Body(mwili), soul(nafsi) and spirit(roho)

Body(mwili), soul(nafsi) and spirit(roho)

Uzi mzuri. Japo nimesoma kwa kuscan.

Tuanzie kwenye uliyoyasema kwenye uzi wako. Hivyo ili kugupisha, "kusummarise" sitarefer qoutes maana ushazionyesha na mimi nazitudia tu.

Kwenye hadithi ya piliya uumbaji( hadithi ambayo binadamu kaubwa kwa udongo). Hadithi imetanabaisha jinsi binadamu alivyo asili ya ardhi(mwili) na Mungu(roho).


Mungu akamfinyanga binafamu kwa vumbi la nchi, kisha akampulizia pumzi yake puani. Na binadamu akawa nafsi hai.

Binadamu alimbwa kwa udongo. Japo haielezewa kwenye biblia. Ila binadamu alimbwa kwa udongo akawa kiumbe hai.

Hivyo baada tu ya kufinyangwa kwa udongo, tayari alikua na nafsi.

Hata hivyo hakua na roho.

Ama kwa maana nyingine nafsi yake haikua hai.

Ila baada ya kupuliziwa Pumzi ya Mungu. Nafsi yale ilihuishwa.

Hivyo kiroho, nafsi ya binadamu ni zao la "reaction kati ya pumzi ya Mungu(roho) na mwili wa binadamu.

Hivyo ndan yetu binadamu, mna roho ya Mungu ilipaswa na inapaswa iwe hivyo.

Pia ndani mwetu mna roho zetu. Roho zetu zi hai. Pale tu ambapo roho ya Mungu i ndani mwetu.

Mda roho ya Mungu inatoka ndani mwetu. Roho zetu zimekufa. Ni hadi zitakapo huishwa tena kwa Roho wa Mungu kurudi ndani mwetu, ndipo zinapo pata na kufanya kazi inavyo paswa.
 
Nakumbuka nimeshawahi kuandika kuhusu hili jambo kwa urefu sana japokuwa si hapa jamiiforums, nilijikita kueleza uhusiano wa mwili na roho katika utendaji wake katika mwanadamu. Lakini hapa nimeona kuna kitu kimeongezeka, “nafsi”. Kuhusiana na neno nafsi tangu awali na hata sasa hivi nimejaribu kupitia ili kujiridhisha zaidi kutoka kwa waandishi wengi na hata kwenye biblia pia, wameileza nafsi kama mwili, kiumbe kilicho hai. Kwa hiyo kwangu mimi nafsi=mwili. Kwa hiyo kwa mantiki hiyo, vitu vinavyomjenga mwanadamu ni mwili(nafsi) na roho.

Vitu vinavyomjenga mwanadamu ni MWILI na ROHO. Tunaweza kuuchukulia muunganiko huu wa mwili na roho uzaao mwanadamu kama vile kompyuta ifanyavyo kazi. Kompyuta ili iwe kompyuta (ifanye kazi) ni lazima kuwe na muunganiko wa vitu viwili nanvyo ni hardware (umbo lionekanalo nje kama vile kioo, motherboard na vingine vingi) pamoja na software (m(i)fumo endeshi ambayo kikawaida haionekani kwa macho). Muunganiko wa software na hardware ndio huwezesha kompyuta kufanya kazi na kukosekana kwa kimoja wapo hufanya kompyuta isiweze kufanya kazi. Uwepo wa mwili na roho ndivyo unaomtengeneza mwanadamu. Kukosekana kwa kitu kimoja kati ya hiki mtu hukosa sifa ya kuwa mwanadamu. Ufanyaji kazi kwa kushirikiana kati ya mwili na roho ndivyo huzaa utendaji kazi wa aina yoyote ile tunaouona katika macho ya kawaida ya kibinadamu. Sasa tuanze kukiangalia kimoja baada ya kingine.

1: ROHO NI NINI
Roho ni umbo lisiloonekana kwa macho ya kawaida ya kibinadaumu(ni kama software kwenye kompyuta). Ni umbo linalobeba utambuzi yakini ambao hufanya kazi ndani mwili katika kumuongoza mwanadamu. Ninaposema utambuzi yakini namaanisha uwezo wa kudhibiti na kuratibu ni kipi cha kufanya na ni kipi si cha kufanya kwa muda husika. Kwa maana hiyo roho zote ni zenye kufanana na zote zina sifa sawa. Lakini utambuzi yakini hauwezi kufanyika kama roho haijawahi kuingia katika mwili wa mwanadamu. Hii ina maana kuwa roho yenyewe haiwezi kufanya kitu chochote chenye kuweza kuleta matokeo yenye kuonekana kiroho au kimwili mpaka iwe ndani ya mwili wa mwanadamu au iwe iliwahi kukaa ndani ya mwili wa binadamu kwa kipindi Fulani japokuwa pia haiwezi kufanya hayo kwa utashi wale pekeyake bali kama kuna mtu anayeiongoza kufanya hayo kwa kutumia nguvu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu.

KABLA YA KUINGIA NDANI YA MWILI, ROHO HUKAA WAPI?
Hili ni swali ambalo majibu yake hayawezi kupatikana kirahisi na hata kama yakipatikana hayawezi kuwa yenye kuaminika. Lakini tunaweza kujibu hili swali kwa kutumia mawazo makuu ya zile nadharia kuu mbili zinazielezea mwanzo wa maisha. Nazo ni; ile inayoeleza kuwa maisha yalijitokeza yenyewe kwa nasibu na ile inayoeleza kuwa maisha yalitokana na uumbaji wa Mungu.

Kwa wale wanaoamini maisha yalijitokeza yenyewe majibu yao majibu yao yanaweza kuwa rahisi na yenye kushangaza hata kutia shaka sana. Ni kwamba kabla ya kuingia katika mwili wa binadamu roho haikuwa mahala popote pale. Kwa maana rahisi ni kuwa roho haiajawahi kuwepo mahala popote pale kwa hiyo roho ni kitu cha kinadharia, HAKIPO.

Kwa wale wanaoamini uwepo wa mungu(nikiwemo mimi) wanaamini kuwa roho zote ni zao la uumbaji wa Mungu. Kwa maana hiyo ni kwamba roho hutoka kwa Mungu. Na katika nadharia hii, kwa kuwa Mungu ndiye muumbaji wa roho zote na ni yeye anayezipa kazi ya kufanya katika miili ambayo ameamuru ziingie.

2 MWILI NI NINI
Mwili ni umbo lenye kuonekana kwa macho ya kawaida ya kibinadamu(ni kama hardware kwenye kompyuta). Mwili ni zao la muunganiko wa kibaiolojia kati ya mbegu ya kiume na ya kike kupitia tendo la ndoa (japokuwa siku hizi muunganiko huu si lazima utokee wakati wa tendo la ndoa, hii haibadili maana. Muunganiko ni muunganiko tu). Katika muunganiko huu, mwili huu mpya unaotengenezwa hubeba sifa za moja za upande wa watu waliohusika ama upande mmoja pekee. Mwili ni ambao hasa hufanya utendaji wa mambo mengi yanayoonekana kwa kuwa unabeba ‘sifa pambanuzi’ ambazo ni muonekano(weupe, weusi urefu, ufupi nk..) na hisia(kupenda, kuchukua, kukasirika, kufurahi, kuhuzunika nk..). sifa pambanuzi hubebwa kwenye vinasaba na ndiyo maana waweza kusikia watu wakisema “Yule mtoto ana hasira kama baba yake”, au “Yule binti ni mrembo kama mama yake”. Hii na kwa sababu sifa pambanuzi hubebwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine kupitia vinasaba.

BINADAMU NI NINI(NANI)
Binadamu ni muunganiko wa mwili na roho. Vyote hivi vikiungana kwa pamoja ndipo tokeo lake huitwa mwanadamu. Kwa maana hiyo ni muunganiko wa umbo linaloonekana na umbo lisiloonekana. Utendaji wa mwanadamu unategemea ushirikiano wa hali wa juu kabisa kati ya mwili na roho. Kazi ya roho ni kuhakikisha mwili unatenda kuendana na matakwa yake (matakwa ya kiroho au matakwa aliyeiumba roho). kwa nini ninasema kutokana na matakwa ya…… ni kwa sababu, mwanzo nimesema kuwa roho zote ziko sawa kwa kuwa muumbaji wake ni mmoja(kama yupo, lakini kwa imani yangu naamini kuwa yupo). Na kazi kazi ya roho ni kudhibiti utedaji wa mwili kwa kuzuia matendo mabaya na kuruhusu matendo mazuri juu ya mwili. Sasa kwa mfano roho ikauingia mwili wenye tabia za hasira na majivuno (nimeshasema kuwa tabia hurithiwa kutoka kizazi na kizazi kwa kupitia vinasaba), kwa hiyo roho inatakiwa kudhibiti tabia ya hasira na majivuno yaliyo katika mwili huo. Na roho ikifanikiwa kudhibiti tabia hizo hapo inahesabika kuwa roho imeweza kutimiza jukumu lake na kama ikawa kinyume chake hapo inachukuliwa kuwa roho imeshindwa kutimiza jukumu lake.

MWILI NA ROHO HUUNGANA WAKATI GANI?
Hapo zamani iliaminika kuwa roho ilikuwa inaingia ndani ya mwili wa mwanadamu punde mtoto anapozaliwa. Na watu waliokuwa wakiamini hivi walitumia ushahidi wa kilio cha mtoto pale anapozaliwa. Kwamba kilio kile ndo kinatambulisha kuwa sasa roho imeingia ndani ya mwili wa mtoto huyo na hii ikiwa na maana kuwa kabla ya hapo mtoto huyu alikuwa na mwili pekee. Wazo hili lilichangia sana vitendo vya utoaji mimba kwa kuwa waliamini kuwa ukitoa mimba hakuna roho inayotolewa kwenye mwili, kwa hiyo hakuna mauaji. Dhana hii ilikuja kukosolewa na wasayansi walipokuja na ushahidi wa sababu yakini zinazoeleza sababu halisi za ni kwa nini mtoto hulia wakati anazaliwa ambazo ni
totauti ya jotoridi katika mji wa uzazi na mazingira ya nje hii humfanya ahisi mabadiliko Fulani na hivyo kulia ni rection yake baada ya kutambua mabadiliko
(ii) kwa kuwa mtoto akiwa tumboni hakuna hewa inayokuwa inaingia mapafuni hivyo mapafu huwa yamesinyaa, kwa hiyo anapozaliwa hewa huingia kwa mara ya kwanza katika mapafu hivyo mapafu hutanuka kwa ghafla na kusababisha maumivu kwa kichanga na kukifanya kilie.
Pia mikwaruzo wakati anatoka katika mji wa muzazi husababisha maimivu hivyo kumfanya alie.
Kwa hiyo, dhana inayokubalika kueleza ni wakati gani mwili na roho huungana ni pale tu mbegu ya kiume naya kike zinapoungana, ndipo roho huingia ndani ya mwili. Na kuanzia muda huo kila kimoja huanza kuwajibika juu ya kingine.
Na ili roho iweze kuingia ndani ya mwili na lizima mwili uwe katika hali ya kukamilika kibailojia katika namna inayoweza kuufanya mwili uwe hai. Ni lazima kuwe na seli hai.
Kwa hiyo hata kwenye kesi ya adam, Mungu alipomuumba adam alimuumba kwa udongo kwa hiyo hiyo kabla ya kupuziliwa pumzi ya uhai adam alikuwa ni donde la udongo lisilo na uhai. Na alipopuliziwa pumzi ya uhai ndipo adam akawa hai. Kwa hiyo mimi naamini kuwa pumzi ya uhai iliupa mwili seli hai na papo hapo roho iliingia kwa adam kwa sababu binadamu ili awe binadamu, muunganiko wa mwili na roho unatakiwa utokee katika wakati mmoja na si kimoja kianze na kingine kikikute kingine.
Huo ndio mtazamo wangu, nakaribisha wengine ili tuzidi kujifunza.
Shukran mkuu Internal
 
Mimi ni changie kuwa kuna aina mbili za vifo. Kifo cha kiroho na kifo cha mwili huu wa nyama/umauti.

Na mleta huu uzi kisha vielezea vizuri tu ingawa sijui kwa nini hakuchora mstari unaoeleweka kwa kila mtu kuvibainisha. Sina hakika anataka kwenda kufanya hitimisho gani? Kuna jambo nililizunguzia juzi kati hapa kuwa ishmaeli ni mfu wa kiroho mbele za Mungu, najua limewasumbua wengi hasa wa imani ile ambayo inajinasibisha kwa Ishmaeli maana wameujua ukweli, kwa wale wanaotaka kuujua ukweli.

Shetani yeye ana mwili wa kiroho na baada ya kuasi kule mbinguni alikufa kiroho. Maana dhambi inaua mwili wa kiroho sio huu mwili wanyama.

Sasa akaona amuingize mwanadamu katika kifo cha kiroho. Alisha jua kuwa Mungu aliwapa Adam na Hawa amri ya kutokula yale matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya na uzima wa milele. Na shetani alijua kwa hakika akifanikiwa kuwa shawishi wa tende dhambi ya kumkaidi Mungu basi atakukwa amepata wafuasi watenda dhambi wenzake walio jumuika naye katika kifo cha kiroho. Na hiki kifo cha kiroho ni kule kuingia katika ile jehanamu/mateso ya milele sio kuwa kuna roho na nafsi zitakazo kuwa zime kakamaa na kutokujitambua/kukosa fahamu. Ni roho na nafsi zitakazo kuwa na mateso ya umilele ndizo hicho kifo ambacho kilikuwa adhabu kuu baada ya kumtendea Mungu dhambi.

Kwa hiyo kuepuka kifo cha milele/ kuingia katika moto wa milele ni kufuata ule utaratibu ambao Mungu aliufanya ili tuufuate kwa ajili ya kujitakasa na dhambi kwa njia ya kutubu na kujisafisha kutokana na dhambi zetu.

Njia hizi zilianzia palepale pale Eden kwa Mungu kuchukua hatua ya kumchinja mnyama na damu yake kumwagika na ngozi yake ikawapa vazi Adam na Mkewe.

Wakati wa Agano la kale Mungu aliwapa wanadamu amri na kanuni za kufuata jinsi gani ya kujitasa na kujiondoa na dhambi watazo kuwa wametenda kinyume na amri na mapenzi yake.

Mungu alipokuja hapa duniani wakati wa Agano jipya akaleta utaratibu mwingine wa Mwanadamu kuufuata ilikuondokana na dhambi na kuupata uzima wa milele. Huu uzima wa mileke ni kule kwenda kuishi milele na Mungu katika ufalme wake. Utaratibu wa Agano jipya ni huu wa Mungu kumtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo, yaani ile nafsi ya Mungu ya Uwana iliyo vyalishwa kiwiliwili cha uwanadamu iteswe na kutundikwa msalabani na ife kifo cha kumwaga damu yake ya thamani kuu, damu hii ya thamani ilifuta zile damu za utakaso wa dhambi za wanyama zilizo tumika katika Agano la kale.

Utaratibu mpya wa kumepusha mwanadamu na dhambi na kifo cha milele ukawa ni kumpokea Bwana Yesu Kristo mwana pendo la Mungu, kwa kutubu dhambi zako zote, halafu kubatizwa kwa maji na kwa jina la Mungu kwa zile nafsi zake tatu za kiutendaji.

Ukisoma Maneno Matakatifu ya Mungu utaona kabisa kasema kuwa atakaye mwamini na kumpokea Yesu hata kama akifa(kifo hiki cha mwili/ kurudi kwa udogo) ataishi kwa maana ya kuishi katika uzima wa milele kwenye ufalme wake Mwenyezi Mungu. Angalia hapa kujiridhisha na hili ninalolisema.

John 11:25 Jesus said to her," I am the resurrection and life. Those who beilive in me will live, even though they die."

Haya maneno alikuwa anamwambia Dada yake na Lazaro, Martha.. Na wakati Bwana Yesu anaelezea kuhusu kifo cha kimwili cha Lazaro alisema, " rafiki yetu Lazaro amelala, lakini nitakkwenda ni pate kumuamsha" Alipoona wanafunzi wake hawa kumuelewa ndipo akawambia waziwazi ,"Lazaro amekufa." Kwa hiyo kifo cha kimwili/umauti kwa watakatifu/waliokoka kweli ni kulala wakisubiri kufufuliwa siku ya mwisho.

Ni muhimu kujua kuwa shetani hapendezwi na wanadamu wanao mcha Mungu na kuamua kujitenga na maisha ya kutenda dhambi. Tuna ona hata alivyo kerwa, pale Mungu alipomrusha roho kwa kumuilizia habari za Ayubu mtumishi wake na yaliyo tokea hatimaye.
 
Hakuna roho wala Mungu.

Na kama kuna mtu anaweza kuthibitisha hivi, athibitishe.
 
Bado nawaza kwa sauti, kwa nini hilo tunda la mti wa mema na mabaya liliumbwa.

Mtihani wa utiifu wa mwanadamu kwa Mungu wake. Mungu anawapa wanadamu mitihani iko mifano wazi, mtihani wa Imani yako. Maneno na iwe kama unavyo amini ni mtihani tosha. Hivi kama huku amini unafikiri itakuwa.
 
Hivi inakuwaje Biblia na Msaafu tu ndio kiwe kimomo cha uthibitisho wa uwepo wa Roho na Mungu? Binafsi uzi huu tangu mwanzo nilipoupitia naona ni blah blah tuu...
 
Hamna namna ya kuzipa nyuzi class, maana hii inafaa iwe first in the hi class thread, Hata Kiranga hana pakutokea.[emoji122] [emoji122] [emoji122]
Shukrani mkuu, ila kiranga namba chafu sana[emoji2][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji3][emoji125]
 
Ni kweli mkuu, Kuna makosa mengi mno nimeyaona, lakini sio kwa makusud kabsa, naamini mnichukulie katikati udhaifu nimerekebisha machache mengi nimeshindwa.
Shukrani mkuu
 
Sioni wapi Mungu amesema utakufa siku hiyo hiyo,neno linasema utakufa hakika,ikiwa na maana kuwa kuanzia pale kutakuwa na kufa na sio kuishi milele,ndio maana baada ya hiyo miaka 139 Adam alikufa...
Nimejaribu kukuwekea kwa kiingereza pale mkuu hujaona ? In the day, najua umesoma na unaelewa vizuri. Biblia ya kiswahili imesema siku utakapo kula utakufa hakika, ya kiingereza imesema in the day, surelly die.
Karibu tena
 
Sioni wapi Mungu amesema utakufa siku hiyo hiyo,neno linasema utakufa hakika,ikiwa na maana kuwa kuanzia pale kutakuwa na kufa na sio kuishi milele,ndio maana baada ya hiyo miaka 139 Adam alikufa...
Siku utakayo kula matunda hakika utakufa utakufa,

Ahadi ya Mungu ilikuwa ni kuishi milele katik hii dunia.
Na Mungu kila jioni alikuwa anaenda kuwatembelea,

Walipokula ndicho kilicho tokea kufa ni adhabu, Mungu hakuweka kifo mwanzoni kifo kilitokana na adhabu ilitokana na kukiuka maagizo ya Mungu katika bustani ya Edeni

Ukisoma mwanzo vizuri utaona adhabu iliyo tolewa na laana ilitolewa

Katika adhabu hizo kifo ni kimojawapo
Mungu hakusema (instantly )or (immeadiately) mtakufa amesema " you shall surely die"

[emoji115] [emoji115] [emoji115]

Hivyo ni kweli walikufa, ile ahadi ya kuishi milele ikaondoka,

Ndio maana ya hakika utakufa. Hii "uta" ni wakati ujao na wakafa baada ya miaka mingi adhabu ya Mungu ikatekelezeka.
Kingine katika summary yako

Adamu hakufa hapo hapo

Adamu alipoteza nafasi(position) ambayo Mungu alimpa alipoteza nafasi ya kuwasiliana na Mungu sababu ya dhambi aliyo itenda

Baada ya kupoteza nafasi ndipo adhabu na laana ikatolewa kutolewa nje ya bustani, kuzaa kwa uchungu, ardhi ikalaaniwa.

Ambayo hii nafasi imekuja kurudishwa na Adamu wa mwisho ambaye ni Yesu

Sioni wapi Mungu amesema utakufa siku hiyo hiyo,neno linasema utakufa hakika,ikiwa na maana kuwa kuanzia pale kutakuwa na kufa na sio kuishi milele,ndio maana baada ya hiyo miaka 139 Adam alikufa...



Siku utakayo kula matunda hakika utakufa utakufa,

Ahadi ya Mungu ilikuwa ni kuishi milele katik hii dunia.
Na Mungu kila jioni alikuwa anaenda kuwatembelea,

Walipokula ndicho kilicho tokea kufa ni adhabu, Mungu hakuweka kifo mwanzoni kifo kilitokana na adhabu ilitokana na kukiuka maagizo ya Mungu katika bustani ya Edeni

Ukisoma mwanzo vizuri utaona adhabu iliyo tolewa na laana ilitolewa

Katika adhabu hizo kifo ni kimojawapo



Mungu hakusema (instantly )or (immeadiately) mtakufa amesema " you shall surely die"

[emoji115] [emoji115] [emoji115]

Hivyo ni kweli walikufa, ile ahadi ya kuishi milele ikaondoka,

Ndio maana ya hakika utakufa. Hii "uta" ni wakati ujao na wakafa baada ya miaka mingi adhabu ya Mungu ikatekelezeka.



Kingine katika summary yako

Adamu hakufa hapo hapo

Adamu alipoteza nafasi(position) ambayo Mungu alimpa alipoteza nafasi ya kuwasiliana na Mungu sababu ya dhambi aliyo itenda

Baada ya kupoteza nafasi ndipo adhabu na laana ikatolewa kutolewa nje ya bustani, kuzaa kwa uchungu, ardhi ikalaaniwa.

Ambayo hii nafasi imekuja kurudishwa na Adamu wa mwisho ambaye ni Yesu

Genesis 2:16-17 "And the Lord God commanded the man, saying of every tree of the garden you may freely eat ; But of the tree of the knowledge of good and evil you shall not eat, for IN THE DAY that you eat of it you shall SURELLY DIE.

(16 And the LORD God commanded the man, saying, Of every tree of the garden thou mayest freely eat:
17 But of the tree of the knowledge of good and evil, thou shalt not eat of it: for in the day that thou eatest thereof thou shalt surely die.)

Aya hii iko wazi na naamini hapo kwenye herufi kubwa panaonekana vizuri, lakink pia uhakika chukja Biblia ya Kikngereza kin james Version usome kwa uhakika zaidi
 
  • Thanks
Reactions: AWM
Rekebeshia mpendwa, biblia imetofautisha kati ya Mungu na mungu, God and god

Rekebisha ili tuelewe najua ni typing error.
Asante
Typing erro, mkuu.
Nimejaribu kurekebisha lakini sikumaliza naomba Radhi kwa makosa hayo mkuu.
 
Uzi ni mtamu sana na unafikirisha kweli kweli.
Lakini kuna hoja nitazipangua hapa.

Kwanza mwanadamu ni roho inayoishi katika nyumba inaoitwa mwili...
Kwa maana hiyo ni kwamba mwanadamu anatakiwa kuangaliwa kwa kigezo cha kiroho na sio nyumba yake anayoishi kwayo, na ndio maana hata hukumu ya mwisho haitakuwa kwa mwili ila kwa roho yake.

Kuna kitu kimoja cha muhimu sana ambacho watu huwa tunachanganya.
Biblia inasema hukumu za Mungu huwa zinatoka lakini kwa rehema zake Mungu huwa zinacheleweshwa kutekelezwa mara moja.

Mfano ni kipindi cha mnara wa Babeli, Mungu alipunguza urefu wa miaka ya mwanadamu kuishi kutoka miaka 900 na ushehe mpaka miaka 120, lakini punguzo hilo halikutokea ndani ya siku moja.


Watu waliendelea kuishi kwa miaka mingi mfano Ibrahimu na Yakobo waliishi miaka zaidi ya 170.
Na punguzo lile liianza rasmi kutekelezeka mpaka kipindi cha Musa.

Ukisoma kwenye Zaburi Daudi mwenyewe anasema kuwa miaka ya kuishi mwanadamu ni miaka 70 mpaka 80, lakini Daudi huyo huyo akaishi miaka 120.

Kwa hiyo nyingi ya hukumu za Kimungu huwa hazitekelezeki kwa kwa timeframe ya kibinadamu katika time limit yetu, ila katika timeframe ya kiroho.

Ni kweli kabisa kuwa siku Adamu alipokula tunda alikufa, lakini kifo kile kilikuwa ni cha kiroho, kilikuja kudhihirika mwilini baadaye kabisa, na ndio maana Biblia inasema "Mlikuwa wafu kwa sababu ya dhambi na makosa yenu".
Kwa hiyo mtu anapotenda dhambi anakuwa mfu pale pale kiroho, Japo anakuwa anatembea na maisha yake yananawiri kama kawaida.

Mfano mzuri ni antivirus ya computer, ukiikatisha kuingia mtandaoni kuji-update inakuwa imekufa maana umeiblock kuingia kwenye source ya life yake, haifanyi kazi, ila kwenye computer itaendelea kuwepo japo haitakuwa inakamata virus.

Kwa hiyo si kwamba Adam siku alipotenda dhambi roho ilichomoka akabaki na nafsi na mwili, ila ni kweli kiroho alikufa.
Na kifo cha kiroho haina maana ya kuzimika kiroho na kukakamaa, hapana.
Kumbuka hata Jehunum ya moto Mungu anaiita kifo cha pili.
Ni kweli watu wataendelea kupumua na kuwa hai, lakini kiroho ile ni mauti.

Nikupenyezee ubuyu tu kuwa Adamu tangu amekufa mpaka wakati Yesu anakufa, hakuna mtu aiyewahi kwenda mbinguni, wote waliishia kuzimu, ni mpaka Yesu alipotoa ruhusa ya nani aende na ani abaki, maana yeye ndiye aliyeishinda mauti.

Na kweli mara baada ya kufa tu msalabani, alishuka huko chini kufanya kazi part tu, ambayo ni kuzihubiria roho za wafu na zilizomkubali zikapata kibali cha kuondoka naye.

Ni kama Yesu aliposema kuwa tubuni kwa kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia, watu wakajua kiama kimekaribia, lakini mpaka leo miaka buku mbili imepita bado tunadunda.
Shukrani Sana mkuu, Na hiki ndicho nilichomaanisha kusema Adam alikufa in the Day wala haikumchukuwa muda. Kwamba taya alishapoyeza form of life (Spirit), tayari kikawa kifo. Pia Biblia iko wazi naamini tutaielewa tu naweka kwa chini muendelezo wa mada hii. Ikiwa na swali je baada ya adam kupoteza sifa ya ukiroho waliendeleajd kueasiliana na Mungu ? Bila adamu kuwa na roho ?
Masna Mwili na nafsi ndicho kilichobakia kwa adam baada ya kula tunda.
 
Back
Top Bottom