Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Nilikuwa pale Kihangaiko Msata wiki jana, kijiji kimegawa miti bure kwa waliojiandikisha na mingine inauzwa pale ofisini Kihangaiko Tsh 500. Sijui ni acrocarpus au Msederela, inaonyesha ina-growth rate nzuri. Nimeona shule ya Madesa iliyopo kijiji cha Kihangaiko wameotesha tayari. Nataka niangalie ukuaji wake ili na mimi nioteshe. Na mimi nina kieneo pale Msata, usikute ni majirani mkuu!!!!

Asante kwa taarifa mkuu. tutatafutana.
 
Hizo njia zote ni effecticve lakini nzuri kuliko zote ni lile ya kubabua mbegu za teak kwa kutumia nyasi(fanya kama wale wanaobabua samaki kwa moto) yaani tandaza mbegu chini halafu tandaza layer ndogo ya nyasi na uziwashe moto ili zile mbegu ziungue kidogo. kisha zipande

Nashukuru, ngoja nijaribu njia hii na nyinginezo halafu nitarudisha majibu njia gani ziliota kwa haraka.
 
Hiyo biashara Mufindi, Njombe na Makete inalipa sana. Kule Njombe vijijini kwa sasa mti mmoja wa kupasua mbao ukiuza jumla unakwenda kwa bei kati 10,000 mpaka 15,000 kutemegea na size yake na wateja wapo sio wakutafuta wanakufuata wenyewe, sasa ukiwa na miti 100,000 tayari milionea. mwenye nimenunua mashamba huko kwaajili ya kupanda Pines .
Mashamba wanauzaje huko? I would wish to venture in this deal this year. Kwa kuwa unasema umennua, nadhan itakuwa vyema kama ukanipa info za bei ya shamba ili niwe jirani yako huko.
 
Jamani maeneo ya chalinze -- lugoba ni miti gani inastawi vizuri..........
Kiongozi katika uwekezeji wa muda mrefu kama huu unahitaji kuwa na taarifa zinazojitosheleza na za kitaalam. Nakushauri wasiliana na ofisi za wakala wa mbegu za miti tanzania TTSA Tel: +255 232 603 192/3903 utajifunza mengi sana hususan mti gani upandwe mkoa gani. Pia wanauza mbegu za aina mbalimbali pale kitu amacho kinaweza kikakupunguzia cost sana kwenye uwekezaji wao. Hawa jamaa wanambegu bora, I would advice you ufike ofcn kwao kama una nia ya kuwekeza kwenye miti.
 
Aisee hizi taarifa ni za muhimu sana,tuna eneo moshi karibu heka kumi sijajua naweza kupata wapi taarifa za miti itakayochukua muda wa wastani chini ya miaka kumi ili nipande,miti baadhi iliyopo ni cyprus ila naona kama inachukua miaka mingi mno,kama naweza kunisaidia ushauri
Kiongozi angalia haraka yako ya kuvuna usije ukajikuta unapanda mabua badala ya miti. Kinachotudrive kupanda mti wa aina fulani ni soko, usije ukajipandia miti inayokua haraka ukasahau kuassess marketability ya hiyo species.

What i would advice you ni kwamba wewe panda miti ambayo soko lake linafahamika kama hiyo Pinus spp, Eucalyptus spp au Teaks. Suala la muda wa kuvuna lisikupe pressure mana nadhan wewe shida yako ni pesa na sio utavuna lini. Ukiona wahitaji pesa haraka, nenda bank kakope harafu hilo shamba la miti litumie kama collateral then utapata hiyo hela utafanyia mambo yako wakati miti yako inaendelea kumea shambani. Yapo mabenk mengi ambayo wanakubali mashamba ya miti kutumika kama Collateral kwenye mikopo yao.
 
Kuna sources nyingi sana kwenye internet ila nafikiri tunaongelea vitu viwili tofauti. Mimi naongelea bei ya mti shambani siongelei bei ya mbao ulaya iliyokuwa processed tayari. Data zipo wizara ya maliasili na utalii na ni juu sana ila ni kwa miti iliyopandwa miaka hamsini iliyopita na serikali. Zinaonyesha bei za juu ila ni za kwenye makaratasi tu (za kisiasa for strategic planning). Nafikiri cha muhimu ni kuanzia na baseline data. Kama una mitiki kwenye uwanja wako Dar, halafu serikali ikakufidia kupanua barabara au kuendeleza hilo eneo, utalipwa kiasi gani? Hiyo ndio bei nzuri ya kutumia kwenye kufanya analysis kwa sababu hata wataalamu wengi ukiwauliza bei wanakwambia hakuna soko la ndani ni la nje tu. Kama utapata mtu ameuza mitiki hapa Tanzania shambani naomba utujulishe miti ilikuwa na umri gani na iliuzwa kiasi gani kwa ujazo au kwa mti.

Tumeanza na trial ya miti 600 kwenye ekari moja tuone kama itakwenda vizuri mwaka ujao tutaingia kwa gia kubwa. Mbegu tunanunua SUA, shs 1,000 kwa mche. Ila mvua zinatusumbua.

Nawasilisha.
Hiyo bei mbona kubwa sana? TTSA Morogoro wanauza kilo moja kwa 7500 ambayo unaweza pata miche mingi sana! Ni mkoa gani huko mvua inaposumbua? Kigoma, ruvuma nadhan ardhi ni kubwa na mvua ni nyingi sana. Nimeona miteak iliyoota maekeo hayo ina afya nzuri sana suggesting that ukipanda huko itakuwa haraka zaid ya ile inayopandwa maeneo yenye uhaba wa mvua.
 
Kiongozi katika uwekezeji wa muda mrefu kama huu unahitaji kuwa na taarifa zinazojitosheleza na za kitaalam. Nakushauri wasiliana na ofisi za wakala wa mbegu za miti tanzania TTSA Tel: +255 232 603 192/3903 utajifunza mengi sana hususan mti gani upandwe mkoa gani. Pia wanauza mbegu za aina mbalimbali pale kitu amacho kinaweza kikakupunguzia cost sana kwenye uwekezaji wao. Hawa jamaa wanambegu bora, I would advice you ufike ofcn kwao kama una nia ya kuwekeza kwenye miti.

Asante kwa ushauri wako
 
Kwa sisi ambao tuko Dar unadhani tunaweza kupanda aina gani za miti ambao ni za muda mfupi?
 
Mimi naishi Mvomero, tayari nimeanza kupanda Mitiki na Nina zaidi ya ekari kumi hadi sasa. Kwa MVOMERO sio wengi waliohamasika kupanda Miti ingawa Miti Ni Bima ya uhakika. Nachukua nafasi hii kumwomba mkuu wa Wilaya yetu Mr. A. Mttaka kuhamasisha, kuhimiza Na kusimamia upandaji wa Miti kama mojawapo ya zao muhimu ili kuokoa mazingira, lakini pia kujijenga kiuchumi.
 
Huku pwani Bagamoyo haioti?

Kuanzia B/moyo mjini kuelekea Msata, ni ukanda ambao mitiki inamea vizuri, na mlingoti nimeuona leo umepandwa kidogo upande wa kulia kama unakwenda Fukayosi, nyuma kidogo.
 
Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.

Huko maeneo wanauzaje ili tuje kuwekeza?
 
Karibu sana,Hakuna kiingilio kabisa,cha umuhimu ni uaminifu wako tu, nipe mail yako kupitia pm ili tuanze mawasiliano ya moja kwa moja.
Hallo Mkuu, hata me nimevutiwa na kilimo hiki na nimeshaanza kujiandaa na ninaomba msaada wenu na hasa kuingia katika organisation yenu ili nijfunze mengi zaidi.
 
Hallo Mkuu, hata me nimevutiwa na kilimo hiki na nimeshaanza kujiandaa na ninaomba msaada wenu na hasa kuingia katika organisation yenu ili nijfunze mengi zaidi..
Tuma mail address ili nikuunganishe tuanze kazi.
 
Mkuu wewe una shamba Dar? mi nilifikiri Dar hata kiwanja tu kupata ni issue
Dar kubwa ndugu yangu. Unadhani dar inaishiaa posta tu? Kuna maeneo kama kimbiji kote huko ni Dar na unaweza kumiliki shamba kwa bei pouwa tu!
 
Back
Top Bottom