Biashara za mitandao (kuunganishana) zinavyowaliza first year vyuoni

Biashara za mitandao (kuunganishana) zinavyowaliza first year vyuoni

Qnet ni mwendo wa kupigwa tu, na ukipigwa inabidi ukomae na wewe kutafuta wengine wa kuwapiga.

Good morning!!!!
 
Hawa ni kukaa nao mbali kabisa
Hao jamaa wa aina zote kuanzia GNLD, Qnet, Forever living etc wamenikaribisha, nimeshawahi kushawishiwa na watu wenye elimu na nyadhifa nijuliunge, ila issue moja in common niliona ni kuwa HAWAKUAMBII SPECIFICALLY unalipwaje.

Niliwashukuru na kuwaambia "waendelee" kutajirika mimi WANIACHE TU na ninacho pata kwa means zangu ambazo zinaeleweka![emoji23][emoji23]
 
Duh [emoji2811]
Soon na wewe utakuwa muhanga wakitaka na wewe ujiunge, na naamini utaleta mrejesho hapa.
Aaah wapi mkuu mimi hawatanipata🤣🤣🤣,

Ila nilitaka kujua tricks zao hasa ziko wapi ili nikiongea na shemeji yangu na sister wangu niwape facts za ubaya wa hiyo network business
 
Kuna jamaa alinishawishi nijiunge , nikamchana live mi borntown kitambo hizo mambo ni ujanja ujanja tu akadai we ngoja uone baada ya muda fulani nitakuwa napiga hela za maana. Nikamjuza time will tell, sasa ushapita mwaka na ushee kila tukitana ana sura ya majonzi tu
 
Huyo binti hapo ndio tayari keshalizwa na Qnet. Ndivyo inavyokuwaga hivyo.
Sasa ajipange kuwa mtumwa wa Qnet mazima, muda sio mrefu ataanza kukushawishi na wewe ujiunge ili kufidia au kurudisha au kuelekea naye kuusaka umilionea alioteshwa ndani ya ofisi za Qnet.
Pole sana kwa dada yetu, maisha ni kujifunza, na wengine hujifunza kwa kulizwa!

Qnet wamejipanga sana kuvuna pesa za watu kirahisi huku wakificha kivuli cha Pyramid scheme kwenye mwamvuli wa bidhaa na huduma fulani fulani zinazoweza kulipwa katika hiyo 4.5milioni mtu anazolipa.
Dah! Wanawaibia kirahisi sana, halafu sijui ni matumaini ya maisha mazuri au kutajirika kwa njia za mkato maana dau wanaloanzia ni kubwa.

Halafu wanawa target watoto waliotoka familia za kawaida na sio za matajiri. Wazazi wa hao watoto wanajikamua sana wakidhani wanawatengenezea watoto wao maisha kumbe kipigo
 
Asante sana mkuu nitafanya hivyo. Dakika chache zilizopita sister katoka kunipigia, kumbe kuna pesa 4.5m walishalipa kwa ajili ya degree course(undergraduate) ya online inayoendeshwa na na University moja inaitwa Quest University ipo Malaysia( ambayo ni Education Institution ya iliyo chini ya hao Qnet). Mtoto wa sister yupo UD mwaka wa kwanza sasa anataka kusoma online degree nyingine through hao Qnet

Kanitumia risiti ya hela waliyolipa bank naona kama ni malipo ya manunuzi ya commodities yaani hata haieleweki. Sasa mtoto ndio anawashinikiza wazazi wajiunge kununua products ili eti watengeneze pesa!
aisee,,pole sana.mwambie dada yako Na wewe mwenyewe mtafute taarifa kuhusu 'pyramid scheme'..mtaelewa kila kitu.
hakuna biashara hapo
 
HIZO hotel haulali bure unalipia japo Kuna discount. Nyingi zipo nje ya nchi hivyo itabidi ujilipie gharama za usafiri kwenda na kurudi, gharama za visa, chakula pamoja na usafiri wa ndani ukiwa huko nje. Aidha utajilipia matibabu au bima pamoja na gharama nyingine zote.
Wala usipate shida, hapa hapa nitatoa maelezo ya QNET wanavyofanya kazi zao, maana wapo jamaa kadhaa waliingia mkenge kujiunga huko wakalizwa hatari.
-Kifupi kabisa, msingi wao mkuu ni ule ule kama Forever Living, Alliance in motion nk, zote ni PYRAMID SCHEME (Yaani wachache wanaotangulia kujiunga wanavuna zaidi kupitia migongo ya wengine wengi wanaofuata nyuma yao katika mnyororo) Katika hilo hakuna tofauti.
-Kuna gharama(mtaji) wa chini wa kujiunga, ambazo kwa sasa ni zaidi ya shilingi 4.5milioni. Bila hicho kiasi kukilipa kwa mara moja huwezi kujiunga na QNET. Wao watakwambia sio gharama za kujiunga bali ni pesa yako unayotumia kununua bidhaa au huduma za Qnet! (Hapo utaambiwa bidhaa zenyewe ni Saa ya mkononi, Pafyumu, kulala kwenye hoteli kali ya kitalii huko Asia nk.)
-Kamwe hawatakwambia kinagaubaga biashara yao kirahisi mtaani, lazima watakuita uje kwenye ofisi zao(ndani ya chumba maalum!), hapo watajipanga watu kadhaa kukufanyia 'brain washout' na kukupa maelezo marefu mazuri na matamu ya kukufanya uwe milionea kupitia Qnet kwa muda mfupi na bila kuhangaika kabisa, na hicho kitu watakifanya kwa ustadi mkubwa sana, kwa hatua au siku kadhaa kabla ya kukwambia utoe pesa kujiunga. (Wakati wote huo watakwambia hiyo ni secret opportunity, usiulize mtu mwingine yoyote wala kusema sema kwa watu ovyovyo!).
-Sasa ukishajiunga tu na Qnet kwa kutoa zaidi ya 4.5milion ndio akili inafunguka na kujua kuwa umelizwa au kugundua kuwa umelionea siyo kitu kirahisi kabisa, sasa mtu ndio anahangaika kutafuta 'wajinga' wengine kadhaa ili wajiunge kwenye mnyororo wake ili kuanza kufidia kile ulicholizwa, na hapo inakuwa ni suala la kufa na kupona.
Kwa leo niishie hapa......
 
Kimsingi kila mtu ajue hakuna utajiri kirahisi rahisi. Wote tukatae hizo biashara za network marketing. Pia kuna hao wanaojiita LIFE COACHES hawako mbali na huu upuuzi wa network marketing.
 
Wengi tuliponda ile kitu inaitwa Bitcoin...any way kuna mtu mmoja amenisanua kuhusu S Block uzuri ama bahati mbaya app imekataa kufanya kazi kwenye Simu yangu.
 
Mimi huwa hata siwapi dk 1 yakuwasilikiza mataepeli Wakubwa hao
 
Wakati namaliza chuo ndio hizi biashara zilikuwa zinaingia kwa kasi na vile tulikuwa tunasomea afya waliteka sana watu pale chuoni

Katika maisha haya nimejifunza kuwa na makini sana na pesa yoyote inayoonekana kupatikana kirahisi.

Ukitoa sports betting za mipira hii ndio njia ambayo mtu anaweza kupata million mia na kuliwa million mia kwa dakika [emoji23][emoji23]

Jamaa alikuwa ananilazimisha kuniuzia dawa ya meno ya aloe vera mara sijui sabuni mara sijui biashara inalipa sana nikajiunge

Aliishia kunichunia na kuona sitaki kumpa sapoti katika maendeleo yake
 
Habari, karibu ndugu msomaji Leo tutaangazia kwa uchache namna biashara za kuunganishana ( biashara za mitandaoni kama wanavyoziita wao)
Hizi sio zile zakuuza bidhaa online kama wafanyavyo Al-Baba, Amazon, E-bay au jumia Bali hizi nizamifumo ya kuunganishana na zitakuwa pyramid in shape yani nikijiunga Mimi nakushawishi na wewe unajiunga chini yangu.

Kwa baadhi ya nchi ni haziruhusiwi na niharamu, kama ilivyo kwa michezo ya kubahatisha, na hata matangazo yake hayaruhusiwi kutangazwa katika vitengo vya matangazo ya mitandao mikubwa kama Facebook ads na google AdWords.

Unachotakiwa kufanya nikujiunga na kisha kutafuta watu wakujiunga chini yako na Mara nyingi kiasi cha kujiunga huwa nikikubwa hadi kufikia 600,000+

Ukishajiunga unaanza kuhangaika kutafuta watu wakuwaunganisha na kuwadanganya kama ulivyo danganganywa. Simaanishi kuwa ni utapeli Bali ni mfumo mgumu na unaoumiza na unaendeshwa kwa uongo yani nilazima udanganye ili upate wafuasi mfano " nimejiunga Nina wiki mbili maisha yangu yamebadilika kabisa na hapo umevaa suti yakuazima na hujui Utakuta nini maana siwashachomoka na na Laki zako haha!

Sasa hawa jamaa wamejikita sana vyuoni na kuwasubiri wale mwaka wakwanza ili kuwaingiza mkenge na kuwaacha wakilia.
Ushawishi mkubwa hutumika kuwadanganya Bila kueleza wazi ugumu wa mfumo.

Watakwambia baada ya mwezi utanunua gari. Haha!

Na mengineyo mengi kukutamanisha. Ukisha jiunga sasa ndio utaanza kuonja joto yajiwe.

Wito kwa watanzania
Anayekushawishi kujiunga na kitu chochote mwambie akwambie madhara yake tuu faida utazipata kwa kutafuta taarifa zingine wewe mwenyewe.

Namshukuru sana padri simplis wa france, maana Mimi nilishawishiwa kidogo niingie mkenge lakini Huyu father alinieleza hii ni black market na anayefanikiwa ni yule wa mwanzo( jaribu kuchora pyramid utaelewa nachoeleza)

Wito kwa serikali.

Hizi biashara zinapaswa kuundiwa bodi ya udhibiti kama ilivyo betting Tena pengine yenye nguvu zaidi

Onyo Kwako usisikie maneno kuwa " Nina project nahitaji watu 20 wanafanya nao kazi hahaha! Au kuna project sijui ikishirikiana na nmb

Fanya real business utafanikiwa
Kwaheri
Share ujumbe kwa watu wako wanguvu.
"[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] acha tuu mzee kuna siku jamaa alinichota kumbe ni qnet banaa, sasa nkashangaa nimefika mchanaa lakini salamu zinazoendelea pale ni goodmorning tuuu"

IMG_20190923_013313_191.jpeg
 
Hivi mpk unaibiwa kiboya Hivyo inamaana hujifikirii...
 
Habari, karibu ndugu msomaji Leo tutaangazia kwa uchache namna biashara za kuunganishana ( biashara za mitandaoni kama wanavyoziita wao)
Hizi sio zile zakuuza bidhaa online kama wafanyavyo Al-Baba, Amazon, E-bay au jumia Bali hizi nizamifumo ya kuunganishana na zitakuwa pyramid in shape yani nikijiunga Mimi nakushawishi na wewe unajiunga chini yangu.

Kwa baadhi ya nchi ni haziruhusiwi na niharamu, kama ilivyo kwa michezo ya kubahatisha, na hata matangazo yake hayaruhusiwi kutangazwa katika vitengo vya matangazo ya mitandao mikubwa kama Facebook ads na google AdWords.

Unachotakiwa kufanya nikujiunga na kisha kutafuta watu wakujiunga chini yako na Mara nyingi kiasi cha kujiunga huwa nikikubwa hadi kufikia 600,000+

Ukishajiunga unaanza kuhangaika kutafuta watu wakuwaunganisha na kuwadanganya kama ulivyo danganganywa. Simaanishi kuwa ni utapeli Bali ni mfumo mgumu na unaoumiza na unaendeshwa kwa uongo yani nilazima udanganye ili upate wafuasi mfano " nimejiunga Nina wiki mbili maisha yangu yamebadilika kabisa na hapo umevaa suti yakuazima na hujui Utakuta nini maana siwashachomoka na na Laki zako haha!

Sasa hawa jamaa wamejikita sana vyuoni na kuwasubiri wale mwaka wakwanza ili kuwaingiza mkenge na kuwaacha wakilia.
Ushawishi mkubwa hutumika kuwadanganya Bila kueleza wazi ugumu wa mfumo.

Watakwambia baada ya mwezi utanunua gari. Haha!

Na mengineyo mengi kukutamanisha. Ukisha jiunga sasa ndio utaanza kuonja joto yajiwe.

Wito kwa watanzania
Anayekushawishi kujiunga na kitu chochote mwambie akwambie madhara yake tuu faida utazipata kwa kutafuta taarifa zingine wewe mwenyewe.

Namshukuru sana padri simplis wa france, maana Mimi nilishawishiwa kidogo niingie mkenge lakini Huyu father alinieleza hii ni black market na anayefanikiwa ni yule wa mwanzo( jaribu kuchora pyramid utaelewa nachoeleza)

Wito kwa serikali.

Hizi biashara zinapaswa kuundiwa bodi ya udhibiti kama ilivyo betting Tena pengine yenye nguvu zaidi

Onyo Kwako usisikie maneno kuwa " Nina project nahitaji watu 20 wanafanya nao kazi hahaha! Au kuna project sijui ikishirikiana na nmb

Fanya real business utafanikiwa
Kwaheri
Share ujumbe kwa watu wako wanguvu.
Jaman mm nimebakia tu kujiunga na ALLINCE IN MOTION GLOBAL na anaenshawishi ni class mate wangu nliegraduate nae. Ananambia iko poa sana na nimehudhuria semina na mafunzo yao kibao na bidhaa zao nazijua A - Z asa nlikosa pesa tu mana ada yao ni laki 5. Jaman mpaka saiv anaendelea kunshawishi ila ni pesa tu sikuwa nazo, jaman hebu anaefaham kidogo pia nae aniokoe hapa nsitumbukie.
 
Hivi unaweza kujua kabisa kua ni wapigaji na ukaingia kwenye ofisi zao usichomoe.
Kwa mfano kwa tahadhari hii tuliyopewa hapa halafu nikaamua kwenda kujionea mwenyew kwenye hizo ofisi zao huku nikiwa najua kabisa sina nia ya kujiunga,inawezekana humo ndani mm kubadili maamuzi kweli?
Mkuu ubarikiwe sana sana hakika umepita mule mule.
Ulivyo eleza ndivyo ilivyo, mtu alie kwisha jiunga NINGUMU kukwambia ukweli maana wewe kwake tayari ni fursa ili arudishe fedha alizo zitoa na ukienda kwenye ofisi zao umeisha kama huna akili ya ziada. Wapo vizuri kwenye ushawishi.
 
Nilifanyiwa hivi tena classmate wa 4yrs! Alinipangia timu km ya mtu 6 zenye high convincing power! Kosa lao ni pale waliposema Alhamis niende tena!
Wala usipate shida, hapa hapa nitatoa maelezo ya QNET wanavyofanya kazi zao, maana wapo jamaa kadhaa waliingia mkenge kujiunga huko wakalizwa hatari.

-Kifupi kabisa, msingi wao mkuu ni ule ule kama Forever Living, Alliance in motion nk, zote ni PYRAMID SCHEME (Yaani wachache wanaotangulia kujiunga wanavuna zaidi kupitia migongo ya wengine wengi wanaofuata nyuma yao katika mnyororo) Katika hilo hakuna tofauti.

-Kuna gharama(mtaji) wa chini wa kujiunga, ambazo kwa sasa ni zaidi ya shilingi 4.5milioni. Bila hicho kiasi kukilipa kwa mara moja huwezi kujiunga na QNET. Wao watakwambia sio gharama za kujiunga bali ni pesa yako unayotumia kununua bidhaa au huduma za Qnet! (Hapo utaambiwa bidhaa zenyewe ni Saa ya mkononi, Pafyumu, kulala kwenye hoteli kali ya kitalii huko Asia nk.)

-Kamwe hawatakwambia kinagaubaga biashara yao kirahisi mtaani, lazima watakuita uje kwenye ofisi zao(ndani ya chumba maalum!), hapo watajipanga watu kadhaa kukufanyia 'brain washout' na kukupa maelezo marefu mazuri na matamu ya kukufanya uwe milionea kupitia Qnet kwa muda mfupi na bila kuhangaika kabisa, na hicho kitu watakifanya kwa ustadi mkubwa sana, kwa hatua au siku kadhaa kabla ya kukwambia utoe pesa kujiunga. (Wakati wote huo watakwambia hiyo ni secret opportunity, usiulize mtu mwingine yoyote wala kusema sema kwa watu ovyovyo!).

-Sasa ukishajiunga tu na Qnet kwa kutoa zaidi ya 4.5milion ndio akili inafunguka na kujua kuwa umelizwa au kugundua kuwa umelionea siyo kitu kirahisi kabisa, sasa mtu ndio anahangaika kutafuta 'wajinga' wengine kadhaa ili wajiunge kwenye mnyororo wake ili kuanza kufidia kile ulicholizwa, na hapo inakuwa ni suala la kufa na kupona.


Kwa leo niishie hapa......
 
Back
Top Bottom