Bila mkataba na kampuni ya uwindaji Ortello kuvunjwa hapatakua na amani Loliondo

Bila mkataba na kampuni ya uwindaji Ortello kuvunjwa hapatakua na amani Loliondo

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Kampuni ya ortello walipewa eneo la uwindaji loliondo mara ilipoingia awamu ya pili ya mzee ruksa.

Baada ya kupewa eneo hilo kampuni hiyo ya UAE yenye wamiliki toka familia ya kifalme tabia yao ikawa kama wamepata koloni.

Pamoja na kwamba wameweza kuepa kutajwa na vyombo vya habari kama zamani kuhusiana na migogoro yao na wenyeji lakini inawezekana ni namna yao kudhibiti mambo tu. Ukweli ni kwamba tangu wamekua hapo hakuna amani kwa wenyeji kuhusiana na maisha yao kama ilivyokua jadi. Kulikua na wakati ukiingia eneo la ortello la uwindaji ilikua kama unaingia katika nchi ya kigeni.

Kwa maoni binafsi naona kama hao waarabu wa UAE wanachukulia loliondo kama mali yao na wana tamaa kuongeza ukubwa kwa hivyo wanachochea chokochoko za kuhamisha wakazi wa jadi.

Kama kuna mtu au seriksli yenyewe ikiweza hebu watupe mapato yanayopatika kwa kitalu cha ortello kwa kila mwaka ili wananchi wapime kama kuna manufaa au kuna vigogo au kigogo anunufaika pekee.

Pia yafaa tujue kama ortello hua anashindanishwa kwa kila muda kwenye kitalu chake.

Itawezekanaje miongo zaidi ya 3 bado wanahodhi kitalu na mipango ya serikali ni kuwahifadhi wao tu?

Tunataka kujua mipango kuwahamisha wenyeji ni kwa ajili ya kuboresha mazingira kwa ustawi wa wanyama tu au ni kuongeza maeneo ya vitalu vya wawekezaji?

Je, ni haki kumuhamisha mtanzania toka eneo lake la asili ili kulitoa kwa biashara ya mgeni huku mapato kwa serikali au mkataba wa huyo mgeni kumiliki eneo hilo sio wazi?
 
Litakuwa jambo la kusikitisha sana kama wananchi wanavurugwa kwa sababu ya kumnufaisha mgeni.

Hili litakuwa ni zaidi ya ukoloni wenyewe tunaoujua. Wakoloni, angalau waliweza kujenga shule, hata kama hazikuwa nyingi. Hawa wamewafanyia wananchi kipi cha maana; tena kutaka hata kuwang'oa kabisa kwenye makazi yao?

Serikali imekuwa na uongo mwingi. Mara waruhusu kusafirisha wanyama, mara wasijue nani karuhusu hilo!

Sasa wanafanya kila juhudi, wamasai wahame haraka; hili limekuwaje jambo la dharura kiasi hiki mara hii?
 
Litakuwa jambo la kusikitisha sana kama wananchi wanavurugwa kwa sababu ya kumnufaisha mgeni.

Hili litakuwa ni zaidi ya ukoloni wenyewe tunaoujua. Wakoloni, angalau waliweza kujenga shule, hata kama hazikuwa nyingi. Hawa wamewafanyia wananchi kipi cha maana; tena kutaka hata kuwang'oa kabisa kwenye makazi yao?

Serikali imekuwa na uongo mwingi. Mara waruhusu kusafirisha wanyama, mara wasijue nani karuhusu hilo!

Sasa wanafanya kila juhudi, wamasai wahame haraka; hili limekuwaje jambo la dharura kiasi hiki mara hii?
Awamu ya 6 imekuwa uchochoro.
 
Nashindwa kuelewa hawa watawala wamepewa nini na Mwarabu au ni tamaa ya nini, ambacho hawewezi kukipata mpaka waharibu maisha ya watu na familia.?
 
Naona ma puppet wa wakenya mmekuja kwa kasi kupigania masilahi ya bwana zenu (wakenya) wafugaji wanaovuka boda kuja kulisha mifugo yao katika ardhi ya Tanzania kwa kisingizio cha ujirani mwema na wengine uraia wa mchongo. Safari hii hatuwezi kukubali kuendelea kuwa shamba la bibi anymore.

Serikali iendelee na oparation yake endelevu hadi hao wafugaji ambao wengi wao wana asili ya Kenya waombe poo. Sijawahi kuona mkenya anasimama na Tanzania kwa kisingizio cha utofauti wa kisiasa uliopo kwao.

Ila kwa Tanzania ni kawaida wakenya kuwatumia watanzania watakavyo kwa masilahi yao, kupitia mgongo wa siasa uchwara za majitaka.
 
Naona ma puppet wa wakenya mmekuja kwa kasi kupigania masilahi ya bwana zenu (wakenya) wafugaji wanaovuka boda kuja kulisha mifugo yao katika ardhi ya Tanzania kwa kisingizio cha ujirani mwema na wengine uraia wa mchongo. Safari hii hatuwezi kukubali kuendelea kuwa shamba la bibi anymore. Serikali iendelee na oparation yake endelevu hadi hao wafugaji ambao wengi wao wana asili ya Kenya waombe poo.
Wewe ni mpumbavu. Mnatengeneza matatizo halafu mnakuja kusema Wakenya wanawahujumu? Mnawadharau wananchi wa Tanzania kwamba hawawezi kutetea haki zao ila Wakenya ndio wanawatuma.
 
Hawa waarabu huwa wanatafuta marafiki zao katika imani ili wapenyeze huu ujinga wao, na kwa ubinafsi wa hao watawala huwa wanaungana nao kutaka kutengeneza watumwa ndani ya nchi yetu.

Hili tatizo huwa linajirudia kwasababu tunaoneana aibu, hatuambiani ukweli, dawa ni kulelezana ukweli ili waijue hali halisi, tusikubali kuchezewa na kikundi cha wachache.

Hawa watu wakemewe sana, kuwapa hao waarabu hilo eneo ni kuudharau utu wetu, kudharau rasilimali za taifa letu, na zaidi kuidharau ardhi tuliyopewa na Mungu.

Ogopa sana pale panapokuwepo na hali kama hii katika taifa lakini bado utaona kuna wanasiasa wako kimya, wanajidai hawaoni tatizo lolote, hawa wanafiki ni maadui wa watanzania, wameweka maslahi yao mbele zaidi ya wengine wote.
 
Wewe ni mpumbavu. Mnatengeneza matatizo halafu mnakuja kusema Wakenya wanawahujumu? Mnawadharau wananchi wa Tanzania kwamba hawawezi kutetea haki zao ila Wakenya ndio wanawatuma.
Safari hii hatuwezi kuwaachia ardhi yetu muichezee mnavyotaka mb.w.a koko nyie.
 
Hawa waarabu huwa wanatafuta marafiki zao katika imani ili wapenyeze huu ujinga wao, na kwa ubinafsi wa hao watawala huwa wanaungana nao kutaka kutengeneza watumwa ndani ya nchi yetu.

Hili tatizo huwa linajirudia kwasababu tunaoneana aibu, hatuambiani ukweli, dawa ni kulelezana ukweli ili waijue hali halisi, tusikubali kuchezewa na kikundi cha wachache.

Hawa watu wakemewe sana, kuwapa hao waarabu hilo eneo ni kuudharau utu wetu, kudharau rasilimali za taifa letu, na zaidi kuidharau ardhi tuliyopewa na Mungu.

Ogopa sana pale panapokuwepo na hali kama hii katika taifa lakini bado utaona kuna wanasiasa wako kimya, wanajidai hawaoni tatizo lolote, hawa wanafiki ni maadui wa watanzania, wameweka maslahi yao mbele zaidi ya wengine wote.
Wanasiasa wakubwa wa upinzani kama Zito, Lipumba, Mbowe nk, kukaa kwao kimya huku sio kwa bahati mbaya. Bali washagundua kuwa hili swala lina mkono wa wakenya ambao wanapata faida kubwa kupitia hifadhi hiyo, hasa kwa wale wakenya wafugaji wa mpakani ambao walikuwa wanavuka boda kuja kulisha mifugo yao kwetu kwa kisingizio cha ujirani mwema na baadhi yao kupata uraia wa mchongo kutokana na muingiliano uliyopo kati ya raia wa nchi zote mbili wanaoishi mpakani hapo. Hili swala halina tofauti na lile la M23 wa Congo.

Ambapo Rwanda imekuwa ikiwatumia M23 ambao wanajifanya wakongo wa mchongo kwa masilahi yao. Pia na huku baadhi ya viongozi wa Kenya mipakani wamekuwa wakiwatumia wamasai wa kenya ambao wana uraia wa mchongo Tanzania kwa masilahi yao.

So ndo maana viongozi hao wa upinzani pamoj na wale wa chama tawala bila kusahau wasomi makini hawaliingilii swala hili. Maana wanajua chanzo cha tatizo ni nini na ni nani.
 
Acheni wagawe au kuuza nchi, alikuwepo chuma a.k.a jiwe hakutaka kupindisha maneno na alitaka kuwaonyesha kuwa inawezekana mwishowe mkafanya yenu ili nchi ifunguliwe leo kilio na kelele kama mtoto anayemlilia mamake.

Suburi iingie vizuri hiyo sindano.
 
Kampuni ya ortello walipewa eneo la uwindaji loliondo mara ilipoingia awamu ya pili ya mzee ruksa.

Baada ya kupewa eneo hilo kampuni hiyo ya UAE yenye wamiliki toka familia ya kifalme tabia yao ikawa kama wamepata koloni.

Pamoja na kwamba wameweza kuepa kutajwa na vyombo vya habari kama zamani kuhusiana na migogoro yao na wenyeji lakini inawezekana ni namna yao kudhibiti mambo tu. Ukweli ni kwamba tangu wamekua hapo hakuna amani kwa wenyeji kuhusiana na maisha yao kama ilivyokua jadi. Kulikua na wakati ukiingia eneo la ortello la uwindaji ilikua kama unaingia katika nchi ya kigeni.

Kwa maoni binafsi naona kama hao waarabu wa UAE wanachukulia loliondo kama mali yao na wana tamaa kuongeza ukubwa kwa hivyo wanachochea chokochoko za kuhamisha wakazi wa jadi.

Kama kuna mtu au seriksli yenyewe ikiweza hebu watupe mapato yanayopatika kwa kitalu cha ortello kwa kila mwaka ili wananchi wapime kama kuna manufaa au kuna vigogo au kigogo anunufaika pekee.

Pia yafaa tujue kama ortello hua anashindanishwa kwa kila muda kwenye kitalu chake.

Itawezekanaje miongo zaidi ya 3 bado wanahodhi kitalu na mipango ya serikali ni kuwahifadhi wao tu?

Tunataka kujua mipango kuwahamisha wenyeji ni kwa ajili ya kuboresha mazingira kwa ustawi wa wanyama tu au ni kuongeza maeneo ya vitalu vya wawekezaji?

Je, ni haki kumuhamisha mtanzania toka eneo lake la asili ili kulitoa kwa biashara ya mgeni huku mapato kwa serikali au mkataba wa huyo mgeni kumiliki eneo hilo sio wazi?
Anaweza kuwa simba wa Maziwa aliyetupiwa jiwe na majirani....
 
Back
Top Bottom