Biashara ya nguo, viatu, mikoba na cosmetics kutoka Uganda

Biashara ya nguo, viatu, mikoba na cosmetics kutoka Uganda

Uganda nguo ni bei nafuu sana kwa sababu nchi za America,Asia na Europe zimefanya uganda kama sehemu ya kupeleke nguo ,begi,viatu etc kutokana na kuwa hawana urasimu wa biashara na kodi ni kidogo sana.Tanzania kuna urasimu na kukandamiza sana wafanyabashara kwa njia za kodi.kule wanasapoti wafanyabiashara kwa vitendo.

Pia soko ni kubwa kuna watu toka tanzania,Kenya ,rwanda,Congo,Burundi,Eritrea,Ethiopia,China,India etc na hakuna sheria kali za uhamiaji kama tanzania kwa ufupi kule hakuna kufatiliana utaifa ni free kabisa.Twende kwenye maswali yako sasa,

Sehemu ambazo unaweza nunua mzigo ni city centre lakin mitaa ya Ben Kiwanuka,Tax park,Copper complex,Arua park na Owino market na sehemu jiran na Owino market.
Kwa vile unataka mitumba ingia Owino Market uko vitu ni bei rahis sana ila inahitaji ubageini na ni lazima ubageini,viatu ( TimberLand )ambavyo nanunua Tanzania 90,000 tzsh kule nanunua kwa 15,000-18,000 tzsh ila wanakuanzia mbali unaomba upunguziwe.
Uko Owino wafanyabiashara wanajua kiswahili vizuri ila ukiambiwa bei,wewe sema ambayo ni kidogo sana kutegemea na mzigo pia wakat unanunua ndio wakat mzuri wa kujua pia utauza kiasi gani.
Tshirt ya 15,000 tzsh pale unapata kwa 1,500 tzsh tena hiyo bei rejareja kwa wewe ukinunua kwa uwingi bei ni rahis sana.Uganda imefanywa kama dampo la bidhaa hizo na watu wa ulaya,asia na america.

Sehemu ya kulala maeneo ya copper complex kuna guest nzuri moja inaitwa Galaxy Guest house ni nzuri sana,bei zake ni ndogo sana kutegemea na unachukua room gani bei uanzia 15,000 ugsh hadi 30,000 Ugsh ndio bei ya juu kabisa.
room zipo ghorofan chini ni mgahawa,pia ukikuta imejaa jiran na hapo kuna nyingine Boston guest house ni nzuri pia na ata wafanyakaz wa hapo uongea kiswahili .bei zake ni ndogo.na hizo sehemu ni jiran na shoprite pia kutoka hapo hadi owino ni dakika 2 tu kutembea na hizo sehemu ndio kwenye maduka mbalimbali.

Kuhusu kodi,kuna mbinu inafanyika nitaku pm si vizuri nikieleza hapa.Kuna njia mbili za kwenda uko kuna njia ya kupitia Nairobi hadi Kampala na kuna jia ya kati hadi Bukoba kisha unapanda bus za Friends huondoka saa moja asubuh kutoka bukoba kwenda kampala,na saa sita na nusu uko kampala,ukifika hapo chukua bodaboda hadi Galaxy Guest house au Boston zipo maeneo ya copper complex jiran na shoprite ambapo kwa bodaboda haizid 2000 ugsh.

Pia ata maeneo ya Arua park kuna guest za kulala pia. ( hayo maeneo ni kama unavyoona kariakoo majina ninayotaja ni kama mitaa tu mfano msimbazi etc hizo sehemu ziko jiran jirani )

Rate za ubadilisha pesa ni 1.5 hadi 1.6
yani 1,000 Tzsh ni 1550-1600 Ugsh.
wakat ambapo shule zinafunguliwa rate inashuka sababu wanafunz wengi wa kitanzania wanakuja na pesa na wanachange inaweza pungua hadi 1.5 au 1.55.

kuna bus kama Falcon utoka dar kupitia njia ya kati hadi bukoba kisha kampala.
njia ya nai mfano kuna spider utokea dar-nairob-kampala.

ni wewe sasa kuamua,nawajua watu wengi wanawake/wanaume wamefanikiwa sana kimaisha kupitia biashara hii.cha muhimu ukinunua kitu uombe sana kupunguziwa pia usiingiwe tamaa za kununua vitu ambavyo hukupanga kuna vitu vizuri sana kule na cha muhimu kuwa makini ili usiibiwe pesa,uporaji kule hakuna labda mtu achane pochi yake bila wewe kujua.

mkiwa na swali ulizeni
mambo vp mkuu kama umenipa mwanga upo hewani kwa no gani nicheki pm tuweze kushea mawili matatu biashara ya uganda
 
Ngoja mm niwe shuhuda wa kile unachotaka kufanya mkuu...last year nilienda uganda mwez wa 6 kuchukua hzo hzo nguo za mtumba, nilikuwa na 5m...nilifikia hotel moja pale mukono inaitwa 24/7 ni hotel nzur na ipo barabaran pia kwenye ground floor pana ofisi za kampala coach hvyo unapata uhakika wa safari na kutunziwa mizigo yako pale ofisini kwao....kwa chini zaidi ya hiyo hotel kuna club wanajaa wanafunzi wa vyuo coz lile eneo la mkono lina vyuo vingi sana na utakutana na wabongo wa kutosha na wakenya......janguuu
wise boy nakuomba pm ndugu yang nahitaji msaada wako kuhusu hii ishu maana next weak nitakuwa na trip uganda so nahitaji muongozo wa kina
 
Habari za usiku huu mabibi na mabwana..
Mimi ni miongoni ya waliokosa ajira mpaka sasa, kutokana na hali hiyo nimejidunduliza na kupata M1. Kipindi nasoma chuo nilikua nafanya biashara ndogondogo nikiwa naishi hapo hapo hostel. Pia nilikua nazunguka hostel nyingine kike mbalimbali jijini Dsm nyakati za jioni, kuwauzia nguo za mitumba,nguo za ndani na chochote kile atakachoniagiza mteja naenda kujumua namletea kama pafyumu, belt au saa.
Naomba nisiwachoshe sana nina mtaji wa Milion 1 tu nataka niende Uganda kununua vitu kule nije kuuza huku kwetu. Nimejaribu kupitia uzi mbalimbali za miaka ya nyuma za biashara hiyo, nimepata mawili matatu.
Sasa kutokana na miaka kwenda naombeni maoni au ushauri kwa watu wanaofanya biashara hii hivi sasa.
Asanteni
 
Hiyo pesa ni ndogo kusafiri mpaka Uganda kuchukua mzigo, utajikuta umekata tsh 200000 kwa ajili ya usafiri tu, kwanini usianze kwanza kuchukua mzigo hapo ulipo kabla ya kuanza kwenda nje, wenye biashara hiyo faida yao kwa robota 1 huwa ni 50,000/= tu, lakini pia fikria mitumba ya Kenya maana wao huchukua Kenya na hawachakachui kabisa na mitumba yao ni kutoka China na Korea ambao miili tunaendana.
 
Lakini pia kulingana na hali mbaya ya uchumi watu hawanunui nguo sana, fanya kuuza chakula kwa pesa uliyo nayo unaweza kununua gunia kadhaa za maharage au mchele, nenda kwenye maduka ya reja reja, mamantilie ukichukua order, sambaza mzigo wako nina uhakika kwa siku utauza maharage au mchele gunia kadhaa na faida utaiona, kila siku watu wanakula ila hawavai nguo mpya.
 
Hiyo pesa ni ndogo kusafiri mpaka Uganda kuchukua mzigo, utajikuta umekata tsh 200000 kwa ajili ya usafiri tu, kwanini usianze kwanza kuchukua mzigo hapo ulipo kabla ya kuanza kwenda nje, wenye biashara hiyo faida yao kwa robota 1 huwa ni 50,000/= tu, lakini pia fikria mitumba ya Kenya maana wao huchukua Kenya na hawachakachui kabisa na mitumba yao ni kutoka China na Korea ambao miili tunaendana.
Hiyo pesa ni mtaji tu wa kununulia mzigo pesa ya nauli na hotel nimetenga lak 3 pembeni, pia nataka nichukue nguo za duka sio mtumba tena na nguo za ndani pichu na sidiria.
 
Lakini pia kulingana na hali mbaya ya uchumi watu hawanunui nguo sana, fanya kuuza chakula kwa pesa uliyo nayo unaweza kununua gunia kadhaa za maharage au mchele, nenda kwenye maduka ya reja reja, mamantilie ukichukua order, sambaza mzigo wako nina uhakika kwa siku utauza maharage au mchele gunia kadhaa na faida utaiona, kila siku watu wanakula ila hawavai nguo mpya.
Nina uzoefu wa hii biashara na wateja wangu wakuu ni wanafunzi wa vyuon nadhani unajua wanafunzi jinsi walivyo, wanapenda kwenda na wakat.
 
Hiyo pesa ni mtaji tu wa kununulia mzigo pesa ya nauli na hotel nimetenga lak 3 pembeni, pia nataka nichukue nguo za duka sio mtumba tena na nguo za ndani pichu na sidiria.
Si uchukue hizo nguo kariakoo ?
 
Si uchukue hizo nguo kariakoo ?
Ni bei sanaaa gauni ndefu nzuri bei ya jumla ni elf 22 had 25...jinsi kali 15 had 18. Chupi nzuri za cotton ni elf 36. Kwa uchunguzi mdogo niliofanya k.koo vitu ni bei sana kuliko ug.
 
Ni bei sanaaa gauni ndefu nzuri bei ya jumla ni elf 22 had 25...jinsi kali 15 had 18. Chupi nzuri za cotton ni elf 36. Kwa uchunguzi mdogo niliofanya k.koo vitu ni bei sana kuliko ug.
Hujaingia machimbo

Kariakoo kuna maduka ya jumla na rejareja unahitaji uchambuzi yakinifu siyo mdogo.

Kwa mfano chupi kuna maduka wanauza kuanzia dozeni kumi kwa 90,000
Hapo hapo kuna anayechukua kwa huyo wa jumla na anauza kwa hiyo 36000
 
Hujaingia machimbo

Kariakoo kuna maduka ya jumla na rejareja unahitaji uchambuzi yakinifu siyo mdogo.

Kwa mfano chupi kuna maduka wanauza kuanzia dozeni kumi kwa 90,000
Hapo hapo kuna anayechukua kwa huyo wa jumla na anauza kwa hiyo 36000
Ni chimbo gani unalosema sijaingia hilo..? Nimezunguka k.koo nzima. Na hyo bei chupi ni zile chupi za kawaida sana hakuna mtu anayeuza chupi za cotton kwa elf 9 hakuna.
 
Ni chimbo gani unalosema sijaingia hilo..? Nimezunguka k.koo nzima. Na hyo bei chupi ni zile chupi za kawaida sana hakuna mtu anayeuza chupi za cotton kwa elf 9 hakuna.
Ok all the best.
 
Wazo zuri, Uganda ni cheaper sana nguo
Ni kweli dada, kama kuna jambo lolote unalifahamu au hata maeneo ya kupatikana mzigo kwa bei nafuu zaid huko Ug naomba uniambie mkuu.
 
Hebu angalia jinsi ya kuchukua Mchuzi wa Zabibu au Mvinyo kuupeleka Uganda na kule ukachukua nguo kuleta Tz.
Asante sana mkuu naomba unielekeze jinsi ya kufanya hiyo biashara.
 
Hebu angalia jinsi ya kuchukua Mchuzi wa Zabibu au Mvinyo kuupeleka Uganda na kule ukachukua nguo kuleta Tz.
Tufungue mamcho kwa mapana juu ya hili mkuu.

Umeandika kwa kifupi sana, huenda ukamsadia sana mleta uzi, lakini hata sisi pia...
 
Asante sana mkuu naomba unielekeze jinsi ya kufanya hiyo biashara.
Kwa ujumla unakwenda kwenye viwanda vinavyochakata zabibu ambavyo vipo Dodoma (Hombolo, Bihawana, au Mpunguzi) utakuta wahusika na watakufamisha meeengi yanayohusu Zabibu.
 
Back
Top Bottom