Fall Army Worm
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 19,355
- 14,408
Imani za hivi huwa sizikubali.Sasa km Maagano yanakuwa na nguvu kuna Sababu gani ya Kumpokea Yesu?,Ina Maana Kazi ya Yesu Kristo kufa msalabani ni ipi sasa?.Huu upuuzi waambie wasiojua nguvu ya Msalaba wa Yesu na damu yake aliyoimwaga msalabani.Ulimwengu wa Roho wa giza unamambo mengi sana...
Kama watu wangefunuliwa waone wangeweza kukwepa hali kama hiyo...
Tatizo watu Bado wanaamini uchawi/mizimu na ushirikina ..
Maagano yake ni magumu sana, unaweza usione Leo ila kizazi chako kitaipata...
Watu wengi wanateseka na maagano yaliyowekwa na wazazi wao au ukoo...
Inaumiza sana wapumzike kwa amani , this is so devastating
Bibi harusi mtarajiwa, Rehema Chao (37) na mama yake mzazi, Agness Chao (75) wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Raum kugonga lori.
Ajali hiyo iliyotokea baada ya Rehema aliyekuwa dereva wa gari hilo kukwepa shimo na kugongana na lori, pia imesababisha kifo cha mfanyakazi wa ndani wa mdogo wake, Irene Shija (15), huku wanafamilia wengine wawili wakijeruhiwa.
Ajali hiyo ilitokea jana Novemba 28,2023 katika eneo la Kichwa cha Ng'ombe, wilayani Mwanga, wakati Rehema akitokea mkoani Morogoro kwenye sherehe ya kuagwa (send-off) iliyofanyika Novemba 24,2023.
Rehema aliyekuwa mwalimu wa Shule ya Sekondari Sua, mkoani Morogoro alikuwa akirejea nyumbani kwao Marangu, Moshi akiambatana na familia yake kwa ajili ya maandalizi ya harusi iliyopangwa kufungwa Desemba 2,2023 mkoani Arusha.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alithibitisha ajali hiyo akisema wanamshikilia dereva wa lori, Joachim Meela (37) kwa mahojiano zaidi.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Abdallah Mwaipaya, amewataja majeruhi kuwa, Veronika Chao (35), mdogo wa Rehema ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Nguzo Mbili, Geita na mwanaye, Jayden Erasto (2).
"Jana kulitokea ajali katika wilaya yetu ya Mwanga, iliyosababishwa na magari mawili, lori aina ya Scania lililokuwa likiendeshwa na mkazi wa Moshi likitokea Arusha kwenda Dar es Salaam lililogongana na Toyota Raum likitokea Morogoro kwenda Marangu,” amesema.
Mwaipaya amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Kisangara, wilayani Mwanga, huku majeruhi wakiendelea na matibabu katika kituo hicho.
Ndugu, marafiki wanena
Ndugu wa marehemu, Elielisa Kombe ameiambia Mwananchi Digital kuwa, harusi ya Rehema ilikuwa ifanyike Oldonyosambo, mkoani Arusha.
Kombe amesema gari lililokuwa na watu watano wa familia moja, wakazi wa Msae Nganyeni, Marangu lilipata ajali wakati Rehema akikwepa shimo.
"Gari lilikuwa na watu watano, mama na watoto wake wawili, mjukuu na msichana wa kazi, ni majonzi makubwa kwa familia," amesema Kombe.
Amesema wamepanga maziko kufanyika Jumamosi, Desemba 2,2023. Amesema wanaendelea na vikao kwa kuzishirikisha pande zote mbili.
"Tunaendelea na vikao kwa sasa, kesho ni lazima tukae pande zote mbili, upande wa waoaji na sisi, lakini tunatarajia kuzika Jumamosi," amesema.
Happyness Msacky, mwalimu mwenzake na Rehema katika Shule ya Sekondari Sua, amesema wamepokea kwa masikitiko msiba huo.
Amesema walikuwa wote siku ya sherehe wakifurahi pamoja na mtumishi mwenzao.
"Msiba huu umetuuma sana, Rehema alikuwa na familia yake, yeye ndiye alikuwa dereva. Hili ni pigo kubwa kwa familia, hatuna cha kusema zaidi ni kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu," amesema.
Mwananchi
Unakwepa shimo kuzuia boll joint isiharibike unalenga uso wa lory. Dereva wa masafa wanaelewa kilichotokea hapo
Bibi harusi mtarajiwa, Rehema Chao (37) na mama yake mzazi, Agness Chao (75) wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Raum kugonga lori.
Ajali hiyo iliyotokea baada ya Rehema aliyekuwa dereva wa gari hilo kukwepa shimo na kugongana na lori, pia imesababisha kifo cha mfanyakazi wa ndani wa mdogo wake, Irene Shija (15), huku wanafamilia wengine wawili wakijeruhiwa.
Ajali hiyo ilitokea jana Novemba 28,2023 katika eneo la Kichwa cha Ng'ombe, wilayani Mwanga, wakati Rehema akitokea mkoani Morogoro kwenye sherehe ya kuagwa (send-off) iliyofanyika Novemba 24,2023.
Rehema aliyekuwa mwalimu wa Shule ya Sekondari Sua, mkoani Morogoro alikuwa akirejea nyumbani kwao Marangu, Moshi akiambatana na familia yake kwa ajili ya maandalizi ya harusi iliyopangwa kufungwa Desemba 2,2023 mkoani Arusha.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alithibitisha ajali hiyo akisema wanamshikilia dereva wa lori, Joachim Meela (37) kwa mahojiano zaidi.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Abdallah Mwaipaya, amewataja majeruhi kuwa, Veronika Chao (35), mdogo wa Rehema ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Nguzo Mbili, Geita na mwanaye, Jayden Erasto (2).
"Jana kulitokea ajali katika wilaya yetu ya Mwanga, iliyosababishwa na magari mawili, lori aina ya Scania lililokuwa likiendeshwa na mkazi wa Moshi likitokea Arusha kwenda Dar es Salaam lililogongana na Toyota Raum likitokea Morogoro kwenda Marangu,” amesema.
Mwaipaya amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Kisangara, wilayani Mwanga, huku majeruhi wakiendelea na matibabu katika kituo hicho.
Ndugu, marafiki wanena
Ndugu wa marehemu, Elielisa Kombe ameiambia Mwananchi Digital kuwa, harusi ya Rehema ilikuwa ifanyike Oldonyosambo, mkoani Arusha.
Kombe amesema gari lililokuwa na watu watano wa familia moja, wakazi wa Msae Nganyeni, Marangu lilipata ajali wakati Rehema akikwepa shimo.
"Gari lilikuwa na watu watano, mama na watoto wake wawili, mjukuu na msichana wa kazi, ni majonzi makubwa kwa familia," amesema Kombe.
Amesema wamepanga maziko kufanyika Jumamosi, Desemba 2,2023. Amesema wanaendelea na vikao kwa kuzishirikisha pande zote mbili.
"Tunaendelea na vikao kwa sasa, kesho ni lazima tukae pande zote mbili, upande wa waoaji na sisi, lakini tunatarajia kuzika Jumamosi," amesema.
Happyness Msacky, mwalimu mwenzake na Rehema katika Shule ya Sekondari Sua, amesema wamepokea kwa masikitiko msiba huo.
Amesema walikuwa wote siku ya sherehe wakifurahi pamoja na mtumishi mwenzao.
"Msiba huu umetuuma sana, Rehema alikuwa na familia yake, yeye ndiye alikuwa dereva. Hili ni pigo kubwa kwa familia, hatuna cha kusema zaidi ni kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu," amesema.
Mwananchi
Mtihani wa safari ni kupishana na kupita magari na kujua kona zenye madhara basi wengine wanafata sana mistari ya Tanroad pana sehemu nilipita mstari wa Tanroad unaruhusu kupita gari ingine karibu kabisa na daraja na huko Njombe kwenye Kona niliona mstari unaruhusu kuyapita magari mengine na mbele kuna kona huoni kitu hapo unatakiwa ujiongeze usisema mstari unaruhusu kwa hiyo bara bara inaongea yenyewe uendeshe vip gari yako...Akishajua kuendesha siku anasafiri nalo anakimbia hajui barabara vizuri pia bumps ziko wapi...hamadi bumps anapaa nayo mnamkuta juu ya mti
Yaani suala la uzembe wanalihusisha na ushiririkina. Barabara mbovu pamoja na dereva kutokuwa mzoefu.Mmeshaanza hbr zenu za maagano,ila Waafrika wakikalilishwa Jambo kila kitu watahusisha na kile walichokalili.Hebu fikiri nje ya kisanduku.
Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Unafikiri mkisafiri kwenye buss ndo hamtapata ajali, hizi fikra kama zako huwa napigana nazo sana tu, hata mkipanda ndege moja kama zimefika zimefika tu,Kusafiri kifamilia kwenye usafiri mmoja wa binafsi ni kujiweka rehani hasa katika safari za mikoani kwenye barabara za Tanzania.
Ajali nyingi zinasababishwa na uzembe na barabara mbovuUnafikiri mkisafiri kwenye buss ndo hamtapata ajali, hizi fikra kama zako huwa napigana nazo sana tu, hata mkipanda ndege moja kama zimefika zimefika tu,
Kuna siku wife alikuwa anaenda Arusha kutokea Dom apite road ya kondoa. Nikamwambia ni bora kupanda bus akakaza anataka aende na gari atumie kwenye mizunguko ya hapa na pale akiwa chuga. Hakutuboa kwenye zile kona ni siku yake haikufika tu.
Hizi road zinataka ujuzi wa barabara sio kujua kuendesha gari tu
Si ndio hapo!!,Yaani Waafrika sijui tupoje.Hata jambo linalohitaji kutumia akili ya Kawaida tunaingiza imani.Yaani suala la uzembe wanalihusisha na ushiririkina. Barabara mbovu pamoja na dereva kutokuwa mzoefu.
Ni Kweli mkuu,siku ya kwanza mimi niliendesha gari kutoka Tunduma (Songwe) hadi Njombe maeneo ya Ludewa aisee sitasahau siku ile Yaani nilisali sana kuomba Mungu aniongoze,na nilijitahidi kwa Msaada wa Mungu kufika kule lkn nilikuwa nimechoka sana.
Inataka umakini sana kama hautaki kuzama korongoniYaani Tena barabara ya Kondoa ilivyo na Kona Kona mweee acha kabisa,ukimaliza Kondoa km unaelekea manyara kuna Kona Kali Fulani hv pale mweee acha tuuu
Halafu ving'ang'anizi kichizi yani ukimwambia haelewi A wala BWanawake mthihan sana, Ma bus siku hizi yamejaa, mazuri, una relax, stress za kuendesha za nini?
Ni mtoto wa mdogo wake ambaye naye ni mwalimu huko Geita.Halafu Bibi hharusi ana mtoto wa miaka 2
Inaweza kuwa kweli maana kwa umri huo aliokuwa nao bibi harusi mtarajiwa si rahisi kupata mme ambaye hajawahi kuoa.Kuna sehemu nimesoma kuwa alikuwa anaenda kuolewa uke wenza kuwa mume aliacha kuoa ndoa na aliyekuwa naye akambwaga akaamua aoe huyo Sina uhakika kama ni kweli au la nilisoma tu mitandaoni maana mitandao habari zote za uongo na kweli pia huwemo
"Age, aint nothing, but a number".....Aaliyah.Bibi hharusi ana miaka 37.
Sawa
Kwanini asipate watu wanawaoa wanawake wenye 45+Inaweza kuwa kweli maana kwa umri huo aliokuwa nao bibi harusi mtarajiwa si rahisi kupata mme ambaye hajawahi kuoa.