Biashara ya Vifaa vya Ujenzi (Hardware Store): Ushauri wa Mtaji, Uendeshaji, Changamoto na Faida

Wanaopata faida kubwa ni watu wanaochukua mzigo mkubwa kwa kufunga ktk containers..kama mjuavyo nchi ya qatar wanaandaa world cup hivyo hotels..viwanja na infrustructures nyingi vinajengwa hivyo kwa sasa cement ipo kwenye high demands jana niliuliza bei ya cement kwa hapa dubai imepanda kufikia tsh 4000 kwa mfuko na bei ya tiles imepanda grade A ni tsh 10,000 kwa box lenye tiles 13 na tsh 7000 grade B lenye tiles 13..visa ya dubai ni rahisi sana maana ata airlines kama emirates wanawezakukupatia
 
mkuu ubarikiwe sana ungekuwa na mimi hapa kijijini ningekupa mbege kidogo na kusema ria see meku nikiwa na maana kunywa tena .aika sana mono mangi.nitaifuatilia by kesho nitakupa mrejesho
 



Mkuu me nilikua nataka nishushe angalau container tatu za cement lakini najaribu kufanya research bado naumwa na kichwa, hata hivyo labda inawezekana kuwa unawajua maagent ambao wanauza cement kwa urahisi zaidi hapo dubai na vitu vyengine vya ujenzi naweza vyengine kutoa turkey, mkuu kama utanipatia email yako nitakupa yangu kwa private kule ili tuwasiliane zaidi ama kama uko poa nipatie yako hapa nianze kufikiria safari ya dubai kwanza.
 

All talk lakini reality zero,kwa akili yako unamwambia mtu anunue cement for 14,000Tshs kwa ajiri ni ya TZ wakati kuna ya 4000Tshs kutoka dubai,mkuu hakuna uzalendo kwa kutiana hasara za kipuuzi hizo,na hakuna uzalishaji kwa sababu umeme na kodi ni bei ya kufa mtu sio watu hawataki kuzalisha vya kwetu...ni Economics tuu hapo na usilete siasa
 
naona wakuu mnachangia tu ila mmesahau kuna kodi ya kuingiza nchini na makato mengine yakulinda viwanda vya ndani! ambayo ukipiga inaweza kuwa the same kama hapa bongo!
 
Tatizo bongo kodi mzigo mzito yan haingii akilini juisi ya azam kuuzwa 3000 na ceres an import 2500 nkt ilibidi hiyo ya ndan ndo iwe buku 2000 au pungufu ukiuliza mr tax man huyo
 
Nataka kufungua biashara ya duka la vifaa vya ujenzi naomba ushauri ni mtaji wa kiasi gani ni nzuri kuanzia na eneo gani ni zuri kibiashara.
 
Eneo lenye wajenzi. Kama wanajenga nyumba za udongo basi weka bidhaa zinazoendana na nyumba hizo; kama wanajenga magorofa hali kadhalika. Mtaji utalingana na aina ya vifaa unavyoweka.
 
Nataka kufungua biashara ya duka la vifaa vya ujenzi naomba ushauri ni mtaji wa kiasi gani ni nzuri kuanzia na eneo gani ni zuri kibiashara.

Usione uzi hauchangiwi ukadhani unachuniwa,tatizo unahitaji ushauri wakati hutaki kutoa maelezo ya kutosha kama vile;
Uko mkoa gani,una mtaji kiasi gani, Aina ya soko unalo target, Usimamizi wako utakuwaje etc

Mfano; Kuna tender nyingi za ku supply nondo kwa Wachina wanaojenga barabara Tabora; Ushauri huu unaweza usiwe msaada kwako kwani hujulikani ulipo, mtaji wako haujulikani ni kiasi gani, uwezo wako wa kuhimili credit sales ukoje.

Weka maelezo ya kutosha utapata ushauri wa kukusaidia.
 
Asante kwa ushauri wako millions movement. Niko Dar na mtaji ni sh. 20m pesa ya frem ni tofauti. Nataka kuweka vifaa mchanganyiko vya ujenzi. Ushauri kuhusu eneo p/s na usimamizi nitakuwa mwenyewe.
 
mkuu acha kumkatisha tamaa anaweza kuanza na mtaji mdogo lkn akiwa makin nao atatoka

Mkuu unajua hata mimi nimemwogopa huyo jamaa anayetaka kukatisha tamaa watu!

Siyo lazima mtu uanze na 60m kwenye hii biashara. Mkuu dunduliza kidogo kidogo utafanikiwa. Ikishakuwa na mwaka mmoja usiogope kwenda benki kukopa mtaji zaidi ili uiendeleze, watu wasikiutishe hao ni wale wanaotaka utajiri wa haraka haraka. Mimi nilianza na 7.5m nililipwa mchango wangu wa nssf baada ya kuacha kazi mahali sasa hivi biashara imekuwa wala huwezi amini kama nilianza na mtaji mdogo kiasi kile.

Kikubwa Mkuu usijelifanya hilo duka kuwa ndo kila kitu, yaani chakula humo humo, watoto kwenda shule humo humo kwa kweli hautafikia mbali. Lakini kama utakuwa na shughuli nyingine tuseme labda una kibarua mahali ambacho ndo kitakuwa kinakutimizia mahitaji mengine basi hapo utaenda tu! Baada ya miaka miwili hutakaa uamini macho yako.

Songa mbele mkuu na hiyo biashara wala usirudi nyuma!!
 
Ushauri wako job k ni mzuri, pia kumbukeni Unaposema Hardware ni pana sana hasa kwenye miji mikubwa inaweza gawanyika zaidi ya mara tatu, mfano Kariakoo Dar yapo maduka ya (Gypsum products board,powder, Hardboard, Belts, chip boards,marine boards,chokaa Rangi zote, tiles n.k) group la pili (bati,bomba maji, mabomba yote,flat bars sq pipies nondo,steel sheets, Glasses, wire mesh, hardboards,misumari, tiles,) tatu (patasi,nyundo,misumari,kufuli, gundi mbao, dawa mbao, pvc sheet,bawaba tape maji) huo ni mfano tu unaweza tofautisha hardware ndg ndg na pia hardware kubwa kubwa wapo watu wanauza aina zote za cement na chokaa tuuuu kwa hardware ndg ndg mtaji hata wa 5 mln unatosha sana hasa ukiwa karibu na mafundi wa vitu hivyo lakini kama ni kubwa mfano ya cement roli moja tu mikoani 10 mln na zaidi kwa hiyo wote muko sawa wa 60 mln na pia 7 mln

Mkuu kama ni HARDWARE kubwa tuwasiliane nitakupa data zote niko kwenye hiyo zaidi ya miaka 20, naijua vema ndogo hapana siijui
 

mkuu mi hii ndyo shuhuli yng nawafanyia shopping wadau walioko mikoan wanatumia pesa nawanunulia mzigo kisha nawatumia nina wadau mpk zambia km utakuwa na interest pliiz ni pm khs uaminifu ndyo key yng ktk hii biashara ucwe na hofu
 
CONSULT nami pia napenda kuwasiliana nawe. xsadala@gmail.com
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…