Biashara ya Nguo za Mtumba: Ushauri na Muongozo wa Kuifanya kwa Mafanikio

Biashara ya Nguo za Mtumba: Ushauri na Muongozo wa Kuifanya kwa Mafanikio

Wadau za Leo,

Nataka kufanya biashara ya kuuza nguo za mitumba za aina mbili kama nilivosema hapo juu za watoto na wanawake.

Lakini sina uzoefu kabisa na biashara hii na wala sjui lolote..sema nimeona ndo biashara ninayoweza kuianza na kuimudu.

Mtaji nilionao ni milioni moja na biashara nataka nifanyie maeneo ya Kibaha maili moja au Kibaha kwa Mathias. Kibaha picha ya ndege au eneo lolote karibu na hapo ntakapopata eneo zuri na lenye uelekeo wa biashara hyo?

Sasa naomba walio na uzoefu wanijuze kipi bora. Nianze kwa kununua balo au nianze kwa kununua moja moja minadani?
Kama ni kununua balo ni wapi ntapata mabalo yaliyo mazuri na bei zake zikoje?

Na kama ni kununua moja moja ni mnada upi uko vzri ili nipate faida?
 
Mkuu,

Mimi pia nitaanza biashara hii wiki ijayo hapa dar es salaam,japokuwa sina uzoefu wowote kuhusu biashara hii isipokuwa imekuwa kichwani muda mrefu na ninaipenda toka moyoni na pia kabla ya kuamua nilipata ABC kuihusu.

Nilipitia maandiko ya wajasiliamali mitandaoni na pia wadau wengine wenye uzoefu wa biashara hii na hata kuomba ushauri kwa wafanyabiashara wenyewe wanaofanya biashara hii pale Kariakoo na kwingineko.

Wengi wanasema biashara ya mitumba kwa ujumla inalipa sana isipokuwa inahitaji umakini katika manunuzi ya mzigo ili utengeneze faida.

Kwa maoni yao wanasema;
~Ukiwa ndo unaanza kufanya biashara hii ni mara mia ukanunue mzigo pale Ilala sokoni has a kwenye ule mnada unaoanza saa 4 aksubuhi kuliko kununua balo kwani wafanyabiashara wa Kariakoo wengi si waaminifu wanaweza kukuuzia balo lenye malonya mengi na hivyo kwa vyovyote mzigo utakukata na kukusababishia hasara.

Wanashauri kwa mfanyabiashara anayeanza ni vema apate uzoefu wa kutosha na connection ya uhakika kabla ya kuamua kwenda kununua balo la nguo pale.

Nyongeza ya hilo,kwa kuwa huna uzoefu wa kutosha,wafanyabiashara wa kariakoo ni rahisi kukuibia kwa kutojua tu grades za mabalo amboyo kimsingi yanatofautiana quality na bei.

Mfano;kuna mabalo yanauzwa kuanzia 150,000-600,000 kwahiyo unaweza hitaji balo let's say la (laki 4) na wao wakakupatia la (laki 1.5),kwa vyovyote hapo itakuwa ngumu kwa wewe kugundua kama umetapeliwa hadi utakapoiona hasara.

Binafsi nakushauri kanunue mzigo wako pale Ilala sokoni,achana na habari za balo katika hatua hizi za awali otherwise uwe na mtu wa kuaminika kwelikweli pale Kariakoo ambaye atakusaidia upate mzigo unaoutarajia japo ni ngumu kidogo ila inawezekana.

Aksante.
 
Wakuu bei za Mitumba nguo za watoto Balo moja inarange kuanzia sh ngapi hadi ngapi? Pia naomba kujulishwa bei ya jumla ya nywele za kinadada Rasta zinauzwajekwa bei ya Jumla Kariakoo?
 
nimeiona mkuu text yako!
ila biashara ipo hivi:

kila baro inavyotoka nje inakua na mchanganyiko wa nguo zote yaani grade A, B,C na zinginezo na haswa kwa zile mixture kinachosumbua kuna aina fulani ya baro huwa wabongo huzifungua na kuchukua nguo nzuri then huzipack tena
sasa hukikumbana nazo hizo zilizofunguliwa unaweza ukakata mtaji

kuna aina kama tatu hivi za baro ambazo ni nzuri kwa mnada kwani zenyewe ni mixture

aina ya kwanza ambazo zenyewe hutoa nguo nyingi ambazo ni grade one ni Australia ambazo zinapatikana ktika uzito wa kg 100 na bei yake ina range Tsh 450000 hadi 500000,hizi ni nzuri na ndio ninazoziuza Mimi nawe nakushauri uzipate hizo kwani si rahisi kukata pesa yako ,umeanguka sana unarudisha pesa yako

za pili ni baro za kichina nazo ni nzuri na hata bei yake ni affordable kg 100 @ Tsh 370000 hadi Tsh 420000

na za tatu ni za kimarekani maarufa kama SUMMER, zinapatikana katika uzito wa kg 50 na 80 na bei zake Tsh 250000 hadi Tsh280000 kwa za kg 50 na Tsh 320000 hadi Tsh370000
ndio hivyo mkuu jipange kachukue mzigo huo
 
Balo zipo sehemu nyingi
Changamoto ni iyo uchakachuzi wa mabalo, niliwai kwenda uganda balo hazifunguliwi.

Mara nyingi balo ikiwa na koa, imefungwa na yale mabati inakuwa haijafunguliwa, ila ikiwa na plastic mara nyingi izo ndizo zimefungwa upya, ila c lazima iwe ivo.

Haya ni jibu swali wanalokwepa wengi zinapatikana wap?

Ukifika mnazi mmoja dar, kama unatoka k.koo nyooka moja kwa moja kama unaenda mnara wa saa au stesheni, unapovuka tu makutano ya pili ya mataa, ya mnazi mmoja kuna maduka wanauza sana kanga na vitenge, kuanzia hapo, maduka ya mitumba nikibao, nenda mtaa wa pili kama sikosei unaitwa sofia, maduka kibao hapo mitumba tupu, yani zunguka eneo ilo utapata mitumba kibao.

Pili ukiwa congo, k.koo kituoni mkono wa kulia ukiwa unaelekea mnazi lipo duka moja hapo kwa mhind linapakana na duka la samsung.

Tatu Magomeni, ni eneo jipya hili, ofis za ttcl ukifika hapo upande wa pili utaona mitumba had ya viatu wholesale bales.

Hapa magomeni ni makutano ya mataa pale ukiuliza ofis za ttcl utaoneshwa.

Changamoto ni kupata bales nzuri, kama unaweza mtafute mteja wao mzoefu wanaempaga vitu bora, akuchukulie.

Au washikishe wale jamaa tingo wa dukani kitu kidogo, wambie nipe kitu cha maaana jifanye ni mzoefu ila unabadili duka tu.

Ukijifanya mzoefu usizubae, kwa mfano ukiuliza mixer ya nguo za kike, akikuuliza kg ngap unakuwa shapu kuonesha unajua, sio wanauliza Kg hujui kuwa balo zina kilogram

Au unaulizwa material inayotaka hukui, either cotton, nylon n.k

Nahs nimesema kidogo kitakachowasaidieni
 
Balo inategemeana kuna laki 3 na kuendelea.
 
Habari ndugu,

Nilikuwa naomba msaada wa taarifa juu ya upatikanaji wa nguo za mitumba za jumla (bale). Naomba kujua mabeli yanapatikana wapi na bei zake zipoje? Nipo interested zaidi na makoti ya suti za kiume na kike pamoja na mapazia.

Asante
 
Back
Top Bottom