Ipi dot com
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 306
- 166
Samahani The Boss nilikuwa kijiji cha wachawi cha Ngende, ndani ya pori kubwa mkoani Lindi nina mengi ya kuwashirikisha, nimepita tu eneo lenye internet, bado niko vijijini.
Watawala wa Taifa la Tanzania, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, walifanya kila aina ya mbinu chafu za kuimarisha utawala wao, ili waweze tena kuongoza taifa la Tanzania.
Nimesema walifanya mbinu chafu zenye makufuru makubwa, na katika ulimwengu usiooneka walionekana waziwazi waliyokuwa wakiyafanya.
Moja ya kufuru walilofanya ni kuwekwa ndani ya majeneza na kushushwa makaburini, ambako walilala huko usiku mzima, huku wachawi wa nchi wakicheza uchi wa nyama juu ya makaburi hayo. Kisha waliapishwa na majini.
Lakini kibao kiligeuzwa ghafula katika ulimwengu usiooneka baada ya kuingiliwa na kundi kubwa la wanadamu waliokuwa wanamlilia Mwenyenzi Mungu juu ya hatima ya baadaye ya taifa la Tanzania.
Katika ulimwengu usioonekana, utawala uliokuwa ukioonekana kama mlima Kilimanjaro, uligeuzwa kichwa chini miguu juu, ulisagwasagwa, ukasambaratishwa kutoka jiwe la mlima hadi kuwa mavumbi matupu.
Kimsingi utawala wa taifa la Tanzania ulioliongoza taifa hili kutoka mwaka 1961 ulikoma rasmi mwezi Septemba 2010 katika ulimwengu usioonekana.
Kazi inayoendelea sasa ni kufanya yale yaliyotendeka katika ulimwengu usioonekana, yadhihirike katika ulimwengu unaooneka. Kawaida nguvu ya mtu au ya taifa ipo katika ulimwengu usioonekana, na matokeo yake hujitokeza taratibu kwenye ulimwengu unaoonekana.
Kwa sababu taifa la Tanzania kwa sasa hivi halipo kabisa katika ulimwengu usioonekana, yapo mambo kadhaa ambayo ni lazima yajitokeze katika ulimwengu unaoonekana.
a) Watawala walioondolewa katika ulimwengu usioonekana, kila jambo watakalojaribu kulifanya au kutenda katika ulimwengu unaoonekana wataishia kwenye aibu ya kukata na shoka.
b) Mambo hayo ya aibu yatakuwa yanafuta hati yao batili ya utawala polepole kwenye utawala unaoonekana.
c) Mwenyenzi Mungu hawezi kusimamisha utawala mpya kwenye utawala uliofanya makufuru makubwa kiasi hicho hadi, utawala huo ufutike kabisa katika ulimwengu unaooneka kama ulivyogeuzwa mavumbi katika ulimwengu usioonekana.
d) Njaa italiandama taifa, kwa sababu Mungu amegeuka, uso wake haupo tena juu ya taifa hili hadi makufuru yaliyofanyika yafutike.
e) Waliofanya makufuru hayo wajitayarishe kwa hasira kali ya Mwenyenzi Mungu.
Hili jambo ni hakika na kweli, na litatimia kwa asilimia 100%
HATI ya KIFO
Nimekuwa mbali na safu hii kwa muda, baada ya safari ya mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma, kwa sasa nipo Mbamba Bay kandokando ya ziwa Nyasa wilayani Mbinga. Yapo mambo yanayoonekana kuwa ni mambo ya heri, yameanza kujiinua kwa nguvu kubwa na bado yanazidi kujiinua ndani ya taifa la Tanzania.
Katika safu zangu ya nyuma niliweka maelezo kama yanavyosomeka hapo juu, kuhusu mambo yaliyolikuta taifa la Tanzania katika ulimwengu usioonekana, leo nitazungumzia baadhi ya mambo na harakati kubwa za kuzimu, wakijaribu kujinasua na anguko lililowapata.
Utawala ulioliongoza taifa ulisambaratishwa na kufutwa kabisa katika ulimwengu usiooneka, mwishoni mwa mwaka jana 2010, baada ya kufanya makufuru makubwa. Kusambaratishwa kwa utawala wa zamani wa dunia ya Tanzania, kumewapa taabu kubwa mamlaka za kuzimu ambazo zimejipanga upya kukabiliana na hali hiyo.
Kwa kuanzia kuzimu wamepandisha duniani majini mengi ya mlipuko, majini haya huwaingia wanaadamu na wakishawaingia hufanya kile walichoamriwa na kuzimu kukifanya wakiwa ndani ya watu hawa. Kujenga utawala ulioanguka katika ulimwengu usioonekana damu ya binadamu ni malighafi muhimu inayohitajika na ni lazima ipatikane kwa namna yoyote. Maazimio ya vikao vya kuzimu ni kupata mapipa mengi yaliyajaa damu za binadamu ili kazi ifanikiwe, na namna ya kuipata ni kusababisha ajali sehemu mbalimbali za nchi yetu, kazi hii kwa sasa inaendelea kufanyika kwa nguvu.
Hatua ya pili ni kuharakisha vifo vya watu kwa kuwauzia hati ya kifo kwa bei nafuu, vikao vilitambua matatizo ya maradhi aina mbalimbali waliyo nayo Watanzania wengi, na wengi wao wamekuwa siyo rahisi hata kidogo kuwatumia mawakala wao waliopo duniani wakijulikana kama waganga wa kienyeji. Hivyo haya majini ya mlipuko yalielekezwa yawaingie viongozi wa dini ya Kikristo, ambao walikuwa na mahusiano na kuzimu, kwa kufanya hivyo watu wengi wasiokubali huduma za waganga wa kienyeji watakamatika kirahisi, majini haya yakiwa ndani ya watumishi hawa huwatokea kwenye ndoto na kupewa miongozo jinsi ya kutenda kazi. Kimsingi kinachofanyika majini haya ndiyo yenyewe yanagawa hizo dawa zilizotoka kuzimu kwa kutumia mikono ya hawa wanadamu. Utabibu huu wa kuzimu unaonekana kuleta ahueni kwa baadhi ya watu, lakini ukweli ni kuwa KILA mtu aliyenyweshwa kikombe na majini haya, mambo makubwa na ya hatari sana yako mbele yake.
Nilizungumzia aibu watakayokuwa wanaipata watawala waliokataliwa, kwani kila jambo watakalolifanya kuwahadaa wananchi wataishia kwenye aibu, tumeshuhudia madudu yao waliyoyafanya katika harakati zao za kuibadili katiba ya Tanzania.
Na sio Loliondo tu, hivi sasa vikombe vipo sehemu nyingi...Unamaanisha kikombe cha babu loliondo ni mpango maalum wa kishetani, kwa maana nyingine unamaanisha watu wasikimbilie kupata kikombe....
HATI ya KIFO
Nimekuwa mbali na safu hii kwa muda, baada ya safari ya mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma, kwa sasa nipo Mbamba Bay kandokando ya ziwa Nyasa wilayani Mbinga. Yapo mambo yanayoonekana kuwa ni mambo ya heri, yameanza kujiinua kwa nguvu kubwa na bado yanazidi kujiinua ndani ya taifa la Tanzania.
Katika safu zangu ya nyuma niliweka maelezo kama yanavyosomeka hapo juu, kuhusu mambo yaliyolikuta taifa la Tanzania katika ulimwengu usioonekana, leo nitazungumzia baadhi ya mambo na harakati kubwa za kuzimu, wakijaribu kujinasua na anguko lililowapata.
Utawala ulioliongoza taifa ulisambaratishwa na kufutwa kabisa katika ulimwengu usiooneka, mwishoni mwa mwaka jana 2010, baada ya kufanya makufuru makubwa. Kusambaratishwa kwa utawala wa zamani wa dunia ya Tanzania, kumewapa taabu kubwa mamlaka za kuzimu ambazo zimejipanga upya kukabiliana na hali hiyo.
Kwa kuanzia kuzimu wamepandisha duniani majini mengi ya mlipuko, majini haya huwaingia wanaadamu na wakishawaingia hufanya kile walichoamriwa na kuzimu kukifanya wakiwa ndani ya watu hawa. Kujenga utawala ulioanguka katika ulimwengu usioonekana damu ya binadamu ni malighafi muhimu inayohitajika na ni lazima ipatikane kwa namna yoyote. Maazimio ya vikao vya kuzimu ni kupata mapipa mengi yaliyajaa damu za binadamu ili kazi ifanikiwe, na namna ya kuipata ni kusababisha ajali sehemu mbalimbali za nchi yetu, kazi hii kwa sasa inaendelea kufanyika kwa nguvu.
Hatua ya pili ni kuharakisha vifo vya watu kwa kuwauzia hati ya kifo kwa bei nafuu, vikao vilitambua matatizo ya maradhi aina mbalimbali waliyo nayo Watanzania wengi, na wengi wao wamekuwa siyo rahisi hata kidogo kuwatumia mawakala wao waliopo duniani wakijulikana kama waganga wa kienyeji. Hivyo haya majini ya mlipuko yalielekezwa yawaingie viongozi wa dini ya Kikristo, ambao walikuwa na mahusiano na kuzimu, kwa kufanya hivyo watu wengi wasiokubali huduma za waganga wa kienyeji watakamatika kirahisi, majini haya yakiwa ndani ya watumishi hawa huwatokea kwenye ndoto na kupewa miongozo jinsi ya kutenda kazi. Kimsingi kinachofanyika majini haya ndiyo yenyewe yanagawa hizo dawa zilizotoka kuzimu kwa kutumia mikono ya hawa wanadamu. Utabibu huu wa kuzimu unaonekana kuleta ahueni kwa baadhi ya watu, lakini ukweli ni kuwa KILA mtu aliyenyweshwa kikombe na majini haya, mambo makubwa na ya hatari sana yako mbele yake.
Nilizungumzia aibu watakayokuwa wanaipata watawala waliokataliwa, kwani kila jambo watakalolifanya kuwahadaa wananchi wataishia kwenye aibu, tumeshuhudia madudu yao waliyoyafanya katika harakati zao za kuibadili katiba ya Tanzania.
Unamaanisha kikombe cha babu loliondo ni mpango maalum wa kishetani, kwa maana nyingine unamaanisha watu wasikimbilie kupata kikombe....
Na sio Loliondo tu, hivi sasa vikombe vipo sehemu nyingi...