Biashara ya ukahaba imekithiri Sinza na kusababisha wakazi kuhama nyumba zao

Biashara ya ukahaba imekithiri Sinza na kusababisha wakazi kuhama nyumba zao

Elitwege

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
5,294
Reaction score
10,970
Dar es Salaam. Biashara ya ukahaba imevamia kwa kasi baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam, na kusababisha kero na adha kubwa katika makazi ya watu, hasa eneo la Sinza kiasi cha kuzifanya baadhi ya familia kuhama nyumba, Mwananchi limebaini.

Wazazi na walezi wanasema hali hiyo pamoja na kelele zinazosababishwa na muziki unaopigwa kwenye baa kubwa vimewasababishia ugumu usizoelezeka wa malezi ya watoto.

Uchunguzi wa Mwananchi umebaini biashara hiyo imekithiri katika mitaa mingi ya Sinza, hasa ile inayozunguka kumbi maarufu za starehe na hoteli kubwa.

Hali hiyo inayomulikwa kwa Sinza, ipo pia maeneo mengine kama Tabata, Ubungo, Kindondoni Buguruni na kwingineko, japokuwa ni kwa viwango tofauti.

Kutokana na hali ilivyo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe hivi karibuni alikutana na watendaji na wenyeviti wa mitaa ili kujadili mambo mbalimbali, likiwemo la biashara hiyo huku akiwataka viongozi wa dini kulikemea suala hilo akisema utamaduni huo si wa Tanzania.

Wakazi wa maeneo husika wanasema mbali na kuwaletea changamoto ya malezi, hali hiyo imewalazimisha kubadili mifumo ya maisha ili kuzilinda familia zao.

“Nimelazimika kuhamia Goba kuwakwepa ‘madada poa’ na kelele za usiku kucha. Jirani na nyumba niliyokuwa naishi na familia yangu kuna gesti wanayotumia hao madada poa. Wanavuta bangi usiku kucha na asubuhi tunapotoka tunakuta kondomu zimetapakaa hadi magetini kwetu.

“Wakati mwingine wateja wao wanapaki magari yao kwenye uzio wa nyumba zetu na kuyatumia kufanya mapenzi badala ya kwenda gesti. Tumeripoti sana polisi hatuoni nafuu yoyote,” anasema Ally Mohamed aliyekuwa akiishi katika nyumba moja, nyuma ya baa ya Meeda, maarufu kama Kitambaa Cheupe.

Anaongeza kuwa “changamoto ya kulea watoto kule ilikuwa kubwa kwa kuwa akirudi saa moja usiku anakuta tayari (madada poa) wamejipanga mtaani, wakiona gari wanajiachia uchi, kumbe mtu unakwenda nyumbani akiwa na watoto.”

Mohamed anasema baadhi ya familia, kama ilivyo kwake, zimehama kuepuka kero na adha za ukahaba pamoja na kelele zinazotoka kwenye kumbi za starehe.
 
Pole zao..kimsingi sio vzr kulea watoto katika mazingira hayo.

#MaendeleoHayanaChama
 
Watu wa Dar ni Wanafiki.

Mkiambiwa kuhama kupisha shughuli za maendeleo mnaandamana na kelele haziishi...leo eti Makahaba wanawahamisha.
 
Tatizo wanaopaswa kushughulikia tatizo la makahaba na wao huenda ni wateja wa makahaba hao!! Ni sawa na kupeleka kesi ya ngedele kwa nyani ukimshitaki kula mahindi shambani kwako, wakati ngedele alikuwa na nyani wakila mahindi hayo!

NAPENDEKEZA: Wakuu wa wilaya zote za Dar wawe wanawake. Makamanda wote wa polisi mikoa yote ya kipolisi Dar wawe wanawake. Wakuu wa vituo vyote vya polisi wawe wanawake. Hao wote chini ya mkuu wa mkoa wa Dar MWANAUME bila shaka watafanya kazi nzuri!
 
Wanao paswa kukomesha hiyo hali nao ni wateja wa hao makahaba, nawambieni hali hiyo sio dar tu ni kote nchini, kwa sasa kulea watoto imekuwa ni mtihani mzito makahaba kila mahali, hakuna anayejali.
 
Angewapiga picha na video halafu akasambaza mtandaoni. Kama unasumbuliwa na vitu kama hivi, piga picha na video za wateja wa hao makahaba na namba zao za magari halafu ziweke Twitter, Insta, JF, Tik Tok, kila mahali.
 
Wanao paswa kukomesha hiyo hali nao ni wateja wa hao makahaba.. nawambieni hali hiyo sio dar tu ni kote nchini, kwa sasa kulea watoto imekuwa ni mtihani mzito.. makahaba kila mahali, hakuna anayejali
Huku mitaa ya kwetu, mtoto wa miaka 12 anakuuzia papuchi, na mama yake anagawa mbususu! Baba mtu ananunua papuchi ya mke wa jirani yake! Yaani ni vurugu bin Vurugu!
 
NAPENDEKEZA SULUHISHO: Iwe ni marufuku mtu kuonekana hadharani iwe usiku au mchana akiwa amavalia mavazi ya kikahaba!! Tukubaliane kuwa:
1. Hadharani maana yake ni mbele ya watu wengine. Hata kwenye kumbi za starehe ni hadharani! Hata kwenye bar na vilabuni ni hadharani!!
2. Mavazi ya kikahaba ni:
* Vazi lolote la kike ambalo halifiki nchi 6 chini ya magoti.
* Vazi lolote ambalo mpasuko wako wa nyuma unazidi sehemu ya mgoti na kuonesha mapaja wakati mhusika anatembea.
* Vazi lolote lililochanwa kwenye sehemu ya mapaja hivyo kuonesha mwili kupitia michaniko hiyo.
* Vazi lolote linaloonesha sehemu ya matiti/maziwa ya mwanamke. Ule mfereji unaotenganisha matiti/maziwa ya
mwanamke haupaswi kuonekana
* Vazi lolote linaloshikamana na mwili/linalobana mwili kiasi cha kutokutenganisha mwili na vazi (skin tight)
* Vazi lolote linaloacha mgongo wazi. Kusiwe na uwazi chini ya mabega.
* Vazi lolote linaloangaza/transparent na kuonesha nguo za ndani!
3. Atakayepatikana kuvaa mavazi ya kikahaba achapwe viboko hadharani.
4. Kama makahaba wanadai wako kwenye biashara, wakubali kufanya biashara zao bila kuleta kero kwa wengine. Kama makahaba nikikutana nao wakati narudi nyumbani usiku nikiwa na watoto wangu, lakini hawajavaa mavazi ya kikahaba, hakutakuwa na athari kwa wanangu!

Na wengine tuongeze makubaliano::
 
Back
Top Bottom