Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Yaani kama vile ulikuwa kwenye akili yangu.
Huu unaweza kuwa ni mwaka wa njaa.
Baada ya kuwepo kwa over supply ya mahindi mwaka jana hivyo kupelekea kuporomoka kwa bei, mwaka huu unaweza kuwa ni wa neema kwa wafanya biashara ya mahindi.
Kama una milioni kumi haina kazi, nunua mahindi sasa uyahifadhi. Unaweza ukaja kuyauza hata kwa milioni 20 mbele ya safari.
Huku kwenye Kangomba ya mahindi ni clean business. Mkono wa dola haufiki huku. Kazi kwenu wasaka fursa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mishe za pesa mingi kwa muda mfupi zipo ni wewe kuamua tu..
Mtaji wa laki 3-5 leo hii unaweza kuukuza hadi million 2-3 au zaidi ndani ya miezi miwili...

Hapa ndio mawazo ya biashara yaliko lala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe unaishi Tanzania mkuu?

Hukuona sukari ilivyotaifishwa kile kipindi !

Hii awamu sio ya kuwekeza pesa, ukiwekeza jiandae kwa lolote.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukiwa na muda, naomba unieleweshe hicho kisa kutaifisha sukari.

Binafsi huwa naona biashara nzuri ni kununua mazao kwa bei ya chini, kipindi cha mavuno na kuyahifadhi ili kusubiri bei ipande ndipo uuze.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wazi zur sana. Biashara ya mahind inalipa sana sema wakat mwingn soko lake linaeza simama ghafla, ila hua ni kwa kipind kifupi sana, huku moshi tunauzwa kwa kilo 1 sh 440-460 kutegemeana na upepo wa mahind. Gunia moja lina kilo 105-110 na kuendelea kutegemeana na maeneo mana mbegu zinatumika tofauti. Tunapoenda yatapanda tena kwa kas mda c mrefu, ukiweza hifadh saiv, lazima ilipe baday
 
Ni kweli kabisa hali ya Mvua haswa Ukanda wa Pwani, Kati, Kaskazini na Ziwa ni mbaya na baadhi ya maeneo mazao yameshakauka.
Huu unaweza kuwa ni mwaka wa njaa.
Baada ya kuwepo kwa over supply ya mahindi mwaka jana hivyo kupelekea kuporomoka kwa bei, mwaka huu unaweza kuwa ni wa neema kwa wafanya biashara ya mahindi.
Kama una milioni kumi haina kazi, nunua mahindi sasa uyahifadhi. Unaweza ukaja kuyauza hata kwa milioni 20 mbele ya safari.
Huku kwenye Kangomba ya mahindi ni clean business. Mkono wa dola haufiki huku. Kazi kwenu wasaka fursa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inawezekana maana masika yanakuja ila ulioposema njaa linawezekana kuja wewe unaujamaa na mungu
 
Hamjajifunza tu kwenye korosho. We Nunua utakapoambiwa uonyeshe shamba utaleta mrejesho...

Sent using Jamii Forums mobile app
Serikali haiwezi taifisha mahindi ya mtu, ila wasiwasi ni kwamba kwa sasa serikali ina hifadhiu kubwa sana ya chakula hasa mahindi, kwa vyovyote vile mahindi yakipanda bei ,serikali inaweza fungulia magala yake na kushusha bei ya mahindi ko mfanyabiashara faida inakuwa kidogo. maana watu watanunua mahindi ya serikali amabapo pia baadhi ya maeneo yaweza kugawiwa bure.
ushauri wekaza kidogo kwa mahindi, mpunga, maharage na karanga ndo mpango mzima havidanganyi.
 
Back
Top Bottom