Biashara ya nguo, viatu, mikoba na cosmetics kutoka Uganda

Biashara ya nguo, viatu, mikoba na cosmetics kutoka Uganda

JF ni zaidi ya shule! Asante sana kiongozi. Vp ukiwa na mtaji wa kama milion 1.5 na uko dar hii biashara mtu unaweza ukaimudu?

hiyo inatosha kwa kuanzia cha muhimu uchukue bidhaa inayotoka kwa urahisi hivyo fanya utafiti hapo kama ni nguo mfano,angalia nguo gani zinatoka kwa urahisi ukishafanya hivyo fata mzigo na uza utaona mtaji wako unakuwa.

cha kuzingatia ukifika ug ununue vitu ulivyopanga maana vizuri viko vingi pia usiingie kwenye starehe,fanya kilichokupeleka na urudi
 
aaah Gaba!!! nilienda pale beach wakati wa honeymoon yangu! Halafu nilifanya shopping ya nguvu pale Mukwano. Nafikiri kuna mambo nahitaji kuyafanya hivi karibuni nitakuja kukutafuta humu kamanda!

yea karibu na gabba beach,poa kuwa free kunitafuta muda wowote JF ni kama nyumbani
 
Mtaji wa kama mil 4.5 upo,ishu ni soko la kuja kuuzia,kwa sehemu kama dar jamani kupata sehemu ambayo biashara ya nguo inalipa kodi yake si ndo itakufilisi

ukitafuta sehemu si lazima utafute jengo la mjini kabisa ata uko kwenye makazi ya watu kuna wateja,kupata sehemu mjini kabisa ni gharama
 
Ngoja mm niwe shuhuda wa kile unachotaka kufanya mkuu...last year nilienda uganda mwez wa 6 kuchukua hzo hzo nguo za mtumba, nilikuwa na 5m...nilifikia hotel moja pale mukono inaitwa 24/7 ni hotel nzur na ipo barabaran pia kwenye ground floor pana ofisi za kampala coach hvyo unapata uhakika wa safari na kutunziwa mizigo yako pale ofisini kwao....kwa chini zaidi ya hiyo hotel kuna club wanajaa wanafunzi wa vyuo coz lile eneo la mkono lina vyuo vingi sana na utakutana na wabongo wa kutosha na wakenya......janguuu

Ila kutoka Kampala hadi mukono parefu kidogo na folen za kule. Mukono kumechangamka sana. Maduka hayafungwi mapema pale.
 
Kweli MUNGU awabariki wote mliochangia humu. Nimepata mengi..!!

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
ukitafuta sehemu si lazima utafute jengo la mjini kabisa ata uko kwenye makazi ya watu kuna wateja,kupata sehemu mjini kabisa ni gharama

Yap mkuu Money Stunna nimekusoma,huko kwenye makazi unaweza pata sehemu,ila pia heri sehemu yenye competition ya biashara ambayo watu wengi wanaifaham ili ukileta mzigo utoke fasta.
 
Last edited by a moderator:
hiyo inatosha kwa kuanzia cha muhimu uchukue bidhaa inayotoka kwa urahisi hivyo fanya utafiti hapo kama ni nguo mfano,angalia nguo gani zinatoka kwa urahisi ukishafanya hivyo fata mzigo na uza utaona mtaji wako unakuwa.

cha kuzingatia ukifika ug ununue vitu ulivyopanga maana vizuri viko vingi pia usiingie kwenye starehe,fanya kilichokupeleka na urudi

Asante sana ndugu. Umenifungua sana macho. Vp lakin ug kuingia ni free kwa njia ya mtukula? Hakuna usumbuf mpakan?
 
maswali yako mengine yanaweza jibiwa na wewe ....kwa nini Kampala,
Nimewahi kuwa Kampala accomadation sio mbaya kwa elfu 30 unaweza lala mahali salama sana
hilo la biashara sijui hata mimi niliwahi tafuta taarifa ....ila kuna mdau alinipa mwanga anaitwa MONEY STUNNA ,KAMA NI MTAALAMU TAFUTA HIYO THREAD
Ila ni kweli Kampala kuna mitumba mizuri kuliko Dr
vipi kuhusu nairobi kikombaa market? , huwa nawaona vijana wengi wakitanzania huku wanakuja kuchukua mzigo.
 
vipi kuhusu nairobi kikombaa market? , huwa nawaona vijana wengi wakitanzania huku wanakuja kuchukua mzigo.

Nairobi kwa suti za mtumba wako vizuri. Kuna suti nzuri sana na bei cheee. Hawachakachui kama Dar kam ni grade one basi huwa hivyo.

Kwa suti na electronics Nai wako poa ila kaa mbali na wakora ( vibaka)
 
Money Stunna km utarudi tena hapa tusaidie pia kujua jinsi ya kuhifadhi mizigo na kusafirisha mpaka dsm baada ya kununua mzigo kampala.
 
Back
Top Bottom