Uchaguzi 2020 Bila unafiki unamshawishije mwalimu ambaye hajaongezwa mshahara kwa miaka mitano na bado ukambambika makato ya bodi kibabe aipende CCM?

Uchaguzi 2020 Bila unafiki unamshawishije mwalimu ambaye hajaongezwa mshahara kwa miaka mitano na bado ukambambika makato ya bodi kibabe aipende CCM?

Huu uzi umevamiwa na maccm, yanajifanya walimu...eti yako pamoja na mawe....mbuzi kabisa!!!!!

Mwalimu anaejitambua kamwe hawezi kukubali manyanyaso na ulaghai uendelee tena kwa miaka mitano mingine....

Mawe ametunyanyasa sana...


kwanza, kwa sisi Graduate alituongezea makato bodi ya mikopo kinyume na utaratibu...

Tulioajiriwa 2014 adi leo tunaisoma no.hatujui daraja ni kitu gani..,

Hivi karibuni ameondoa daraja I, hivo kuishia daraja H....

Manyanyaso yako mengi mno.....,,yote haya yameletwa na mawe...

Kwa hivo kura yangu....iko wazi tu wala sihitaji kampeni..

Lissu atosha....#NI YEYE,,...

pombe peleka burigi
 
sawa mkuu ila hicho chama cha waalim naona kinawakamua pesa tu wanaishia kuletewa mitshrt ambayo haiendan na wanachochangia
CWT...ni wezi na kiukweli wanamnyonya sana mwalimu ...

Ni lichama la hovyo kuwepo duniani
 
CWT...ni wezi na kiukweli wanamnyonya sana mwalimu ...

Ni lichama la hovyo kuwepo duniani
Yaan ni danganya toto mkuu,unaweza kukatwa almost karbia lak na nus kwa mwaka ila unaletewa tishrt ya elfu 10,ni fedheha sanaaa mkuu,sema ndo ivo ualimu ushakuwa punching bag kwa serikal ya awamu hii
 
Yaan ni danganya toto mkuu,unaweza kukatwa almost karbia lak na nus kwa mwaka ila unaletewa tishrt ya elfu 10,ni fedheha sanaaa mkuu,sema ndo ivo ualimu ushakuwa punching bag kwa serikal ya awamu hii
Hawa wezi (CWT) wanatumia woga wa walimu hasa wa msingi..kutuburuza.

Ndio maana wanapomuona mwalimu anaejitambua akiwahoji sana...basi humjengea chuki na wako tayari kumfanyia figisu ahamishwe hadi mkoa...ili asiwaamshe walimu wengine....

Kama walimu wakijitambua basi CWT itakufa asubuhi na mapema sana
 
Namwambia kuwa kama yuko dar es salaam anahitaji tuu kitambulisho kwenda kazini, pia umeme umeshuka na utashuka zaidi bwawa letu likikamilika, njia ni nzuri anaweza tumia private car yake kwenda kazini. Pia wakati wa corona kapokea salary yake kama kawaida. Sokoni hakuna mfumuko wa bei. Nyanya 500, karoti 500, hoho 500, na mihogo na mbaazi vipo kwa afya. Asisahau kuwa bima ya familia nzima ya afya ipo anahitaji nauli tuu kwenda hospitali.
Sijui tusi gani linakufaa papuchi ww
 
Uko sahihi mkuu na hata hayo mateso hawajayapata walimu. Shida ni pale mtu anapotaka kutyaminisha walimu ndo watumishi wa umma wenye hali mbaya kitu ambacho si kweli. Na nashindwa kuelewa inapokuja agenda yoyote inayohusu wafanyakazi wa Umma wachangiaji wote wanakimbilia kwa walimu. Kutakuwa na shida kwenye kufikiri kwenye upande wa wanafunzi.
Shida ipo Mkuu. Na ni kweli kabisa walimu ndo watumishi wenye maisha magum saaana
Hakuna marupurupu tofauti na kada nyingine
Hakuna posho
Mwl hana kipato chochote tofauti na mshahara,
Askari ana mshahara na viposho kibao, utaskia posho ya mavazi, vinywaji utadhan mwalim ye hanywi
So shida ipo ila Nina Imani kubwa sana na Rais wangu MAGUFULI.
 
Hebu tuwàsaidie hawa wenzetu kujibu swali hili japo naamini watumishi wote hawajaongezewa mishahara kwa miaka mitano mfululizo.

Mimi sio mwajiriwa wa Government Ila hebu leo nivae viatu vyao.

Imagine wewe ndio mwenyekiti wa chama cha siasa taifa unakuja kumuomba kura mwalimu ambae hujamuongeza mshahara wake kwa miaka mitano na Kama haitoshi ukampiga makato ya bodi ya mikopo ya 8% kibabe je mwalimu huyu unamshawishije akupe kura leo?

Hebu nisaidieni Mimi nimeshindwa.

Tiririka namna utakavyomshawishi mwalimu huyu akupe kura, tena mwaka huu na asahau ubaya uliomfanyia.

Kazi kwenu mabingwa wa kutongoza!
Pagumu hapo.Na hawa walimu wana familia zao na ndugu na jamaa.Kupata kura za hawa watu ni pagumu saaana
 
Pagumu hapo.Na hawa walimu wana familia zao na ndugu na jamaa.Kupata kura za hawa watu ni pagumu saaana
Dunia haiishi maajabu bado Kuna walimu wakereketwa makada wa CCM.

Ila nadhani Hawa wengi wako kimaslahi wanamendea u VEO/DEO nk
 
Sijui tusi gani linakufaa papuchi ww
Mkuu hakuna chochote kinachomfunga mwalimu kuendelea kuwa mwalimu. Najua changamoto zipo lakini utatuzi wa changamoto anao yeye mwenyewe ikiwa haridhiki na hali aliyonayo. Na hii sio kwa mwalimu yoyote kazi yoyote.
 
Toka nizaliwe walimu always hua wanalia kuhusu mishahara kutokutosha so sioni hata awamu kama wangeongezewa wangepunguza vilio vya kila siku. Huenda vilio vyao havihusiani na uhalisia bali ubinafsi. Angalia hata Mkwere aliekuwa anawaongezea mishahara kila meimosi bado kuna waliomtosa na kuondoka na Lowasa alivohamia Chadema
 
Kampuni ya Airbus, Boeing na nchi ya Uturuki watampigia kura maana hela nyingi kapeleka huko
 
Kampuni ya Airbus, Boeing na nchi ya Uturuki watampigia kura maana hela nyingi kapeleka huko

Miradi yenyewe karibia yote ni pasua kichwa tu! Wanajifanya kutoa elimu bure na kuigharamia kwa mabilioni ya shilingi kila mwezi, lakini cha kushangaza watoto wao hawasomi kwenye hizo shule za elimu bure!!

Ni unafiki uliopitiliza. Nitafurahi sana Ccm ikiadabishwa ipasavyo mwaka huu, kuanzia kwa huyo magufuli wao! maana inaleta maudhi mpaka inapitiliza.
 
Tumeleta mikopo nafuu kwenye halmashauri zenu, inaweza wasaidia pia
 
Miradi yenyewe karibia yote ni pasua kichwa tu! Wanajifanya kutoa elimu bure na kuigharamia kwa mabilioni ya shilingi kila mwezi, lakini cha kushangaza watoto wao hawasomi kwenye hizo shule za elimu bure!!

Ni unafiki uliopitiliza. Nitafurahi sana Ccm ikiadabishwa ipasavyo mwaka huu, kuanzia kwa huyo magufuli wao! maana inaleta maudhi mpaka inapitiliza.

Wewe ndio mnafiki maana unafikiri kuleta miradi rahisi na midogo midogo ndio kuwasaidia wananchi. Lazima tufanye miradi migumu na mikubwa ambayo itasolve changamoto once and for all. Kwa mfano miradi mikubwa ya umeme, Reli, miundombinu ya maji na barabara. Sisi tunafanya magumu, vitu rahis vidogo vidogi na kuzodoa na kukejeli na mambo mengine ya kimbuzi mbuzi mabeberu waendelee nayo.

Hebu ona tumeingia uchumi wa kati, vivuko vinanunuliwa, madaraja yanajengwa, viwanda vinajengwa.
CCM itashinda na itaendelea kuwa imara, na utazidi kuwa na adabu.
 
Pagumu hapo.Na hawa walimu wana familia zao na ndugu na jamaa.Kupata kura za hawa watu ni pagumu saaana
Sio kweli kura zao zipo za kutosha. Unajua wapo wangapi? Na wanachama wetu huko unajua ni wangapi? Na ndugu na jamaa zao ni wangapi? Kama hujui haya basi hujui ugumu au urahisi uliopo
 
Et Magu yuko taabani unajuwa wafanyakazi wapo wangapi kura zipo kijijini bwashee
huko kijijini pia wanategemea wafanyakazi kwa sababu
i.wana ndugu zao waishio mjini
ii. Ndugu waishio mjini wakiombwa hela wanasema hali ngumu Serikali haijaongeza mshahara kwa miaka mitano hivyo kipato hakitoshi.
iii. Hivyo basi kutokuongezwa mshahara wa watumishi wa umma kumeathiri wategemezi mfano wazazi wa mtumishi,watoto wa mtumishi wa umma,ndugu,nk hivyo maumivu siyo ya watumishi tu bali hadi kwa ndugu.
 
Toka nizaliwe walimu always hua wanalia kuhusu mishahara kutokutosha so sioni hata awamu kama wangeongezewa wangepunguza vilio vya kila siku. Huenda vilio vyao havihusiani na uhalisia bali ubinafsi. Angalia hata Mkwere aliekuwa anawaongezea mishahara kila meimosi bado kuna waliomtosa na kuondoka na Lowasa alivohamia Chadema
Tatizo la kutokutosha kwa mshahara mnalichukulia kimasihara sana.Mh.Magufuli aliwahi kusema hata yeye mshahara wake pia hautoshi,wabunge mishahara haitoshi,Wafanyakazi serikalini pia haitoshi.
Kitu ambacho hakijadiliwi ni uwiano wa kutokutosha kwa mishahara kati ya wafanyakazi ndani ya Taifa/nchi maskini/ya kipato cha kati chini.Hapa Tanzania kuna watumishi wa umma/serikali na walioajiriwa katika sekta binafsi.Sitawajadili waliopo sekta binafsi kwa sababu hawa malipo yao yanaendana na nguvu ya kiuchumi ya taasisi husika,mahitaji ya soko au ujuzi wa mwajiriwa kulingana na mahitaji ya mwajiri.
Watumishi wa umma ndiyo wenye changamoto nyingizaid kwa sababu mishahara yao hupangwa na watunga sera ambao ni Wabunge na Serikali Kuu/Mitaa kupitia kwa Madiwani.(Naweza kusahihishwa) ambapo Kima Cha Chini sasa hivi ni <300,000/= kwa mwezi na wakati huo huo Kima Cha Juu hakifahamiki(Sikifahamu),ila nasikia wengine wanalipwa hadi >30 milioni kwa mwezi.Sasa tuambiane mshahara hautoshi,tusubiriane tumalize kujenga miradi ambayo hata wakati wa kuanzishwa kwake hatukuulizwa au kushirikishwa.Wapo watakaosema kuwa kisomo ndiyo kinazingatiwa kupanga mishahara,sawa.Je,tumewahi kujiuliza kuwa aina hii ya madaraja kati ya Wafanyakazi ilipendekezwa na nani,je huo msaafu huo unakuwa chini ya usimamizi wa nani?
Ushauri wangu ni kuwa,kama mfanyakazi wa chini kabisa anatakiwa kuwa na cheti,wote wenye cheti walipwe mshahara sawa kwa wote,Diploma zote walipwe mishahara sawa,Digrii au PhD nk.Hata kama kuna tofauti ziwe si kubwa kiasi cha moja kuweza kuharibu morali ya watumishi na iwe based kwenye ufanisi wa mtumishi.
Pia wanasiasa wasipewe mishahara minono kama ilivyo sasa ili kuepusha wafanyakazi wengi kukimbilia huko kwa sababu ya green pastures katika siasa na watumishi wasizuiliwe kushiriki siasa.Haya yakifanyika tutakuwa tumeondoa rushwa automatically na uchakachuaji wa michakato ya chaguzi zetu.
Tukifanya hivyo vile vile tutakuwa tumeokoa fedha nyingi sana na miradi ingekamilika ndani ya muda mfupi tofauti na sasa ambapo hakuna ajuaye inaenda kukamilika lini/au kama wataanzisha mingine bila kuathiri huduma zingine.Tanzania tunaweza kuibadilisha ndani ya muda mfupi sana kwa kubana pia maeneo kama ya magari ya serikali,sasa hivi tunaona magari ya gharama kubwa sana serikalini ilhali kuna magari ya bei nafuu na yenye ufanisi sawa na haya tuliyonayo.
Hatupaswi kuwaminya wafanyakazi kukamilishaau kujenga miradi,maisha yanaendelea.Mambo ni mengi...
 
Tumeleta mikopo nafuu kwenye halmashauri zenu, inaweza wasaidia pia
Wanapenda kukopesha wakati wao wenyewe wanakopa,ongeza mishahara mkusanye kodi mtarejesha mzunguko wa fedha badala ya kuwakopesha watumishi.Mikopo haiongezi morali ya kazi na huleta msongo wa akili.
Pia hata hiyo mikopo siyo endelevu na wanaitoa kwa maelekezo na upendeleo mkubwa.Halmashauri yenye watumishi 500 halafu fedha za mikopo sh 200,000,000/=,hapo utawapa mkopo wa shilingi ngapi wajikwamue?Tusipende kuwadhihaki watumishi wetu.Mkumbuke hawa ndio watekelezaji wa Ilani mnayotamba kuwa mliitekeleza kikamilifu.Kumkamua ng'ombe maziwa bila kumpatia malisho ni sawa?
 
Bado wale vyeti feki maumivu yao sipatii picha😱🙆🏽‍♀️
 
Back
Top Bottom