Huu ni mwendelezo wa kuhusu biashara ya mtumba kutoka Kampala.
Unapokuwa Owino market jaribu kuuliza sehemu wanazouza kwa bei ya jumla. Sehemu ziko nyingiiiii sana kwani hata baadhi ya maeneo yaliyo mbali kidogo na Owino Kuna maduka ya Second hand whole salers kwa mfano maeneo ya kisenyi bus terminal.
Ndani ya Owino market ni mwendo wa kutoa mguu niweke mguu maana ni watu wengi na kelele za wachuuzi za kukaribisha wateja wa retail. Ukitaka kununua kwa rejareja poa tu kwani ukiamka asubuhi saa moja, ukiwa na speed mpaka saa tano unaeza kuwa umenunua mzigo wa kutosha.
Kampala Kuna masharti ya mtumba mazuri sana. Mi huwa hata ofisini wanakubali na hata wale wa masharti ya shop special nawatoa knock out. Bei za masharti mazuri ni elfu kumi mpaka 20 ya kiganda. Ila kwa hapa nazunhumzia kwa wale ambao wanaotafuta ya kuvaa wao na sio ya biashara.
Kuna magauni na tops, pia blouse za kina dada nzuri sana yaani ukiingia Owino for the first time unaeza changanyikiwa.
Ukiwa Owino jaribu kukalili njia za kutoka maana unaeza jikuta unachanganya uliingilia wapi.
Kuna nguo za watoto nzuri sana. Unaeza nunua kwa issue binafsi au unaenda uza na kupata faida Kubwa
Karibu Owino sio kibiashara tu hata wale wapenda bling bling just go to Kampala for vacation and do shopping utaniambia mtumba ule hakunaga.
Kuna mikoba na mabegi ya mtumba mazuri sana. Hapa ngoja nikazie.
BIASHARA YA MTUMBA ILIYOPEWA KISOGO NA WENGI
Hapa naomba kuzungumzia second hand bags (mabegi, mikoba na pochi za mtumba).Wengi tumekuwa tukiangalia nguo na viatu tu na kusahau biashara moja ya bags. Napenda hapa nijikite na bags from Kampala (mivumba).Kampala Kuna bags nzuri sana, kuna mikoba, mabegi na pochi amazing. Unajua wanafunzi wanapenda begi nzuri na ngumu yaani kwa Kampala ni noma.
Vipi kuhusu mama zetu na dada zetu kwenye mikoba ;wanawake wa mji wanapenda kuwa na vitu unique bhana, Leo msibani ana pochi hii, kesho sokoni ana mkoba huu, keshokutwa saloon au jumatatu mpaka ijumaa kazini ana change mikoba tu sio anarudia mkoba mpaka unapauka kwa Jua.
Unajua Akina dada wakikutana kwenye shughuli zao hupenda kuwa wamependeza from toe to head, sasa mkoba muhimu au pochi. Kuna Luis Vuitton, Anna Sui, Gucci, Prada etc za mtumba.
Mabegi ya shule pia yapo mazuri sana na ukiwa mjini yapo unauza hata 40 kulingana na uzuri na ugumu wake.
Jaribu kufanya hii biashara kwani ukichukua mzigo the mtaji flani mkubwa hautajuutia aisee kwani biashara hii inaihitaji iwe na mzigo wa kutosha.
Kwa mfano umechukua mzigo wa milioni mbili za kibongo ukapata mzigo wenye items 600, ukaamua kila item uuze elfu 10000 utapata ngapi? Na hapa umepigia kwa bei flatlet, kumbuka Kuna mikoba ipo ya mpaka 20,, 30 na zaidi kulingana na eneo ulipo, sio uwe Chato au Buseresere afu utegemee uuze kwa bei kubwa utajikuta biashara yako unasubiri mwisho wa mwezi tu salary itoke ndio uuze.
[HASHTAG]#karibu[/HASHTAG] tuunge umoja kibiashara yaani kufanya safari za kibiashara Kampala tupige hela kabla mtumba hujapigwa stop 2018
Wale wa Mwanza, Dodoma,Geita Musoma n. K nafasi ni hii sio lazima tuende Dar. Afu mtumba wetu unachachuliwa sana.