Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Hakuna ujasiriamali wa kuwekeza ktk kilimo nanao vutiwa nao na ninaota kuufanya kama wa kilimo cha chai. Nilihamasika sana siku nilipotembelea central and eastern part of Kenya.
 
Hello;
Kwa yeyote anayependa kununua mbao za mninga size 1x10x10 au 2x10x10 unaweza wasiliana nami. Ninauza kwa bei ya jumla na rejareja pia..Na kama unahitaji size nyingine pia waweza niambia na zitaandaliwa kwa ajili yako.
 
Mkuu weka mawasiliano yako na wapi unapatikana na bei ya hizo mbao kwa reja reja na jumla pia.

Kuwa na tangazo linalojieleza na mvuto wa kibiashara zaidi mkuu.
 
Weka bei na pia mawasilino, maana hata keko wanauza mbao za mninga jumla na rejareja. Tushawishi zaidi tuje kununua kwako
 
Hizi mbao ziko Tanzania, ukiwa unazihitaji unasema uko wapi na bei inategemeana na eneo uliloko maana pia inategemea na gharama za usaifiri kuzileta huko uliko. Ni mbao za mninga kutoka kusini mwa Tanzania, kwa sasa size ambayo ipo ni 2x10x10, kama uko Dar es salaam bei ya rejareja ni tsh.46,000/=,ni grade A na ni mbao nzuri sana ukiziona utapenda na kwa dar utakubaliana nami kuwa huwezi pata size ya 2x10x10 kwa elfu 46 hii ni bei poa sana kwa mninga. Mzigo umeisha ila ziko zingine porini nategemea kuzileta DSM mwishoni mwa mwezi huu wa kumi. Bei ya jumla tunaweza ongea.
 
Nashukuru mkuu kwa ushauri mzuri. Je, ni mikoa gani ninaweza kupata ardhi ya kununua kwa ajili ya kupanda miti ya mbao tukiachana na mikoa ya njombe na Iringa?
 
Mkuu Malila, nimeku-PM kukuomba msaada wa mawazo kuhusu miti. Ikikupendeza na nafasi ikakuruhusu, naomba jibu lako

Mitiki inamea vizuri sehemu zenye joto na unyevunyevu wa kutosha kama Kilombero, Longuza,Kyela, Muhoro nk. Sehemu zingine inaota lakini haifikii viwango.
 
Nashukuru mkuu kwa ushauri mzuri. Je ni mikoa gani ninaweza kupata ardhi ya kununua kwa ajili ya kupanda miti ya mbao tukiachana na mikoa ya njombe na Iringa?

Mikoa yote unaweza kuotesha miti ya mbao kwa sababu kila mkoa kuna aina ya mti unaomea vizuri, sasa kuna miti ya muda mfupi (10yrs to 15yrs), kuna miti ya muda mrefu ( 15yrs to 25) na kuna miti ambayo ukiotesha wewe, hata mtoto wako hatavuna.

Tatizo linaanzia hapo kwenye muda, mikoa yote ambayo inaangukia kundi la pili,wengi wanadhani haiwezi kuotesha miti ya mbao, kwa hiyo tunadhani ile mikoa ya kundi la kwanza ndio pekee.

Mtiki ni 25yrs, upo tayari kusubiri?
Cyprus ni 15/25yrs je utasubiri?
Pinus patula 10/15yrs
Eucalyptus 6yrs to infinite - kuanzia poles,nguzo mpaka mbao
Accrocarpus 9yrs to 12yrs.

Pinus patula inamea vizuri nyanda za juu kusini, sasa hivi hadi Bukoba/Pemba iko na inavunwa mapema. Lakini ukiniambia nipande Mvule unaomea vizuri Tabora, halafu nivune baada ya miaka 70, hesabu inakataa.
 
Somo zuri sana na mie mwakani nianze. Ngoja nianze usafi taratibu
 
Mikoa yote unaweza kuotesha miti ya mbao kwa sababu kila mkoa kuna aina ya mti unaomea vizuri, sasa kuna miti ya muda mfupi ( 10yrs to 15yrs), kuna miti ya muda mrefu ( 15yrs to 25) na kuna miti ambayo ukiotesha wewe, hata mtoto wako hatavuna.

Tatizo linaanzia hapo kwenye muda, mikoa yote ambayo inaangukia kundi la pili,wengi wanadhani haiwezi kuotesha miti ya mbao, kwa hiyo tunadhani ile mikoa ya kundi la kwanza ndio pekee.

Mtiki ni 25yrs, upo tayari kusubiri?
Cyprus ni 15/25yrs je utasubiri?
Pinus patula 10/15yrs
Eucalyptus 6yrs to infinite - kuanzia poles,nguzo mpaka mbao
Accrocarpus 9yrs to 12yrs.

Pinus patula inamea vizuri nyanda za juu kusini, sasa hivi hadi Bukoba/Pemba iko na inavunwa mapema. Lakini ukiniambia nipande Mvule unaomea vizuri Tabora, halafu nivune baada ya miaka 70 !!!!!!! hesabu inakataa.
Mkuu KVM na Malila! Nawashukuru sana kwa moyo wenu wakupenda ku-share information ambazo zinaweza zikafuta ufukara kwa watu tuliowengi. Ni watu wachache wenye mioyo ya kutaka kujuza wengine kwenye mambo yamaana kama haya.

Nimefuatilia thread yote toka ilipoanza Aprili 2012 (mwaka juzi sasa) mpakapost ya mwisho na niko very moved and geared!

Naomba mnishike mkono na mniongoze ili name nijifunze na nifuate njiayenu japo kwa mbali! Naomba mnijuze kuhusu malengo ya association yenu na jinsiya kujiunga.

Mungu awabariki sana.
 
Wauza unga wanatushangaa tunaonea nini eti miaka 15 unsuburi miti ahahahaah ila nimependa uliposema ni kiinua mgongo kizuri kweli kaisa kama una miaka 40 now ukifika mika 55 unastafu kwa hiari ukiwa milione.
 
Asante kwa kunisaidia yaani umenifungua macho nami itabidi nianze biashara ya miti naona ni nzuri sana.
Mimi nigependa kuwahamasisha wanjf kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.

Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.

Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa shs 50 na kuupanda kwa shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.

Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.

Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.
 
Mlio anza zoezi la kupanda miti tunaomba uzoefu ili na sisi tujitose.
 
Mlio anza zoezi la kupanda miti tunaomba uzoefu ili na sisi tujitose

Naweza kukupa abc kadhaa za miti ambayo tayari nimeshaotesha, kumbuka maisha ni kujifunza, hata mimi najifunza habari za miti kila siku. Mfano, nilibobea ktk pinus patula zaidi, kumbe kuna akina acrocarpus, sedrela na Eucalyptus from Zimbabwe generation ya tatu, sisi tulikuwa na generation ya pili, cyprus, teaks, wattle etc

Kuna changamoto za manpower, moto,mbegu bora. Cha msingi, ukiamua kuingia ktk biashara hii, kamata nguli mmoja ili hizi changamoto zisikusumbue kwa sababu yy atakuwa na majibu tayari.
 
Mkuu KVM na Malila! Nawashukuru sana kwa moyo wenu wakupenda ku-share information ambazo zinaweza zikafuta ufukara kwa watu tuliowengi. Ni watu wachache wenye mioyo ya kutaka kujuza wengine kwenye mambo yamaana kama haya.

Nimefuatilia thread yote toka ilipoanza Aprili 2012 (mwaka juzi sasa) mpakapost ya mwisho na niko very moved and geared!
Naomba mnishike mkono na mniongoze ili name nijifunze na nifuate njiayenu japo kwa mbali! Naomba mnijuze kuhusu malengo ya association yenu na jinsiya kujiunga.

Mungu awabariki sana.

Kigolla,

Mbona mwaliko wako bado uko hewani,au uko shamba bado?
 
Hiyo biashara Mufindi, Njombe na Makete inalipa sana. Kule Njombe vijijini kwa sasa mti mmoja wa kupasua mbao ukiuza jumla unakwenda kwa bei kati 10,000 mpaka 15,000 kutemegea na size yake na wateja wapo sio wakutafuta wanakufuata wenyewe, sasa ukiwa na miti 100,000 tayari milionea. mwenye nimenunua mashamba huko kwaajili ya kupanda Pines .

Mkuu sumbawanga miti hiyo yaweza stawi?
 
Karibu sana,
Hakuna kiingilio kabisa,cha umuhimu ni uaminifu wako tu, nipe mail yako kupitia pm ili tuanze mawasiliano ya moja kwa moja.

Mkuu naomba na mie nijiunge na umoja huu ambao ni tunu kubwa ya maisha ya baadae. Naku PM contact yangu sasa hivi.
 
Back
Top Bottom