UZOEFU KATIKA UVUAJI NA UUZAJI WA SAMAKI
Mimi Nimevua SANGARA ziwa Victoria, Sato tulikuwa tukiwakamata mara chache kwasababu tulikuwa tuna vua maji ya kina kirefu.
Mimi nimewahi kuvua ziwa Victoria kisiwa cha kome na visiwa jirani huko. Biashara ya uvuvi siyo rahisi na siyo ngumu. Urahisi wa biashara hii ikiwa wewe mwenye mtaji utaamua kuishi kambini na wavuvi wako, ukisimamia ukiwa site kabisa, yani anzisha kambi, wavuvi wengi tu, wanakuja wenyewe mnaanza kazi.
Malipo inategemea na wewe mwenyewe, unaweza kuwaliapa pesa, au ukawapa siku zao za uvuvi kama sehemu ya malipo yao. Yaani wanakuvulia Jumatatu mpaka Ijumaa, Jumamosi na Jumapili wanavua lakini nizao au ndio malipo yao, wakipata sawa wakikosa pia wanelewa. Ila gharama za kuwalisha ni zako mwenye kambi, unanunua Unga tu, samaki wanapatikana ziwani kama kitoweo.
Unaweza ukawa unauza samaki wabichi, kwa wamiliki wa viwanda au kuna wachuuzi wa wenye viwanda wanazunguka na mzani wananunua na kupeleka kiwandani, ama unaweza wachana samaki ukawatia chumvi na kuwakausha juani kule wanaitwa Kayabo, soko lao ni Zaire, na Zambia kwa sana.
Unahitaji kuwa na mitumbwi ya kuvulia kadhaa kutokana na mtaji wako na mahitaji yako, unahitaji kuwa na Injini za boti atleast Mbili. Kwasababu unahitaji pia kufanya doria ya nyavu zako, wavuvi ni wezi kama ilivyo kwa sehemu zingine, kama huna speed bot na hufanyi doria, hao hao wavuvi wako wanongea na wenzao wa maeneo mengine wanakuja kukuibia nyavu zote.Lakini wakijua una speed boti na unafanya doria pia umiliki bunduki wataogopa. Nimefanya kazi hizo za usimamizi miaka mingi kidogo imepita lakini huo ni uzoefu nilio upata huko.
Najua uzi huu labda ume expire lakini niliona ni shere labda uhitaji bado upo.
Naomba kuwasilisha.