Bilioni 14 kuhamisha Gereza la Kilimo Mbeya kupisha uchimbaji wa madini ya Niobium

Bilioni 14 kuhamisha Gereza la Kilimo Mbeya kupisha uchimbaji wa madini ya Niobium

Piga hesabu ya haraka haraka utaona huyo mzungu anainflate gharama za mradi,kuhamisha gereza billioni 400 ni nyingi mno.Usishangae akapiga gharama za mradi sawa sawa na idadi ya madini atakayochuma miaka 30 ambayo ndio lifespan ya mradi.Chunga sana na hivi vikampuni chai rangi ya wazungu.
Maneno yako ni ukweli lakini ukijuwa life span 30 yrs ndio watu wakujadili PSA ndio kazi yao kuweka mipaka ya mkataba 15 yrs done we own 100% halafu kama serikali inataka kuuza share kwa wananchi fine 50% ndio business.
 
daaah!! Tanzania yangu wapi unaenda?! mwalimu aliweka hivyo vituo ili kuzuia hayo mambo mpaka tutakapo kuwa na UHURU WA KIFIKRA! cha ajabu viongozi wetu wamekuwa WAKURUPUKAJI NDIYO MAANA HATUFANIKIWI HATUNA BUDI KUTUBU MBELE YA M/MUNGU NA BABA YETU WA UKOMBOZI WA KWANZA mwl NYERERE!
 
Wasije kilalamika kama Mbunge Nkono huko Mara, walibomoa shule na dispensary madini yalipoisha wakasepa na kuishia kuacha mahandaki tu.
 
huo mlima umeanza kuangaliwa/ kuchunguzwa kuanzia 2002 au 2001 na wanasayansi wa chuo kikuu....nadhani serikali iliyopita ndio ilitoa mkataba....ila kuna gereza na shule pandahili secondary sijui nao watalipwa fidia
Sawa kiongozi
 
Mbona Mali nyingi sana nchini na kodi imekusanywa vizuri kwa nini Hospitali ya taifa Muhimbili iko vile vile
Mara ya mwisho kwenda muhimbili ni lini ndugu?au umeiona kwenye picha?
 
Mara ya mwisho kwenda muhimbili ni lini ndugu?au umeiona kwenye picha?
Kuna jipya gani muhimbili zaidi gharama za matibabu kuwa kubwa

Na mashine zingine kusinzia ilhali utajiri ndo huo.
 

Source : wasafi Media

Gereza la Songwe mkoani hapa linatarajiwa kuvunjwa na kujengwa sehemu nyingine kupisha uchimbaji wa madini adimu duniani ya niobium.

Gereza la Songwe kuvunjwa kwa madini



Mbeya. Gereza la Songwe mkoani hapa linatarajiwa kuvunjwa na kujengwa sehemu nyingine kupisha uchimbaji wa madini adimu duniani ya niobium.

Ni baada ya madini hayo kugundulika kuwapo kwenye eneo la gereza hilo.

Taarifa za uhakika zimeonyesha michoro ya ujenzi wa gereza jipya imeandaliwa.

Mhandisi wa Migodi wa Kanda ya Kusini Magharibi, Zephania Nsungi alisema Kampuni ya Panda Hill Niobium Project Tanzania imefanikiwa kupata madini hayo karibu na gereza hilo.

“Madini haya ni adimu duniani na yanapatikana katika nchi chache sana, hivyo yakianza kuchimbwa upo uwezekano wa kuliondoa Gereza la Songwe na kujengwa upya eneo jingine,” alisema.

Mfanyakazi wa kampuni hiyo, Emmanuel Kisasi alisema jana kwamba, viongozi wao wako likizoni Ulaya na wanatarajia kurejea nchini mwezi ujao.

Kisasi ambaye hakutaka kuzungumza kwa kina juu ya madini hayo, alithibitisha kuwapo kwa mpango wa kuanza kwa mgodi eneo hilo na kwamba, unatarajiwa kudumu kwa zaidi ya miaka 30.

Mkuu wa Magereza mkoani hapa, Julius Sang’udi naye alithibitisha kuwapo kwa mpango huo na kusisitiza kwamba, unasimamiwa na Wizara ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza chini ya Kamishna aliyemtaja kwa jina moja la Chamlesile.

“Maofisa wa Serikali na wataalamu wa madini hayo wakitaka kwenda eneo hilo wanatoa taarifa hapa na wanakwenda huko moja kwa moja, hivyo mimi siyo msemaji wa mpango huo,” alisema.

Kwa mujibu wa taarifa za mtandao, madini hayo huchanganywa na metali zingine na vyuma vyake hutumika kwenye ujenzi wa bomba la kupitishia mafuta.

Vilevile hutumika kama metali kwa injini za ndege na husaidia kuzuia mitambo yake kutopata joto kali.

The Panda Hill Niobium Project is located approximately 26km from the city of Mbeya, in south-western

Panda Hill Project – On Track to Be Africa’s First Niobium Mine
The Project is fairly unique in that it has excellent nearby infrastructure including: TAZARA Rail line (2km away), a dry port located in Mbeya (26km away), the Dar es Salaam – Tunduma Highway (5km away), Songwe Airport (8km away), the La Farge Songwe Cement Factory (6km away) and a major fuel depot in Mbeya.

Access to water and power is also relatively simple with the Songwe River, a major water course, running next to the mining tenements and TANESCO planning a new 400kV power line that will run past the licence area.

The Mbeya region is also a developing mining area with the established Shanta goldmine less than 100km away and Peak Resources developing a rare earths mine nearby.

Mbeya city is a growing city with good educational and medical facilities, including technical colleges that are expected to be a source of personnel for the operations.
 
The tragedy is that we don't know, or do we care what we are hauling away on the cheap.

We make no efforts whatsoever in attempting to develop our own capability to derive the maximum benefits from our God given wealth!

Did God make a mistake in locating these minerals in our country? We seem only too eager to cart away such wealth on the cheap.
 
Panda Hill Project – On Track to Be Africa’s First Niobium Mine
Tunapata raha sana kuandika au kusikia sifa kama hizi: "On truch to be Africa's First Niobium Mine".

Tunapojipiga vivifua vyetu kwa majigambo, utadhani tumemaliza msokoto wa bangi!

Kumbe tunachoambulia si lolote wala chochote cha maana sana.
 
30 September 2020
Brasil, Brazil

Bolsonaro Niobium and Graphene to revolutionize industry



Speaking at the launching of the mining and development program at the ministry of mines and energy, Brazilian President Jair Bolsonaro says that the development of a "Super battery" of Niobium and Graphene will revolutionize the world's auto industry. | via Chris Aclo

Source : Notìcias da America do Sul
 
The tragedy is that we don't know, or do we care what we are hauling away on the cheap...
kalumu

The fact is we as state we don't have long and short term project relating to what we need or what we want to do
It's matter of time every thing will pave it's own way
 
Tunapata raha sana kuandika au kusikia sifa kama hizi: "On truch to be Africa's First Niobium Mine".

Tunapojipiga vivifua vyetu kwa majigambo, utadhani tumemaliza msokoto wa bangi!

Kumbe tunachoambulia si lolote wala chochote cha maana sana.
Tunakaza fuvu kama kicheche aliye pata mlo wa kujikimu.

Sasa utajashangaa hiyo project itakavyo kuwa na upigaji wa kutosha
Sisi kama taifa tunabaki kupiga miayoo
 
Tanzania imebarikiwa kwa kupewa railimali zote, lakini ikalaaniwa kwa kupewa CCM.

So, ukijumlisha hapo kisha ukatoa, jibu linakuja zero.
 
Back
Top Bottom