Biashara ya ukahaba imekithiri Sinza na kusababisha wakazi kuhama nyumba zao

Biashara ya ukahaba imekithiri Sinza na kusababisha wakazi kuhama nyumba zao

Haina sera za kueleweka za mipango miji! mfano kutenganisha maeneo ya starehe, ibada, nyumba za kulala wageni, nk. kutoka kwenye maeneo ya makazi ya watu.

Una swali lingine?

Ni kama ilivyokuwa kwa kule jijini Dodoma. Mamlaka ya Jiji wakati ule (CDA) walilipanga vizuri na maeneo ya makazi kuzingatia utulivu na heshima. Ila kwa sasa ile mandhari ya Magomeni, Sinza nk. imehamia kule.

Eneo la kisasa lilikuwa mahsusi kwa makazi sasa ni baa, grocery na vurugu kama hizo kila kona.

Kwenye mipango miji nchi hii tumefeli.
 
Sasa viongozi wa dini watakemeaje makahaba wasio na dini?
Hawa makahaba sehemu kubwa wana dini! Ni waislamu na wakristo hawa na hawakosi misikitini na makanisani siku ya ijumaa na jumapili!!! Kwa hiyo inabidi dozi ya kukemea ukahaba iwepo kwa wingi huko misikitini na makanisani!! Utakuta mtoto wa kike anatoka nyumbani kajifunika baibui lakini kwenye begi kuna kivazi cha kazi!! anaporudi nyumbani anaingia tena kwenye baibui lake na akifika nyumbani anawasalimia wazazi na "salamaleku" !!!
 
Ni kama ilivyokuwa kwa kule jijini Dodoma. Mamlaka ya Jiji wakati ule (CDA) walilipanga vizuri na maeneo ya makazi kuzingatia utulivu na heshima. Ila kwa sasa ile mandhari ya Magomeni, Sinza nk. imehamia kule.

Eneo la kisasa lilikuwa mahsusi kwa makazi sasa ni baa, grocery na vurugu kama hizo kila kona.

Kwenye mipango miji nchi hii tumefeli.
Kule dodoma maeneo ya "chako ni chako" ni hatari!! Kila siku wanakesha kabisa!! Zamani makabila yaliyokuwa yamebobea kwenye ukahaba yalikuwa machache kama wah*y*, lakini sasa hakuna kuchekana, makabila yote yametumbukia huko hata wah*y* chini sana kwenye ligi hiyo na wako karibu kushuka daraja!! Nawapongeza!!
 
Laana ya kuharibu chaguzi za 2019 na 2020. Ngoja maridhiano yaendelee labda Mungu atatuonea huruma tena Kama terehe 17/3/2021. Sijui ingekuwaje kama tungeendelea kuwa zama za giza mpka mda sasa.
Siyo kweli, kwani hukuwahi kuwaona wale "wapinzani" wakiwa nadhani mahakamani lakini wanapeana namba za simu!!
 
Ila tuambizane ukweli humu, wazazi wameshindwa sana kutimiza wajibu wao katika malezi ya watoto!! mtoto wa kike unamwona anavaa uchi uchi hata mbele yako unategemea nini! Kina mama ndio kabisaa!!! mtoto uchi uchi na mama uchi uchi!!
 
NAPENDEKEZA SULUHISHO: Iwe ni marufuku mtu kuonekana hadharani iwe usiku au mchana akiwa amavalia mavazi ya kikahaba!! Tukubaliane kuwa:
1. Hadharani maana yake ni mbele ya watu wengine. Hata kwenye kumbi za starehe ni hadharani! Hata kwenye bar na vilabuni ni hadharani!!
2. Mavazi ya kikahaba ni:
  • Vazi lolote la kike ambalo halifiki nchi 6 chini ya magoti.
  • Vazi lolote ambalo mpasuko wako wa nyuma unazidi sehemu ya mgoti na kuonesha mapaja wakati mhusika anatembea.
  • Vazi lolote lililochanwa kwenye sehemu ya mapaja hivyo kuonesha mwili kupitia michaniko hiyo.
  • Vazi lolote linaloonesha sehemu ya matiti/maziwa ya mwanamke. Ule mfereji unaotenganisha matiti/maziwa ya
mwanamke haupaswi kuonekana
  • Vazi lolote linaloshikamana na mwili/linalobana mwili kiasi cha kutokutenganisha mwili na vazi (skin tight)
  • Vazi lolote linaloacha mgongo wazi. Kusiwe na uwazi chini ya mabega.
  • Vazi lolote linaloangaza/transparent na kuonesha nguo za ndani!
3. Atakayepatikana kuvaa mavazi ya kikahaba achapwe viboko hadharani.
4. Kama makahaba wanadai wako kwenye biashara, wakubali kufanya biashara zao bila kuleta kero kwa wengine. Kama makahaba nikikutana nao wakati narudi nyumbani usiku nikiwa na watoto wangu, lakini hawajavaa mavazi ya kikahaba, hakutakuwa na athari kwa wanangu!

Na wengine tuongeze makubaliano::
Sijui hata unaongea nini!!
[emoji848][emoji848][emoji848]
Wengine raha yetu ni fahari ya macho!
 
Sijui hata unaongea nini!!
[emoji848][emoji848][emoji848]
Wengine raha yetu ni fahari ya macho!
Hiyo fahari ya macho utaifanyia faraghani!! Mchukue akiwa kavaa vizuri kama unataka, ukifika huko faraghani akuvalie unavyotaka. Lakini fahari yako ya macho ni kero kwa wengine!!
 
Haya yote ni matokeo ya sera mbovu za serikali ya CCM.
Wananufaika na matatizo ya wananchi. Wachache Wana kipato kikubwa, wengi ni maskini wa Kutupwa.

KATIBA mpya itasaidia kuondoa TATIZO Hilo sababu, tulitoa maoni ktk Rasimu mkt akiwa Warioba, kwamba Katiba mpya ipendekeze njia Bora za kupunguza gap kati ya maskini na matajiri.

Mf Mikopo ifike Kwa walengwa kuwakwamua ktk umaskini Si kama sasa utaskia Bungeni, wanadai vijana wamepewa mikopo ktk vikundi kumbe MAKADA wamegawana.
 
Kenya , South Africa, Dubai, UK, USA kote kuna madada poa, huko ni CCM pia?
Sie hatuishi Kenya au s.afrika, TANZANIA tuna miiko yetu na utamaduni wetu.

Sisi ni Watanzania, usihalalishe UOVU, CCM ni WA kulaumiwa Kwa kila baya Kwa kuwa wanatoa watu wanaofanya maamuzi Kwa niaba yetu. Amen
 
Kenya , South Africa, Dubai, UK, USA kote kuna madada poa, huko ni CCM pia?
issue hapa si chama bali ni maadili,tutafakari wapi tumeangukia na tujisahihishe.hao ni watoto wetu na ni dadai zetu hivyo wazazi tujiulize wapi tumefeli ktk jukumu letu la kuwalea ktk maadili mema.
 
Wananufaika na matatizo ya wananchi. Wachache Wana kipato kikubwa, wengi ni maskini wa Kutupwa.

KATIBA mpya itasaidia kuondoa TATIZO Hilo sababu, tulitoa maoni ktk Rasimu mkt akiwa Warioba, kwamba Katiba mpya ipendekeze njia Bora za kupunguza gap kati ya maskini na matajiri.

Mf Mikopo ifike Kwa walengwa kuwakwamua ktk umaskini Si kama sasa utaskia Bungeni, wanadai vijana wamepewa mikopo ktk vikundi kumbe MAKADA wamegawana.
....
 
ZAMANI SINZA ILIKUNI FAHARI KUPANGA NYUMBA, KWA SBB YA UWEPO WA WASOMI.
SIKU HIZI NI MAKAZI YA NYUMBA NDOGO NA MAKAHABA NA MASHOGA NA WALEVI NA MATAPELI
 
Back
Top Bottom