Binadamu: Kiumbe chenye chanzo kisichojulikana, yupoyupo tu hana mwanzo wala mwisho

Binadamu: Kiumbe chenye chanzo kisichojulikana, yupoyupo tu hana mwanzo wala mwisho

Na kuhusu chanzo chake kwa madai yako kuwa ipo tu haina chanzo ? Umejuaje kama sio fikra zako tu
Nimejua kwa kuona kwamba Hakuna wakati ambapo Dunia haikuwepo Halafu ghafla ikawepo.

Dunia ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo.

Hakuna wakati wowote ule ambapo Dunia haikuwepo kisha ikawepo.

Lakini Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Mungu huyo kama yupo aje hapa ajidhihirishe na athibitishe kwamba yeye ndiye Muumbaji wa dunia.

Niko nimekaa paleeee.....👉👉😄😄
 
Dunia haina miaka, Dunia ipo siku zote.

Miaka ipo kwa binadamu na viumbe hai tu.

Dunia ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo.
Jibu kimantiki tu...

umri wako unakuwezesha kuthibitisha kuwa dunia haikuwahi kutokuwepo.

Hebu kwa mfano tuseme miaka 300 iliyopita ulikuwepo??
 
Jibu kimantiki tu...

umri wako unakuwezesha kuthibitisha kuwa dunia haikuwahi kutokuwepo.
Ndio unathibitisha.

Kila binadamu amezaliwa ndani ya dunia, Hakuna binadamu yeyote aliye zaliwa nje ya dunia.

Hakuna mwanadamu aliyeona na kushuhudia dunia ikiumbwa maana binadamu wote tumezaliwa ndani ya dunia.

Hakuna binadamu yeyote aliye zaliwa nje ya dunia.

Hebu kwa mfano tuseme miaka 300 iliyopita ulikuwepo??
Sikuwepo.

Ila kwa wakati huo naamini kabisa kuna binadamu wengine walikuwepo duniani.

Maana Haiwezekani kwamba Dunia haikuwepo Halafu binadamu akawepo.

Je huyo binadamu alikuwepo sehemu gani?

Kwa mantiki hii, Ni kwamba Dunia ilikuwepo kwanza kisha binadamu akazaliwa ndani ya dunia.
 
Ndio unathibitisha.

Kila binadamu amezaliwa ndani ya dunia, Hakuna binadamu yeyote aliye zaliwa nje ya dunia.

Hakuna mwanadamu aliyeona na kushuhudia dunia ikiumbwa maana binadamu wote tumezaliwa ndani ya dunia.

Hakuna binadamu yeyote aliye zaliwa nje ya dunia.
Hii hoja yako huoni kama ni dhaifu. Maana kuzaliwa ndani ya dunia haimaanishi kwamba dunia ipo ipo milele yote. Unachotakiwa kuonesha ni kwa nini dunia ipo tu haina mwanzo na huo mwanzo wake ni kwa nini usiwe na chanzo.

Nimetumia mantiki yako kukujibu.
Sikuwepo.
Kama miaka 300 iliyopita hukuwepo na wanasayansi wanasema kuwa dunia ina mamilioni ya miaka, unabishaje kwamba kabla ya wewe kuna watu walikuwepo na kushuhudia viashiria vya kuumbwa kwa dunia??
Ila kwa wakati huo naamini kabisa kuna binadamu wengine walikuwepo duniani.
Unaposema "unaamini" hapo unaleta mambo ya imani. Kwa nini unataka Imani yako kwamba kulikuwa na watu wengine miaka 300 iliyopita ikubalike na "imani" ya wengine kwamba Dunia iliumbwa isikubalike??
Maana Haiwezekani kwamba Dunia haikuwepo Halafu binadamu akawepo.
kwa nini unaamini kwamba dunia hawezi kuwepo bila ya binadamu kuwemo ndani mwake!?
Je huyo binadamu alikuwepo sehemu gani?
Kwa mujibu wa imani za wengine, ni kwamba Dunia iliumbwa kwanza kisha ndipo binadamu akaumbwa. Hii inaleta mantiki sana.
Kwa mantiki hii, Ni kwamba Dunia ilikuwepo kwanza kisha binadamu akazaliwa ndani ya dunia.
Binadamu alitokana na nini? Jinsi maumbile ya binadamu yalilvyo na mpangilio maalum unadhani alitokana na nini. Hakuna mbunifu wake??
 
Hii hoja yako huoni kama ni dhaifu. Maana kuzaliwa ndani ya dunia haimaanishi kwamba dunia ipo ipo milele yote.
Kwani kuna wakati dunia haikuwepo kisha ikawepo?
Unachotakiwa kuonesha ni kwa nini dunia ipo tu haina mwanzo na huo mwanzo wake ni kwa nini usiwe na chanzo.
Hakuna ulazima wa dunia iwe na mwanzo.

Kama ulazima huo upo, Hata huo mwanzo wa dunia lazima uwe na mwanzo wake.

Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na mwanzo, Hata mwanzo wa mwanzo lazima uwe na mwanzo.

Hivyo basi Dunia ni mwanzo usio na mwanzo mwingine.

Na dunia ipo inaonekana, Na hakuna uthibitisho wowote ule unao onyesha kwamba dunia haikuwepo.

Dunia ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo.
Nimetumia mantiki yako kukujibu.

Kama miaka 300 iliyopita hukuwepo na wanasayansi wanasema kuwa dunia ina mamilioni ya miaka,
Dunia ina mamilioni ya miaka kwa vile wanasayansi hawana majibu sahihi ya wakati gani dunia ilianza.

Ni makisio yao tu (predictions) kusema kwamba dunia ina mamilioni ya miaka, Wanasayansi hao hawana uthibitisho wowote ule.

Ushahidi na uthibitisho wa kwamba Dunia iliumbwa mamilioni na mabilioni ya miaka huko nyuma Haupo.

Hivyo hata kusema kwamba Dunia ina mabilioni ya miaka ni makisio tu.

Ukweli ni kwamba Dunia haina mwanzo, wala mwisho.

Dunia ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo milele.
unabishaje kwamba kabla ya wewe kuna watu walikuwepo na kushuhudia viashiria vya kuumbwa kwa dunia??
Watu hao walio shuhudia viashiria vya kuumbwa Dunia walikuwa wanaishi kwenye nini?

Watu hao walio shuhudia kuumbwa Dunia walikuwa wakiishi sehemu gani tofauti na duniani?

Hiyo sehemu walioishi watu hao ni ipi?

Na sehemu hiyo ilitoka wapi?
Unaposema "unaamini" hapo unaleta mambo ya imani. Kwa nini unataka Imani yako kwamba kulikuwa na watu wengine miaka 300 iliyopita ikubalike
Kwani miaka 300 iliyopita kulikuwa hakuna watu?

Watu walikuwepo, wapo na wataendelea kuwepo.

Hakuna wakati ambao Binadamu hakuwepo halafu ghafla akawepo.

Binadamu (watu) walikuwepo, wapo na wataendelea kuwepo milele.
na "imani" ya wengine kwamba Dunia iliumbwa isikubalike??
Dunia hiyo iliumbwa kutoka wapi?

Na huko ilikokuwa kuliumbwa na nani?

Yani sehemu iliyotumika kuumba dunia iliumbwa na nani?
kwa nini unaamini kwamba dunia hawezi kuwepo bila ya binadamu kuwemo ndani mwake!?
Dunia inaweza kuwepo bila ya binadamu.

Lakini hakuna wakati wowote ule ambapo Dunia ilikuwepo bila binadamu.

Mfano mabomu ya nyuklia yakalipuliwa dunia nzima binadamu tutatoweka wote na dunia itabaki.

Hivyo dunia inaweza kuwepo bila ya binadamu, Lakini binadamu hawezi kuwepo bila ya dunia.

Kwa mujibu wa imani za wengine, ni kwamba Dunia iliumbwa kwanza kisha ndipo binadamu akaumbwa. Hii inaleta mantiki sana.
Dunia hiyo iliumbwa kutoka wapi?

Huyo aliye umba dunia aliumbwa na nani?

Kabla ya kuumba Dunia, Sehemu aliyokuwepo huyo muumbaji ili umbwa na nani?
Binadamu alitokana na nini?
Binadamu alitokana na binadamu ndio uthibitisho uliopo mpaka sasa.

Kwamba binadamu mwanaume na mwanamke wanazaa binadamu mwingine kwa mbegu zao.

Hakuna uthibitisho mwingine wa kuthibitisha kwamba binadamu alitokana na kiumbe kingine au namna nyingine.

Nadharia zote za kisayansi, kihistoria na kidini hazina uthibitisho wa uhakika mpaka sasa zaidi ya makisio tu.
Jinsi maumbile ya binadamu yalilvyo na mpangilio maalum unadhani alitokana na nini. Hakuna mbunifu wake??
Mpaka sasa hakuna majibu sahihi yenye uthibitisho wa uhakika kwamba mpangilio huu ulitokana na nini.

Mbunifu wake hayupo mpaka sasa na hathibitishiki yupo zaidi ya mawazo ya kufikirika tu kwamba mbunifu huyo yupo.
 
Kwa mantiki hii, Ni kwamba Dunia ilikuwepo kwanza kisha binadamu akazaliwa ndani ya dunia.
Ukirudisha nyuma kumbukumbu je akili yako inakubali kuamini kwamba kuna binadamu wa mwanzo aliyezaliwa kama ulivyosema kisha ndio kutokea kwake wakatokea wengine ?

Au hauamini kama binadamu ana mwanzo bali walikuwa wanazaliwa tuu tangu na tangu wala hakuna chanzo au mwanzo wa binadamu ?
 
Ukirudisha nyuma kumbukumbu je akili yako inakubali kuamini kwamba kuna binadamu wa mwanzo aliyezaliwa kama ulivyosema kisha ndio kutokea kwake wakatokea wengine ?

Au hauamini kama binadamu ana mwanzo bali walikuwa wanazaliwa tuu tangu na tangu wala hakuna chanzo au mwanzo wa binadamu ?
Yeye anaamini eti dunia ilikuwapo tu na kisha binadamu ndiyo akazaliwa. Jee kabla ya kuzaliwa binadamu alikuwa wapi??
 
Kama unakubaliana na nadharia hii je unakubali pia nadharia ya wanaosema kwamba Mungu hana chanzo bali alikuepo tangu na tangu ?
Mungu huyo ni nini haswa?

Ana muonekano gani na umbo gani?

Angalau dunia ipo na kila mtu anatambua hilo.

Ndio maana Hujawahi kusikia kwamba mtu anasema Dunia haipo.

Ila Mungu hayupo na hata ukitaka kuthibitisha kwamba Mungu yupo huwezi.

Kwa vile Mungu huyo hayupo kwa namna yoyote ile zaidi ya mawazo ya kufikirika tu.
 
Alikuwa duniani.

Unataka kusema alizaliwa nje ya dunia?
Duniani sehemu gani?? Kwa ramani ya sasa ya dunia huyo binadamu alikuwa yupo nchi gani??

Na alikuwa peke yake au alikuwa na nini au na nani!!??

Ilikuwaje kukawa na utofauti kati ya maumbile ya Kike na yale ya Kiume. Hakuna aliyeyabuni maumbile hayo!!??
 
Ukirudisha nyuma kumbukumbu je akili yako inakubali kuamini kwamba kuna binadamu wa mwanzo aliyezaliwa kama ulivyosema kisha ndio kutokea kwake wakatokea wengine ?
Binadamu wa mwanzo hayupo.

Kila mtu ana mwanzo wake hapa duniani.

Dunia na binadamu hawana mwanzo wala mwisho.
Au hauamini kama binadamu ana mwanzo bali walikuwa wanazaliwa tuu tangu na tangu wala hakuna chanzo au mwanzo wa binadamu ?
Mwanzo huo haupo.
 
Binadamu wa mwanzo hayupo.
Tukubali kwamba binadamu wa mwanzo hayupo.

Kila Mwaka inapofanyika sensa huonesha watu huongezeka, kwa maana nyingine tunakotoka kulikuwa kuna watu wachache zaidi kuliko sasa. Jee akili yako haikugutushi kwamba zamani zaidi watu walikuwa wachache zaidi kuliko sasa.

Ilikuwaje dunia na watu wakatokea tu kusikojulikana???
 
Back
Top Bottom