Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Hii ni Falacy of Generalization. Sio Wanasayansi wote wanakataa uwepo Wa Mungu. Tuwe makini na Hearsay.
uwe unasoma kwa makini mkuu, itakusaidia kujibu majibu sahihi kwa kile unachokiquote.
'' hapo nimekuwa specific kwa wanasayansi wasio amini Mungu'' Sijasema wanasayansi wote hawaamini Mungu Tangu comment ya kwanza.
 
Mkuu kwa umakini wako sitegemei na wewe uingie kwenye mlolongo wa kutafsiri maandiko lateral kabisa nakumbuka hata nyuma niliwahi fanya sana na ulikua mstari wa mbele kupinga hilo mfano mada ya Leviathan,Rangi ya Yesu na laana ya canaan so sitegemei kuwepo double standards.

Mfano mwanzo 33 inasema Yakobo alipigana na mtu akamshinda alafu huyo mtu akamuita Israel kisa alipigana na Mungu akashinda je hapo ni lateral kuwa alipigana na Mungu???

Pia ufunuo 5:11 inasema Namba ya malaika ni 10,000×10,000 je unaweza nisaidia kma ni lateral

Ufunuo 7 still inasema waisrael 144000 ndio watakuwa present kwenye mkutano ule je nayo ni lateral??

Labda niulize je ni wakati gani unajua Biblia iko lateral au figurative

Joshua 5:1
1 Ikawa, wafalme wa Waamori, waliokaa ng?ambo ya Yordani pande za magharibi, na wafalme wote wa Wakanaani, waliokuwa karibu na bahari, waliposikia jinsi BWANA alivyoyakausha maji ya Yordani mbele ya wana wa Israeli, hata tulipokwisha kuvuka, basi mioyo yao iliyeyuka
Mkuu ni kweli na nakubaliana na wewe kuwa sitakiwi kuwa lateral kwenye kila kitu cha kwenye bibilia, Ila nakubaliana na kuwa Rateral kwenye mambo ambayo ni rateral katika bibilia na Yamethibitika kuwa lateral kwenye Bibilia.
Ungeonyesha madhaifu ya hiyo kutoka20 kwa nini sio lateral ili namimi nionyeshe kuwa ni lateral tuchanganua vizuri zaidi.

Binafsi naamini.
Matukio ya Mwanzo sio mafumbo au mambo ya kufikilika ni historia halisi. Yesu aliamini hivyo Mitume waliamini hivyo. Katikati ya Historia hiyo kunaweza Kuwa na Matukio ya Njozi, na mengine ya Mifano. Ila Hili la Uumbaji ikiwa Muhusika amelitolea ufafanuzi sioni haja ya kulazimisha usayansi, au kuliforce tukio linyenyekee wanasayansi hata kama Mungu amefafanua.
 
Kwa Sababu alichokisema kwa habari za Siku kulikuwa na practical reference na hata sasa uzao wa walioambiwa wanaendelea kukitekeleza practically sio njozi au hekaya. Siku sita wanafanya kazi siku ya Saba wana Pumzika sawasawa na maelezo manyoofu ya Muumbaji.

Baada ya uthibitisho wa Ellen kwenda Mbinguni bila kufa kwanza na huko kuona Amri ya sabato imezingirwa na "utukufu?"
 
mpendwa mitale na midimu ahsante na hongera kwa maelezo yako nimekupata uzuri sana. lakini kadili ya maelezo yako binafsi ninamaswali kama mawili tu ivi:

1: kuna mahali umedai kuwa biblia toka mwanzo mpaka ufunuo ina kila kitu na kila fomula (kwa maana kwamba imejibu kila kitu ikiwemo na sayansi yenyewe kwa jinsi nilivokuelewa mimi). swali langu ni hil: ni nini lengo la biblia kwa mwanadamu, ni nini kusudi la biblia kwa mwanadamu, Mungu alikusudia biblia iwe na kazi gani kwa mwanadamu, au kwa nini biblia ???

mpendwa mitale na midimu kama jibu la swali hilo hapo juu kuhusu lengo la biblia kwa mwanadamu ni tofauti kabisa na sayansi na haikukusudiwa kufundisha sayansi, unafikiri ni sahihi au ni haki tunapongangania kutafuta sayansi/ kujifunza sayansi toka kwenye kitabu ambacho hakikukusudiwa kwa kazi hiyo ?.

sikitai kwamba kuna sayansi mbaya na wanasayansi wapinga Mungu/wakana Mungu uwepo wa hao hauifanyi sayansi yote kuwa ni dhambi au kuwalaumu wapinga Mungu kwa kila jambo kwa Mgongo wa sayansi sidhani kama ni sahihi. ninachojua mimi ni kuwa sayansi ni pato la AKILI na MAARIFA tuliopewa na Mungu kama zawadi itusaidie kumpenda, kujua zaidi nk katika maisha yetu ya kila siku. ndio maana imeandikwa usimwache elimu aende zake na pia mpende bwana Mungu wako kwa AKILI zako zote. sasa sayansi ndio moja ya mapato ya izo AKILI au tunaweza kusema ndo AKILI zenyewe. tulipewa mikono na miguu kwa ajili ya kazi njema ya kumtumikia Mungu na jirani lakini kuna watu wanaitumia iyo mikono na miguu kwa kuvunja amri za Mungu kama kuiba, kuumiza, kupigana nk sasa hapo sidhani kama kosa ni mikono au miguu ndivo ilivo kwenye sayansi pia.
1: Bibilia imeweka msingi wa Kila kitu hiyo ndiyo point yangu kuu katika maelezo niliyokupa. Imeweka facts za Milele ambazo uvumbuzi wowote wa kisayansi unajengwa juu yake, na haziyumbishwi na wasanasayansi na mavumbuzi yao. Na kuyumba kwa wanasayansi hakuwezi kuziyumbisha zitadumu milele hata kama zikiaminiwa na watu wawili tu dunia nzima.

Miongoni mwa facts kuu hizo au naziita evalasting principles au formula
* Mungu ndiye Muumbaji. Hili Litabaki hivyo hata dunia ikatae.
*Mungu aliyemuumbaji, Anapaswa kuaminika kwa Kauli zake mwenyewe kuliko Kauli za Kiumbwaji.
*Wanasayansi wanajaribu kuchunguza kazi za Mungu za Uumbaji, Uchunguzi huo unaweza kupelekea kuvumbua ukweli wa kazi zake au Kupotosha ukweli huo. Katika Hili Kilichosemwa wazi kwenye Maandiko Matakatifu ndio Basis ya Ukweli huo.
*Sayansi inamipaka, ya ufahamu na uelewa Juu ya Kazi nzuri ya Mungu.
Bibilia haijatoa kila formula ya kisayansi na sijasema hayo maana haijazungumzia hata pai. Ila inatoa msingi au general formula za kumsaidia Mcha Mungu asivurugwe na kuchanganyikiwa na chochote kutoka kwa Mwanasayansi haramu au Halali.

####
Lengo la Bibilia ni nini?
'' Kwa Maana Jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanaye wa pekee, ili kila amuaminie asipotee bali awe na Uzima wa Milele'' Yohana 3:16
Kwangu mimi hili ndio lengo na dhumuni kuu la Maandiko Matakatifu. Ukombozi wa Mwanadamu. Ndio maana Yesu mwenyewe alisema Maandiko Yote yanamuelezea Yeye. Hata Hiyo Mwanzo ni Yeye ndiye Muhusika wa uumbaji.
Lakini pia Bibilia inasema '' Neno Lako ndiyo taa ya Miguu yangu na mwanga wa njia yangu''. Nje ya Bibilia utatembea gizani, na Kila kilichonje ya Bibilia ikiwa kitakizana na Ukweli mkuu wa Bibilia ni GIZA.
Bibilia inatufanya Tusewe watoto wachanga tena, Tukitupwa huku na kule na Kila upepo wa Elimu na mafunzo.

Pili
Sijasema Popote Kuwa Bibilia ikikusudia Kufundisha Sayansi, Bali Nimesema na nasema Bibilia ni Kitabu sahihi Kilichoweka kanuni/Formula na Misingi zinazoweza Kumsaidia Mwanadamu Asipotoshwe na Sayansi Potoshi na Awe Bora na Imani Yake kwa Mungu Ikue kwa Mavumbuzi na sayansi Sahihi.
Lakini Kusema hili Haimaanishi hakuna tips katika Bibilia ambazo ni scientifically correct, maana Bibilia imegusia vitu kama Rain formation Mungu akimthibitishia Ayubu Kuwa Yeye ndiye fundi wa hizo mifumo, Dunia duara kama mdau Kituko kazungumzia na tips kadhaa ila sio lengo kuu la Bibilia Maana Yote hayo hayatakuwa na Maana kama ukayajua na ukachepuka kwenye Lengo Kuu Wokovu wa Mwanadamu Kupita Kristo Yesu.

tatu
Hatujifunzi Sayansi Kutokea Kwenye Bibilia. Ila kama nilivyoonyesha Huko Juu Bibilia Ni nanga ambayo itamsaidia anayeiamini asiyumbishwe na tafiti potoshi au sahihi za Kisayansi. Mfano wa Tafiti Potoshi kwa Imani Yangu ni kudanganya watu Dunia imeumbwa miaka mamilioni Kisa Sayansi imesema Imegundua huku Bibilia Imeliweka wazi Kuwa ni Siku sita ambazo kwa Genealogy za watu wa Bibilia hatufikishi huko wanakozungumiza. Pia Basis na assumptions wa hizo observation ni kanusho la kazi njema ya Mungu aliyoweka msingi wa Kuikumbuka kupitia Sabato ambayo Yesu anasema waliwekewa wanadamu ili wakumbuke hilo zoezi ingawa mabillioni hawaoni umuhimu wa kufanya hilo.

nne
Pamoja na Kazi njema ya Ukombozi ambayo ndiyo msingi wa Bibilia, Imekusudiwa kuzuia upotoshaji wote wa kisayansi, kiphilosophia, Modernism, historia, elimu etc. Na Inatutaka Kuweke kando Kila fikra ijiinuayo KINYUME NA ELIMU YA MUNGU bila kujali inatoka kwa prof,scientist,padri,mchungaji hata Malaika.

SAYANSI NA AKILI ALIZOTUPA MUNGU.
Bibilia inasema '' Moyo (Human Mind) ni mdanganyifu na Unaugonjwa wa Kufisha, ni nani awezae Kuujua? Yeremia 17:9
Hii tu, inatosha kuendea tafiti za Kisayansi na Kisomi kitaaluma kwa utulivu huku tukiwa na taadhari kwa sababu zimefanyika kwa sababu zao na watu wa kawaida wenye ubinadamu uliofungamana na dhambi wanaweza kuja na hitimisho potoshi au sahihi, Danganyifu au Lenye muelekeo sahihi.
Mfano: Utasimama upande upi katika jambo ambalo hata wanasayansi wanapingana japo ni tokeo la akili hizo Mungu alizotupatia?
Utayaacha katika viwango Vya Nadharia tu au assumptions hata kama zinaungwa na dunia nzima haimaanishi ni Kweli. Sio mimi tu nasema haya hata galileo alisema ''
KATIKA SAYANSI MAMLAKA YA MAONI YA WATU ELFU MOJA, YANAWEZA YASIWE NA THAMANI SAWA NA FIKRA YA MTU MMOJA ''.

HITIMISHO.
Sipingi Sayansi, Ila siungi mkono Kila kitu katika Sayansi kama Fact. Kwanza hata wenyewe huwa wanaziita NI NADHARIA. Ila Kauli za Mungu sio NADHARIA. Kwa nini Sayansi unaona kama naijadili kwa Kutumia Bibilia japo Bibilia ijazungumzia UKOMBOZI. Sayansi ya Sasa Inafunua Pazia na Kuingia Kwenye mambo ya Imani na Bibilia Na Kuanza kuyatafsri na Kuyatolea Matamko. Mfano hata hili La Uumbaji na Umri wa Duñia. Ninaona ni Heshima Kubwa mno Kusimama na Kauli ya Mungu na Kuweka kando nadhalia zote katika hili. Hii hainifanyi nizichukie. Mimi nimesoma sayansi japo kwa kupapasa hadi elimu ya juu ya awali, hata nikiamua kutafuta PHD ya Geology nitasoma hayo yote ya mamilioni ya miaka kama nadharia ila fact ni Kauli ya Mungu kuwa Dunia Iliumbwa Siku sita Ya Saba akapumzika. Hakuwaandikia wasomi wa theolojia aliwaandikia wakina mama na wababa waliotoka utumwani, masikini wasio na elimu, akaagiza watoto wajulishwe katika hilo nimechagua kuelewa kama hao walioandikiwa na kuambiwa Wasiyaache maana hiyo ndiyo akili yao na ufahamu wao.

mkuu nimeandika maneno mengi ili kuchambua kwa kirefu kidogo maana inainekana hunielewi vizuri naamini nini na siamini nini.
 
Utofauti lazima utakuwepo kwa sababu Bible inafanya hesabu kuumbwa kwa Adam ndo mahesabu yameanzia hapo wakati science inapima miamba. Ikumbukwe kwenye Bible binadamu ndo wa mwisho kuumbwa na mchakato wa uumbaji ulikuwa wa miaka mingi sana.
 
Dunia wala Ulimwengu kwa maana ya miamba haukuumbwa kwa siku sita, mnamtafsiri Mungu tofauti. Zile siku sita za Kimungu kwa sababu Gregory calendar tunayoifuata haikuwepo wakati huo Mungu aliumba vitu vya kuujaza Dunia. Mwanga siku ya kwanza na uumbaji mwingine siku zilizofuata. Tahadhari tu, Hizi siku sita ni za Kimungu na sio 24hrs za kwetu. Uumbaji wa kibiblia unaendana kabisa na ugunduzi wa kisayansi. Kulikuwepo kwanza na uumbaji wa miamba ambao haukuzungumziwa kwenye Biblia, ukafuata kuwepo kwa mfumo wa mwanga nk. Mwanzo 1 haikuenda mbali kuelezea uumbaji kwa sababu sio objective ya Bible. Kwa wale wasomaji watanielewa. Main objective ya Bible ni Salvation of Mankind baada ya anguko. Na ndio maana mimi sitaki kwenda deep kutumia Bible kwenye kuelezea mambo ya uumbaji
sio Kweli.
Kabla ya Gregory Calender kuwepo Siku ya Kuanza Jioni hadi Jioni ambayo inahitimisha masaa Ishirini na nne ilikuwepo.
Ni Mungu aliyeumba Dunia na Vyote Vilivyomo aliyesema Alifanya YOTE sio baadhi Ndani ya Siku sita.
Na Alipozungumzia hilo, alisema literally kuwa Siku sita alifanya Yote kwa Kutamka.
Unadhani Mungu anahitaji miaka Millioni ngapi Kusema Neno Likawawa Mwamba???
Huku ni Kumshushia Heshima Mwenye enzi.
 
Utofauti lazima utakuwepo kwa sababu Bible inafanya hesabu kuumbwa kwa Adam ndo mahesabu yameanzia hapo wakati science inapima miamba. Ikumbukwe kwenye Bible binadamu ndo wa mwisho kuumbwa na mchakato wa uumbaji ulikuwa wa miaka mingi sana.
Hesabu ya bibilia inakamilikia Kuumbwa kwa adamu, haianzii kuumbwa Kwa Adamu.
na Ilikuwa ni SIKU ya Sita ya Uumbaji.
Mungu akamuumbia adamu siku ya SABA Ili angalau Iwe weekend ya Mwanadamu akumbuke kuumbiwa uumbaji wa siku Sita.
Ila Kwa Sababu adamu wa leo tumegoma, na hatutaki kusikia hilo, na wengine wameamua kuwa wakorofi zaidi kwa kunyofoa hayo maelezo kwenye Amri za Mungu. Upotofu huu utakuwa mkubwa sana, na Wengi wanaoamini haya soon watakuwa atheists.
 
Baada ya uthibitisho wa Ellen kwenda Mbinguni bila kufa kwanza na huko kuona Amri ya sabato imezingirwa na "utukufu?"
Kutoka 20:11. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.

'' Petro na Mitume wakajibu wakasema, IMETUPASA KUMTII MUNGU KULIKO MWANADAMU'' Matendo 5:29
Nje ya 24hrs Creation Kuna maelfu ya nadharia kwa jina la Uumbaji wa mamiaka ya milioni.
Jiandae kuogelea kwenye Bottomless pit la mamilioni ya miaka huku unaacha ukweli mwororo wa Kauli sahihi na dhahiri ya Mungu huku ukitumia vikokotoo vya lugha za kiebrania kama mbeleko.
Kufanya Tallying ya Uumbaji wa Bibilia na secret evolution Ideas based on bible utafanikiwa at Infinity.
 
Ulimwengu ama dunia???,kama ni dunia sidhani hataka miaka 6000 imefikisha??

dunia haijafikisha hata miaka 10000,fatilia ujio wa sirians from planet x..
 
Kutoka 20:11. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.

'' Petro na Mitume wakajibu wakasema, IMETUPASA KUMTII MUNGU KULIKO MWANADAMU'' Matendo 5:29
Nje ya 24hrs Creation Kuna maelfu ya nadharia kwa jina la Uumbaji wa mamiaka ya milioni.
Jiandae kuogelea kwenye Bottomless pit la mamilioni ya miaka huku unaacha ukweli mwororo wa Kauli sahihi na dhahiri ya Mungu huku ukitumia vikokotoo vya lugha za kiebrania kama mbeleko.
Kufanya Tallying ya Uumbaji wa Bibilia na secret evolution Ideas based on bible utafanikiwa at Infinity.
Kabla ya day 1 Biblia inasema
‘In the beginning God created the heavens and the earth. And the earth was formless and void, and darkness was over the surface of the deep; and the Spirit of God was moving over the surface of the waters. Then God said, “Let there be light”; and there was light. And God saw that the light was good; and God separated the light from the darkness. And God called the light day, and the darkness He called night. And there was evening and there was morning, one day.’

Hii mistari inaonyesha kwamba UUMBAJI ulianza baada ya kuwepo a VOID and FORMLESS EARTH. Roho ya Mungu ikielea juu ya maji
Hayo yalitokea kabla ya kuanza uumbaji wa day one. Hata mtoto wa kindergarten anaweza kudadavua hii.
Umbaji wa mwanga ulianza day one wakati maji na miamba ilishakuwepo, Ndio maana nasema UUmbaji wa Miamba hakufanyika katika six day (This are NOT literal days, utaendelea kujidanganya mpaka lini ndugu
 
Kabla ya day 1 Biblia inasema
‘In the beginning God created the heavens and the earth. And the earth was formless and void, and darkness was over the surface of the deep; and the Spirit of God was moving over the surface of the waters. Then God said, “Let there be light”; and there was light. And God saw that the light was good; and God separated the light from the darkness. And God called the light day, and the darkness He called night. And there was evening and there was morning, one day.’

Hii mistari inaonyesha kwamba UUMBAJI ulianza baada ya kuwepo a VOID and FORMLESS EARTH. Roho ya Mungu ikielea juu ya maji
Hayo yalitokea kabla ya kuanza uumbaji wa day one. Hata mtoto wa kindergarten anaweza kudadavua hii.
Umbaji wa mwanga ulianza day one wakati maji na miamba ilishakuwepo, Ndio maana nasema UUmbaji wa Miamba hakufanyika katika six day (This are NOT literal day, utaendelea kujidanganya mpaka lini ndugu
Mungu aliumba Mbingu na Nchi hapo mwanzo. Sio Maji na Miamba.
Hapo Kuna Mawili Sentensi hiyo inaanza na summary ya kazi Yote aliyoifanya kisha akaanza kuichanganua.

Pili, Aliumba hayo Mwa Milisecond ambayo inamezwa na Siku ya Kwanza.
2
Kwa nini najenga hoja hizi ambazo unaweza kuona natembea juujuu bila ufahamu wa Bibilia na siri zake.
Mungu anataka tusitafute habari za Mqmbo yake kwa waganga, wqchawi wasihiri hata wasomi.
Kuhusu hili, Bibilia au mwqnzo Ingeishia hapo tungekubaliana ila Mungu alieyeumba Vyote Kuanzia Mbingu na Nchi na Vyote Vilivyomo amerudia mahala mahala kuwa alifanya Yote kwa Muda wa siku sita. Sio alizijaza mbingu na nchi ndani ya Siku Sita.

Kosa mnalofanya kulazimisha nadharia za Sayansi zitally na mambo ambayo Mungu ameshayafafanua huku mkiegemea kwenye evolution. Bibilia Ingeishia Mwqnzo 1 na 2 Tungechanganyikiwa ilq hili limefafanuliwa vizuri kwenye amri Kumi. Yesu naye akatia Muhuli kuwa Aliumna Siku ya Saba kwa aajili ya Wanadamu.
Wakosoaji wa Bibilia Waislam, Atheists na Higher cliticals ndio wanautamaduni wa kung'ang'ania kistali huku wakiwa hawataki ufafanuzi ndani ya Bibilia ulio wazi mahala pengine pakifafanua tukio hilohilo.
Katika Hili naomba niendelee kuwa mjinga kuliko kujiunga na wenye hekima wa dunia hii.
 
Mungu aliumba Mbingu na Nchi hapo mwanzo. Sio Maji na Miamba.
Hapo Kuna Mawili Sentensi hiyo inaanza na summary ya kazi Yote aliyoifanya kisha akaanza kuichanganua.

Pili, Aliumba hayo Mwa Milisecond ambayo inamezwa na Siku ya Kwanza.
2
Kwa nini najenga hoja hizi ambazo unaweza kuona natembea juujuu bila ufahamu wa Bibilia na siri zake.
Mungu anataka tusitafute habari za Mqmbo yake kwa waganga, wqchawi wasihiri hata wasomi.
Kuhusu hili, Bibilia au mwqnzo Ingeishia hapo tungekubaliana ila Mungu alieyeumba Vyote Kuanzia Mbingu na Nchi na Vyote Vilivyomo amerudia mahala mahala kuwa alifanya Yote kwa Muda wa siku sita. Sio alizijaza mbingu na nchi ndani ya Siku Sita.

Kosa mnalofanya kulazimisha nadharia za Sayansi zitally na mambo ambayo Mungu ameshayafafanua huku mkiegemea kwenye evolution. Bibilia Ingeishia Mwqnzo 1 na 2 Tungechanganyikiwa ilq hili limefafanuliwa vizuri kwenye amri Kumi. Yesu naye akatia Muhuli kuwa Aliumna Siku ya Saba kwa aajili ya Wanadamu.
Wakosoaji wa Bibilia Waislam, Atheists na Higher cliticals ndio wanautamaduni wa kung'ang'ania kistali huku wakiwa hawataki ufafanuzi ndani ya Bibilia ulio wazi mahala pengine pakifafanua tukio hilohilo.
Katika Hili naomba niendelee kuwa mjinga kuliko kujiunga na wenye hekima wa dunia hii.
Hii ya microsecond tukubaliane ni ya kwako tu!
Hakuna mtu anayekataa kuwa Mungu hakuumba mbingu na nchi
Ila haya mambo ya uumbaji kuna a lot of misinterpretations kuanzia kwenye tafsiri ya hizo siku sita na the creation process
Nataka tu kukuambia kuwa intentively Mungu ametuficha kabisa juu ya uumbaji wa dunia na ulimwengu na ndio maana alianzia kutufunulia pale kwenye mwanga na kuendelea ambayo hata hizo alizotufunulia alieleza in pieces.
Hivi unajua kuwa Mungu aliumba tena kwenye Chapter 2
Chapter 1 aliwaumba mwanamume na mwamake kwa pamoja Mwanzo 1-26
Na katika chapter 2 akamuumba mwanamume kwanza halafu akaja kumuumba mwanamke kutoka kwenye ubavu wa mwanamume
Kama Miamba na maji iliumbwa kwa microsecond kama unavyosema halafu mwanadamu akaumbvwa kwa siku nzima si unaona hapo unaleta confusion na hata mwenyewe baada ya miucrosecond ijayo hutaelewa umeandika ninmi?
 
Mkuu ni kweli na nakubaliana na wewe kuwa sitakiwi kuwa lateral kwenye kila kitu cha kwenye bibilia, Ila nakubaliana na kuwa Rateral kwenye mambo ambayo ni rateral katika bibilia na Yamethibitika kuwa lateral kwenye Bibilia.
Ungeonyesha madhaifu ya hiyo kutoka20 kwa nini sio lateral ili namimi nionyeshe kuwa ni lateral tuchanganua vizuri zaidi.

Binafsi naamini.
Matukio ya Mwanzo sio mafumbo au mambo ya kufikilika ni historia halisi. Yesu aliamini hivyo Mitume waliamini hivyo. Katikati ya Historia hiyo kunaweza Kuwa na Matukio ya Njozi, na mengine ya Mifano. Ila Hili la Uumbaji ikiwa Muhusika amelitolea ufafanuzi sioni haja ya kulazimisha usayansi, au kuliforce tukio linyenyekee wanasayansi hata kama Mungu amefafanua.
Mkuu ndio maana nimeuliza je ni wakati gani ambapo unagundua ni lateral au figurative language ndio imetumika.... Mfano Yesu kasema kuhusu hao waisrael 144000 na malaika wapo 10,000×10,000 je na sisi tuisome hiyo lateral kisa tu Yesu ndio kafafanua?? Ama unakubaliana na mimi kuwa zote ni parables zenye mafumbo ikiwemo creation process???

Kuhusu kutoka 20 pia ni fumbo mkuu ikimaanisha kwa VIPINDI vyote Mungu alifanya kazi ila kuna siku aliitenga akapumzika sasa akaitranslate kwa hali ya binadamu maana kama angesema achukue siku zake saba ina maana sabato ingekuwa let's say kila baada ya miaka kadhaa sio siku!!! Ni sawa tu na ufunuo wa Yohana aliandika mambo ya siku za mwisho lakini kutumia maelezo na uelewa wa enzi zake mfano vita kupiganwa kwenye farasi na mapanga ilihali leo hii vita zinapiganwa na bunduki sasa mtu akitafsiri lateral si atadhani vita za siku za mwisho ni mpaka watu washike mapanga tena sio bunduki!!

Je kwakuwa ufunuo wa Yohana ulielezewa na Yesu kupitia Yohana je na sisi tusubiri vita za mapanga ???
 
Hii ya microsecond tukubaliane ni ya kwako tu!
Hakuna mtu anayekataa kuwa Mungu hakuumba mbingu na nchi
Ila haya mambo ya uumbaji kuna a lot of misinterpretations kuanzia kwenye tafsiri ya hizo siku sita na the creation process
Nataka tu kukuambia kuwa intentively Mungu ametuficha kabisa juu ya uumbaji wa dunia na ulimwengu na ndio maana alianzia kutufunulia pale kwenye mwanga na kuendelea ambayo hata hizo alizotufunulia alieleza in pieces.
Hivi unajua kuwa Mungu aliumba tena kwenye Chapter 2
Chapter 1 aliwaumba mwanamume na mwamake kwa pamoja Mwanzo 1-26
Na katika chapter 2 akamuumba mwanamume kwanza halafu akaja kumuumba mwanamke kutoka kwenye ubavu wa mwanamume
Kama Miamba na maji iliumbwa kwa microsecond kama unavyosema halafu mwanadamu akaumbvwa kwa siku nzima si unaona hapo unaleta confusion na hata mwenyewe baada ya miucrosecond ijayo hutaelewa umeandika ninmi?
Nani kwanini hizo siku zingine hakuumba kwa microsecond wakati yeye ni Mungu mwenye uwezo?
 
Habari za mchana wakuu kama kawaida huwa nakuja na mada za kuchokoza fikra zetu hasa kwenye mambo ya kiimani hivyo mada hizi sio za kukosoa dini fulani au vitabu vya imani ila ni kuhoji tu ili tupanue fikra zetu kwenye masuala haya kwa faida yetu sote so sitegemei iibue mijadala ya kidini bali kuelimishana juu ya mambo haya baada ya kusema hayo twende moja kwa moja kwenye mada husika ya leo.
View attachment 948749
Biblia na umri wa Dunia
Mwaka 1650 professor wa masuala ya theologia na Askofu wa makanisa ya protestant wa Ireland John Ussher aliandaa maandiko yake kupitia mfululizo wa vitabu vyake kuanzia cha Annals of the Old Testament: Origins of the world ambacho ndani yake aliibua mjadala mpana sana wa karne nyingi sana. Ussher alipiga hesabu ya muda ulivyopita kati ya Adam kuumbwa hadi Yesu kuzaliwa na kugundua kwamba ni miaka 4000 imepita tokea Adam aumbwe hadi Yesu kuzaliwa hivyo kufanya dunia yetu ikiwa na wanadamu kuwa na miaka elfu 6 pekee mpaka sasa!!. Ussher alitumia maandiko kama chanzo cha nadharia yake alitumia nyaraka za masoretic zilizotumika kuandaa Biblia za agano la kale ili kuweza hesabu umri wa Adam hadi vizazi vya Abraham hadi kufikia Yesu na baada ya mnyambuliko huo alifanikiwa kugundua kwamba dunia iliumbwa usiku wa October 23 4004 kabla ya kristo.

Young Earth Creationists
Vuguvugu hili la YEC lilianza miaka ya 1960 ambapo iliasisiwa na wasomi 9 chini ya PhD wa theolojia na uhandisi Bwana Henry Morris wakijikita kwenye utafiti wa uhalisia wa umri wa dunia na uumbaji na wakahitimisha rasmi kuwa dunia tunayoishi iliumbwa ndani ya miaka elfu 10 pekee na sio zaidi ya hapo na wao pia walitumia maandiko ya Biblia ya kiebrania ili kufikia hitimisho hilo hivyo na wao wakaunga mkono hoja za hapo nyuma za Professor John Ussher na hata leo hii wameweza shawishi zaidi ya 40% ya wakazi wa marekani kwa takwimu za 2017 wanaamini nadharia hii kwamba uumbaji wa dunia ni kwa mujibu wa Biblia hauzidi miaka 10,000 iliopita.

View attachment 948751
SAYANSI inasemaje??
Baada ya sayansi na teknolojia kukua na kuongezeka vifaa vya kupima umri wa miamba,mazao na mifupa ya wanyama wakaibuka wasomi wa sayansi waliohoji kuhusu uhalali wa nadharia hizi na imeleta utata na mjadala mzito kwa miaka mingi sasa. Mwanasayansi wa karne ya 20 Clair Cameron Patterson baada ya tafiti kadhaa juu ya miamba akagundua ulimwengu toka uanze una miaka billion 4.5 na baadae wanasayansi mbalimbali wakaja na tafiti mbalimbali zikidai kwa usahidi wa kisayansi na kiacholojia kwamba uhai duniani umekuwepo miaka takriban 3.8 Billion iliopita hivyo kukinzana kabisa na nadharia hizo mbili za juu kuwa Biblia

Jinsi ya kupima
Kwa upande wa Young Earth wao wanalalia maandiko kwa kiasi kikubwa na kupiga hesabu miaka ya kibiblia tokea Adam hadi Yesu lakini wanasayansi wamepiga hesabu zao kwa ushahidi wa kushikika wakitumia mfumo unaitwa radiometric dating ambacho kinapima miamba hasa stage tofauti za jinsi miamba inavyooza na ambapo kila stage ina umri wake yake yaani miaka kadhaa ili ifike stage nyingine ya kuoza hivyo wanapiga hesabu kuanzia layer ya mwisho mpaka ya kwanza na kufikia hitimisho la umri wa mwamba huo na wakafanikiwa kugundua mwamba wa kwanza ulitokea miaka 3.8 Billioni iliyopita.
View attachment 948748
Utafiti wangu (Primary)
Binafsi nilichukua hatua kuonana na wanatheolojia kadhaa kutoka chuo fulani cha Biblia wenye ngazi ya PhD na wamenijuza kwamba Biblia haikuandikwa kwa maneno bali mafumbo hivyo isitafsiriwe kwa maana zetu bali kwa mafunuo na maana zilizo kwa Biblia... Mfano wanadai Dunia haikuumbwa kwa siku 7 kama zetu hizi bali miaka mamilion na wakaenda mbali kusema Biblia haikuanza kuandika matukio yote bali imeandika matukio juu ya watu waliochaguliwa tu hivyo wanakiri kuwa kweli dunia ina miaka mabillion na sio miaka elfu 6 pekee bali wanaotafsiri maandiko kwa akili zao ndio wanapotosha sababu wameitafsiri maneno kama yalivyo badala ya kutafuta maana ya hayo mafumbo na wakanipa mistari michache.

Yohana 16:25
25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa yaja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba.

Na wakaenda mbali kusema hata hayo mafumbo walioambiwa kuandika Biblia hawakuyaelewa sababu ni siri imewekewa hadi wakati muafaka yaani mwisho wa dunia ufike soma hapa kisa cha Daniel

Daniel 12:4
4 Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.

Hapa tunaona kuna maandiko na nabii zimefichwa kwa uelewa wetu kabisa hata Daniel hakuelewa!!

Daniel 12:8-9
8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?
9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa
mwisho.

Hivyo kama hata Daniel kuna baadhi ya vitu alifichwa na mpaka anaandika hakuvijua basi hata sisi hatuwezi vijua mpaka siku ya mwisho hivyo wakahitimisha mjadala kwa kusema huenda ni kweli dunia ina 4.5 Billion years ila sio 6000 kama YEC inavyosema maana Biblia haielezi hicho kuwa ni miaka 6000 bali watu wanatafsiri maandiko kwa akili zao ilihali YAMEFICHWA!!
View attachment 948750
Hitimisho
Ukinzano huu kati ya maandiko na sayansi juu ya asili ya umri wa ulimwengu umezua mjadala mpana sana huku kila upande ukivutia kwake nikaona kwa kuwa JF ni kisima cha maarifa nilete hii mada ili tuweze kufikiria pamoja je umri wa dunia upi ni halisi

4.5 Billion ama 6000?

Naomba kuwasilisha

Hakuna ukidhani wowote kwani bibilia inatoa majibu kwa kuanza na neno hapo mwanzo Dunia ilikuwa utupu ikionyesha kuna jambo nyuma hapo ,lakini vile vile umeeleza vyema biblia imaanzia history kuanzia kwa adamu ambapo dunia kwa maana ya sayari ilikuwepo miaka mingi kabla ya adamu na tena sijaona popote ambapo biblia inataja umri wa dunia ili kuweka ukidhani bali umri na calenda kuanza kwa adamu
 
Hii ya microsecond tukubaliane ni ya kwako tu!
Hakuna mtu anayekataa kuwa Mungu hakuumba mbingu na nchi
Ila haya mambo ya uumbaji kuna a lot of misinterpretations kuanzia kwenye tafsiri ya hizo siku sita na the creation process
Nataka tu kukuambia kuwa intentively Mungu ametuficha kabisa juu ya uumbaji wa dunia na ulimwengu na ndio maana alianzia kutufunulia pale kwenye mwanga na kuendelea ambayo hata hizo alizotufunulia alieleza in pieces.
Hivi unajua kuwa Mungu aliumba tena kwenye Chapter 2
Chapter 1 aliwaumba mwanamume na mwamake kwa pamoja Mwanzo 1-26
Na katika chapter 2 akamuumba mwanamume kwanza halafu akaja kumuumba mwanamke kutoka kwenye ubavu wa mwanamume
Kama Miamba na maji iliumbwa kwa microsecond kama unavyosema halafu mwanadamu akaumbvwa kwa siku nzima si unaona hapo unaleta confusion na hata mwenyewe baada ya miucrosecond ijayo hutaelewa umeandika ninmi?
nimekupa option mbili ila umechagua Moja. kwa hii uliyoichagua nimesema microsecond kwa sababu hajasema ila anasema yeye mwenyewe aliyeumba kasema siku sita alimaliza kila kitu, na akasema alifanya yote siku sita.
Ila sio ugomvi mkuu, Huu unqodhani ni upumbavu na ufinyu wa uelewa wa maandiko ya siri yalifichwa sana na Mungu ambao unapelekea niamini SIKU SITA LATERAL mimi kwangu naona ni hekima. Unaweza kuendelea na hekima ya Wanadunia na wanasayannsibibilia wanaosema ulimwengu uliumbwa kwa miaka milioni nne.
 
Jambo jingine la kutia changamoto watafsiri wa bible ni kwenye zile siku 6
Biblia inasema Mungu alifanya kazi siku sita na siku ya saba akapumzika
Swali je siku ya nane Mungu aliendelea kufanya kazi?
Na siku zingine je ukiondoa siku ya saba?
Tunaposema hizi siku ni siku katika format ya Mungu mnatubishia
Kwa Mungu hakuna siku ya nane na kuendelea, Maana yake ni nini?
Mungu anaposema siku ya kwanza, ya pili mpaka ya saba kila siku ina maana yake katika mahesabu ya Mungu

Kwa haraka tu
3 ina maana ya ukamilifu
7 ina maana ya undefine au indefinitely au eternity au milele
Maana ya Mungu kufanya kazi siku sita nitaeleza baadaye lakini kumpunzika siku ya saba maana yake amepumzika milele, kazi Mungu alishafanya yooote na hana kazi tena ya kufanya, Ukinibishia hii nitakuja na maandiko punde
so 7 means eternity rest na origin ya sabato ndio huyo
 
Umri wa vyote sio mmoja.Ulimwengu uliumbwa takribani miaka bilioni 13.5 kisha baadaye zikaja kutokea galaxy mbalimbali na baadaye sana dunia pamoja na solar system katika ukanda wa milky way ziliumbwa pamoja na sayari zingine takribani miaka bilioni 3.5 iliyopita
Tofauti ni sizes lakini vyote vimepatikana pamoja kama zao la Big Bang (a.k.a Big explosion). Umri wa vyote ni mmoja.
 
Back
Top Bottom