Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Ni sahihi mbingu,duniabna vilivyomo kuumbwa katika siku sita,. Ilaa hesabu hasa ya siku kwa mujibu Wa muumba ni miaka elfu kwaa masaa haya 24

Ata kwenye kitabu hichi kitukufu kimeeleza hivyo,



( الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۚ الرَّحْمَٰنُ فَاسْأَلْ بِهِ خَبِيرًا )

الفرقان (59) Al-Furqaan

Ambaye ameziumba mbingu na ardhi, na viliomo ndani yake kwa siku sita. Kisha akatawala juu ya A'rshi, Arrahman, Mwingi wa Rehema! Uliza khabari zake kwa wamjuaye.
ubunifu wa miaka mamilioni ni tafrisi za kisasa za mamno ya Mungu, hasa watu wa dini walipojilazimisha kujipendekeza kwenye kila sayansi bila kujua pamoja na uzuri wake wote wanasayansi wanaoaminini hayo mamiaka milioni wanawachukia kabisa na kuwatenga wenzao wanasayansi wanaoamini uumbaji wa siku sita tu.
mmoja wao ni mvumbuzi wa MRI scanner, alinyimwa hadi tuzo ya nobel 2003 na akapewa jamaa mwingine.

Kuna watu wa dini nao wameingia kwenye huu mtego. Dunia inahamishwa kwa kasi kutoka katika original creation na kwa ujanja wa hali ya juu tunafanywa kuamini evolution theory.

Kama Kitabu Quran kimesema jambo ambalo Kaka yake Bibilia imeliweka sawa miaka mingi kabla yake. Basi pia ni habari njema katika hilo.

Hata kwenye sayansi tunapaswa kujua kuna mgawanyiko, wapo wanaoamini creation ya siku sita, na mainstream wanaoamini mamilioni.
 
Kwa kuwa huuuu ni mjadala huu, Maoni yangu ni kuwa Dunia hii ina umri mrefu sana kuliko miaka 6,000/=. Aidha mwanadamu atakuwa na umrefu mrefu kushinda hiyo miaka 6000.

Machache ninayoelewa kutoka ndani ya kitabu kitukufu cha Qur'an ni kuwa: Ulimpitikia umri mrefu sana (Dahari ya miaka) mwanadamu alikuwa sio kiumbe mwenye kutajwa katika dunia hii.

Qur'an 76: 1 - 3
Hakika kilimpitia binadamu kipindi (dahari) katika zama ambacho kwamba hakuna kitu kinachotajwa.
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hiyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
Hakika Sisi tumembainishia njia, Ama mi mwenye kushukuru, au ni mwenye kukanusha.

Kwa hiyo, ni wazi kuwa kulikuwa na kipindi kirefu sana toka Dunia ilipoumba kama zao la Big Bang hadi pale mwanadamu (Adam) alipoumbwa na kuletwa Napa duniani.
Sihitaji kuhoji umakini wa vifaa vilivyotumika kisayansi kupima umri wa Dunia na kuja na conclusion ya 4.5B years lakini dunia ina umri mrefu sana kuliko umri halisi wa mwanadamu.
"Hakika sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika"
Samahani Kiongozi,hiyo SISI inasimama kuwawakilisha wakina nani?
Mungu alishirikiana na nani kwenye uumbaji wa binadamu?
Nahitaji kuelewa,nitashukuru kama utanielewesha.
 
mkuu zitto junior
mada yako inazungumzia birthday ya dunia.
Radiometric dating haijawahi kutoa usahihi wa umri wa kitu based on its birthday.
hata kama ipo hapo UDSM tunaweza kuomba experiment hata moja inayoongesha hata mtoto wa Mbuzi kazaliwa leo, akawekwa kwenye cage baada ya mwaka akapimwa ikathibitika anamwaka hata mmoja.

Tukikimbilia kwenye mamilioni ambayo hayana ushahidi, wala hakuna wa kuulizwa ambaye atatumika kama ushahidi wa jibu kuna uwezekano kudanganywa.
Labda kama wapo maarchealogists, Paleantologists na geologists humu waje watusaidie.
 
Dunia ina umri 0.00000000000000000000000000000000001microtrilosecond
Yap wewe ndio kila kitu

Waumini wa Mungu kitabu wanaamini kwenye time travel mwenye upako na aende arudi na majawabu
 
Asante Makosa kwa kuniita! Mjadala huu ni mzuri sana. Na ningependa niutendee haki. Kwa harakaharaka tu ni kwamba Wanasayansi wameshathibitisha kwa kutumia vifaa vya kisasa kabisa kwamba dunia na ulimwengu vimekuwepo kwa zaidi ya miaka 4.5 bilioni iliyopita. Na mimi nasema,matokeo ya utafiti ya hawa jamaa yanatupatia ile picha kwamba Uumbaji Ulimwengu ulitokea muda mrefu sana uliopita.

Ukokotoaji uliofanywa na Mprotestanti Ussher una mapungufu kwa sababu yeye amekaba kanuni yake kwa kuangalia miaka wanayotajwa watu muhimu katika historia ya Wayahudi kuishi. Sasa kanuni hiyo ina makengeza kwa sababu dunia hii haikuwa na watu wanaotokana na Lineage ya Kiyahudi tu. Dunia imekuwa na watu wengi tu waliokuwa wakihama kutoka sehemu moja hadi nyingine ambako walianzisha Jumuia zingine au Mataifa mbalimbali. Kwa hiyo ukitumia Umri Wa watu wanaotokana na Taifa moja tu unakuwa umeingia katika upotoshaji.

Sababu ya pili ya upungufu katika kanuni hiyo ni kwamba namba zinazotajwa katika Biblia hazina maana ya moja kwa moja katika uhesabuji namba(Literal meaning). Kwa mfano,Yesu alipofunga kwa siku 40 Arobaini haina maana ya siku 40 kweli Bali kwamba mfungo wake ulikuwa Wa muda mrefu na ulikamilika kama alivyokuwa amepanga. Yaani, Ratiba ya mfungo ilifika mwisho kabisa na haikukatishwa licha ya changamoto ya njaa iliyojitokeza.

Kwa hiyo, tutumie Sayansi katika kufahamu Umri Wa Ulimwengu na Dunia.
mkuu wanasayansi umetumia kama kokoro.
unaweza kuchanganua wanasayansi gani, maana sio wote wanaoamini hayo.
wapo creation scientist mamia ulimwenguni wanaamini katika 24 hrs day creation.
Newton aliamini.
Galileo aliamini.
Johan Kepler, Boyle, M. Faradays etc
na wengine wengi wa kisasa wanaamini.
Wapo wa creationscience UK wanahadi Lab ya kuthibitisha kuwa dunia ni changa kabisa kwa mujibunwa bibilia.

changanua vizuri mkuu ili uelewa uwe sawia
Pia kama Muumini wa Neno la Mungu, Unapaswa kuwa makini na kila kinachotoka kwa wanasayansi sio kila wanachosema ni sahihi kulingana na biblical basis. Mfano leo wanasema Ushoga ni matokeo ya Vinasaba. Watu wa Mungu wanaoamini kila kitu cha mwanasayansi wajiandae kuhalalisha ushoga kwa vizazi vyao maana umehalalishwa maabara ya wanasayansi wanaowapenda na kuamini kila wanachosema.
Basisi ya Research nyingi ninabsence ya Mungu, hivyo sio tusiamini bali wanaweza kuja na conclusion inayopromote upingwaji wa Mungu. Hivyo wanadini wanaouwaunga mkono itabidi wakubaliane nao ili kudumisha upenzi wao.

Haya Yote yanatutaka tuwe makini siontupuuzekila kitu, ila pembeni Bibilia pembeni science as a tool of exploring creation.
Ndivyo alivyoamini Galileo, corpenicos na wakagundua mambo makubwa ya ukweli kutoka katika uumbaji wa Mungu.

Pia kama mkuu Sala na Kazi alivyotoa hoja, kwa sababu science ni progressive kila siku wanavumbua mapya wanaweza kuvumbua kile ambacho tunakisema pia, ingawa trend haionyeshi hilo.
 
Habari za mchana wakuu kama kawaida huwa nakuja na mada za kuchokoza fikra zetu hasa kwenye mambo ya kiimani hivyo mada hizi sio za kukosoa dini fulani au vitabu vya imani ila ni kuhoji tu ili tupanue fikra zetu kwenye masuala haya kwa faida yetu sote so sitegemei iibue mijadala ya kidini bali kuelimishana juu ya mambo haya baada ya kusema hayo twende moja kwa moja kwenye mada husika ya leo.
View attachment 948749
Biblia na umri wa Dunia
Mwaka 1650 professor wa masuala ya theologia na Askofu wa makanisa ya protestant wa Ireland John Ussher aliandaa maandiko yake kupitia mfululizo wa vitabu vyake kuanzia cha Annals of the Old Testament: Origins of the world ambacho ndani yake aliibua mjadala mpana sana wa karne nyingi sana. Ussher alipiga hesabu ya muda ulivyopita kati ya Adam kuumbwa hadi Yesu kuzaliwa na kugundua kwamba ni miaka 4000 imepita tokea Adam aumbwe hadi Yesu kuzaliwa hivyo kufanya dunia yetu ikiwa na wanadamu kuwa na miaka elfu 6 pekee mpaka sasa!!. Ussher alitumia maandiko kama chanzo cha nadharia yake alitumia nyaraka za masoretic zilizotumika kuandaa Biblia za agano la kale ili kuweza hesabu umri wa Adam hadi vizazi vya Abraham hadi kufikia Yesu na baada ya mnyambuliko huo alifanikiwa kugundua kwamba dunia iliumbwa usiku wa October 23 4004 kabla ya kristo.

Young Earth Creationists
Vuguvugu hili la YEC lilianza miaka ya 1960 ambapo iliasisiwa na wasomi 9 chini ya PhD wa theolojia na uhandisi Bwana Henry Morris wakijikita kwenye utafiti wa uhalisia wa umri wa dunia na uumbaji na wakahitimisha rasmi kuwa dunia tunayoishi iliumbwa ndani ya miaka elfu 10 pekee na sio zaidi ya hapo na wao pia walitumia maandiko ya Biblia ya kiebrania ili kufikia hitimisho hilo hivyo na wao wakaunga mkono hoja za hapo nyuma za Professor John Ussher na hata leo hii wameweza shawishi zaidi ya 40% ya wakazi wa marekani kwa takwimu za 2017 wanaamini nadharia hii kwamba uumbaji wa dunia ni kwa mujibu wa Biblia hauzidi miaka 10,000 iliopita.

View attachment 948751
SAYANSI inasemaje??
Baada ya sayansi na teknolojia kukua na kuongezeka vifaa vya kupima umri wa miamba,mazao na mifupa ya wanyama wakaibuka wasomi wa sayansi waliohoji kuhusu uhalali wa nadharia hizi na imeleta utata na mjadala mzito kwa miaka mingi sasa. Mwanasayansi wa karne ya 20 Clair Cameron Patterson baada ya tafiti kadhaa juu ya miamba akagundua ulimwengu toka uanze una miaka billion 4.5 na baadae wanasayansi mbalimbali wakaja na tafiti mbalimbali zikidai kwa usahidi wa kisayansi na kiacholojia kwamba uhai duniani umekuwepo miaka takriban 3.8 Billion iliopita hivyo kukinzana kabisa na nadharia hizo mbili za juu kuwa Biblia

Jinsi ya kupima
Kwa upande wa Young Earth wao wanalalia maandiko kwa kiasi kikubwa na kupiga hesabu miaka ya kibiblia tokea Adam hadi Yesu lakini wanasayansi wamepiga hesabu zao kwa ushahidi wa kushikika wakitumia mfumo unaitwa radiometric dating ambacho kinapima miamba hasa stage tofauti za jinsi miamba inavyooza na ambapo kila stage ina umri wake yake yaani miaka kadhaa ili ifike stage nyingine ya kuoza hivyo wanapiga hesabu kuanzia layer ya mwisho mpaka ya kwanza na kufikia hitimisho la umri wa mwamba huo na wakafanikiwa kugundua mwamba wa kwanza ulitokea miaka 3.8 Billioni iliyopita.
View attachment 948748
Utafiti wangu (Primary)
Binafsi nilichukua hatua kuonana na wanatheolojia kadhaa kutoka chuo fulani cha Biblia wenye ngazi ya PhD na wamenijuza kwamba Biblia haikuandikwa kwa maneno bali mafumbo hivyo isitafsiriwe kwa maana zetu bali kwa mafunuo na maana zilizo kwa Biblia... Mfano wanadai Dunia haikuumbwa kwa siku 7 kama zetu hizi bali miaka mamilion na wakaenda mbali kusema Biblia haikuanza kuandika matukio yote bali imeandika matukio juu ya watu waliochaguliwa tu hivyo wanakiri kuwa kweli dunia ina miaka mabillion na sio miaka elfu 6 pekee bali wanaotafsiri maandiko kwa akili zao ndio wanapotosha sababu wameitafsiri maneno kama yalivyo badala ya kutafuta maana ya hayo mafumbo na wakanipa mistari michache.

Yohana 16:25
25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa yaja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba.

Na wakaenda mbali kusema hata hayo mafumbo walioambiwa kuandika Biblia hawakuyaelewa sababu ni siri imewekewa hadi wakati muafaka yaani mwisho wa dunia ufike soma hapa kisa cha Daniel

Daniel 12:4
4 Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.

Hapa tunaona kuna maandiko na nabii zimefichwa kwa uelewa wetu kabisa hata Daniel hakuelewa!!

Daniel 12:8-9
8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?
9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa
mwisho.

Hivyo kama hata Daniel kuna baadhi ya vitu alifichwa na mpaka anaandika hakuvijua basi hata sisi hatuwezi vijua mpaka siku ya mwisho hivyo wakahitimisha mjadala kwa kusema huenda ni kweli dunia ina 4.5 Billion years ila sio 6000 kama YEC inavyosema maana Biblia haielezi hicho kuwa ni miaka 6000 bali watu wanatafsiri maandiko kwa akili zao ilihali YAMEFICHWA!!
View attachment 948750
Hitimisho
Ukinzano huu kati ya maandiko na sayansi juu ya asili ya umri wa ulimwengu umezua mjadala mpana sana huku kila upande ukivutia kwake nikaona kwa kuwa JF ni kisima cha maarifa nilete hii mada ili tuweze kufikiria pamoja je umri wa dunia upi ni halisi

4.5 Billion ama 6000?

Naomba kuwasilisha

Fungu la kwanza hapo chini linalotoka kitabu cha Mwanzo 1, linasema wazi kabisa kuwa Mungu alianza akaumba Mbingu na Nchi kwanza halafu ukapita muda ambao hatujaelezwa ni muda gani, halafu ndiyo akafanya yale yote yanayoelezwa kuanzia fungu la 3.

Kwa hiyo ieleweke wazi kuwa
MOJA Alichofanya Mungu kinachoelezwa kuanzia Mwanzo 1:3 na kuendelea si uumbaji bali ilikuwa ni urekebishaji, nyongeza vikiambatana na upambaji wa kile ambacho tayari alikuwa aameshaumba huko nyuma.
MBILI Mungu huwa hahitaji kitu phsical katika uumbaji, huwa anatamka tu halafu kilichokuwa hakipo kinakuwepo. Ukiona anatamka kwa kitu kitu phsical, ujue hapo haumbi ila anafanya marekebisho, yaani modification.
TATU Aliwaumba Adam na Hawa kwa kutamka wakiwa ni roho zisizokuwa na mwili ndani ya NAFSI MOJA, baadaye tena akawafanyia marekebisho kwa kufinyanga udongo akawapa miili.Huu udongo ulikuwepo kabla ya watu hawa, Mungu alikuwa ameshauumba huko nyuma
NNE Kutokana na hoja hizo hapo juu,Mungu hakuumba ulimwengu kipindi anawaumba Adam na Eva ila ulimwengu ulikuwepo tangu kipindi kirefu huko nyuma. Hii inathibitishwa na hilo fungu la Mwanzo 1:1 na na mengine yote yanayofuata kwenye sura hiyo
TANO. Muumini yeyote wa dini anayeaamini kuwa ulimwengu una miaka 6000 hayuko sahihi, bali tangu kuumbwa Adam ndiyo miaka 6000. Ulimwengu ulikuwepo kabla ya Adam
SITA Wana Sayansi wanaofanya tafiti kwa mfano za miamba na kugundua kuwa kuna miamba ina miaka mabillion tangu kuwepo kwake, WAKO SAHIHI NA HAWAPINGANI NA BIBLIA, kwa sababu Biblia yenyewe inathibitisha kuwepo kwa ulimwengu kabla ya Adam, kwenye hilo fungu la Mwanzo 1:1
SABA Muumini yeyote ambaye alikuwa na taarifa zisizo sahihi kuwa ulimwengu uliumbwa miaka 6000 iliyopita, naomba arejee tena kusoma Mwanzo 1:1 na atusaidie kutoa tafsiri upya, kama pengine kama haya niliyoyasema hapo juu anadhani hayako sahihi

1Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi
2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.
4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.
5 Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.
6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.
10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
11 Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo.
12 Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
13 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tatu.
14 Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka;
15 tena iwe ndiyo mianga katika anga la mbingu itie nuru juu ya nchi; ikawa hivyo.
16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia.
17 Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi
18 na kuutawala mchana na usiku na kutenga nuru na giza; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
19 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya nne.
20 Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.
21 Mungu akaumba nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
22 Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi.
23 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tano.
24 Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo.
25 Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
29 Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;
30 na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo.
31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.
 
ubunifu wa miaka mamilioni ni tafrisi za kisasa za mamno ya Mungu, hasa watu wa dini walipojilazimisha kujipendekeza kwenye kila sayansi bila kujua pamoja na uzuri wake wote wanasayansi wanaoaminini hayo mamiaka milioni wanawachukia kabisa na kuwatenga wenzao wanasayansi wanaoamini uumbaji wa siku sita tu.
mmoja wao ni mvumbuzi wa MRI scanner, alinyimwa hadi tuzo ya nobel 2003 na akapewa jamaa mwingine.

Kuna watu wa dini nao wameingia kwenye huu mtego. Dunia inahamishwa kwa kasi kutoka katika original creation na kwa ujanja wa hali ya juu tunafanywa kuamini evolution theory.

Kama Kitabu Quran kimesema jambo ambalo Kaka yake Bibilia imeliweka sawa miaka mingi kabla yake. Basi pia ni habari njema katika hilo.

Hata kwenye sayansi tunapaswa kujua kuna mgawanyiko, wapo wanaoamini creation ya siku sita, na mainstream wanaoamini mamilioni.
Mbona sekta nyingi tu biblia na Quran vinafanana, hasa visa. Sema mjinga aliyekuja kututofautisha ndiyo kazingua Tungekuwa wamoja.
 
mkuu zitto junior
mada yako inazungumzia birthday ya dunia.
Radiometric dating haijawahi kutoa usahihi wa umri wa kitu based on its birthday.
hata kama ipo hapo UDSM tunaweza kuomba experiment hata moja inayoongesha hata mtoto wa Mbuzi kazaliwa leo, akawekwa kwenye cage baada ya mwaka akapimwa ikathibitika anamwaka hata mmoja.

Tukikimbilia kwenye mamilioni ambayo hayana ushahidi, wala hakuna wa kuulizwa ambaye atatumika kama ushahidi wa jibu kuna uwezekano kudanganywa.
Labda kama wapo maarchealogists, Paleantologists na geologists humu waje watusaidie.
Ngumu kupata jawabu halisi wengi wanakadiria na hata makadirio yenyewe tu yanautata
 
Kaka Bishop Hiluka , mitale na midimu , mshana jr naona mnaitendea haki sana Maada iliyopo Mezani,
Mimi naamini kuwa Sayansi inaconfirm kilichopo kwenye Bible, Fungu la kwanza la kitabu cha Mwanzo kinasema,
Mwanzi 1:1-2 Hapo Mwanzo Mungu aliziumba mbingu na Nchi, 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; roho ya mungu ikatua juu ya uso wa Maji. UKIANGALIA NA KUTAFAKARI HAYO MANENO YA MWANZO 1:1-2 UTAONA KUWA MUNGU ALIZIUMBA MBINGU NA NCHI NA MAJI SIKU NYINGI KABLA YA ZILE SIKU SABA, HATUNA UHAKIKA NI SIKU AU MIAKA MINGAPI, LAKINI MUNGU ALIUMBA MBINGU NA NCHI NA MAJI KWANZA

ukija kwenye Mwanzo 1:3 ndio zile siku saba zinapoanza, je kabla ya siku saba kuanza Dunia ilikuwa na miaka mingapi?, kwa uwezo tuliopewa na Mungu kwa kutumia sayansi ndio tunaweza kung'amua hiyo code kuwa Dunia ni nzee sana Probably 4.5 bil yrs, miaka 6000 wanayoizungumza hao makasisi ni kuanzia zile siku saba, je kabla ya hapo?

CC: zitto junior
Mkuu asante kwa hoja.
hoja hii aliyoleta mkuu inachangamoto kubwa sana na inaleta uelewa mpya na migogoro hata kwa waumini wa bibilia.
wengi hata wa imani moja wanaibuka na kutofautiana pia.

Makasisi/wachungaji na wanatheolojia wengi wa kisasa wanabishana na kutofautiana katika hili wengine wakiungana na wanasayansi wanaoamini miyo miaka mamilioni wengine wakiungana na wanasayansi wanaosema ni miaka kama 6000 tu.

Msingi wa hoja yangu katika hili. Hatujui ilichukua muda gani kwenye mwanzo 1:1 au Mwanzo 1:3
Ila kabla hatujaruka bibilia na kuwauliza wanasayansi tukiiuliza bibilia inasema wazi kupitia Mungu huyohuyo aliyehusika kuumba kuwa yote yalifanyika kwa siku sita. Na Kumbukumbu ya siku hizo sita ilimtofautisha Mungu wa waisrael na Miungu mingine yoyote iliyokuwepo enzi zile. Na wakristo wanamuamini Yesu, Na Bibilia Inasema Hakuna kilichofanyika pasipo yeye Yesu, Basi naamini hata Yesu anatutaka Turudi kuheshimu Ufafanuzi wa Bibiliq kqbla ya sayansi.

Kwa nini?
Sayansi Inabadilika, na Bado inagap Kubwa la ufahamu kuliko ilivyovifahamu, Haina Vifaa reliable undebatable vya kutatua utata huu bila shida.
Ila Bibilia Inatutaka tuiamini kama Ultimate truth na ukweli usiobadilika hadi mwisho hivyo inatoa mwanya mpana wa kujadili pia. Ndio maana naamini mada hizi zote zinaibuka na zitaendelea kuibuka kwa sababu tuliutupilia mbali ule mpango wa Ile amri Ya sabato ambayo inawataka wanadamu wakumbuke 6 literal days of creation na sio mamilioni.

maoni mkuu, tunaweza kupingana bila kukwanguana piq. Maana haya mambo sio yetu ni Ya yeye aliyeumba.
 
"Hakika sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika"
Samahani Kiongozi,hiyo SISI inasimama kuwawakilisha wakina nani?
Mungu alishirikiana na nani kwenye uumbaji wa binadamu?
Nahitaji kuelewa,nitashukuru kama utanielewesha.

Ahsante kwa swali lako zuri: Nina lako linasadifu vizuri - Ngumbaru.
Ngoja tumuulize Mwenyezi Mungu mwenyewe aliye Mtaalamu na mwanzilishi wa Lugha:

"Na hatukumtuma kabla yako mtume yeyote Ila tulimfunulia ya kwamba Hapana mungu Ila MIMI. Basi niabuduni MIMI tu". (Qur'an 21:25)

"Hakika MIMI ndiye Mwenyezi Mungu, Hapana mungu ila MIMI tu. Basi niabuduni MIMI na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka MIMI." (Qur'an 69:14).

Naamini umeelewa vizuri kakangu. Kama hujaelewa naomba karibu uulize tena.

NB: Kwa msaada Zaidi kama wewe ni Mkristo nenda kasome mwanzo pale Mungu anaposema "Natufanye MTU kwa mfano WETU. ……..Kisha Mungu akamuumba MTU kwa mfano WAKE.
SIYO KWA MFANO WAO.
 
Wamepima kuanzia Adam alipoumbwa!
Mbona tunasoma humu ndani Kuwa Dunia ilikuwa ina watu kabla ya Ujio wa Adamu?

Samahani kama nitakuwa sijaeleweka maana sipo vizuri kwenye hizi mambo.
Adam ni mapokeo ya Wayahudi tu.

Zamani, watu walikuwa wanaishi tofauti tofauti. Hawachangamani sana.

Katika kuishi tofauti huko, hawakuwahesabu watu walioishi mbali nao kama watu.

Wayahudi wakajitungia hadithi yao ya mtu wa jwanza. Ndiyo huyo Adam.

Adam hawezi kuwa mtu wa kwanza, kwa sababu hata hadithi ya mtoto wake Cain alipofukuzwa Eden, alikimbia pembe i akakutana na watu.

Sasa kama Adam alikuwa mtu wa kwanza, huko nje ya bustani ya Eden watu walifikaje?

Pia, kisayansi, watu walitokea Africa maelfu na maelfu ya miaka kabla ya habari za Adam miaka 6000 iliyopita.

Sasa unakuwaje watu watoke Afrika maelfu na maelfu ya miaka iliyooita, halafu Adam awe mtu wa kwanza kaumbwa miaka 6000 iliyopita?

Kama dunia imeumbwa miaka 6000 iliyopita, mbona ina mawe yenye mamilioni ya miaka?

Mbona ina milima iliyofanyika mamilioni ya miaka?
 
sio kweli
Ukweli ni upi kaka. He, Dunia kama part and parcel ya solar system sio zao la Big Bang?

"Have those who disbelieved not considered that the heavens and the earth were a joined entity, and We separated them and made from water every living thing? Then will they not believe?" (Qur'an 21:30)
 
Ahsante kwa swali lako zuri: Nina lako linasadifu vizuri - Ngumbaru.
Ngoja tumuulize Mwenyezi Mungu mwenyewe aliye Mtaalamu na mwanzilishi wa Lugha:

"Na hatukumtuma kabla yako mtume yeyote Ila tulimfunulia ya kwamba Hapana mungu Ila MIMI. Basi niabuduni MIMI tu". (Qur'an 21:25)

"Hakika MIMI ndiye Mwenyezi Mungu, Hapana mungu ila MIMI tu. Basi niabuduni MIMI na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka MIMI." (Qur'an 69:14).

Naamini umeelewa vizuri kakangu. Kama hujaelewa naomba karibu uulize tena.

NB: Kwa msaada Zaidi kama wewe ni Mkristo nenda kasome mwanzo pale Mungu anaposema "Natufanye MTU kwa mfano WETU. ……..Kisha Mungu akamuumba MTU kwa mfano WAKE.
SIYO KWA MFANO WAO.
Hivi umeelewa kweli swali langu?
Au username yangu imekuzuzua,kiasi kwamba ukashindwa kabisa kusoma swali vizuri?
 
Mbona sekta nyingi tu biblia na Quran vinafanana, hasa visa. Sema mjinga aliyekuja kututofautisha ndiyo kazingua Tungekuwa wamoja.
Yanayofanana na Bibilia huwa nayakubali, yanayotofautiana ,Bibilia ni Sahihi kuliko hiyo quran. Maana Bibilia imeanza kuyaandika kabla ya quran.
Binafsi huo ndio ufahamu wangu, unaweza usiwe mzuri sana.
 
Hivi umeelewa kweli swali langu?
Au username yangu imekuzuzua,kiasi kwamba ukashindwa kabisa kusoma swali vizuri?
Na Je, umesoma post yangu ukaielewa vizuri kabla ya kua-assume kuwa nimezuzuliwa na jina lako??.
Hebu some vizuri kisha utafakari halafu onyesha ni wapi hujaelewa. Nimekuelimisha kama mwanafunzi usiyejua taawili ya maana ya Lugha.
 
kwa kifupi Biblia hipo kwenye code au tuseme fumbo/mafumbo sana, unapoisoma unatakiwa uwe na uelewa mpana sana wa vitu vingi na uwe na busara ya kutafakari kwa kina, mfano operation ya kutoa kiungo (mfano figo) kwa mtu mmoja na kupandikiza kwa mtu mwingine ni ugunduzi wa miaka ya 1900, lakini ukisoma Biblia tunaona uwezekano huo ulikuwepo tangu MWANZO, kwani hata Adam alipigwa nusu kaputi na kiungo kikatolewa kwenye mwili wake na kupandikizwa mtu mwingine (Hawa), kwa mtu anayesoma Biblia kwa tafakari hawezi kushangaa mtu kupandikizwa Figo. Mfano mwingine ni jinsi Galileo alipokuwa akipingwa na Makasisi wa pale Vatican aliposema Dunia ni duara, alipingwa sana na wanasayansi wa Kikakotliki lakini ukisoma kitabu cha isaya 40:22 kinasema "Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya Dunia" sasa Biblia inasema Dunia ni Duara mbona wao walikuwa wanAmpimga mtu aliyekuja kuthibitisha maneno ya Biblia?

tukirudi kwenye maada, mimi naamini siku zote sayansi inayozungumwa ukiitafuta utaipata kwenye Biblia kwa uwiano wenye kuingiliana/Kufanana, kwa hoja iliyotolewa na hao makasisi kuwa Dunia ina miaka 6,000 tu sio sahihi nakubaliana na wana sayansi kuwa dunia ni nzee kufikia umri huo wa miaka 4.5bil.

zitto junior umeelezea njia moja ya kisayansi ya kuweza kutambua umri wa Dunia kwa kutumia Radiometric, lakini pia kuna njia ya pili ya kuweza kutambua umri wa Dunia kwa njia ya kulinganisha matukio (Correlations) hapa kuna kanuni moja inasema 'vitu vinvyofanyika leo na kuviona basi ni somo la kutuelezea vitu vilivyofanyika kipindi cha nyuma' (The Present is the key to the Past),

Tunafahamu mwamba wa asili kabisa ni mwamba moto (igneous rock), huu mwamba ukimegekamegeka vipande vyake vinaweza kujiunga tena kwa uwezo wa kukusanywa aidha na maji, upepo au barafu na kutengeneza mwamba mwingine wa kitabaka (Sedimentary Rock) hili tukio la kutengenezwa kwa mwamba wa kitabaka bado linaendelea lakini ni zoezi la taratibu mno (miaka mingi), so wataalamu wa miamba wanachunguza na kuona kwa hali ya kikawaida kabisa tabaka dogo tu la mwamba huo say mita 10 x10 na kina cha mita 1(100 Cibic Mita) linaweza kutengenezwa kwa miaka zaidi ya 100, swali wanalojiuliza je tabaka la 1kmx1kmx1km (1km Cubic mita) litatengenezwa kwa muda gani? obvious ni muda mrefu sana.

Mfano wa pili tunaona Bonde la ufa la Africa Mashariki (East Africa lift Valley) linapanuka, na miaka ya mbele kuna kipande kitatenganishwa na maji, utafiti uliofanywa maeneo ya Arusha unaonyesha kuwa bonde hilo linapanuka kwa 10-14cm kwa mwaka, Bahari Nyekundu (Red Sea) ni sehemu ya ufa huo na ilitokea kwa utaratibu unaofanyika huku East Africa, na sehemu pana kabisa ya bahari hiyo ina upana wa 355Km, sasa tukirudi kwenye ile kanuni yetu kuwa The Present is the key to the past, yaani tunachokiona sasa Arusha ndicho kilichotokea Red sea basi hiyo Red sea ilipanuka mpaka kufikia ilipo sasa kwa muda gani?
1Km =100,000cm
355Km=35,500,000cm
Bonde la ufa linapanuka kwa rate ya 10cm kwa mwaka kwa hiyo 35,500,000cm zitapanuka kwa muda wa miaka 3,550,000, so kama Bahari Nyekundu imepanuka na kufikia ilipofika sasa kwa muda wa miaka 3.5mil iweje dunia iwe na miaka 6000 tu?

kifupi, Dunia ni nzee sana na ukifumbua code za Biblia utaona uzee wa Dunia
Mkuu shukrani kwa kudadavua vizuri kabisa juu ya credibility ya vipimo vya kisayansi katika lugha inayoeleweka ningependa mkuu mitale na midimu aione hii atupe maoni yake.
 
Yanayofanana na Bibilia huwa nayakubali, yanayotofautiana ,Bibilia ni Sahihi kuliko hiyo quran. Maana Bibilia imeanza kuyaandika kabla ya quran.
Binafsi huo ndio ufahamu wangu, unaweza usiwe mzuri sana.

Unaweza kuwa sahihi lakini Jeremia 8:8 inaweza kukufundisha kinyume cha ukweli. Na hapo ndipo huyo au hao wajinga walianza kupotoa na kukoroga mambo.
 
Back
Top Bottom