Bodaboda zimekuwa nyingi, vifo vinavyotokana na ajali vimekuwa ni vingi mno

Naungana nawe hapa "kazi imekuwa ya mateso sana vijana kwa wazee wanafanya kazi masaa mengi sana"
Siku hizi hata wazee wapo wanafanya.
Naam,serikali iongeze kodi maradufu.
Yaani maradufu maana tunakoelekea watabadili kazi waanze kuzitumia kwa uhalifu
 
Kama huamini kawaangalie siafu wanavyopishana wakiwa kwenye harakati zao kwenye ile njia yao kisha angalia na bodaboda.
 
Zambia hakuna bodaboda wala bajaji za abiria kama Tanzania! Na maisha yanaendelea vizuri tu.
 
Umeanza vizuri kwa angalizo kwamba bodaboda zimekuwa nyingi na vijana wanafanya kazi mchana na usiku ili kujipatia kipato. Umekosea sana tena sana ulipopendekeza kuongeza kodi kwenye bodaboda, sasa hiyo ni solution au ni kuongeza machungu zaidi juu ya maswahiba uliyoyatamka mwanzo. Mimi sielewi kabisa ctitical thinking yetu. Mtu anasema kitu sahihi lakini akija kwenye kupendekeza anapendekeza a very inconsistent suggestion. Utafikri siye aliyeyatamka maneno ya mwanzo
 
Vijana shambani pia kuna hela nzuri tu. Njooni tulime.
Mitaji braza kilimo kinahitaji mtaji....wakati unasubiri mazao yakue unakuwa unakula nini na ukute unategemewa na family.....

Nilichogundua maisha ni mipango yaani mipangilio, ukijichanganya ukapangilia vibaya imekula kwako mazima.....

Mfano mtu yupo mjini maisha ya kuunga unga kaenda mjini hajui akafanye nini.....

kapata kazi ya kuunga kaweka mwanamke ndani, kamzalisha mtoto au watoto kwenye nyumba za kupanga, kodi elfu 60 kwa mwezi, bado bills nyingine, kajichanganya na vikundi vya kuchangishana, mara kakopa kila mahali.....huyu mtu ukimwambia kuhusu shamba yaani atoke mjini anatokaje pengine ashachukua boda boda ya mkataba.....

Ndugu kuna maisha ukiishi unatengeneza umaskini, utajiri sahau.

Maisha bila mipango ni kuumia mkuu....
 
Akili mavi hizi, halaafu ajira mbadala ulizoandaa ni zipi? Na usafiri mbadala kwenye haya mafoleni baada ya kuoandisha kodi ni upi kwa mtu mwenye haraka dharura
 
Tukubaliane bado nchi ina watu wajinga mno.
 
Mfano Dodoma,Boda ni nyingi kuliko Idadi ya watu.Bajaji nazo zinaelekea huko huko.
Yani upo Jijini kama Dodoma Makao Makuu ya Nchi barabarani ni uchafu wa boda na Bajaji-shida tupu.
 
3/4 ya vijana ni waendesha bodaboda,Serikali,Samia,Wabunge wote wakotaka kusaidia vijana ni ku supply bodaboda majimboni.
Toka lini nchi changa kiuchumi kama Tanzania ikakuq kwa kutegemea service sector-yani tuna viongozi wa hovyo sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…