Biashara ya vipuri vya pikipiki: Ushauri, michango, mawazo

Biashara ya vipuri vya pikipiki: Ushauri, michango, mawazo

ImageUploadedByJamiiForums1415996356.496133.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996384.822694.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996459.170176.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996512.537167.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996543.184578.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996633.352271.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996729.404654.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996810.792078.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996857.842540.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996955.097581.jpgImageUploadedByJamiiForums1415996729.404654.jpg
 
WAWA ni tairi ya uhakika inakupa hadi kilometa 35000 kabla ya kutoa nyuzi. Ina viwango (TBS) na guarantee ..
 
Wadau ni wapi naweza pata spea za pikipiki kwa bei nafuu kwa jumla?Mi niko chato.naomba mawasiliano kwa wahusika ili niweze kuwasiliana nao nijue bei zao.
Wenu katika ujasilia mali
Mdau.
 
Sokoni Kariakoo. Wapo suppliers wakubwa. Sina Mawasiliano yao,naamini kuna Wadau watakuja nayo hapa
 
nenda kwa Said pale aggrey/Uhuru jamaa DSM mzima anakimbiza ukienda maduka mengi ya vifaa vya pikipiki au bajaji kama hawana wanakuambia nenda kwa said,kama hana kupata tena ishu,sina namba yake ila nitatafuta
 
Njoo ununue kwangu hiyo inatosha! teh teh!
 
Yah! Asante.
Karibu Sikukuu/Amani tuongee kaka pia no. Yangu ni 0658131333. Pia iko kwenye whatsapple .
 
Habari ndugu,
Kwa wakat mwingi nimekuwa nikitamani sana kufungua duka la spare za pikipiki lakini bahat mbaya nimekosa taarifa zaidi kuhusu biashara hii,namna gani nitapata bidhaa na je mtaji wa chini wa kuanzia ni kiasi gan.nitashukuru kama nitapata mwongozo kutoka kwenu
 
Habari ndugu,
Kwa wakat mwingi nimekuwa nikitamani sana kufungua duka la spare za pikipiki lakini bahat mbaya nimekosa taarifa zaidi kuhusu biashara hii,namna gani nitapata bidhaa na je mtaji wa chini wa kuanzia ni kiasi gan.nitashukuru kama nitapata mwongozo kutoka kwenu

Wazo zuri mimi cha kukushauri ni hivi kama unategemea kuifanya mwenyewe kama sehemu yako ya kujipatia mkate wa kila siku,tafuta sehemu wanayouza vifaa hivyo omba kufanya kazi ya kuuza pamoja nao free of charge.
Uwe muwazi kabisa lengo la kutaka kufanya nao ni nini.Uwaombe usihusike na kushika fedha wewe ni kuongea na wateja na kujua zaidi aina ya spares.Naamini hapo hapo utaanza kufahamu njia gani wanatumia kupata mzigo namna gani wanapata wateja na vitu kadha wa kadha.
Ni mawazo yangu
 
Upo mji/mahali gani? unataka kuuza kwa jumla au rejareja? tuanzie hapo.
 
kuna web ya mkenya mmoja ilikua na taarifa zote,mpaka adress za wholeseller pamoja na bei za spare,alikua anaresearch na kuuza infor.unamtumia mpesa yeye anakuwekea infor kwenye email.

nimeimissiplace sijui wapi.nikiipata ntakuwekea
 
Wazo zuri mimi cha kukushauri ni hivi kama unategemea kuifanya mwenyewe kama sehemu yako ya kujipatia mkate wa kila siku,tafuta sehemu wanayouza vifaa hivyo omba kufanya kazi ya kuuza pamoja nao free of charge.
Uwe muwazi kabisa lengo la kutaka kufanya nao ni nini.Uwaombe usihusike na kushika fedha wewe ni kuongea na wateja na kujua zaidi aina ya spares.Naamini hapo hapo utaanza kufahamu njia gani wanatumia kupata mzigo namna gani wanapata wateja na vitu kadha wa kadha.
Ni mawazo yangu

thankx brother kwa ushaur wako na mawazo.nitafanyia kazi
 
Wakuu heshima kwenu,

Baada ya kupita pilikapilika za uchaguzi, sasa tuachane nazo, maana watanzania hawataki mabadiliko, kila mmoja atakura kwa ulefu wa akiri zake.

Wakuu naomba mwenyeuzoefu wa hii biashara ya kuuza vifaa vya pikipiki, naomba anisaidie.

Je, mtaji wa milioni moja utafaa?

Vifaa gani muhimu kwenye duka?

Je, faida yake inakuaje, na hasara zake inakuaje na changamoto zake pia?

Mimi naishi Kimanzichana mkoa wa Pwani.

Asante
 
Back
Top Bottom