Biashara ya Kuonesha Mpira wa Miguu (Kibanda-umiza): Fahamu Kiasi cha Mtaji, Vifaa na Mbinu za Uendeshaji

Biashara ya Kuonesha Mpira wa Miguu (Kibanda-umiza): Fahamu Kiasi cha Mtaji, Vifaa na Mbinu za Uendeshaji

Usisahau feni kama kuna joto, Pia kama utaweka viti vizuri ikawa kama V.I.P Nakulotelea mfano;

Kuna Banda niliwahi kuliona sehemu jamaa ameweka benchi nzuri kama za kanisani kwa kiingilio cha 500 then akaweka mbele kabisa makochi 4 yale ya watu 3 ikawa kama V.I.P kwa kiingilio cha 1500 + free soda.

Kuwa na lugha nzuri kwa wateja usisahu Spika kubwa au subwoofer kubwa.

Vinywaji usisahau.
Asante mkuu kwa mawazo yako hakika yamenipa mwanga zaidi wa kuongeza mapato, hasa kuanza kuuza vinywaji na mahala pa VIP.

Thanks[emoji120]
 
Mkuu sijaona jambo muhimu kuliko yote. Unachaji kiasi gani, unategemea kupata watu kiasi gani na watu wana uwezo wa kutoa kiasi gani as well as competition karibu yako kuna wangapi wanafanya unayofanya wanachaji ngapi na huduma yao ipo vipi.

Unless otherwise faida ya kwenye makaratasi itabaki kwenye makaratasi while practically iwe kilio.
 
Mkuu sijaona jambo muhimu kuliko yote..., Unachaji kiasi gani.., unategemea kupata watu kiasi gani na watu wana uwezo wa kutoa kiasi gani as well as competition karibu yako kuna wangapi wanafanya unayofanya wanachaji ngapi na huduma yao ipo vipi...

Unless otherwise faida ya kwenye makaratasi itabaki kwenye makaratasi while practically iwe kilio
Fata ushauri huu.nipo kwenye game msimu wa tatu huu ila hakuna faida kubwa labda icheze simba Vs yanga kila weekend
huko vijijini EPL hakuna wadau wengi wanachagua game zao ..hicho kingilio cha 500 utakuwa unacheza tu
 
Nyongeza, angalia wenzio wana vitu gani then wewe boresha uwe zaidi yao.

Jitahidi mafuta yawemo muda wote kwenye jenereta kama itatokea umeme kukatika unawasha haraka .

kabla ya mechi hakika jenereta linakuwa nje tayari ili umeme ukikatika unawasha chap kwa haraka.

usiweke viti vya plastic utakula hasara kubwa sana.

Mkuu usisahu kitambulisho cha mjasilimali kama uwekezaji wako hauzidi 4M.

NB: kwa Tv moja huwezi kufanikiwa, chukulia kwa mfano
15:00 Nyumbu vs Arsenal
15:00 Chelsea vs Spurs
utaweka ipi na utaacha ipi?
 
Nyongeza, angalia wenzio wana vitu gani then wewe boresha uwe zaidi yao.

Jitahidi mafuta yawemo muda wote kwenye jenereta kama itatokea umeme kukatika unawasha haraka .

kabla ya mechi hakika jenereta linakuwa nje tayari ili umeme ukikatika unawasha chap kwa haraka.

usiweke viti vya plastic utakula hasara kubwa sana.

Mkuu usisahu kitambulisho cha mjasilimali kama uwekezaji wako hauzidi 4M.

NB: kwa Tv moja huwezi kufanikiwa, chukulia kwa mfano
15:00 Nyumbu vs Arsenal
15:00 Chelsea vs Spurs
utaweka ipi na utaacha ipi?
Kitambulisho muhimu nalifahamu hilo, thanks kwa kunikumbusha pia.

Kuhusu TV ndugu ntaanza na moja mbeleni ntaongeza nyingine kadiri ya mapato yatakavyo kuwa.

Asante Tena.
 
Moja kati ya michezo pendwa sana kwa vijana na hata wazee na watoto kwa ujumla ni mchezo wa miguu, mpira (Football). Ligi nyingi sana zimeanza na zinatarajiwa kuanza ndani ya mwezi huu, huku tayari ligi pendwa ya EPL imeanza kutimua vumbi huku ligi ya Tanzania soon kuanza nayo.

Napenda kuanza biashara hii ya kuonyesha mpira hasa kwa ving'amuzi vya DSTV na AZAM ikiwa kuonyesha mechi za nje ya nchi na ndani hasa timu pendwa za watani wa jadi (Simba na Yanga).

Huu ndo uchambuzi wangu ambao nategemea kufanya makadirio kabla ya kuanza ujenzi na biashara kwa ujumla:

*Ujenzi wa Banda kwa kutumia Mabati pamoja na umeme hasa kutokana na sehemu niliyopo ni ya kijijini (sio sana) itanigharimu Tshs 900,000

*TV ya Kisasa (LED Inch 43) itanigharimu Tshs 900,000

*Manunuzi ya Ving'amuzi vyote viwili (AZAM - Tshs 135,000 & DSTV - Tshs 109,000)
Jumla = Tshs 244,000

*Vifurushi Vya Kujiunga Ndani husika (AZAM PLUS - Tshs 23,000 & DSTV Compact - Tshs 69,000)
Jumla = Tshs 92,000

*Kabati kwa ajili ya kuwekea/kuhifadhi TV itanigharimu Tshs 85,000

*Matumizi mengine ya dharura (Emergency) ndani ya ujenzi ni Tshs 200,000

Jumla Ya Mahitaji Na Gharama Kwa Ujumla Itanigharimu Kiasi Cha Tshs 2,421,000

Nakaribisha maoni na mapendekezo yenu yaweze kunisaidia mimi pamoja na wanajukwaa wengine wenye malengo kama yangu ya kuanzisha biashara hii.

Asanteni[emoji120]
DSTV ni 99,000 mkuu. Mimi staff ingawa nipo ZANZIBAR. Kisha wewe upo wapi?
 
Back
Top Bottom