Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,294
- 10,970
Dar es Salaam. Biashara ya ukahaba imevamia kwa kasi baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam, na kusababisha kero na adha kubwa katika makazi ya watu, hasa eneo la Sinza kiasi cha kuzifanya baadhi ya familia kuhama nyumba, Mwananchi limebaini.
Wazazi na walezi wanasema hali hiyo pamoja na kelele zinazosababishwa na muziki unaopigwa kwenye baa kubwa vimewasababishia ugumu usizoelezeka wa malezi ya watoto.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini biashara hiyo imekithiri katika mitaa mingi ya Sinza, hasa ile inayozunguka kumbi maarufu za starehe na hoteli kubwa.
Hali hiyo inayomulikwa kwa Sinza, ipo pia maeneo mengine kama Tabata, Ubungo, Kindondoni Buguruni na kwingineko, japokuwa ni kwa viwango tofauti.
Kutokana na hali ilivyo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe hivi karibuni alikutana na watendaji na wenyeviti wa mitaa ili kujadili mambo mbalimbali, likiwemo la biashara hiyo huku akiwataka viongozi wa dini kulikemea suala hilo akisema utamaduni huo si wa Tanzania.
Wakazi wa maeneo husika wanasema mbali na kuwaletea changamoto ya malezi, hali hiyo imewalazimisha kubadili mifumo ya maisha ili kuzilinda familia zao.
“Nimelazimika kuhamia Goba kuwakwepa ‘madada poa’ na kelele za usiku kucha. Jirani na nyumba niliyokuwa naishi na familia yangu kuna gesti wanayotumia hao madada poa. Wanavuta bangi usiku kucha na asubuhi tunapotoka tunakuta kondomu zimetapakaa hadi magetini kwetu.
“Wakati mwingine wateja wao wanapaki magari yao kwenye uzio wa nyumba zetu na kuyatumia kufanya mapenzi badala ya kwenda gesti. Tumeripoti sana polisi hatuoni nafuu yoyote,” anasema Ally Mohamed aliyekuwa akiishi katika nyumba moja, nyuma ya baa ya Meeda, maarufu kama Kitambaa Cheupe.
Anaongeza kuwa “changamoto ya kulea watoto kule ilikuwa kubwa kwa kuwa akirudi saa moja usiku anakuta tayari (madada poa) wamejipanga mtaani, wakiona gari wanajiachia uchi, kumbe mtu unakwenda nyumbani akiwa na watoto.”
Mohamed anasema baadhi ya familia, kama ilivyo kwake, zimehama kuepuka kero na adha za ukahaba pamoja na kelele zinazotoka kwenye kumbi za starehe.
Wazazi na walezi wanasema hali hiyo pamoja na kelele zinazosababishwa na muziki unaopigwa kwenye baa kubwa vimewasababishia ugumu usizoelezeka wa malezi ya watoto.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini biashara hiyo imekithiri katika mitaa mingi ya Sinza, hasa ile inayozunguka kumbi maarufu za starehe na hoteli kubwa.
Hali hiyo inayomulikwa kwa Sinza, ipo pia maeneo mengine kama Tabata, Ubungo, Kindondoni Buguruni na kwingineko, japokuwa ni kwa viwango tofauti.
Kutokana na hali ilivyo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe hivi karibuni alikutana na watendaji na wenyeviti wa mitaa ili kujadili mambo mbalimbali, likiwemo la biashara hiyo huku akiwataka viongozi wa dini kulikemea suala hilo akisema utamaduni huo si wa Tanzania.
Wakazi wa maeneo husika wanasema mbali na kuwaletea changamoto ya malezi, hali hiyo imewalazimisha kubadili mifumo ya maisha ili kuzilinda familia zao.
“Nimelazimika kuhamia Goba kuwakwepa ‘madada poa’ na kelele za usiku kucha. Jirani na nyumba niliyokuwa naishi na familia yangu kuna gesti wanayotumia hao madada poa. Wanavuta bangi usiku kucha na asubuhi tunapotoka tunakuta kondomu zimetapakaa hadi magetini kwetu.
“Wakati mwingine wateja wao wanapaki magari yao kwenye uzio wa nyumba zetu na kuyatumia kufanya mapenzi badala ya kwenda gesti. Tumeripoti sana polisi hatuoni nafuu yoyote,” anasema Ally Mohamed aliyekuwa akiishi katika nyumba moja, nyuma ya baa ya Meeda, maarufu kama Kitambaa Cheupe.
Anaongeza kuwa “changamoto ya kulea watoto kule ilikuwa kubwa kwa kuwa akirudi saa moja usiku anakuta tayari (madada poa) wamejipanga mtaani, wakiona gari wanajiachia uchi, kumbe mtu unakwenda nyumbani akiwa na watoto.”
Mohamed anasema baadhi ya familia, kama ilivyo kwake, zimehama kuepuka kero na adha za ukahaba pamoja na kelele zinazotoka kwenye kumbi za starehe.