Bibi harusi mtarajiwa, mama yake wafa ajalini wakielekea Kilimanjaro kwenye maandilizi ya harusi yake

Bibi harusi mtarajiwa, mama yake wafa ajalini wakielekea Kilimanjaro kwenye maandilizi ya harusi yake

Ulimwengu wa Roho wa giza unamambo mengi sana...

Kama watu wangefunuliwa waone wangeweza kukwepa hali kama hiyo...

Tatizo watu Bado wanaamini uchawi/mizimu na ushirikina ..

Maagano yake ni magumu sana, unaweza usione Leo ila kizazi chako kitaipata...

Watu wengi wanateseka na maagano yaliyowekwa na wazazi wao au ukoo...
Imani za hivi huwa sizikubali.Sasa km Maagano yanakuwa na nguvu kuna Sababu gani ya Kumpokea Yesu?,Ina Maana Kazi ya Yesu Kristo kufa msalabani ni ipi sasa?.Huu upuuzi waambie wasiojua nguvu ya Msalaba wa Yesu na damu yake aliyoimwaga msalabani.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 

Bibi harusi mtarajiwa, Rehema Chao (37) na mama yake mzazi, Agness Chao (75) wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Raum kugonga lori.

Ajali hiyo iliyotokea baada ya Rehema aliyekuwa dereva wa gari hilo kukwepa shimo na kugongana na lori, pia imesababisha kifo cha mfanyakazi wa ndani wa mdogo wake, Irene Shija (15), huku wanafamilia wengine wawili wakijeruhiwa.

Ajali hiyo ilitokea jana Novemba 28,2023 katika eneo la Kichwa cha Ng'ombe, wilayani Mwanga, wakati Rehema akitokea mkoani Morogoro kwenye sherehe ya kuagwa (send-off) iliyofanyika Novemba 24,2023.

Rehema aliyekuwa mwalimu wa Shule ya Sekondari Sua, mkoani Morogoro alikuwa akirejea nyumbani kwao Marangu, Moshi akiambatana na familia yake kwa ajili ya maandalizi ya harusi iliyopangwa kufungwa Desemba 2,2023 mkoani Arusha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alithibitisha ajali hiyo akisema wanamshikilia dereva wa lori, Joachim Meela (37) kwa mahojiano zaidi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Abdallah Mwaipaya, amewataja majeruhi kuwa, Veronika Chao (35), mdogo wa Rehema ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Nguzo Mbili, Geita na mwanaye, Jayden Erasto (2).

"Jana kulitokea ajali katika wilaya yetu ya Mwanga, iliyosababishwa na magari mawili, lori aina ya Scania lililokuwa likiendeshwa na mkazi wa Moshi likitokea Arusha kwenda Dar es Salaam lililogongana na Toyota Raum likitokea Morogoro kwenda Marangu,” amesema.

Mwaipaya amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Kisangara, wilayani Mwanga, huku majeruhi wakiendelea na matibabu katika kituo hicho.

Ndugu, marafiki wanena
Ndugu wa marehemu, Elielisa Kombe ameiambia Mwananchi Digital kuwa, harusi ya Rehema ilikuwa ifanyike Oldonyosambo, mkoani Arusha.

Kombe amesema gari lililokuwa na watu watano wa familia moja, wakazi wa Msae Nganyeni, Marangu lilipata ajali wakati Rehema akikwepa shimo.

"Gari lilikuwa na watu watano, mama na watoto wake wawili, mjukuu na msichana wa kazi, ni majonzi makubwa kwa familia," amesema Kombe.

Amesema wamepanga maziko kufanyika Jumamosi, Desemba 2,2023. Amesema wanaendelea na vikao kwa kuzishirikisha pande zote mbili.

"Tunaendelea na vikao kwa sasa, kesho ni lazima tukae pande zote mbili, upande wa waoaji na sisi, lakini tunatarajia kuzika Jumamosi," amesema.

Happyness Msacky, mwalimu mwenzake na Rehema katika Shule ya Sekondari Sua, amesema wamepokea kwa masikitiko msiba huo.

Amesema walikuwa wote siku ya sherehe wakifurahi pamoja na mtumishi mwenzao.

"Msiba huu umetuuma sana, Rehema alikuwa na familia yake, yeye ndiye alikuwa dereva. Hili ni pigo kubwa kwa familia, hatuna cha kusema zaidi ni kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu," amesema.

Mwananchi
Inaumiza sana wapumzike kwa amani , this is so devastating
 

Bibi harusi mtarajiwa, Rehema Chao (37) na mama yake mzazi, Agness Chao (75) wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Raum kugonga lori.

Ajali hiyo iliyotokea baada ya Rehema aliyekuwa dereva wa gari hilo kukwepa shimo na kugongana na lori, pia imesababisha kifo cha mfanyakazi wa ndani wa mdogo wake, Irene Shija (15), huku wanafamilia wengine wawili wakijeruhiwa.

Ajali hiyo ilitokea jana Novemba 28,2023 katika eneo la Kichwa cha Ng'ombe, wilayani Mwanga, wakati Rehema akitokea mkoani Morogoro kwenye sherehe ya kuagwa (send-off) iliyofanyika Novemba 24,2023.

Rehema aliyekuwa mwalimu wa Shule ya Sekondari Sua, mkoani Morogoro alikuwa akirejea nyumbani kwao Marangu, Moshi akiambatana na familia yake kwa ajili ya maandalizi ya harusi iliyopangwa kufungwa Desemba 2,2023 mkoani Arusha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alithibitisha ajali hiyo akisema wanamshikilia dereva wa lori, Joachim Meela (37) kwa mahojiano zaidi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Abdallah Mwaipaya, amewataja majeruhi kuwa, Veronika Chao (35), mdogo wa Rehema ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Nguzo Mbili, Geita na mwanaye, Jayden Erasto (2).

"Jana kulitokea ajali katika wilaya yetu ya Mwanga, iliyosababishwa na magari mawili, lori aina ya Scania lililokuwa likiendeshwa na mkazi wa Moshi likitokea Arusha kwenda Dar es Salaam lililogongana na Toyota Raum likitokea Morogoro kwenda Marangu,” amesema.

Mwaipaya amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Kisangara, wilayani Mwanga, huku majeruhi wakiendelea na matibabu katika kituo hicho.

Ndugu, marafiki wanena
Ndugu wa marehemu, Elielisa Kombe ameiambia Mwananchi Digital kuwa, harusi ya Rehema ilikuwa ifanyike Oldonyosambo, mkoani Arusha.

Kombe amesema gari lililokuwa na watu watano wa familia moja, wakazi wa Msae Nganyeni, Marangu lilipata ajali wakati Rehema akikwepa shimo.

"Gari lilikuwa na watu watano, mama na watoto wake wawili, mjukuu na msichana wa kazi, ni majonzi makubwa kwa familia," amesema Kombe.

Amesema wamepanga maziko kufanyika Jumamosi, Desemba 2,2023. Amesema wanaendelea na vikao kwa kuzishirikisha pande zote mbili.

"Tunaendelea na vikao kwa sasa, kesho ni lazima tukae pande zote mbili, upande wa waoaji na sisi, lakini tunatarajia kuzika Jumamosi," amesema.

Happyness Msacky, mwalimu mwenzake na Rehema katika Shule ya Sekondari Sua, amesema wamepokea kwa masikitiko msiba huo.

Amesema walikuwa wote siku ya sherehe wakifurahi pamoja na mtumishi mwenzao.

"Msiba huu umetuuma sana, Rehema alikuwa na familia yake, yeye ndiye alikuwa dereva. Hili ni pigo kubwa kwa familia, hatuna cha kusema zaidi ni kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu," amesema.

Mwananchi
Unakwepa shimo kuzuia boll joint isiharibike unalenga uso wa lory. Dereva wa masafa wanaelewa kilichotokea hapo

Serikali imeendelea kusisitiza Ukiwa na Gari yako unayotumia huku mjini Siku ya Safari kodisha Dereva akupeleke . (Udereva ni professional) Ni zaidi ya kulenga Barabara
Kuna saa unatakiwa ufikiri na upate majibu sahihi Ndani ya nusu sekunde Kati ya kuharibu boll joint Ambayo ungeenda Kwa fundi kubadili Kwa 25000 Au ulenge lory usoni ufe

Huyu alikosa Driving skills

KIROHO:
Huyu mtu amepata mume na 37 years. Unajua kwa nini alikaa muda wote huo?
Sababu zingine ni kwamba kuna watu walinenewa hawataolewa ..akilazimisha sana
Kuna Roho inaitwa kisasi Kama hajui vita vya kiroho Ndio itammaliza

So tunaweza kumuona alikuwa si Dereva mzuri ila amekoseshwa. Ulimwengu wa roho ni very technically. Ndio maana Mungu anafundisha watu wake maarifa ya rohoni. Wakolosai 1:9
Mtume Paulo anasema na Ninanukuu
Tangu tuliposikia hatuachi kufanya Dua na maombi Kwa ajili yenu Ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake Katika Hekima yote na ufahamu wa Rohoni .

So ukikosa ufahamu wa Rohoni Hutajua wakati sahihi Ni ipi wa kufanya jambo Au wakati sio sahihi ni upi usifanye Ndio maana mwisho ni hasara Kwa wengi.

Poleni wafiwa wote Mungu awape faraja.
WOKOVU NI SASA BAADA YA KUFA NI HUKUMU.
Usipoteze muda kumuombea mtu akifa Eti awekwe pema peponi Hiyo si kazi yako
Ibada ya mazishi ni Kwa ajili ya walio hai basi.
 
Akishajua kuendesha siku anasafiri nalo anakimbia hajui barabara vizuri pia bumps ziko wapi...hamadi bumps anapaa nayo mnamkuta juu ya mti
Mtihani wa safari ni kupishana na kupita magari na kujua kona zenye madhara basi wengine wanafata sana mistari ya Tanroad pana sehemu nilipita mstari wa Tanroad unaruhusu kupita gari ingine karibu kabisa na daraja na huko Njombe kwenye Kona niliona mstari unaruhusu kuyapita magari mengine na mbele kuna kona huoni kitu hapo unatakiwa ujiongeze usisema mstari unaruhusu kwa hiyo bara bara inaongea yenyewe uendeshe vip gari yako...
 
Kusafiri kifamilia kwenye usafiri mmoja wa binafsi ni kujiweka rehani hasa katika safari za mikoani kwenye barabara za Tanzania.
Unafikiri mkisafiri kwenye buss ndo hamtapata ajali, hizi fikra kama zako huwa napigana nazo sana tu, hata mkipanda ndege moja kama zimefika zimefika tu,
 
Unafikiri mkisafiri kwenye buss ndo hamtapata ajali, hizi fikra kama zako huwa napigana nazo sana tu, hata mkipanda ndege moja kama zimefika zimefika tu,
Ajali nyingi zinasababishwa na uzembe na barabara mbovu
Kama mtu huna uzoefu panda public transport. Mabasi mengi pia yana madereva vichaa ndio maana ajali nyingi.
 
Kuna siku wife alikuwa anaenda Arusha kutokea Dom apite road ya kondoa. Nikamwambia ni bora kupanda bus akakaza anataka aende na gari atumie kwenye mizunguko ya hapa na pale akiwa chuga. Hakutuboa kwenye zile kona ni siku yake haikufika tu.
Hizi road zinataka ujuzi wa barabara sio kujua kuendesha gari tu


Wanawake mthihan sana, Ma bus siku hizi yamejaa, mazuri, una relax, stress za kuendesha za nini?
 
Ni Kweli mkuu,siku ya kwanza mimi niliendesha gari kutoka Tunduma (Songwe) hadi Njombe maeneo ya Ludewa aisee sitasahau siku ile Yaani nilisali sana kuomba Mungu aniongoze,na nilijitahidi kwa Msaada wa Mungu kufika kule lkn nilikuwa nimechoka sana.

Na hapo ulikuwa na kipande kibaya cha Mbeya - Igawa, kina barabara mbaya ina mashimo na matuta ya lami kufimba karibia sehemu nyingi...

Kingine ni kile cha Makambako - Njombe kuna baadhi ya maeneo kuna vipande vibaya vya barabara...
 
Yaani Tena barabara ya Kondoa ilivyo na Kona Kona mweee acha kabisa,ukimaliza Kondoa km unaelekea manyara kuna Kona Kali Fulani hv pale mweee acha tuuu
Inataka umakini sana kama hautaki kuzama korongoni
 
Kuna sehemu nimesoma kuwa alikuwa anaenda kuolewa uke wenza kuwa mume aliacha kuoa ndoa na aliyekuwa naye akambwaga akaamua aoe huyo Sina uhakika kama ni kweli au la nilisoma tu mitandaoni maana mitandao habari zote za uongo na kweli pia huwemo
Inaweza kuwa kweli maana kwa umri huo aliokuwa nao bibi harusi mtarajiwa si rahisi kupata mme ambaye hajawahi kuoa.
 
Back
Top Bottom