Biashara ya Nafaka mtaji mkubwa faida kiduchu

Biashara ya Nafaka mtaji mkubwa faida kiduchu

Nakubaliana na wewe. Biashara ya mazao ina faida kuliko kilimo chenyewe. Inahitaji timing ya muda wa soko zuri. Kuna high season na low season kama zilivyo biashara zingine. Pia itategemea unajumua wapi na kuuzia nani

February 2024 kuna maeneo mkoa wa Songwe plastic ya maharage ilikuwa 25,000-27,000. Usafirishaji usiopungua 15,000 kwa gunia la plastic 10. Ukifika sokoni bei ya Magarage ilikuwa 37,000 kwa madalali na pesa unaipata siku inayofuata kwa gunia zisizozidi 3. So unaweza kuona mtaji mdogo tu wa 3M kwa wiki unaingiza kiasi gani kama utaenda porini angalau mara mbili na kwa mwezi itakuwaje.

Changamoto inakuwa biashara nzuri huwa si ya muda mrefu. Ni miezi miwili tu February-March. Na kipindi hiki ndio biashara za nafaka zinakuwa na pesa nyingi sana. Ukiingia kwenye biashara ya nafaka na kutegemea kuwa na biashara nzuri yenye faida nono kati ya June na October utakuwa disappointed.

Kila biashara inataka ujue seasons nzuri na mbaya ili ujue wakati gani utapiga pesa.
Ni sahihi kuna msimu wa faida kubwa na msimu wa faida kidogo ata hivyo inatakiwa ustick mwaka mzima kwenye bashara pia uwe mtafiti mzuri wa masoko na machimbo ya kununus mzigo usilenge eneo moja tu hapo utafulu kwenye hii biashara


😁😁 ila mkuu nilivoona neno KUJUMUA nikajua lazima utakua pande hizo mbeya/songwe 😂 maana hili neno limewakaa na unalikuta mikoa hiyo tu😃
 
Ni sahihi kuna msimu wa faida kubwa na msimu wa faida kidogo ata hivyo inatakiwa ustick mwaka mzima kwenye bashara pia uwe mtafiti mzuri wa masoko na machimbo ya kununus mzigo usilenge eneo moja tu hapo utafulu kwenye hii biashara


😁😁 ila mkuu nilivoona neno KUJUMUA nikajua lazima utakua pande hizo mbeya/songwe 😂 maana hili neno limewakaa na unalikuta mikoa hiyo tu😃
Ndi ghwa nkatefu kabisa 🤣
 
Biashara ya kuuza mahindi ni pasua kichwa.

Hii kazi kwa sasa ishakua ngumu, saivi watu wengi mitaji yao imekuwa mikubwa ila kwenye jambo la biashara hawana mbinu ya kufanya biashara mpya, wamebaki kuiga tu.

Unakuta mtu ana pesa ndani ila biashara ya kufanya hajui, anakaa anaangalia mafanikio ya mtu kwanza kisha kazi gani anafanya ili aige.

Basi yeye mzima mzima anaingia kwenye hyo kazi ambayo ameiga kutoka kwa mtu fulani, bila kujua mwenzie amefanya lipi na lipi mpaka akasimama kibiashara.

Biashara ya mahindi kwa sasa sio biashara, KWANINI?

Hii kazi kwa sasa ni ngumu, una kwenda shamba kununua, kule unakuta kuna dalali wa mahindi shambani.

Huyo dalali ana kwambia (niache pesa nikukusanyie mzigo)


Ili ukusanye mzigo haraka inabidi uitawanye pesa yako kwa madalali wengi na sehemu nyingi tofauti tofauti.

Kila dalali unaweza kukusanya roba 10-15 kwa wiki, inategemea pesa yako na hali ya hewa kama inaruhusu.


Sasa kuna mawili, dalali wa shamba akimbie na pesa au akupe mzigo wako.

Sasa tatizo lingine ni unakuta mabosi mpo wengi mnao mwachia pesa dalali, labda ww ni wa4 kat ya hao mabosi mpaka kufikia zamu yako.

Hivo hali hyo itafanya ushindwe kwenda na muda, utakuta unakaa cku nyingi bila kutoa mzgo shamba na kipengele kingine ni usafiri.

Pesa nyingi sana inaishia kwenye usafiri wa kutoka shamba hadi kufika barbrn, baada ya hapo ndo upakie mzigo kwenye gari ya 1kwa1 mpaka mjini.

Kipnd cha nyuma tulikuwa tunapata faida ya elfu 7 kwa roba moja lenye uzito wa wastani kilo 128, ila kwa sasa bei ya shamba na mjini utakuta inapishana elfu 10, sasa ukipiga hesabu ya kibiashara inakuwa hailipi!

Kutoka nlipo hadi ufike huko mashambani unatumia saa 1-2 (spidi 50-70) kwa pkpk na inategemea na kasi yako.

Kutoka nyumbani nilipo mpaka mjini (km 110) na ukisema ununulie hapa hapa nyumbani unachelewa kueneza mzigo kwa muda unaotakiwa na bei inakuwa kubwa tofauti na shamba, maana bei za mahindi huwa znapanda na kushuka.

Muda mwingine baadhi ya madalali wa mjini pia huwa ni vipengele. Unampa mzigo afu yeye hakupi pesa taslimu, au anatengeneza mazingira akupige pesa kwa njia ya uchafu au vumbi la mahindi.

Kabla ya kupima roba lazima dalali alikague kwa kulipiga bambo kisha anaangalia mahindi kama mapya, zamani, meupe, njano, machafu(vumbi) au fangasi.

Sasa dalali anapga bambo roba la kwanza la pili la tatu kisha anakwambia mahindi yako machafu, yana vumbi hivyo nakata kilo moja kila roba na wengine anakukata hadi kilo 2, kwa7b unakua huna jinsi inabidi ukubaliane naye kupima ivo ivo.

Sasa ukipiga hesabu unakuta dalali ashakupga zaidi ya shilingi 300-600 mara idadi ya roba zako.

Kwa haraka haraka unaweza kuona hyo pesa anayokukata dalali ni ndogo ila ukija kuzidisha mara mzigo wako wote, anakuwa amekuvuta shat pakubwa sana yaan anaweza akachukua roba 1 kwenye roba 60.

Hizo ni baadhi ya changamoto ambazo unaweza kukutana nazo kazini.
Mkuu vipi ukinunua mzigo ukausagavuuze unga, hapa faida yake vipi na kipi rahisi kupiga pesa
 
Mkuu vipi ukinunua mzigo ukausagavuuze unga, hapa faida yake vipi na kipi rahisi kupiga pesa
Inawezekana pia, lakini kuna ushindani mkubwa sana , lazima uwe na mtaji wa kufanyia Promotion ya soko, sababu viwanda vya unga ni vingi sana, ukiwa na Mashine 1 tu umemaliza kila kitu!!


Fursa kubwa hapo ni wewe kuwauzia hao wenye viwanda, wanaosagisha , wanahitaji sana Nafaka .
 
Acha 50 hata Tshs 5 ni kubwa kama kuna uhakika wa percent mia moja..., sasa issue ya ukipata sana faida ni 50/= na haichelewi siku nyingine kukata mtaji hio tena sio biashara bali kiwanda cha stress...
upo sahihi kikubwa kuongeza bidii
 
Mkuu vipi ukinunua mzigo ukausagavuuze unga, hapa faida yake vipi na kipi rahisi kupiga pesa
Ni vizuri, ila mwanzo si unajua mgumu ndugu.

Hapo kikubwa unatakiwa uwe na soko kubwa.

Lazima uwe na jina la kampuni yako.

Uwe na vifungashio vinavyo kutangaza.

Kuwa na mashine yako sio lazima, kwa7b ni mwanzo unaweza kuelewana na mwenye mashine anakuwa anakusagia unga we unaweka kwenye vifungashio vyako.

Unatakiwa uwe na ofisi yako(fremu) ila nayo sio lazima kama huna pesa ya fremu, unakuwa una hifadhi kwa mwenye mashine.

Pia unatakiwa uwe na mashine ya kushonea mifuko(lazima) ila nayo pia ina tegemea kama mwenye mashine ya kukoboa na kusaga anayo, utatumia hiyo hyo kwa makubaliano yenu.
Unatakiwa ununue mzani wako ule wa kukalisha mzigo (wa utosi) 200kg au 300kg.
Mifuko yako inatakiwa uweke ujazo huu…
2.5kg
5kg
10kg
25kg.

Kikubwa: Tafuta soko la uhakika kwanza la watu wa kuwauzia bidhaa yako…

Hoteli au migahawa.
Shule, bweni au chuo.
Maduka ya jumla.

Tafuta namna nzuri ya KUJITANGAZA…
Unaweza kutumia redio au ukaanzisha kombe la mpira wa miguu, kwa vijana wagombanie mbuzi, ng'ombe au pkpk nk.
Pia kwenye hilo kombe unaweka logo yako au unaliita kwa jina lako la biashara.

Nna uhakika ukitumia njia hizo unaweza kufika mbali kiuchumi.

Sijajua vibali huko TRA.

Changamoto nyingine utaziona na kuzitatua ukiwa kazini.

Kumbuka: kuna faida nyingine hapo huwezi kuziona kwa haraka haraka kama kuuza pumba za mahindi nk.
 
Nina milioni 5 nimeipata kwenye kazi zangu za umeme nilikuwa nawaza niingie kwenye biashara ya nafaka hasa maharage niyatafute vijijini huko niyalete mjini

Ila naona ninavunjika moyo na hizi comment za watu wengi.

Ngoja niendelee kufikiria biashara ya kufanya
 
Nina milioni 5 nimeipata kwenye kazi zangu za umeme.

Ngoja niendelee kufikiria biashara ya kufanya.
Fanya biashara ya mahindi kichele, nunua mashambani au vijijini huko kisha peleka mjini.

Kazi yako una nunua na kuuza jumla jumla.

Pia hii kazi unatakiwa uwe na mzani wako ili usipigwe kwenye kilo huko utakapofika kuuza.

Kikubwa uwe na watu wa uhakika wa kuwauzia mzigo huko MJINI.

Pia uwe na taarifa za uhakika kuhusu bei ili usipate hasara.
__________________________

Kama barabara nzuri na usafiri hausumbui na hata hao mabosi wako watakao nunua hayo mahindi yako huko mjini hawasumbui, utapiga BAO.

Hiyo biashara ni nzuri kama utakuwa hukai siku nyingi kukusanya na kupata mzigo huko vijijini.

Pia kuhusu bei ya kununua huko vijijini inatakiwa upange ww kama utaona bei ya mjini hailipi, maana mahindi yanatabia ya kupanda na kushuka BEI wakati wowote.

Nakutakia kila la kheri.
 
Nina milioni 5 nimeipata kwenye kazi zangu za umeme nilikuwa nawaza niingie kwenye biashara ya nafaka hasa maharage niyatafute vijijini huko niyalete mjini

Ila naona ninavunjika moyo na hizi comment za watu wengi.

Ngoja niendelee kufikiria biashara ya kufanya
Nunua viwanja au kiwanja pembeni mwa Dar Es Salaam au nje kidogo ya Dar Es Salaam

Hela inayobaki kapande miti
 
It is almost 10%
Fikiria mtu aliyewekeza 300milion kwenye nyumba za kupangisha atapata only 1.0m per month.
Aliyewekeza 30m kwenye nyumba ya kupangisha ataingiza only 150k per month.
Tafauti ya hizi biashara mbili ni security ya mtaji na usimamizi wa biashara.




Chunya
 
Nina milioni 5 nimeipata kwenye kazi zangu za umeme nilikuwa nawaza niingie kwenye biashara ya nafaka hasa maharage niyatafute vijijini huko niyalete mjini

Ila naona ninavunjika moyo na hizi comment za watu wengi.

Ngoja niendelee kufikiria biashara ya kufanya
Hela nyingi hiyo tafuta mzoefu akupe mbinu unatobo.
 
Ni vizuri, ila mwanzo si unajua mgumu ndugu.

Hapo kikubwa unatakiwa uwe na soko kubwa.

Lazima uwe na jina la kampuni yako.

Uwe na vifungashio vinavyo kutangaza.

Kuwa na mashine yako sio lazima, kwa7b ni mwanzo unaweza kuelewana na mwenye mashine anakuwa anakusagia unga we unaweka kwenye vifungashio vyako.

Unatakiwa uwe na ofisi yako(fremu) ila nayo sio lazima kama huna pesa ya fremu, unakuwa una hifadhi kwa mwenye mashine.

Pia unatakiwa uwe na mashine ya kushonea mifuko(lazima) ila nayo pia ina tegemea kama mwenye mashine ya kukoboa na kusaga anayo, utatumia hiyo hyo kwa makubaliano yenu.
Unatakiwa ununue mzani wako ule wa kukalisha mzigo (wa utosi) 200kg au 300kg.
Mifuko yako inatakiwa uweke ujazo huu…
2.5kg
5kg
10kg
25kg.

Kikubwa: Tafuta soko la uhakika kwanza la watu wa kuwauzia bidhaa yako…

Hoteli au migahawa.
Shule, bweni au chuo.
Maduka ya jumla.

Tafuta namna nzuri ya KUJITANGAZA…
Unaweza kutumia redio au ukaanzisha kombe la mpira wa miguu, kwa vijana wagombanie mbuzi, ng'ombe au pkpk nk.
Pia kwenye hilo kombe unaweka logo yako au unaliita kwa jina lako la biashara.

Nna uhakika ukitumia njia hizo unaweza kufika mbali kiuchumi.

Sijajua vibali huko TRA.

Changamoto nyingine utaziona na kuzitatua ukiwa kazini.

Kumbuka: kuna faida nyingine hapo huwezi kuziona kwa haraka haraka kama kuuza pumba za mahindi nk.
Asante sana mkuu
Umemaliza Kila kitu
 
Nina milioni 5 nimeipata kwenye kazi zangu za umeme nilikuwa nawaza niingie kwenye biashara ya nafaka hasa maharage niyatafute vijijini huko niyalete mjini

Ila naona ninavunjika moyo na hizi comment za watu wengi.

Ngoja niendelee kufikiria biashara ya kufanya
Jikite kwenye fani yako fungua duka la vifaa vya umeme
 
Biashara ya nafaka usifanye kama huna mtaji, milioni 6 kafungue duka la nyakula vya nyumbani. Huko wanaanza na nilioni 100 kuendelea hapo utaona faida.
 
Back
Top Bottom