mitale na midimu
JF-Expert Member
- Aug 26, 2015
- 10,420
- 17,735
uwe unasoma kwa makini mkuu, itakusaidia kujibu majibu sahihi kwa kile unachokiquote.Hii ni Falacy of Generalization. Sio Wanasayansi wote wanakataa uwepo Wa Mungu. Tuwe makini na Hearsay.
Mkuu ni kweli na nakubaliana na wewe kuwa sitakiwi kuwa lateral kwenye kila kitu cha kwenye bibilia, Ila nakubaliana na kuwa Rateral kwenye mambo ambayo ni rateral katika bibilia na Yamethibitika kuwa lateral kwenye Bibilia.Mkuu kwa umakini wako sitegemei na wewe uingie kwenye mlolongo wa kutafsiri maandiko lateral kabisa nakumbuka hata nyuma niliwahi fanya sana na ulikua mstari wa mbele kupinga hilo mfano mada ya Leviathan,Rangi ya Yesu na laana ya canaan so sitegemei kuwepo double standards.
Mfano mwanzo 33 inasema Yakobo alipigana na mtu akamshinda alafu huyo mtu akamuita Israel kisa alipigana na Mungu akashinda je hapo ni lateral kuwa alipigana na Mungu???
Pia ufunuo 5:11 inasema Namba ya malaika ni 10,000×10,000 je unaweza nisaidia kma ni lateral
Ufunuo 7 still inasema waisrael 144000 ndio watakuwa present kwenye mkutano ule je nayo ni lateral??
Labda niulize je ni wakati gani unajua Biblia iko lateral au figurative
Joshua 5:1
1 Ikawa, wafalme wa Waamori, waliokaa ng?ambo ya Yordani pande za magharibi, na wafalme wote wa Wakanaani, waliokuwa karibu na bahari, waliposikia jinsi BWANA alivyoyakausha maji ya Yordani mbele ya wana wa Israeli, hata tulipokwisha kuvuka, basi mioyo yao iliyeyuka
Kwa Sababu alichokisema kwa habari za Siku kulikuwa na practical reference na hata sasa uzao wa walioambiwa wanaendelea kukitekeleza practically sio njozi au hekaya. Siku sita wanafanya kazi siku ya Saba wana Pumzika sawasawa na maelezo manyoofu ya Muumbaji.
1: Bibilia imeweka msingi wa Kila kitu hiyo ndiyo point yangu kuu katika maelezo niliyokupa. Imeweka facts za Milele ambazo uvumbuzi wowote wa kisayansi unajengwa juu yake, na haziyumbishwi na wasanasayansi na mavumbuzi yao. Na kuyumba kwa wanasayansi hakuwezi kuziyumbisha zitadumu milele hata kama zikiaminiwa na watu wawili tu dunia nzima.mpendwa mitale na midimu ahsante na hongera kwa maelezo yako nimekupata uzuri sana. lakini kadili ya maelezo yako binafsi ninamaswali kama mawili tu ivi:
1: kuna mahali umedai kuwa biblia toka mwanzo mpaka ufunuo ina kila kitu na kila fomula (kwa maana kwamba imejibu kila kitu ikiwemo na sayansi yenyewe kwa jinsi nilivokuelewa mimi). swali langu ni hil: ni nini lengo la biblia kwa mwanadamu, ni nini kusudi la biblia kwa mwanadamu, Mungu alikusudia biblia iwe na kazi gani kwa mwanadamu, au kwa nini biblia ???
mpendwa mitale na midimu kama jibu la swali hilo hapo juu kuhusu lengo la biblia kwa mwanadamu ni tofauti kabisa na sayansi na haikukusudiwa kufundisha sayansi, unafikiri ni sahihi au ni haki tunapongangania kutafuta sayansi/ kujifunza sayansi toka kwenye kitabu ambacho hakikukusudiwa kwa kazi hiyo ?.
sikitai kwamba kuna sayansi mbaya na wanasayansi wapinga Mungu/wakana Mungu uwepo wa hao hauifanyi sayansi yote kuwa ni dhambi au kuwalaumu wapinga Mungu kwa kila jambo kwa Mgongo wa sayansi sidhani kama ni sahihi. ninachojua mimi ni kuwa sayansi ni pato la AKILI na MAARIFA tuliopewa na Mungu kama zawadi itusaidie kumpenda, kujua zaidi nk katika maisha yetu ya kila siku. ndio maana imeandikwa usimwache elimu aende zake na pia mpende bwana Mungu wako kwa AKILI zako zote. sasa sayansi ndio moja ya mapato ya izo AKILI au tunaweza kusema ndo AKILI zenyewe. tulipewa mikono na miguu kwa ajili ya kazi njema ya kumtumikia Mungu na jirani lakini kuna watu wanaitumia iyo mikono na miguu kwa kuvunja amri za Mungu kama kuiba, kuumiza, kupigana nk sasa hapo sidhani kama kosa ni mikono au miguu ndivo ilivo kwenye sayansi pia.
sio Kweli.Dunia wala Ulimwengu kwa maana ya miamba haukuumbwa kwa siku sita, mnamtafsiri Mungu tofauti. Zile siku sita za Kimungu kwa sababu Gregory calendar tunayoifuata haikuwepo wakati huo Mungu aliumba vitu vya kuujaza Dunia. Mwanga siku ya kwanza na uumbaji mwingine siku zilizofuata. Tahadhari tu, Hizi siku sita ni za Kimungu na sio 24hrs za kwetu. Uumbaji wa kibiblia unaendana kabisa na ugunduzi wa kisayansi. Kulikuwepo kwanza na uumbaji wa miamba ambao haukuzungumziwa kwenye Biblia, ukafuata kuwepo kwa mfumo wa mwanga nk. Mwanzo 1 haikuenda mbali kuelezea uumbaji kwa sababu sio objective ya Bible. Kwa wale wasomaji watanielewa. Main objective ya Bible ni Salvation of Mankind baada ya anguko. Na ndio maana mimi sitaki kwenda deep kutumia Bible kwenye kuelezea mambo ya uumbaji
Hesabu ya bibilia inakamilikia Kuumbwa kwa adamu, haianzii kuumbwa Kwa Adamu.Utofauti lazima utakuwepo kwa sababu Bible inafanya hesabu kuumbwa kwa Adam ndo mahesabu yameanzia hapo wakati science inapima miamba. Ikumbukwe kwenye Bible binadamu ndo wa mwisho kuumbwa na mchakato wa uumbaji ulikuwa wa miaka mingi sana.
Kutoka 20:11. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.Baada ya uthibitisho wa Ellen kwenda Mbinguni bila kufa kwanza na huko kuona Amri ya sabato imezingirwa na "utukufu?"
Kabla ya day 1 Biblia inasemaKutoka 20:11. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.
'' Petro na Mitume wakajibu wakasema, IMETUPASA KUMTII MUNGU KULIKO MWANADAMU'' Matendo 5:29
Nje ya 24hrs Creation Kuna maelfu ya nadharia kwa jina la Uumbaji wa mamiaka ya milioni.
Jiandae kuogelea kwenye Bottomless pit la mamilioni ya miaka huku unaacha ukweli mwororo wa Kauli sahihi na dhahiri ya Mungu huku ukitumia vikokotoo vya lugha za kiebrania kama mbeleko.
Kufanya Tallying ya Uumbaji wa Bibilia na secret evolution Ideas based on bible utafanikiwa at Infinity.
Mungu aliumba Mbingu na Nchi hapo mwanzo. Sio Maji na Miamba.Kabla ya day 1 Biblia inasema
‘In the beginning God created the heavens and the earth. And the earth was formless and void, and darkness was over the surface of the deep; and the Spirit of God was moving over the surface of the waters. Then God said, “Let there be light”; and there was light. And God saw that the light was good; and God separated the light from the darkness. And God called the light day, and the darkness He called night. And there was evening and there was morning, one day.’
Hii mistari inaonyesha kwamba UUMBAJI ulianza baada ya kuwepo a VOID and FORMLESS EARTH. Roho ya Mungu ikielea juu ya maji
Hayo yalitokea kabla ya kuanza uumbaji wa day one. Hata mtoto wa kindergarten anaweza kudadavua hii.
Umbaji wa mwanga ulianza day one wakati maji na miamba ilishakuwepo, Ndio maana nasema UUmbaji wa Miamba hakufanyika katika six day (This are NOT literal day, utaendelea kujidanganya mpaka lini ndugu
Hii ya microsecond tukubaliane ni ya kwako tu!Mungu aliumba Mbingu na Nchi hapo mwanzo. Sio Maji na Miamba.
Hapo Kuna Mawili Sentensi hiyo inaanza na summary ya kazi Yote aliyoifanya kisha akaanza kuichanganua.
Pili, Aliumba hayo Mwa Milisecond ambayo inamezwa na Siku ya Kwanza.
2
Kwa nini najenga hoja hizi ambazo unaweza kuona natembea juujuu bila ufahamu wa Bibilia na siri zake.
Mungu anataka tusitafute habari za Mqmbo yake kwa waganga, wqchawi wasihiri hata wasomi.
Kuhusu hili, Bibilia au mwqnzo Ingeishia hapo tungekubaliana ila Mungu alieyeumba Vyote Kuanzia Mbingu na Nchi na Vyote Vilivyomo amerudia mahala mahala kuwa alifanya Yote kwa Muda wa siku sita. Sio alizijaza mbingu na nchi ndani ya Siku Sita.
Kosa mnalofanya kulazimisha nadharia za Sayansi zitally na mambo ambayo Mungu ameshayafafanua huku mkiegemea kwenye evolution. Bibilia Ingeishia Mwqnzo 1 na 2 Tungechanganyikiwa ilq hili limefafanuliwa vizuri kwenye amri Kumi. Yesu naye akatia Muhuli kuwa Aliumna Siku ya Saba kwa aajili ya Wanadamu.
Wakosoaji wa Bibilia Waislam, Atheists na Higher cliticals ndio wanautamaduni wa kung'ang'ania kistali huku wakiwa hawataki ufafanuzi ndani ya Bibilia ulio wazi mahala pengine pakifafanua tukio hilohilo.
Katika Hili naomba niendelee kuwa mjinga kuliko kujiunga na wenye hekima wa dunia hii.
Mkuu ndio maana nimeuliza je ni wakati gani ambapo unagundua ni lateral au figurative language ndio imetumika.... Mfano Yesu kasema kuhusu hao waisrael 144000 na malaika wapo 10,000×10,000 je na sisi tuisome hiyo lateral kisa tu Yesu ndio kafafanua?? Ama unakubaliana na mimi kuwa zote ni parables zenye mafumbo ikiwemo creation process???Mkuu ni kweli na nakubaliana na wewe kuwa sitakiwi kuwa lateral kwenye kila kitu cha kwenye bibilia, Ila nakubaliana na kuwa Rateral kwenye mambo ambayo ni rateral katika bibilia na Yamethibitika kuwa lateral kwenye Bibilia.
Ungeonyesha madhaifu ya hiyo kutoka20 kwa nini sio lateral ili namimi nionyeshe kuwa ni lateral tuchanganua vizuri zaidi.
Binafsi naamini.
Matukio ya Mwanzo sio mafumbo au mambo ya kufikilika ni historia halisi. Yesu aliamini hivyo Mitume waliamini hivyo. Katikati ya Historia hiyo kunaweza Kuwa na Matukio ya Njozi, na mengine ya Mifano. Ila Hili la Uumbaji ikiwa Muhusika amelitolea ufafanuzi sioni haja ya kulazimisha usayansi, au kuliforce tukio linyenyekee wanasayansi hata kama Mungu amefafanua.
Nani kwanini hizo siku zingine hakuumba kwa microsecond wakati yeye ni Mungu mwenye uwezo?Hii ya microsecond tukubaliane ni ya kwako tu!
Hakuna mtu anayekataa kuwa Mungu hakuumba mbingu na nchi
Ila haya mambo ya uumbaji kuna a lot of misinterpretations kuanzia kwenye tafsiri ya hizo siku sita na the creation process
Nataka tu kukuambia kuwa intentively Mungu ametuficha kabisa juu ya uumbaji wa dunia na ulimwengu na ndio maana alianzia kutufunulia pale kwenye mwanga na kuendelea ambayo hata hizo alizotufunulia alieleza in pieces.
Hivi unajua kuwa Mungu aliumba tena kwenye Chapter 2
Chapter 1 aliwaumba mwanamume na mwamake kwa pamoja Mwanzo 1-26
Na katika chapter 2 akamuumba mwanamume kwanza halafu akaja kumuumba mwanamke kutoka kwenye ubavu wa mwanamume
Kama Miamba na maji iliumbwa kwa microsecond kama unavyosema halafu mwanadamu akaumbvwa kwa siku nzima si unaona hapo unaleta confusion na hata mwenyewe baada ya miucrosecond ijayo hutaelewa umeandika ninmi?
Habari za mchana wakuu kama kawaida huwa nakuja na mada za kuchokoza fikra zetu hasa kwenye mambo ya kiimani hivyo mada hizi sio za kukosoa dini fulani au vitabu vya imani ila ni kuhoji tu ili tupanue fikra zetu kwenye masuala haya kwa faida yetu sote so sitegemei iibue mijadala ya kidini bali kuelimishana juu ya mambo haya baada ya kusema hayo twende moja kwa moja kwenye mada husika ya leo.
View attachment 948749
Biblia na umri wa Dunia
Mwaka 1650 professor wa masuala ya theologia na Askofu wa makanisa ya protestant wa Ireland John Ussher aliandaa maandiko yake kupitia mfululizo wa vitabu vyake kuanzia cha Annals of the Old Testament: Origins of the world ambacho ndani yake aliibua mjadala mpana sana wa karne nyingi sana. Ussher alipiga hesabu ya muda ulivyopita kati ya Adam kuumbwa hadi Yesu kuzaliwa na kugundua kwamba ni miaka 4000 imepita tokea Adam aumbwe hadi Yesu kuzaliwa hivyo kufanya dunia yetu ikiwa na wanadamu kuwa na miaka elfu 6 pekee mpaka sasa!!. Ussher alitumia maandiko kama chanzo cha nadharia yake alitumia nyaraka za masoretic zilizotumika kuandaa Biblia za agano la kale ili kuweza hesabu umri wa Adam hadi vizazi vya Abraham hadi kufikia Yesu na baada ya mnyambuliko huo alifanikiwa kugundua kwamba dunia iliumbwa usiku wa October 23 4004 kabla ya kristo.
Young Earth Creationists
Vuguvugu hili la YEC lilianza miaka ya 1960 ambapo iliasisiwa na wasomi 9 chini ya PhD wa theolojia na uhandisi Bwana Henry Morris wakijikita kwenye utafiti wa uhalisia wa umri wa dunia na uumbaji na wakahitimisha rasmi kuwa dunia tunayoishi iliumbwa ndani ya miaka elfu 10 pekee na sio zaidi ya hapo na wao pia walitumia maandiko ya Biblia ya kiebrania ili kufikia hitimisho hilo hivyo na wao wakaunga mkono hoja za hapo nyuma za Professor John Ussher na hata leo hii wameweza shawishi zaidi ya 40% ya wakazi wa marekani kwa takwimu za 2017 wanaamini nadharia hii kwamba uumbaji wa dunia ni kwa mujibu wa Biblia hauzidi miaka 10,000 iliopita.
View attachment 948751
SAYANSI inasemaje??
Baada ya sayansi na teknolojia kukua na kuongezeka vifaa vya kupima umri wa miamba,mazao na mifupa ya wanyama wakaibuka wasomi wa sayansi waliohoji kuhusu uhalali wa nadharia hizi na imeleta utata na mjadala mzito kwa miaka mingi sasa. Mwanasayansi wa karne ya 20 Clair Cameron Patterson baada ya tafiti kadhaa juu ya miamba akagundua ulimwengu toka uanze una miaka billion 4.5 na baadae wanasayansi mbalimbali wakaja na tafiti mbalimbali zikidai kwa usahidi wa kisayansi na kiacholojia kwamba uhai duniani umekuwepo miaka takriban 3.8 Billion iliopita hivyo kukinzana kabisa na nadharia hizo mbili za juu kuwa Biblia
Jinsi ya kupima
Kwa upande wa Young Earth wao wanalalia maandiko kwa kiasi kikubwa na kupiga hesabu miaka ya kibiblia tokea Adam hadi Yesu lakini wanasayansi wamepiga hesabu zao kwa ushahidi wa kushikika wakitumia mfumo unaitwa radiometric dating ambacho kinapima miamba hasa stage tofauti za jinsi miamba inavyooza na ambapo kila stage ina umri wake yake yaani miaka kadhaa ili ifike stage nyingine ya kuoza hivyo wanapiga hesabu kuanzia layer ya mwisho mpaka ya kwanza na kufikia hitimisho la umri wa mwamba huo na wakafanikiwa kugundua mwamba wa kwanza ulitokea miaka 3.8 Billioni iliyopita.
View attachment 948748
Utafiti wangu (Primary)
Binafsi nilichukua hatua kuonana na wanatheolojia kadhaa kutoka chuo fulani cha Biblia wenye ngazi ya PhD na wamenijuza kwamba Biblia haikuandikwa kwa maneno bali mafumbo hivyo isitafsiriwe kwa maana zetu bali kwa mafunuo na maana zilizo kwa Biblia... Mfano wanadai Dunia haikuumbwa kwa siku 7 kama zetu hizi bali miaka mamilion na wakaenda mbali kusema Biblia haikuanza kuandika matukio yote bali imeandika matukio juu ya watu waliochaguliwa tu hivyo wanakiri kuwa kweli dunia ina miaka mabillion na sio miaka elfu 6 pekee bali wanaotafsiri maandiko kwa akili zao ndio wanapotosha sababu wameitafsiri maneno kama yalivyo badala ya kutafuta maana ya hayo mafumbo na wakanipa mistari michache.
Yohana 16:25
25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa yaja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba.
Na wakaenda mbali kusema hata hayo mafumbo walioambiwa kuandika Biblia hawakuyaelewa sababu ni siri imewekewa hadi wakati muafaka yaani mwisho wa dunia ufike soma hapa kisa cha Daniel
Daniel 12:4
4 Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.
Hapa tunaona kuna maandiko na nabii zimefichwa kwa uelewa wetu kabisa hata Daniel hakuelewa!!
Daniel 12:8-9
8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?
9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa mwisho.
Hivyo kama hata Daniel kuna baadhi ya vitu alifichwa na mpaka anaandika hakuvijua basi hata sisi hatuwezi vijua mpaka siku ya mwisho hivyo wakahitimisha mjadala kwa kusema huenda ni kweli dunia ina 4.5 Billion years ila sio 6000 kama YEC inavyosema maana Biblia haielezi hicho kuwa ni miaka 6000 bali watu wanatafsiri maandiko kwa akili zao ilihali YAMEFICHWA!!
View attachment 948750
Hitimisho
Ukinzano huu kati ya maandiko na sayansi juu ya asili ya umri wa ulimwengu umezua mjadala mpana sana huku kila upande ukivutia kwake nikaona kwa kuwa JF ni kisima cha maarifa nilete hii mada ili tuweze kufikiria pamoja je umri wa dunia upi ni halisi
4.5 Billion ama 6000?
Naomba kuwasilisha
nimekupa option mbili ila umechagua Moja. kwa hii uliyoichagua nimesema microsecond kwa sababu hajasema ila anasema yeye mwenyewe aliyeumba kasema siku sita alimaliza kila kitu, na akasema alifanya yote siku sita.Hii ya microsecond tukubaliane ni ya kwako tu!
Hakuna mtu anayekataa kuwa Mungu hakuumba mbingu na nchi
Ila haya mambo ya uumbaji kuna a lot of misinterpretations kuanzia kwenye tafsiri ya hizo siku sita na the creation process
Nataka tu kukuambia kuwa intentively Mungu ametuficha kabisa juu ya uumbaji wa dunia na ulimwengu na ndio maana alianzia kutufunulia pale kwenye mwanga na kuendelea ambayo hata hizo alizotufunulia alieleza in pieces.
Hivi unajua kuwa Mungu aliumba tena kwenye Chapter 2
Chapter 1 aliwaumba mwanamume na mwamake kwa pamoja Mwanzo 1-26
Na katika chapter 2 akamuumba mwanamume kwanza halafu akaja kumuumba mwanamke kutoka kwenye ubavu wa mwanamume
Kama Miamba na maji iliumbwa kwa microsecond kama unavyosema halafu mwanadamu akaumbvwa kwa siku nzima si unaona hapo unaleta confusion na hata mwenyewe baada ya miucrosecond ijayo hutaelewa umeandika ninmi?
Tofauti ni sizes lakini vyote vimepatikana pamoja kama zao la Big Bang (a.k.a Big explosion). Umri wa vyote ni mmoja.