HATI ya KIFO
Nimekuwa mbali na safu hii kwa muda, baada ya safari ya mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma, kwa sasa nipo Mbamba Bay kandokando ya ziwa Nyasa wilayani Mbinga. Yapo mambo yanayoonekana kuwa ni mambo ya heri, yameanza kujiinua kwa nguvu kubwa na bado yanazidi kujiinua ndani ya taifa la Tanzania.
Katika safu zangu ya nyuma niliweka maelezo kama yanavyosomeka hapo juu, kuhusu mambo yaliyolikuta taifa la Tanzania katika ulimwengu usioonekana, leo nitazungumzia baadhi ya mambo na harakati kubwa za kuzimu, wakijaribu kujinasua na anguko lililowapata.
Utawala ulioliongoza taifa ulisambaratishwa na kufutwa kabisa katika ulimwengu usiooneka, mwishoni mwa mwaka jana 2010, baada ya kufanya makufuru makubwa. Kusambaratishwa kwa utawala wa zamani wa dunia ya Tanzania, kumewapa taabu kubwa mamlaka za kuzimu ambazo zimejipanga upya kukabiliana na hali hiyo.
Kwa kuanzia kuzimu wamepandisha duniani majini mengi ya mlipuko, majini haya huwaingia wanaadamu na wakishawaingia hufanya kile walichoamriwa na kuzimu kukifanya wakiwa ndani ya watu hawa. Kujenga utawala ulioanguka katika ulimwengu usioonekana damu ya binadamu ni malighafi muhimu inayohitajika na ni lazima ipatikane kwa namna yoyote. Maazimio ya vikao vya kuzimu ni kupata mapipa mengi yaliyajaa damu za binadamu ili kazi ifanikiwe, na namna ya kuipata ni kusababisha ajali sehemu mbalimbali za nchi yetu, kazi hii kwa sasa inaendelea kufanyika kwa nguvu.
Hatua ya pili ni kuharakisha vifo vya watu kwa kuwauzia hati ya kifo kwa bei nafuu, vikao vilitambua matatizo ya maradhi aina mbalimbali waliyo nayo Watanzania wengi, na wengi wao wamekuwa siyo rahisi hata kidogo kuwatumia mawakala wao waliopo duniani wakijulikana kama waganga wa kienyeji. Hivyo haya majini ya mlipuko yalielekezwa yawaingie viongozi wa dini ya Kikristo, ambao walikuwa na mahusiano na kuzimu, kwa kufanya hivyo watu wengi wasiokubali huduma za waganga wa kienyeji watakamatika kirahisi, majini haya yakiwa ndani ya watumishi hawa huwatokea kwenye ndoto na kupewa miongozo jinsi ya kutenda kazi. Kimsingi kinachofanyika majini haya ndiyo yenyewe yanagawa hizo dawa zilizotoka kuzimu kwa kutumia mikono ya hawa wanadamu. Utabibu huu wa kuzimu unaonekana kuleta ahueni kwa baadhi ya watu, lakini ukweli ni kuwa KILA mtu aliyenyweshwa kikombe na majini haya, mambo makubwa na ya hatari sana yako mbele yake.
Nilizungumzia aibu watakayokuwa wanaipata watawala waliokataliwa, kwani kila jambo watakalolifanya kuwahadaa wananchi wataishia kwenye aibu, tumeshuhudia madudu yao waliyoyafanya katika harakati zao za kuibadili katiba ya Tanzania.
Bravo Majimoto waambie bana mimi nikisema the power hand is changed hawaamini. Wanadhani ni mastermind fulani ndo anatengeneza anguko la mafisadi na utawala wao uliojifungamanisha na kuzimu. Hakuna atakaye salia then they would come to understand what it means by the mighty hand of God; Jesus and the mighty power of God; The Hollyghost. Tuko hapa Kings katika newly established Kingdom tumeamua kusimama kwa zamu zetu hadi tuhakikishe kila kona ya Tanzania iko huru na anga lote liko wazi dhidi ya marine waters and powers and prinicipalities. Yupo mnajimu wao mmoja atakuwa anaona maruwe ruwe maana nimesha toboa mboni za macho yake kiasi kuwa katika TV yake antena haikamati tena anaona chenga chenga station zote nimeng'oa minara. Sasa wako confused na soon wataanza kunyanyua silaha na kuuana wao kwa wao. Hakuna damu ya innocent mtanzania itamwagika ole wao na watoto wao maana wakikosa damu inabidi watoe kafara uzao wa matumbo yao! Glory and honour to our God almighty for without you nothing is possible. Let your name increase and mine decrease continue to use me Lord for your own Glory. In Jesus name I thank you Amen!