Biashara ya nafaka ina umafia mwingi. Kwa wanaotarajia kuanza kuuza nafaka chukueni tahadhari

Biashara ya nafaka ina umafia mwingi. Kwa wanaotarajia kuanza kuuza nafaka chukueni tahadhari

Niliwahi kufanya biashara ya mafuta ya alizeti..

Wahuni wakanichanganyishia na maji kwenye madumu ya njano.

Nafikisha sokoni juu mafuta chini maji.. dadeki nilijifunza kitu! Umakini na kufanya kazi kwa watu makini
Aisee , hizi roho za kishetani wabongo sijui huwa tunazitolea wapi
Mbongo ni mwizi na mharibifu sana ,sasa imagine Kenge aliyefanya hivyo na short aliyokupigisha , yaani jitu halioni aibu wala huruma
 
Biashara ya mahindi ni nzuri sana kama ukiuzia nje ya nchi,mfano kenya au sudan kusini, ikiwa uko mikoa ya arusha au manyara ni bora zaidi, ila sasa! Ni hadi uunge chain na wafanyabiashara wazoefu,wakubali kukupa ushirikiano na kukupa hints kadha wa kadha,otherwise hawa ndiyo ma mafia wenyewe,nipo kwenye circle ya biashara hiyo,ila kwa angle tofauti,kuna jamaa alijiingiza kibabe kwenye game bila kusajiliwa kwenye chama cha wafanyabiashara ya nafaka huko arusha, kilichomkuta alijuta, mzigo wa tani 30 ulizuiliwa mpakani namanga,akaambiwa yana aflatoxin,marufuku kuingia kenya, alipambana kuhonga na nini lakini hakufanikiwa kuuingiza,, ipo hivi=mfanyabiashara wa mazao anayeuzia kenya anapaswa kuwa na namba za askari wa barrier zote kutokea arusha mpaka sokoni kenya,na pale border vilevile, kwa hiyo mzigo ukifika kabla haujafika barrier askari wanajua mzigo wa fulani unakuja,border vilevile,na wanakuwa kwenye payrol yako,unakuwa unawatoa kwa chochote kitu, sasa kama hujulikani wale wazoefu wakijua unapeleka mzigo, simu zinapigwa kote, zuieni huo mzigo! Baba hupiti!! Ukivuka barriers zote safari yako inaishia namanga, utatoboka hela hadi mzigo unakupiga hasara takatifu, pale border mwishoni watakuja wafanyabiashara wazoefu, wakukatishe tamaa kabisa, kisha wakuambie uwauzie wao kwa bei ya hasara, ukikubali(probably utakubali tu) wao wanayanunua, na kuyavusha kiulaini kabisa,unarudi home na hasara yako.
Aisee umeandika kitu kizito ,mwaka juzi nilikuwa nataka kuanza hii biashara
Vipi ,bado unapeleka nafaka kenya ?
 
Biashara ya mahindi ni nzuri sana kama ukiuzia nje ya nchi,mfano kenya au sudan kusini, ikiwa uko mikoa ya arusha au manyara ni bora zaidi, ila sasa! Ni hadi uunge chain na wafanyabiashara wazoefu,wakubali kukupa ushirikiano na kukupa hints kadha wa kadha,otherwise hawa ndiyo ma mafia wenyewe,nipo kwenye circle ya biashara hiyo,ila kwa angle tofauti,kuna jamaa alijiingiza kibabe kwenye game bila kusajiliwa kwenye chama cha wafanyabiashara ya nafaka huko arusha, kilichomkuta alijuta, mzigo wa tani 30 ulizuiliwa mpakani namanga,akaambiwa yana aflatoxin,marufuku kuingia kenya, alipambana kuhonga na nini lakini hakufanikiwa kuuingiza,, ipo hivi=mfanyabiashara wa mazao anayeuzia kenya anapaswa kuwa na namba za askari wa barrier zote kutokea arusha mpaka sokoni kenya,na pale border vilevile, kwa hiyo mzigo ukifika kabla haujafika barrier askari wanajua mzigo wa fulani unakuja,border vilevile,na wanakuwa kwenye payrol yako,unakuwa unawatoa kwa chochote kitu, sasa kama hujulikani wale wazoefu wakijua unapeleka mzigo, simu zinapigwa kote, zuieni huo mzigo! Baba hupiti!! Ukivuka barriers zote safari yako inaishia namanga, utatoboka hela hadi mzigo unakupiga hasara takatifu, pale border mwishoni watakuja wafanyabiashara wazoefu, wakukatishe tamaa kabisa, kisha wakuambie uwauzie wao kwa bei ya hasara, ukikubali(probably utakubali tu) wao wanayanunua, na kuyavusha kiulaini kabisa,unarudi home na hasara yako.
Soko la mahindi kenya ni kubwa sana hasa Mombasa na Nairobi ,
Vipi kwa sasa Mzigo wa mahindi bado unaenda mombasa ?
 
Huo sio umafia ni upuuzi.

Siku nilipojua kwamba mawe yanawekwa ktk mchele ili kuzidisha kilo,na mchele unapakwa mafuta ili ung'ae kuonekana ni mpya,nilijiskia aibu sana kuwa mbongo.

Kuna vitu vya kijinga vinatugharimu sana hasa mbele huko katika masoko ya watu makini, nimekumbuka story ya wanunuzi wa pamba kukuta mawe ktk marobota🤮🤮🤮
Hapa ndipo waKenya wanapotupiga bao
 
Mimi ni muelimishaji ujasiriamali naandika pia kitabu cha ujasiriamali ambacho nadhani ni fikirishi kinajaribu kutafakari kwanini biashara zinakufa na suluhu inayowezekana kwakifupi kinamuelimisha msomaji kujenga biashara ya kudumu kuna mambo mengi hayako sawa kwenye jamii ya waafrika kuhusu ujasiriamali na biashara hasa jinsi ya kukabiliana na tusiyoyatarajia ktk maishani na biashara
Hongera sana ndugu muelimishaji, uwepo wako ni muhimu sana.

Vipi kwa sasa hivi unafanya biashara gani Mkuu?
 
Hongera sana ndugu muelimishaji, uwepo wako ni muhimu sana.

Vipi kwa sasa hivi unafanya biashara gani Mkuu?
Nauza akili, (selling services), ni fundi wa vifaa vya kielecktroniki ,(general electronics repair), simu software and hardware, radio and tv repair, labda niseme chochote kinachopita mbele yangu km akili yangu ikiamua kuamsha ubongo wangu nitaweza
 
Nimeona mdau mmoja humu anahamasisha watu wazame bush wakanunue kwa bei ndogo walete mazao mjini wauze kwa bei kubwa ili wapige pesa.

Hili wazo ni zuri sana lakini ni vyema tupeane tahadhari. Katika biashara zenye umafia mwingi basi hii ya nafaka kwangu ndio namba moja kwa umafia yaliwahi kunikuta.

Nitatoa umafia niliokutana nao ila pia wadau wengine watakuja kuleta ushuhuda.

Miaka flani Niliwahi kuzama bush na milioni moja nikakusanya magunia ya mpunga 20 ya debe 6 yale nkaenda kukoboa kisha nkaweka kwenye fremu yangu lengo niwe nauza kwa bei ya jumla, ule mchele ulitoka vizuri mno changamoto ikawa wali wake ukipikwa hauna ladha, wateja wote wakanikimbia nikaanza kuuza reja reja kwa bei ndogo lakini bado wakanikimbia walikuja mwanzo mwanzo kisha wakaishia mitini.

Baada ya kufanya uchunguzi nikagundua niliuziwa mpunga uliokaa miaka mingi stoo (kumbuka niliununulia bush) pia ile mbegu ya huo mpunga hutoa kilo nyingi lakini wali wake hua hauma radha. Niliuza kwa bei ya hasara mzigo wote kwa wauza vitumbua.

Nkajipanga tena awamu hii nkaamua niende mashineni nikanunur mzigo kwa bei chee kisha niuze kwa bei ya hapo mtaani. Nilinunua kilo 500 kufikisha mzigo kwenye fremu wateja wakafurika nkauza sana hiyo siku. Nashangaa jioni watu wanarudisha mchele wanadai unamawe meupe. Kuuangalia vizuri ni yale mawe meupe wahuni walinipiga walaaniwe sana washenzi wale. Wateja wote wakanikimbia.

Nkajipanga tena nafika mashineni kuchukua mzigo nakutana na madalali wengi sana nkaona hii biashara pasua kichwa nkaachana nayo

Kwa mlio wahi kukumbana na umafia kwenye nafaka njooni hapa mtoe ushuhuda.
😂😂😂
 
Maisha ni Biashara Usipofanya biashara utafanywa ww Biashara uamuzi ni wsko uwe upande gani wa mfanya Biashara au mfanywa Biashara na kila upande una changamoto zake kubwa tena na hakuna upande ulio Salama kote ni Shida.

Nilichokigundua ww jamaa ni mkata tamaa mapema sana changamoto kidogo tu tayar ushazira na umekuwa mshauri nasaha hivi unafikiri biashara ni rahisi et. Mfanyabiashara inatakiwa uwe na roho ya kikomandoo usiwe lele mama life ni gumu sana chaliii yangu.

Ww ulitaka uchukue mpunga uwe mzuri upige hela au uchukue mchele uwe safi upige hela life lisingekuwa gumu jombaa pambana na roho ngumu, uwe mnyama.

Mimi nafanya izo biashara za nafaka nachukua mchele na Asali Tabora tena nachukulia mjini wala sijawahi kuenda shambani napeleka Dar na Zenj na mambo yanakwenda kiubishi ubishi na wala mm sio mzoefu kivile kwa industry.

Kuwa mjanja, jichanganye, jua namna ya kutengeneza chawa ili akupe habari , madalali hawaepukiki, be creative na uwe na initiative sio kulia lia hakikisha unapata codes sahihi na uwe too much inquisitive.

All in all biashara ya mchele ni nzuri na inalipa hasaa ujinga wako ndio hasara yako.

Na ukiendelea na Tabia ya kukata tamaa Mbinguni utapasikia tu
 
Niliwahi kufanya biashara ya mafuta ya alizeti..

Wahuni wakanichanganyishia na maji kwenye madumu ya njano.

Nafikisha sokoni juu mafuta chini maji.. dadeki nilijifunza kitu! Umakini na kufanya kazi kwa watu makini
Nahisi Kwenye Tano Bora ya utapeli TANZANIA tupo
 
Watu humu wqnajifanya wajuaji wakati hawajawahi hata kuuza pipi.

Mtu anakuambia ukomae na hiyo hiyo wwkati umechoma milioni mbili kwa awamu mbili tofauti.

Kama unataka kuwajua vizuri wauza mchele walivyo wezi wewe nenda mashineni umeshikilia kiroba watakupigania kama wapiga debe, na hao ni madalali, picha kamili ni kwenye mchele wenyewe. Hiyo biashara ingekuwa nyepesi madalali wasingejazana mashineni kwa wingi kuliko idadi ya wateja
Mkuu kubali hukuwa mwenyeji. Kuna jamaa nilikutana nae anahitaji kununua mchele mashineni kipindi hicho nilikuwa nakoboa gunia 4 zangu kisha niuze na akaniomba nimuuzie ....nilimwambia bado sijajua kama utatoka vziei unaweza kuvunjika japo hii ni mbegu nzuri.

Hivyo akasubiri hadi nikakoboa kupima kisha akanilipa ikabidi aulize kama niano mwinginge kule home na ninauza nikamwambia upo ila siuzi.Tukaenda mahali kupiga story yeye alikuwa mganda nilimshauri kitu kuwa kama anahitaji mchele quality kabisa aende kijijni anunue mpunga kwa wakulima kisha aanike then akoboe na kupaki hapo atapata faida nzuri na mchele utakuwa mzuri sana.

Jamaa akasema hana mwenyeji kwa sasa yule aliyemleta katika maeneo hayo alimtapeli kama nitakuwa na nia ya kumsaidia yupo tiyr kweli tuliingia kijijni yeye akapanga senta tuligawa hela kwa watu 5 tu maarufu na tukaongeza 5000 kwenye gunia la debe6 tofauti na wenzetu wao walikuwa chini ya hio bei hivyo ndani kama ya wiki tu magunia yapo ya kutosha kabisa na jamaa hakuamini.

Kwa kifupi jamaa alinipa mtaji wa m3 namimi nikaanza baishara hiyohiyo japo msimu ulikuwa umeisha nikawa na nunua kama wewe unalivyokuwa unanunua mashineni hapo ndo kunaumafia sasa wa kila aina sema mimi nilikuwa najua kila uhuni wao hadi wanacheka tu.

Ukiamua kufanya biashara hii fanya hivyo nenda kanunue mpunga kama sio mwenyeji tafuta mwenyeji utafaulu
 
Aisee , hizi roho za kishetani wabongo sijui huwa tunazitolea wapi
Mbongo ni mwizi na mharibifu sana ,sasa imagine Kenge aliyefanya hivyo na short aliyokupigisha , yaani jitu halioni aibu wala huruma
sio mbongo sema ngozi nyeusi
 
Aiseeee
Hata biashara ya wanyama ni mbaya. Niliwahi kununua Ng'ombe Mia kutoka Mbeya kwa ajili ya kuja kuuza Dar.

Kufika Iringa nikakuta Ng'ombe wote wamekonda.

Sijui wale wahuni waliwapiga sindano wale.

Kufikika Kibaha nilikokuwa napaki 21 wakafa.
ee
 
Ushawahi kufanya biashara ya Mbao wewe? Omba Mungu sana yasikukute😀😃😄😁

Vipi kuhusu Malimbichi? We dalali uliyenidhulumu Mahindi yangu ya Gobo niliyohangaika nayo miezi 4 huku Makete Mungu anakuona.
Biashara ya mbao inashida gani mkuu !?
 
Back
Top Bottom