Biashara ya nguo, viatu, mikoba na cosmetics kutoka Uganda

Biashara ya nguo, viatu, mikoba na cosmetics kutoka Uganda

mkuu money stunna na wadau wengine je hizo nguo special zinazopatikana huko ni latest kwamba ziko kweny fashion ya kisasa kwa mfano tshirt.,jeans
 
Habari wana jamvi,naomba ushauri nataka kwenda uganda kuleta nguo za mitumba,pochi na viatu pamoja na vipodozi napenda kujua cha kufanya maana ndo nataka kuanza ikiwemo accomodation nikiwa uganda,je huku Tanzania nitaziuzaje,mtaji kwa mzigo wa kwanza uwe shingapi vip usafiri,Ushuru na TRA? Msaada plz.

Habari? Unaweza kuni pm manake nilishakusanya mtaji wangu,nataka kwenda kuchukua viatu

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
ngojea ntafute karamu nakaratasi niupeluz uzi vizur

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
ngojea ntafute karamu nakaratasi niupeluz uzi vizur

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Yan Baraka kwa hapa nilipo kwa mujibu wa hii thread nasisimka tuu naona kila kitu sasa nahisi harufu ya utajiri. Yan kwa mchango wa money stunna nashukur sana katufungua kichwa money stunna una mchango mkubwa juu ya kila mtu hapa mana kila nipitapo nkikukuta nakuta umeshusha nondo za ukwel. Daah Jf kweli kisima cha maarifa ngoja nianze kuandaa michakato ya safari sasa mbarikiwe kwa michango yenu yote.
 
Wakuu me nataka kufanya biashara ya nguo but mtaji Wang ni 2m msaada tafadhali
 
Inatosha kabisa. Ukianza anza na zile zinazo uzika sana kwenye soko

Mtaji ninao,knowledge nimepata, vipi kuhusu soko nitalipataje na mie sina fremu?? ...Nipe idea ndio nataka nianze hii biashara sina uelewa wa soko.
 
Yoyote mwenye uelewa wa masoko ya hii biashara ya mavazi tujulishane..
 
Umetoa maelezo mazur sana kwa maana hiyo ukiwa na mtaji wa m5 unaweza pata mzigo mkubwa na mzuri me napenda sana biashara aisee asante sana kwa maelekezo yako..
Dada yangu hebu nisaidie. Je,mtaji wa sh milioni 2 za TZ naweza kuanza?
 
mkuu stunna nakukubali na tusaidie kidogo kuhusu mambo kadhaa.
1: Je utaratibu upi unatumika wakati wa ununuzi? namaanisha wauzaji kule uganda wauza kwa robota au mtu unaweza chagua kidogokidogo haswa ukizingatia mitaji yetu midogo?
2: Je ukitokea moshi arusha nairob then uganda kunaweza usafiri huu umekaaje,? Namaanisha itachukua siku ngapi kufika uganda na njia hii inaweza kuwa na changamoto gani?
3: Je kama nafuata taratibu,itanilazimu kuwa na nini au kufanya nini mpaka mmzigo wangu ufike moshi?
4; Kwa ujumla kuna changamoto gani zingine za hii biashara maana wengine tunahamu na ndoto za kuifanya ila hatujawahi hata kuuza vocha,so tusaidie kujua lolote lingine kwenye hii biashara hasa changamoto za namna ya kununua na kusafirisha mizigo.
Hasante sana mkuu
 
mkuu stunna nakukubali na tusaidie kidogo kuhusu mambo kadhaa.
1: Je utaratibu upi unatumika wakati wa ununuzi? namaanisha wauzaji kule uganda wauza kwa robota au mtu unaweza chagua kidogokidogo haswa ukizingatia mitaji yetu midogo?
2: Je ukitokea moshi arusha nairob then uganda kunaweza usafiri huu umekaaje,? Namaanisha itachukua siku ngapi kufika uganda na njia hii inaweza kuwa na changamoto gani?
3: Je kama nafuata taratibu,itanilazimu kuwa na nini au kufanya nini mpaka mmzigo wangu ufike moshi?
4; Kwa ujumla kuna changamoto gani zingine za hii biashara maana wengine tunahamu na ndoto za kuifanya ila hatujawahi hata kuuza vocha,so tusaidie kujua lolote lingine kwenye hii biashara hasa changamoto za namna ya kununua na kusafirisha mizigo.
Hasante sana mkuu

jibu kwa swali la kwanza.Yote yanawezekana ukitaka kununua moja moja au kwa robota,ni utashi wako tu.

jibu la pili,bus zinazoenda kampala kupitia moshi na arusha zinafika moshi kama saa 9 na arusha kama saa 10 jioni kama hazikuchelewa njiani,na nairobi mnafika kuanzia saa 3 usiku kisha mnaanza tena safari saa 4 usiku na bus ilo ilo.Boda (mpakani) mnafika alfajili saa 12 pia kuna boda 2 moja ya Malaba kama mtakuwa mlipitia eldoret au Busia kama mlipitia Kisumu.

Kampala mnafika saa 3 asubuhi.

swali la 3 hakuna utaratibu wowote zaidi ya wewe kuwa na passport na nauli tu.

swali la 4,changamoto kubwa ni namna ya kufahamu wapi ununue mzigo na lazima uombe kupunguziwa bei ata kama utaona bei ndogo.pia kuhusu kusafirisha utaongea na konda kila kitu kitaenda poa.

Cha muhimu ukienda uko nenda kwa kazi uliyoendea kamwe usiingie kwenye starehe
 
Mtaji ninao,knowledge nimepata, vipi kuhusu soko nitalipataje na mie sina fremu?? ...Nipe idea ndio nataka nianze hii biashara sina uelewa wa soko.

Mkuu kwanza ungesema uko wapi na mazingira gani kwa maana ya mjini au nje ya mji.

Unaweza ukaenda kununua mzigo kisha ukawa unatembeza maofisini, make watu wa maofisini wengi huwa hawazunguki madukani kutokana na kutokuwa na nafasi.

Kuna changamoto ya watu kukopa hivyo basi uwe na uhakika na watu unaowauzia, kwa mwanzoni uza kwa cash ama mkopo kwa watu wachache unaowaamini.

Vile vile watu wanaokuzunguka ndio wateja wako!
 
Uganda nguo ni bei nafuu sana kwa sababu nchi za America,Asia na Europe zimefanya uganda kama sehemu ya kupeleke nguo ,begi,viatu etc kutokana na kuwa hawana urasimu wa biashara na kodi ni kidogo sana.Tanzania kuna urasimu na kukandamiza sana wafanyabashara kwa njia za kodi.kule wanasapoti wafanyabiashara kwa vitendo.

Pia soko ni kubwa kuna watu toka tanzania,Kenya ,rwanda,Congo,Burundi,Eritrea,Ethiopia,China,India etc na hakuna sheria kali za uhamiaji kama tanzania kwa ufupi kule hakuna kufatiliana utaifa ni free kabisa.Twende kwenye maswali yako sasa,

Sehemu ambazo unaweza nunua mzigo ni city centre lakin mitaa ya Ben Kiwanuka,Tax park,Copper complex,Arua park na Owino market na sehemu jiran na Owino market.
Kwa vile unataka mitumba ingia Owino Market uko vitu ni bei rahis sana ila inahitaji ubageini na ni lazima ubageini,viatu ( TimberLand )ambavyo nanunua Tanzania 90,000 tzsh kule nanunua kwa 15,000-18,000 tzsh ila wanakuanzia mbali unaomba upunguziwe.
Uko Owino wafanyabiashara wanajua kiswahili vizuri ila ukiambiwa bei,wewe sema ambayo ni kidogo sana kutegemea na mzigo pia wakat unanunua ndio wakat mzuri wa kujua pia utauza kiasi gani.
Tshirt ya 15,000 tzsh pale unapata kwa 1,500 tzsh tena hiyo bei rejareja kwa wewe ukinunua kwa uwingi bei ni rahis sana.Uganda imefanywa kama dampo la bidhaa hizo na watu wa ulaya,asia na america.

Sehemu ya kulala maeneo ya copper complex kuna guest nzuri moja inaitwa Galaxy Guest house ni nzuri sana,bei zake ni ndogo sana kutegemea na unachukua room gani bei uanzia 15,000 ugsh hadi 30,000 Ugsh ndio bei ya juu kabisa.
room zipo ghorofan chini ni mgahawa,pia ukikuta imejaa jiran na hapo kuna nyingine Boston guest house ni nzuri pia na ata wafanyakaz wa hapo uongea kiswahili .bei zake ni ndogo.na hizo sehemu ni jiran na shoprite pia kutoka hapo hadi owino ni dakika 2 tu kutembea na hizo sehemu ndio kwenye maduka mbalimbali.

Kuhusu kodi,kuna mbinu inafanyika nitaku pm si vizuri nikieleza hapa.Kuna njia mbili za kwenda uko kuna njia ya kupitia Nairobi hadi Kampala na kuna jia ya kati hadi Bukoba kisha unapanda bus za Friends huondoka saa moja asubuh kutoka bukoba kwenda kampala,na saa sita na nusu uko kampala,ukifika hapo chukua bodaboda hadi Galaxy Guest house au Boston zipo maeneo ya copper complex jiran na shoprite ambapo kwa bodaboda haizid 2000 ugsh.

Pia ata maeneo ya Arua park kuna guest za kulala pia. ( hayo maeneo ni kama unavyoona kariakoo majina ninayotaja ni kama mitaa tu mfano msimbazi etc hizo sehemu ziko jiran jirani )

Rate za ubadilisha pesa ni 1.5 hadi 1.6
yani 1,000 Tzsh ni 1550-1600 Ugsh.
wakat ambapo shule zinafunguliwa rate inashuka sababu wanafunz wengi wa kitanzania wanakuja na pesa na wanachange inaweza pungua hadi 1.5 au 1.55.

kuna bus kama Falcon utoka dar kupitia njia ya kati hadi bukoba kisha kampala.
njia ya nai mfano kuna spider utokea dar-nairob-kampala.

ni wewe sasa kuamua,nawajua watu wengi wanawake/wanaume wamefanikiwa sana kimaisha kupitia biashara hii.cha muhimu ukinunua kitu uombe sana kupunguziwa pia usiingiwe tamaa za kununua vitu ambavyo hukupanga kuna vitu vizuri sana kule na cha muhimu kuwa makini ili usiibiwe pesa,uporaji kule hakuna labda mtu achane pochi yake bila wewe kujua.

mkiwa na swali ulizeni

Good Idea
 
Back
Top Bottom