Biblia ndio kitabu pekee kinachojibu maswali Mengi kumuhusu binadamu na maisha yake

Sayansi ni maisha ya duniani, Biblia ina maisha ya Mbinguni.

Hapo sasa utalinganishaje? Unajua nini maisha ya mbinguni?

Broo, usichukulie poa.
Umeshawahi kufika mbinguni?
Hebu tuelezee mbingu ipo wapi?
 
Sasa kama Mungu mwenyewe na Malaika ndio wanazifahamu?

Wewe ni Mungu au Malaika?
Bro, don't act dumb. Ulimwengu wa roho upo, na kama unataka kumjua Mungu, na habari za Mbinguni na kadhalika, jifunze kwanza kuhusu Ulimwengu wa roho.

Hayo maswali yako hayawezi kuthibitika kwenye ulimwengu wa mwili,

Utaona ni uzushi tuu na uwongo kwa sababu haupo mahala sahihi.


Ni sawa na mtoto wa darasa la pili ukimuuliza nne toa sita atakuambia haiwezekani, lakini wa darasa la saba anakuambia kuwa ni hasi mbili (-2).

Sijui unaelewa??

NB: kwa wote mnaotaka kujua Mungu yupo au hayupo, Mbinguni pakoje, na maswali ya hivyo, hauwezi kujua kitu mpaka uujue kwanza ulimwengu wa roho upoje.

Kwa sasa huenda kuujua ulimwengu wa kiroho ni aidha uwe kwenye imani (kuokoka) au kuwa mchawi, au vitu vya kiimani...meditations, na astral projections, etc. Naskia hadi wanajimu pia wanafahamu sana mambo haya...hata mabudha pia..

Ila miaka kadhaa ijayo, hii dhana itakua na uhalisia maana mwanadamu anahangaika kuzifungua senses zilizofungwa, uelewa wake unakua, na si punde atafikia kuweza kutumia na kuishi ulimwengu wa kiroho yeye mwenyewe pasipo imani, wala unajimu, wala asili, na kadhalika.

So, usipaniki, muda utafika tuu, ni aidha usubiri au utafute maarifa kwa namna ingine possible..au uendelee tuu kubishiabishia ujinga na kubaki kwenye giza nene/darkness
 
Wewe umejuaje?

Hapo Sasa hivi upo katika ulimwengu wa nini?
Nakunukuu:
Hayo maswali yako hayawezi kuthibitika kwenye ulimwengu wa mwili,

Tena ukasema anayejua ni Mungu na Malaika.

Naona Contradiction kwenye maelezo yako mengi unayoandika.

Muda? ni kipimo gani Cha muda ndio utasema hayo mambo yapo?

Maisha yana 3.5 billion na Dunia Ina 4.5 billion.

Sisi modern man tuna miaka 2E5.

Sasa muda Gani unataka?
 
01. Roho
02. Mwili
03. Nafsi.


Don't forget to Meditate 🧘‍♂️
Sijajua kama wengine wameuliza,ila mtumishi kama nitapata kibari rohoni mwako,nielezee Nini maana ya nafsi na roho,vinanipa shida kuelewa ,naona ni kama ni kitu kilekile
 
Sijajua kama wengine wameuliza,ila mtumishi kama nitapata kibari rohoni mwako,nielezee Nini maana ya nafsi na roho,vinanipa shida kuelewa ,naona ni kama ni kitu kilekile

Nafsi ndani yake hukaa Akili (mind).

binadamu hufanya lile ambalo akili yake imekubaliana nalo kuwa lipo sawa.
Kichaa anakula jalalani akiamini ni chakula kizuri tu kwake.

sasa iko hivi.

Roho yako + na roho mtakatifu au+ Roho za Majini au+ Roho za Kishetani.

hizo Roho zote zinaweza kufanya kazi kwa pamoja (combined) as Power Supply.

Nikuelezee kwa Mfano.
Roho - Soket ya Umeme/Generator/Power supply.

Nafsi - waya (wire) wa umeme sasa.

Mwili - Bulb 💡.

Binadamu wote tunazo Taa, na waya tunao lakini tumeshindwa kupata soket ya kuchomeka.

Pole kama nimekuchanganya zaidi.


Lakini kwa ufupi, Nafsi hubeba Akili.
na Nafsi yako kuwa na Nguvu ya kupitisha vitu Vikubwa lazima uwe na Maarifa ya Kutosha ya Kujua Mungu au
Kujua shetani kama ndie umechagua kumtumikia.
 
Nashukuru,nmeelewa Asante mkuu,umeniongezea dawa
 
Kilichoumbwa kwa mfano wa Mungu ni Roho, sio Mwili.
Mbona uzi huu umejibu swali lako.
Kati ya roho na mwili kipi Mungu alianza kukiumba?
 
Swali lako limejibiwa vizur tu huko juu shida hujasoma uzi wote kwa utulivu.

Ni roho ilianza kuumbwa.
Wewe muongo sana. Mungu alianza kumfinyanga mtu kutoka udongo wa ardhi then ndo akampilizia puani pumzi ya uhai mtu ndo akawa nafsi hai.

Sasa roho ilianzaje kuumbwa before mwili?
 
Wewe muongo sana. Mungu alianza kumfinyanga mtu kutoka udongo wa ardhi then ndo akampilizia puani pumzi ya uhai mtu ndo akawa nafsi hai.

Sasa roho ilianzaje kuumbwa before mwili?
Kasome biblia yako vizuri utaona kipi kilianza.

Mwanzo sura ya 1
Inasema aliumba mtu kwa mfano wake na Mungu ni roho, kwahiyo ni Roho ilianza kuumbwa.

Kisha ukiendelea kusoma
Mwanzo sura ya 2
Utaona ndio mwili unafinyangwa kutoka mavumbi ya ardhi.

Akampulizia pumzi yake mtu akawa Nafsi hai.

Kwahiyo nafsi zetu zimetokana na Pumzi ya Mungu.
 
Nioneshe jinsi bible inavoeleza kuhusu uumbaji wa mwanadamu,kuhusu mirathi,kuhusu ufufuo,maisha ya siku ya kiama,maziko yni naomba unifundishe hayo kupitia bible tu
 
Again, don't act dumb.

Wakati unaendelea kubishana hapa wapo wengine wana access maisha ya ulimwengu wa roho wakiwa hapahapa duniani, na wanafanya mambo yao, tena makubwa kuliko maelezo, na unawatii na kuwashabikia, na hawakuambii, kwa sababu ukijua utashindana nao au kuwapita.

So, kama unaendelea kuboji ujinga ukitegemea nikufundishe kila kitu ukiwa umelala...pole.

Endelea kulala hivyoivyo.

Vitu ushaambiwa vipo, vitafute, hautaki unaanza kuleta akili nyingi..ambazo hazina maana yoyote na hazikupeleki popote.

Watu wengine sijui mpoje...bure kabisaaa[emoji23][emoji23][emoji23]

(No offense kama una nia ya kujifunza)

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
 
Hapa lazima apotee[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Naamini umemvuruga kabisaaa[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
 
Sijajua kama wengine wameuliza,ila mtumishi kama nitapata kibari rohoni mwako,nielezee Nini maana ya nafsi na roho,vinanipa shida kuelewa ,naona ni kama ni kitu kilekile
Mi naomba nikueleweshe kwa urahisi.

Mwamba amesema kuna mwili, nafsi na roho.

Mwili ni jumba (body) ambalo linaishi katika dunia hii, Biblia inasema neno Vazi.

Hii kwanza ili uelewe, ni kuwa kwenye kila ulimwengu kuna vazi lake.

Ukiwa unaishi duniani, au kwenye ulimwengu huu tunaoishi ni lazima utatumia vazi la mwili.

Hapa kwanza tupo pamoja. Si ndio?

Haya twende sasa...

Kuna nafsi,

Hii ndio identity yako wewe, yaani hii ndio wewe. Nafsi ndipo inakaa id yako kuwa wewe ni nani.

Kwenye mwili huu wa ulimwengu wetu nafsi hatuioni, ila inajificha ndani yetu inabeba vitu vyake kadhaa, mf. Self (inner conscience); hii ni ile hali yako ya kutambua mema na mabaya, kufanya maamuzi binafsi, ni ile sauti flani unaisikiaga au inakuambiaga wakati mwingine unapotaka kufanya maamuzi ya hiari au ya lazima (hatari), na kadhalika.

Nikiielezea hizo sauti za ndani zinaweza kukuchanganya ukaamini ubonho ndio unafanya kazi zote, ila ni hapana, ubongo ni kama computer system tuu ya body zima la mwili, au kama unajua computer, brain ni kama CPU au processor kwenye computer.

Lakini kwenye nafsi hakuna kitu kimoja tuu, kuna vingine ambavyo kuvifahamu ni mpaka uwe na full access ya ulimwengu wa roho, namaanisha, uweze kuwa umefunguka zile SENSES zako zilizofungwa, zikiwemo THIRD EYE na zinginezo. Zinafika hata saba au zaidi, ndio Zile Higher dimensions. Usijali sana kama huzijui maana bado hazijagundulika vizuri kwenye ulimwengu wa mwili, so..yah.

Ila kwa ufupi, nafsi ni identity yako wewe.

Sawa. Mpaka hapo nadhani tupo pamoja.

roho sasa....

Roho ni power grid, light au energy source ya kila kitu chako. Maana rahisi ni chanzo cha nishati ambacho Mungu kakupa. Na hiki anakiona yeye mwenyewe. Na kikizima hiki, anajua, kikiendelea kuwaka anajua.

Kumbuka kuwa wewe ni system, so kila system ni lazima iwe na power source/ chanzo cha nishati, ndio roho sasa.

Watu wa dini na imani wanasemaga roho imetoka kwa baba, maana yake ni roho ni ya Mungu mwenyewe, ndio maana ukisali au usiposali, Mungu anakusikia, anakuona, na anakujua popote pale ulipo.

Wengine hufika mbali zaidi kuwa hii ndio inayompelekea taarifa Mungu kuwa unafanya mema au mabaya, well, kwa hilo sina uhakika...ila najua tuu NAFSI ndio itakayohukumiwa siku ya mwisho coz ina matendo yako yote, tangu kuzaliwa mpaka kuda kwako duniani, na itaendelea kurekodi maisha yako yote ya milele.

Anyway, tusipotelee huko, turudi kwenye reli.

So, Hauwezi kutengeneza roho, wala kuiona, wala kujua inavyofanya kazi...sanasana utasoma na kuelewa, lakini ni tech ya Mungu mwenyewe, hauwezi uifanyia manouver, kwa sababu roho ni ya milele.

Mnaosoma biblia mlionaga lines zinasema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu, maana yake mtu amepewa roho. Ndicho pekee kinachokufananisha na Mungu, na si kingine. So hapa kwa wengine majibu wamepata, kuwa mwanadamu amefananaje na Mungu.

Mpaka hapo sasa umeelewa?

SASA INAKUWAJE MTU ANA VYOTE HIVI KWA PAMOJA???

Nafsi na roho zinaweza kushikamana na kukaa pamoja, lakini mwili hauwezi kushikamana na vyote hivi kwa muda mrefu, kwa sababu mwili ni wa muda, mpito, unaishia kwenye ulimwengu huu pale unapokufa (iwe duniani au mars au hata sayari yoyote ile, au galaxy gani sijui ukiweza kuishi huko)
Lakini Nafsi ni ya milele, na roho ni ya milele. Havifi, havipotei na wala havichakai.

NINI KUHUSU STORI ZA KWENDA MBINGUNI?

Kwa watu wa dini na imani mbalimbali wanaamini kuhusu kwenda mbinguni, ila endapo wakibahatika kwenda huko ni kuwa wataenda na NAFSI (mwili utauacha) na wakifika kwenye ulimwengu husika, watakuta au kupewa vazi jipya la ulimwengu huo, ili waishi maisha ya huko.

Sasa kama umeenda Mbinguni utapewa vazi la huko ambalo naskia ni zuri ajabu, lipo so pure, so real, na soo perfect, (kama ambavyo Zumaridi amejaribu kuelezea kwenye interview yake na MillardAYO na akashindwa[emoji23][emoji23])

Na kama ukibahatika kwenda motoni, basi utapewa vazi la huko ambalo limejaa mateso, taabu, funza, wadudu, moto na maumivu ya milele.

Mpaka hapo sijui kama umenielewa??

Na haya hadi zumaridi amejaribu kuelezea pia, ila inabidi umsikilize kwa makini sana ili upatepate idea.
 
Mwili ndio unabeba Akili (Brain), yes, ila ni kwenye ulimwengu wa mwili (flesh) ila mind inakaa kwenye ulimwengu wa roho..ambapo tukisema tutaje eneo ni lazima litakuwa ni maeneo ya hukohuko kwenye ubongo.

Hii inawapa shida sana hawa watu wanaoendeleza tafiti za Neuro-link kuhusu ni namna gani ya kusoma mind ya mwanadamu na kuichakata kwenye computer.

Tafiti bado zinaendelea na zikifanikiwa maana yake zitakua zimesaidia mwanadamu kupona sana maradhi mengi ya ubongo, neva na magonjwa mengine magumu ambayo yametutesa wanadamu kwa muda mrefu

Mungu sayansi yake ni noma sana, ameunganisha vitu vya ulimwengu wa mwili na roho pamoja ila wanadamu tunapata sanaa tabu kuvijua.

Usione wachawi wajinga kukuchanja machale usiku, wanajua baadhi ya links na gateways za mwanadamu zinazomuunganisha na ulimwengu wa mwili na roho. Hivi vitu vinafuatana.

Mfano, yapo mahusiano ya karibu mno kati ya pumzi na roho...ila tafiti zake hata kama ni wewe, utaanzia wapi??[emoji23][emoji23][emoji23]

Au ndoto, na brain, ambazo hizi tafiti zinaendelea kufanyika na zina matokeo chanya, au mind na ile inner voice ya mtu binafsi, na kadhalika, na kadhalika.

So, ukisikia au kuona mtu anajadili mambo haya, ni busara kumsikiliza kwani huenda kuna vitu utajifunza na kuuongezea uelewa wako.

Nawapa tahadhari wasiosoma na kuelekeza zaidi kwenye imani pekee..au akili pekee. Ninasema hivi kwa maana siutetei upande wowote ule.

Siri kuu nawapa ni hii. Ili mwili ufanye kazi kikamilifu, kuna muda ni lazima uamini. Nenda mbele au urudi nyuma ni lazima uamini. Suala la kuichagua imani ni la kwako wewe, ila ni uamue tuu kuwa unataka imani ya positive force au negative force

Tafakari na kisha uchukue hatua.
 
Nadhani anataka usahihi kuwa Mungu alimuumba mwanadamu, akampulizia pumzi, so, technically, pumzi imetoka kwa Mungu,

Hapa nadhani anamaanisha kuwa pumzi (roho) ni sehemu ya Mungu, so, haijaumbwa...bali kilichoumbwa ni udongo, ambao ndio mwanadamu.

So nadhani anataka kuwa sahihi kwa namna hii.

Jibu sahihi ni hili...

Kuanza kuumbwa hiki au kile sio tija.

Kuna stori nilizisikia humuhumu miaka kadhaa nyuma kuwa kabla ya kuumbwa kwa mwanadamu, Mungu aliumba mwanamke na mwanaume..ila wakamzinguaga, nadhani ni lilith, ndio mpaka akaja tena kutulia vizuri na kumuumba Adamu, sawa na kusema kwa lugha za kisayansi kuwa ni creation project 2.0

Hili nalo ni suala lingine..ila tusipotelee huko, tutachanganyikiwa..maana vichwa vyetu bado havijakua sana..wengine



Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
 
I will never forget to meditates
 
Wakati unaendelea kubishana hapa wapo wengine wana access maisha ya ulimwengu wa roho wakiwa hapahapa duniani,

Watu gani hao?
Lete ushahidi usio na shaka?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…