwezo wa kufuata au agiza mzigo mkubwa toka Shinyanga, Mbeya au Morogoro au Dodoma. Pia kama uko vizuri zaidi unaweza chukulia hapa mjini (Dar) na kuuza popote unapoona inafaa hata nje ya nchi kama kibali kinaruhusu.

Biashara hii iko poa huwezi jutia japokuwa mwaka huu kidogo kodi zinasumbua kwa mfano Shinyanga vijijini kodi imekuwa kubwa sana (imepanda toka 500 hadi 2000) ndani ya wiki hii halimashauri ilipochukua jukumu la kukusanya kodi yenyewe badala ya mudhabuni kitu ambacho kitapandisha bei ya mchele maradufu na kama itapanda zaidi itapunguza faida kwa mfanyabiashara ya mchele hususani yule mwenye kununua na kuuza mchele badala ya mpunga toka kwa mzalishaji.
Naweza wasiliana na wewe mkuu maana na mimi nataka nijikite huko sasa.
 
Mkuu napenda kujua yafuatayo:

1: Msimu wa mavuno ni upi?
2: Kama nataka kuchukulia mchele kati ya Shinyanga au Mwanza halafu nisafirishe Burundi au Rwanda,itanigharimu kiasi gani kwa kuanzia na tani mbili?
3: Kuhusu vibali vya kutoa mchele hapa na kupeleka kwenye nchi nilizotaja hapo juu vikoje?
4: Kwa wastani gunia inafika kiasi gani kwa kipindi cha mavuno na soko lake kwenye nchi hizo likoje?

Naonba yeyote mwenye ufahamu wa hayo anisaidie kunijibu.

1. Msimu wa mavuno ni kipindi ambacho wakulima wanavuna mpunga toka shambani na kupeleka majumbani mwao au kwenye maghala yao. Ni kipindi ambacho mpunga ni mwingi sana pia bei yake mara nyingi huwa ya chini sana- Demand and Supply principles zinaapply.

Misimu hii hutofautiana miongoni mwa mikoa inayozalisha mpunga kwa wingi kwa mfano leo hii mpunga umeshaisha mashambani huko Shinyanga wakati Morogoro wakulima bado wanatoa mashambani.

2. Tani mbili ni chache sana kupeleka Rwanda ama Burundi, itakupa hasara tu kwa sababu gari za kwenda huko toka Shinyanga ni sawa na hamna kwani zinazoenda huko ni zile semi kubwa ambazo kuibebesha tani mbili tu hadi Kigali hakuna mwenye gari atakaekubali kuacha kubeba saruji, nondo ama makontena ya shehena ya kemikali toka bandarini ukilinganisha na kuvizia gari hizo wakati zikirudi toka Kigali na kuzipatia tani moja kwa 45,000/- kwenda Dar kwani zinakuwa tupu dreva anabeba chochote hata kama ni mkaa au kuku ili tu dreva apate kidogo.
Hivyo kwa tani chini ya 100 ni vizuri kupigia Dar, Arusha na inalipa tu tena sana.

3. Kiufupi vibali vinasumbua isipokuwa kwa wale wateule kwani hakuchelewi kutolewa zuio la kuuza nafaka nje ya nchi japo wateule huendelea. Sijui labda safari hii mambo yatakuwa laini au magumu zaidi katika kuuza nje ya nchi muda utaingea kufukia mwezi wa 9/10.

4. Bei hutegemeana na mkoa husika kwa mfano Shinyanga (45,000 hadi 55,000/-) wakati wa mavino na vile 35,000/- hadi 40,000/- Mpanda, n.k.

Kwa upande wa Rwanda na Kenya wakati wote bei inakuwa juu ukilinganisha na hapa Tz kwa mfano kama Dar unanunua kwa Tsh. 22,000/- Kigali inakuwa Tsh. 3,000/- kwa kilo kutegemea na muda (miezi).
 
Habari,

Kwa anayetaka tufanye biashara ya mchele, nipo kahama na nina connection na watu wa malori yanayoenda dar, if ur interested lets join hands.
 
Okay, kama utakuwa poa biashara iko poa sana tena sana hususan kama utakuwa na uwezo wa kufuata au agiza mzigo mkubwa toka Shinyanga, Mbeya au Morogoro au Dodoma. Pia kama uko vizuri zaidi unaweza chukulia hapa mjini (Dar) na kuuza popote unapoona inafaa hata nje ya nchi kama kibali kinaruhusu.

Biashara hii iko poa huwezi jutia japokuwa mwaka huu kidogo kodi zinasumbua kwa mfano Shinyanga vijijini kodi imekuwa kubwa sana (imepanda toka 500 hadi 2000) ndani ya wiki hii halimashauri ilipochukua jukumu la kukusanya kodi yenyewe badala ya mudhabuni kitu ambacho kitapandisha bei ya mchele maradufu na kama itapanda zaidi itapunguza faida kwa mfanyabiashara ya mchele hususani yule mwenye kununua na kuuza mchele badala ya mpunga toka kwa mzalishaji.

Nipo Dar natamani sana kufanya hii Biashara naomba ila sijui lolote mtaji ninao naomba unisaidie mkuu asante nina uwezo wa kuanza na tani 5 mpaka 10 itategemea na bei ya manunuzi.
 
Nina dada yangu alifeli form 2 mara mbili akaamua kuacha shule akawa anashinda maporini kununulia watu mipunga anapata faida kidogo sasa may nilienda likizo home yaani huyo dadaangu anahela za kumtosha na kashajenga nyumba mm msomi na degree yangu na cpa ila hela alizonazo huyo dadaangu smtyms naona kuajiliwa sio kabisa.
Hata siku 1 usidanganyike na mafanikio ya akina dada, wanambinu na mitaji mingi ambayo wewe huwezi, ukivutiwa na hao umepotea mkuu.
 
Back
Top Bottom