stickvibration
JF-Expert Member
- Feb 7, 2017
- 3,226
- 5,147
Ungeanza kumuuliza kwanza babu yako kwanini hajafanikiwa?kila kitu ni .majaaliwa na mungu ndio anayempangia.acha roho ya kwanini ukimwona mwenzio kapata mafanikio
ndiomaana huwa hamjaaliwi kutokana na roho zenu za kwann
Hata mh. Waziri Mkuu alimnunulia mkewe pia,tuendele kujipa moyo mkuu labda Msipofaidika nazo nyinyi basi hata huko mbeleni wanaweza wakafaidika watoto/wajukuu wenu.kuna wale walionunua hisa huko vodacom mambo yaliishia wapi
Kwa hiyo Rostam kaamua kuwarudishia wa south VODA yao ili CCM wakiitaka Vodacom yao walio pewa na Madiba waifute huko South upya?Huyo jamaa ni noma..
Kapiga bei fasta kabla kitumbua hakijaingia Mchanga..
Musiba aliwahi kusema Vodacom ni msaada wa Mandela kwa CCM , sasa sijui ni akina nani ndani ya CCM waliichomoa Vodacom ndani ya CCM kiaina..
Sasa hiyo ni Vodacom , vp kuhusu mali zingine za chama zilizokwapuliwa kiujanja ujanja...!
Siyo vitu vyoye ni majaliwa kutoka kwa Mungu ,vingine vina mkono wa binaadamu!kila kitu ni .majaaliwa na mungu ndio anayempangia.acha roho ya kwanini ukimwona mwenzio kapata mafanikio
ndiomaana huwa hamjaaliwi kutokana na roho zenu za kwann
NA YEYE ATARUDISHA BILIONS ZA CCM, NGOMA DROO HIYO...Kwa hiyo Rostam kaamua kuwarudishia wa south VODA yao ili CCM wakiitaka Vodacom yao walio pewa na Madiba waifute huko South upya?
Voda Tz walitoa asilimia 25 tu za Hisa zao kuingizwa sokoni Rostam alibaki na zake kama zilizvyoHalafu haziuziki Rostam kawezaje kuuza? Soko la hisa litoe utafanunuzi kwa Nini hisa zingine Kama hizo za Rostam zinauzika na zingine haziuziki kwa Nini? Waandishi wa habari fuatilieni hilo
Kama huna nafasi utaibaje sasa?Kaibe na wewe CCM,
Haya ndio matatizo ya Mswaha,mtu akifanikiwa tu kimaisha mnamwita mwizi
kaibe na wewe sasa tuone kama utafanikiwa[emoji2211]
Hata mh. Waziri Mkuu alimnunulia mkewe pia,tuendele kujipa moyo mkuu labda Msipofaidika nazo nyinyi basi hata huko mbeleni wanaweza wakafaidika watoto/wajukuu wenu.
Kwenye hisa kuna aina 2 za kufaidika
1.Kupata dividend/gawiwo
2.Kupata Capital gains(unapouza hisa zako)
So mjiulize wkt mnanunua mlilenga kupata nini kati ya hivyo viwili.
Bado sijaelewa mnunuzi akija sokoni anataka hisa milioni 100 lazima ziwe za Rostam tu au humu ndani haziwezi kuwemo hata Mia mbili za watu wengine? Ina maana Rostam alizipeleka sokoni kuwa nauza na huko sokoni Kuna hisa za watu wengine mnunuzi akija si ananunua hisa anazozikuta sokoni..Fafanua hapo je za Rostam ziliingia sokoni au hazikuingia?Demand&Supply ina rule kwny uuzaji wa hisa
Rostam alikua at 1st ana 35% percent ya tota shares,so alikua ni minor s/holder akauza akabakiza 17.5% alizozimalizia kuuza sasa.
So point ya msingi hapa ni kwamba rostam alikua anauza shares mil. 588 at per zinazo represent 17.5%,kitu ambacho lazima akitaka kuuza shars zake Major shareholder watazitaka fasta kuongeza % ya umiliki wa hisa kwny Co.
Nyie wananchi mnaouza hisa zenu sijui 100 au 500 mjiulize zina represent % ya total shares za Voda?Mngekua na shares za maana wala msingepata tabu kuuza,brokers wangewagombania wale commision ya maana.
Asante kwa ufafanuzi mzuri mtaalamuVoda Tz walitoa asilimia 25 tu za Hisa zao kuingizwa sokoni Rostam alibaki na zake kama zilizvyo
Basi hapo ni kusikilizia gawiwo tu likitoka unavuta chako,maana ukisema uziuze sokoni kwenyewe hakuja kaa vzr.kuna wale tulionunua bila mipango yoyote swala lilikuwa umenunua hisa tu
Conglomerates investment model,Hii ni ngumu sana kujua mmiliki ni nani,.Kama Rastam angalia compuni inayomiliki hisa imasajiliwa Jersey Island.Ukifuatilia tena unakuta ukifuatilia tena Iyo kampuni pia inamilikiwa na kampuni nyingine uko Solomon Island labda..Hdi kujua nani anastahili kulipa kodi ni shughuli,,Hapo Tanzania na Magufuli wetu hatupati kitu, Rostam Aziz ni mkwepa kodi mahiri
Wakati Vodacom inaingia Tanzania Rostam hakuwa mweka hazina wa Ccm wala kiongozi wa ngazi yeyote wa chama zaidi ya kuwa mbunge.Channel 10&Magic fm-Ilikua Mali ya Rostam kwa sasa inamilikiwa na CCM,jiulize ilikuaje ikarudi CCM?
Vodacom Tz-Ililetwa na CCM nchini wkt Jamaa akiwa mweka hazina wa CCM,akaipiga juu kwa juu.
Leo ukiwauliza mlipateja pesa nyingi hivi?zina anza story ooh babu yetu alikua anafanya biashara za ngozi kutoka huko Igunga&Bukene kupeleka nchi za nje,hajah kalaghabaho.
Pesa huenda kwenye pesaView attachment 1214645
Tanzanian Tycoon Rostam Aziz Sells Last Tranche Of Vodacom Shares For $220 Million
Tajiri Kongwe nchini Tanzania Rostam Aziz, Hatimaye amemalizia Ngwe ya Mwisho ya Mauzo fungu la mwisho la Hisa zake za Vodacom Tanzania kwa kuwauzia Vodacom South Africa.
Kwa Mujibu wa report kutoka Citizen newspaper, Aziz ameuza fungu lake la 588 million (Shea) iliyokuwa imebaki Vodacom Tanzania, ambayo ilikuwa ikisimamiwa na Mirambo Holdings, Moja ya kampuni zake za uwekezaji kwendaVodacom South Africa, kwa dili lililokamilishwa kupitia Dar es Salaam Stock Exchange Jumatano iliyopita.
Shea (Shares) hizo zilithaminishwa kwa takribani dola milioni mbili na ishirini $220 wakati wa mauzo. Msemaji wa Vodacom Tanzania hakutaka kutoa ushirikiano wakati alipoombwa kutoa maoni yoyote juu ya hilo.
Dili hilo limekuja karibu Miezi kumi tangu 'Washikadau' (shareholders) wa Dar es Salaam Stock Exchange-kuorodhesha kupitishwa kwa mauzo ya sehemu ya Mirambo Holdings iliyobaki Vodacom Tanzania
Rostam Aziz (55) ndiye aliyewezesha kuingia kwa Vodacom South Africa nchini Tanzania, awali alikuwa akimili wastani wa asilimia ya 35% fungu ndani ya Vodacom Tanzania.
Mwaka 2014, aliuza asilimia 17.2% ya fungu la Vodacom Tanzania iliyokuwa ikimilikiwa na kampuni yake ya binafsi ya uwekezaji Cavalry Holdings, iliyosajiliwa Jersey Island ikiwa na umiliki wa 17.8% ya hisa.
Rostam Aziz, ni bilionea wa kwanza nchini na bado anaongoza kwa biashara. Mbali na kumiliki hisa zake Vodacom Tanzania, amepata utajiri mkubwa kupitia mikataba ya uwekezaji na ujenzi wa Biashara za Mgodi Caspian Mining, Bandari ya Dar es Salaam, Majengo ya Biashara na Makazi nchini na Mashariki ya kati sambamba na uwekezaji kupitia vyombo vya habari nchini Tanzania (Channel Ten/Magic FM/ DTV/CTN/C2C nk).
Mwezi July Mwaka huu alizindua Biashara ya kiwanda cha Ujazaji gesi, Dar es Salaam (Petroleum Gas-LPG) yenye thamani ya dola za kimarekani $65Millioni.
[emoji16][emoji16][emoji16] wanapenda chai Sana ....asilimia 99 wanabackground za kimagumashi tu..tuendelee kupambana kwa njia zetu tu.Channel 10&Magic fm-Ilikua Mali ya Rostam kwa sasa inamilikiwa na CCM,jiulize ilikuaje ikarudi CCM?
Vodacom Tz-Ililetwa na CCM nchini wkt Jamaa akiwa mweka hazina wa CCM,akaipiga juu kwa juu.
Leo ukiwauliza mlipateja pesa nyingi hivi?zina anza story ooh babu yetu alikua anafanya biashara za ngozi kutoka huko Igunga&Bukene kupeleka nchi za nje,hajah kalaghabaho.
Kwani Vodacom iliingia nchini mwaka gani?Huyo jamaa ni noma..
Kapiga bei fasta kabla kitumbua hakijaingia Mchanga..
Musiba aliwahi kusema Vodacom ni msaada wa Mandela kwa CCM , sasa sijui ni akina nani ndani ya CCM waliichomoa Vodacom ndani ya CCM kiaina..
Sasa hiyo ni Vodacom , vp kuhusu mali zingine za chama zilizokwapuliwa kiujanja ujanja...!