Jaji kuwa biased ni suala la kidhahania na kihisia kuliko uhalisia.
Kuhusu case ya Mkataba kule Mbeya, kila upande uliweza kuishawishi Mahakama ili upate ushindi.
Sasa Serikali imepata ushindi na upinzani ukashindwa.
Siyo rahisi sana wala kawaida kuona kwamba mtu anashindwa kesi na anakubali matokeo. Na ndiyo maana kuna Mahakama ngazi tofauti ili kama mtu kaona au kuhisi kutotendewa haki, basi akate rufaa ngazi ya juu.
Mahakamani, Jaji ni refa na Mawakili wa pande zote ni player. Na hii ni dhana ya kisheria na wala Haina Siasa.
Tena kwa kuongeza tu, katika tasnia ya sheria kuna msemo kwamba "Mahakama siyo mama yako kwamba itakupa kitu ambacho hujaomba"
Mahakama siyo mama kwamba ikuonee huruma, ikuulize una Hali gani na ikupe ushindi wa mezani.
Pambana!