BMW SUV (X3,X5) zinatelekezwa garage

Hizi ni gari za kipekee ndio maana ni rahisi kuonekana! Garage hata ikiwa na gari 40 za kijapan na BMW mbili na Range 3, hizi zitafunika zile 40 za kijep

Sent using Jamii Forums mobile app
Kinachofunika sio uwepo wa gari bali ushamba. Kumiliki gari ya kijerumani imekuwa sifa ya kijinga. Wengine yanawatesa ila wafanyaje sasa wamaindi mauzo.
 
Hahahah ndio muone kuwa hizo gari sio za kumiliki ukiwa hohehahe
 
Foleni ndio zinaniboaga mno. Gari naliachaga hadi weekend ndio natembelea. Foleni za kijinga zinaboa sana. Unasimama mahali lisaa lizima. Uko foleni si ujinga wakati weekend unateleza tu weekdays mahali pa kutumia litre moja utatumia litre 3 uneccessarily!
 
Hizo gari mafundi wazuri na wasio na tamaa wapo (though wachache sana)
Changamoto kubwa ya hizo gari ni kutambua tatizo halisi na upatikanaji wa genuine spare parts.
Kuna kipindi chombo ilizingua kubadili gear, fundi akaniambia kuna kijiwaya ndani ya gearbox kimeloga. Tulikitafuta kwa zaidi ya mwezi bila mafanikio (while gari ikiwa bado garage). Aliniambia baadhi ya mafundi wangeniambia ni badili gearbox.
Nilikuja kupata hicho kiwaya kwa 20k tu toka kwa mshikaji hadi leo 4yrs chuma inadunda road.
Issues kubwa hapo ni kungundua tatizo sahihi na upatikanaji wa genuine spare.
 
Shida sana mkuu foleni zinakwazaa mnoo yani hata mood ya gari huwa inakataa... mimi folini zikidii sana huwa nalipark tu kwa kweli licha ya mafuta sipendi kudrive na foleni balaaa
 
Ilikuwa gari gani?
 
Nadhani mandela rd ndio inaongoza kwasasa si asubuhi si mchana
Nusu saa mguu kwenye brake mpaka msuli unakaza
 
Shida sana mkuu foleni zinakwazaa mnoo yani hata mood ya gari huwa inakataa... mimi folini zikidii sana huwa nalipark tu kwa kweli licha ya mafuta sipendi kudrive na foleni balaaa
Kuna siku nilikua na cc3000 foleni ilianzia karibia na mataa ya sokota mpaka tazara maroli kibao yani kuanzia saa 11 jioni mpaka saa 1 jua linazama hatujavuka mataa ya tazara boss yuko pembeni ananung'unika tu Vumbi kama lote ebu zima gari bhana na kipindi kile petrol buku tatu na ushee
 
Boss aliamuru chombo kizimwe🤣🤣🤣
 
[emoji16][emoji16]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…