Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mwili wa kuharibika ni mwili wa Nyama uliobeba roho ya kibinadamu ila mwili usiharibika ROHO YA KIBINADAMU iliyohuishwa kwa ROHO WA MUNGU ambao mtu hupata kwa kubatizwa kwa Moto
Ngoja nijaribu. Kama utakuwa umepitia mchango wangu (sijui ni post namba ngapi). Nimejaribu kuonyesha ni vitu gani vinamtenheneza mwanadamu. Vitu hivyo ni mwili na roho. Kwa mfano; mimi naitwa stephen chelu, na nimetengenezwa na mwili na roho. Siku nikifa mtauita mwili wangu 'mwili wa stephen chelu'. Sasa stephen chelu ni yupi ambaye ameuacha mwili wake hapo. Stephen chelu ni ule muunganiko wa mwili na roho. Kwa hiyo mwili na roho kutengana ndo stephen ameondoka hivyo. Kwa hiyo stephen siyo roho wala mwili, bali ni muunganiko.Hivi tunaposema ``mwili wa fulani`` huyu fulani tunayemrefer ni nafsi au roho?
Neno 'Eden' kwa kiebrania maana yake ni 'Presence[uwepo][uwepo wa Mungu in fact].Hapa najua kuna watu wakubwa mno, wenye ufahamu sana, nimeamua kujitupa uku nijifunze zaidi.
Je mtu ana mwili na nafsi au mwili nafsi na roho?
Naamini kwa hakika hili ni swali la msingi sana kwa kila mtu anahitaji kupata majibu sahihi na yakuaminika zaidi (correctly an reliable answered).
Ni vyema zaidi kujadili na kufahamu kwa undani juu vitu hivi vitatu ki ujumla wake.
Katika makala hii nitaangazia japo kwa ufupi saana kile ninachofahamu, naamini ni wengi wametia mikono na kuandika na kuchambua kinaga ubaga juu ya mada hii, lakini si vibaya na mimi nikitia mikono na mchango wangu kwa ufupi.
1. Body, Soul And Spirit
Kabla ya kwenda moja kwa moja kwenye mada yetu ya mwili, nafsi na Roho turejee kwanza kwenye kitabu cha mwazno cha biblia (Genesis). Kitabu cha mwanzo ndio msingi mzima kila kitu, kimeandikwa kwa ufupi lakini kimebeba mwanzo wa kila chenye mwanzo, naamini hata mada tajwa hapo juu hapa ndipo inapoanzia.
GENESIS 2:16-17
16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, matunda ya kila mti wa bustani wawezakula,
17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku(in the Day.. Biblia ya kingereza) utakayokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
Katazo au maagizo Mungu aliompatia adamu ni kwamba asile matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, kwa lugha nyepesi ya kueleweka ni kwamba siku atakapoyagusa na kuyala atakufa kwa hakika ndani ya siku hio hio.
NOTE:
Mambo mawili muhimu yanapatikana hapo…
1: in the Day(ndani ya siku hio hio)
2: Surely die ( Hakika utakufa)
Kifo ilikuwa ni 100% kitokee siku adam angegusa na kula matunda ya mti aliokatazwa.
Sasa katika Mwanzo 3:1-6 tunajua vile shetani alivyo mdanganya hawa na adam hatimaye wakavunja agizo walilopewa na Mungu, na kasha wakala tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Baada ya kula tunda kulingana na agizo la Mungu ilikuwa lazima wapatwe na kifo hapo hapo (at a moment) kama Mungu alivyosema Mwanzo 2:17.
17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku(in the Day.. Biblia ya kingereza) utakayokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
Tatizo liko hapa Mwanzo 5:5-6, Inasemaje kuhusu Adam?
5 “Siku zote za adam alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.
Kwahiyo; kulingana na biblia, adam aliendelea kuwa na maisha au kuwa na uhai ndani yake kwa miaka mingi baadaye baada ya kula tunda hali ya kuwa Mungu alisema kwamba siku utakapo kula hakika utakufa ndani ya siku hio. Sasa nini kilitokea ndani ya siku hio amabapo adam na hwa walipokula tunda? Did they die as God said, au hawakufa?
Who will solve us this problem?
Man’s ideas, theories, religion and tradition? No Only one can give us answer na si mwingine ni Mungu mwenyewe kupitia Neno lake. Na kama unataka biblia kukupatia jibu ni lazima tuiruhusu ijitafsiri yenyewe. Biblia na biblia pekee yatosha.
Kumbuka Hesabu 23:19 inasema.. “mungu si mtu aseme uongo…..”
Tuendelee.. siku Adam na hawa walipokula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya walikufa kwa hakika(they real died). Actually, alikuwa ni sheta aliyesema hamtakufa hakika wakati anamrubuni hawa. Hivyo basi kama wasingekufa siku ile, kama Mungu alivyosema basi shetani angekuwa sahihi kabsa kuwaambia hamtakufa hakika na mungu angekuwa muongo kwa kuwaambia mtakufa hakika, kitu ambacho isingewezekana Mungu kuwa muongo.
Hesabu 23:19. inasema.. “Mungu si mtu aseme uongo…..” Hata hivyo wengi leo hufundisha kwamba wakati Mungu aliposema utakufa hakika alimaanisha kuna mbegu ya kifo itakuwa planted ndai ya adam baada ya kula tunda. Nene la Mungu halihitaji kukingiwa kifua kwa namna hio.
Halihitaji kutetewa wala kukingiwa kifua kwa kile ilichosema kabla badala yake ni ukweli ukweli pekee utasimama. Returning to our topic: Tangu Mungu aliposema wangekufa siku hio, kwa hakika walikufa siku hio hio (SINCE GOD SAID THAT THEY WOULD SURELY DIE THAT VERY DAY, THEY INDEED DIED THAT DAY).
Hata kama waliendelea kuwa na uhai ndani yao baada ya kula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya, ni dhahiri kwamba baada ya kula tunda kuna kitu walikipoteza ndani ya miili yao. Hicho walichokipoteza siku hio baada ya kula tunda kulingana na maneno ya Mungu ndio kifo (absence of a form of life). Hivyo basi tuanapaswa kuangalia ni kitu gani kilichopotea kwa wazaz wetu wa kwanza baada ya kula tunda ambacho ndio kusema adam na hawa walikufa baada ya kukipoteza.
2. Body, soul and spirit: the body and soul aparts
Tunaanza kufanya uchunguzi wetu jinsi gani mtu wakwanza aliumbwa, kitabu cha Mwanzo.
Genesis 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi…”(“and the Loard formed man of the dust of the groung……”)
Ni sehemu gani ya mtu Mungu alioifanya kwa mavumbi ya ardhi? Mwili. Ndiyo maana element za mwili wa binadamu zinapatikana kwenye madini ya ardhi. Kwahio sehemu ya kwanza ya mtu ilikuwa ni mwili(body).
Let’s countinue:
Genesis 2:7 …..and breath into his noistrils the breath of life and man become a living soul.
Tumeona jinsi Mungu alivyomuumba mtu kwa mavumbi ya ardhi, hata hivyo haukuwa na uhai ndani yake. Uliumbwa bila uhai, kIsha Mungu akaupilizia ule mwili (body) pumzi katika pua zake pumzi ya uhai na mtu akawa nafsi hai(living soul. Soul is what givies life to the body. Hapa neon la Mungu linatuambia bila nafsi mwili umekufa.
Where is soul(nafsi iko wapi?), uhai wa mwili, the life of the flesh?
Mambo ya walawi 17:11, 13-14
11 “Kwa kuwa uhai wa mwli u Ktika hiyo damu;….. “(for the life of the flesh is in the blood…)
13 ‘’Mtu yeyote aliye wa wana wa Israeli, au hao wageni wakaao kati yenu, ambaye amemshika mnyama, au ndege ambaye huliwa, katika kuwinda kwake;atamwaga damu yake, na kuifunika mchanga. 14 kwa maana kuliko huo uhai wa mnyama, hiyo damu ni moja na uhai wake……”
Tumekwisha kuona katika kitabu cha mwanzo kuwa nafsi(soul) ndiyo huupa mwili uhai. Hapa katika mambo ya walawi tunaona uhai wa mwili upo katika damu, kwahio uhai wa mwili ni nafsi. How this soul life passes from generation to generation? Through the blood. Acts 17:26“and he has mada from one blood every nation of men to dwell on all the face of the earth”.
Actually, sol is not something only man has. Animals have also soul which again is in the blood.
Mwanzo 1:20-21.
20 Mungu akasema maji na yajawe kwa wingi a kitu kiendacho chenye uhai……..
21 Mungu akaumba nyangumi wakubwa na kila kiumbe chenye uhai kiendacho…….”
Kwahiyo, sio binadamu tu bali hata wanyama wana nafsi hai, hili naamini sio jipya, kama tumeelewa kuwa nafsi hai(soul) ndio huupa mwili uhai, wakati tunapokufa hatuna uhai tena hatuna nafsi(soul). Vile vile hata kwa wanyama nao.although, there is no problem about what is defined as soul in the bible, the problem is created when we go to the bible with the preconceived ideas that soul is immortal. Soul is not something immortal. It just gives life to the body. When you stop having life in your body, you have no more soul.
Sasa tumeona vile Mungu alivyomfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi kasha akapulizia pumzi katika pua zake pumzi ya uhai ili kuupa mwili uhai. Kila mmoja wetu anakubali kabsa kwamba ana mwili na nafsi, tunaweza kuhitimisha kuwa adamu wakati anakufa akiwa na umri wa miaka930, wakati anakula tunda la mti wa mema na mabaya kwa hakika hakupoteza mwili wala nafsi.
Ikiwa hakupoteza mwili wala nafsi wakati alipokula tunda je alipoteza nini ambacho ndio kifo kama alivyosema Mungu?
Let’s continue searching…..
3: Body, Soul And Spirit: The Spirit Apart.
Mwanzo 1:26-27
The god said “Let us make man in our image, according to our likeness… so God created man in his own image, in the image of God he created him; male and female he created them.”
Kulingana na aya hii, mungu alimuumba mtu kwa mfano wa sura yake( zingatia sana hii point) swali la kujiuliza what is the image of God?? Anaonekanaje(what does he look like?
Yohana 4:24 inatuambi hivi…
God is not flesh but is spirit….(Mungu ni roho..). that is his image. Kwahiyo biblia inaposema Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake na kwa sura yke, ina maana kando ya mwili na nafsi bali pia alikuwa na mfanano na Mungu yaani roho.
God is not flesh. He does not have feet, hands,head, yeye ni roho.kama Mungu ni roho na adamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu ni dhahiri kuwa adamu naye ni roho. Mmoja anaweza akauliza kwanini Mungu amuumbe adamu na mwili, nafsi na roho pia?
Jibu rahisi ni kuwa bila adamu kuwa na form ya roho asingeweza kumuona mungu na kuwasiliana naye ana kwa ana kama walivyokuwa wanaonana katika bustani ya edeni, ikiwa mmoja angekuwa kiumbe cha roho na mwingine kiumbe chenye mwili isingekuwa rahisi adamu kumuona mungu maana mungu ni roho. Kama vile usivyoweza kupokea mawimbi ya sauti kutoka radio station nyumbani kwako bila kuwa na radio receiver ndivyo isingewezekana kwa adamu na Mungu.
Unahitaji radio receiver kusudi kupata mawimbi ya suti kutoka radio station.
1wakorintho 2:14 “basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuuzi,wala hawezi kuyafahamu, maana yatambulikana kwa jinsi ya rohoni”.
“But the natural, man does not receive the things of spirit of God, for they are foolishness to him: nor can he know, because they are spiritually discerned.”
Kulingana aya hapo juu mtu ambaye ana mwili na nafsi does not receive the things of the spirit of God. Kama nilivyokwisha kusema mambo ya roho ya mungu. Ili kuwasiliana na mungu unapaswa uwe na receiver i.e. spirit.
Summary
Adam alikuwa na mwili uliumbwa kutoka katika mavumbi ya ardhi, akapewa nafsi kwa kupuliziwa pumzi puni ilioupa flesh body uhai kisha akapewa na roho ili kuwasiliana na mungu. He was body, soul and spirit.baada ya adamu na hawa kula tunda ambapo mungu aliwaambia wakila hakika watakufasiku hio, ni hakika walikufa siku hio hio. Bearing in mind that death means the absence of form of life, tunaweza kuona sasa kifo kilichotokea siku ile.
Adam alikuwa ni mwili, nafsi na roho na mwili wake ulikufa miaka mingi baadaye after tht day that he ate, nafsi ndio inayoupa mwili uhai kama tulivyoona hapo awali, hivyo ni kusema baada ya kula tunda mwili na nafsi bado viliendelea kuishi miangi tu.
Mungu alisema kwa hakika siku utakayo kula utakufa hakika, tumeona vile mungu asingeweza kusema uongo kwamba adamu ale na asife, kabla ya admu kula alikuwa na sifa zote tatu body, soul, and spirit ilikuwa ni lazima afe maana alishakiuka masharti ya muumba wake. Baada ya kula tunda adamu alipoteza roho ambacho ndicho kifo chenyewe cha kiroho.
Baada ya adamu kula tunda alikuwa mfu mbele za Mungu, alikosa sifa ya kuwa na sura ya mfano wa mungu, hivyo akawA mfu. Na huu ndio ulikuwa mpango wa shetani kumfanya mungu na mwanadamu wakosane ili wasiweze kuwasiliana tena.
But God is I love, kupitia kwa mwanae tunakuwa viumbe vipya tena kwa kumuamuni tunarejeshewa kile kilichopotea pale tu adamu alipokula tunda.
1 Wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyeweawatakase kabsa;nanyi nafsi zenu na roho zenuna miili yenu mhifadhiwemuwe kamili,……”
Asanteni...
Karibuni siwezi ku-tag, ningewatag wengi tu. Karibuni kwa ujumla wenu.
Sasa kama ndio hivyo kwanini tunatubuAlikuwa nazo zote, roho, nafsi na mwili
Ndio maana ukisoma vizur mwanzo sura ya 3 utaona
Laana iliyo tolewa kwa nyoka na laana pamoja na adhabu aliyo pewa Adamu
Adamu (ambaye ni msaidizi naye alipata adhabu yake)
Mwisho wa adhabu ndio inakamilika kuwa hakika utakufa na mwishoni wakafa baada ya miaka kupita
Kutolewa tu nje ya bustani ilikuwa adhabu tosha kwao, hawkuzoea kulima, hawakutakiwa kula kwa jasho, haikutakiwa kuzaa kwa uchungu
Ndani ya ile hakika mtakufa ndani yake kumebeba adhabu hiyo
Mauti ni pigo la mwisho.
Hizo gharama ni zipi ambazo tunatakiwa kuziripia ili tulipate hilo vazi.Mwili umewekwa tayar kubeba nafsi na roho
Mwili ni kibebeo tu
Nataka niwaze kwa upana, walipo kula hilo tunda la mti wa ujuz wa mema na mabaya
Nawaza hivi kwanini walijiona uchi?
Kwan mwanzo hawakuwa uchi?
Ina maana kuna vazi ambalo Mungu aliwaficha nalo liliondoka muda ule
Ni kama mtu aliyefunikwa baadaye akaondolewa ktk mfuniko huo ndio akajua yupo uchi
Na hicho ndicho kitu shetan alitaka akipate
Asingeweza kuwagusa katika lile vazi ambalo Mungu aliwavisha na shetan asingeweza kuwadhuru hadi wawe uchi
Kama wakiwa hawana nguo ndio ilimpa shetan uhalali wa kuwagusa sasa
Ndio maana Mungu akaamua kutekeleza adhabu aliyo waambia kuwa hakika mtakufa
Nawaza katika Roho kuwa
Kuna uwepo ambao Mungu aliwafunika nao kias kwamba alikuwa na uwezo wa kuja jioni kuwatembelea
Kuwa kwao uchi walipoteza kibali, nafasi na nguo ambayo Mungu aliwapa
Nawaza kuwa lilikuwa vazi special ktk Roho
Vazi ambalo ukilipoteza kulipata ni gharama kubwa sana kuirudisha
Ndio maana utakuja kukuta Yesu alikufa ili atukomboe
Mtu kufa kwaajil ya wengi nawaza ni kipi Adamu alichopoteza Eden hadi Mungu kuamua kumachilia mtoto wa pekee afe
Kilikuwa kitu kikubwa mno, ulinzi mkubwa mno, tena cha thamani ambacho kinacost Damu imwagike
Hivyo Adamu alibak na mwil nafsi na roho alichopoteza ni kitu kama hicho juu
Ushirika na Mungu uliondoka, uhusiano na Mungu ulipotea, urafiki na Mungu ulipotea
Yesu atupe kujua thamani Yetu rohoni
Amen
Hapa kuna kitu nimekiona,Shukrani Sana wadau kwa hoja zenu mnanifanya nizid kugain vitu ambavyo nivyamsingi sana kuvijua.
Naanza na hoja ya kuwa je adam baada ya kula tunda alibaki kuwa na mwili, nafsi na roho au mwili na nafsi pekee ??
Divine: maelezo yako hapo juu nimeyaelewa sana na siitaji kutia neno tena apo maana umeeleza hata zaidi ya nilivyokuwa nawaza mimi.
Adam alibakia kuwa na sifa mbili tu ! Nazo ni mwili na nafsi(kuna uzi nitaweka chini hapo kuelezea zaidi hili navyofahamu ila hapa najibh kwa ufupi tu).
Tusome haya maandiko yatatusaidia kuelewa zaidi
Thessalonians 5:23 says:
“Now may the God of peace Himself sanctify you completely; and may your whole spirit, soul, and bodybe preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.”
(23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.)
Kulingana aya hii, inaonyesha wazi kuwa hatuko kamili yaani kuna kitu kimepungua kwetu, viko vitatu amejaribu kuviorodhesha hapo. Mwili, nafsi na roho.
Wote tunakubaliana kuwa mwili ni kibebeo cha nafsi na roho, sasa swali la kujiuliza ni kipi ambacho hakijakamilika kinachoelezwa hapo ? Je ni nafsi au Roho ?
Mwanzoni nilieleza kwa mafungu kuwa mwili hauwezi kuwa hai bila nafsi hivyo nafsi ndiyo inayoupatia mwili uhai. Kwa maelezo haya tunaona kuwa hatuko kamili kwa kukosa sifa ya tatu yaani roho(spirit).
John 3:1-6
"There was a man of the Pharisees named Nicodemus, a ruler of the Jews. This man came to Jesus by night and said to him, "Rabbi, we know that you are a teacher come from God; for no one can do these signs that you do unless God is with him." Jesus answered and said to him, "Most assuredly, I say unto you, unless one is born again [the Greek text reads "born from above"], he cannot see the kingdom of God."
(1 Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.
2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.
3 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili,........
Baada ya adamu kula tunda ni wazi kuwa alikufa maana alipoteza form of life ya spirit(ukiroho), hivyo akawa mfu mbele za Mungu, hapa kristo anasema ili tuingie kwenye ufalme wa mbinguni au ili tuonane na Mungu ni lazima tuzaliwe tena mara ya pili. Tuzaliwe ndio maana hatupo, kinachozaliwa ni kana kwamba hakikuwepo hivyo kinazaliwa ili kiwepo. Na sisi ni kana kwamba hatupo maana hatuna sifa ya ukiroho ambayo ndio image of God.
Questions may come immediately to our minds: "How does this birth occur?"
birth?", "what do I receive from this birth?".
John 3:4-5
"Nicodemus said to him, "How can a man be born when he is old? Can he enter a second time into his mother’s womb and be born? Jesus answered, "Most assuredly, I say to you, unless one is born of water and of the Spirit, he cannot enter the kingdom of God."
(4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho,.......)
In this passage Jesus Christ explains us that for a man to enter the kingdom of God he should be born of water and of the spirit. To be born of water means the first birth. Without having been born once, how could you be born again? He tells us also that one should be born of the spirit.
John 3:6
"That which is born of the flesh is flesh, and that which is born of the Spirit is spirit."
(6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.)
Again the two births are put together in the same sentence but this time the purpose is to contrast them and to show that they are entirely different. From the first birth you received what your parents are i.e. flesh. Similarly, from the second birth you received what your parent, God, is i.e. spirit
Karibuni tena tuendelee na mada.
Dhambi sio kifo, kifo ni matokeo ya dhambi, Dhambi ni nafsi,Kweli yameniingia, Kumbe dhambi ni kifo. Na je kama ndio hivo mbona kuna mahali inasema tukisema hatuna dhambi tunajidanganya? Pili na je kama mtu akitenda dhambi anakufa kiroho, Je Petro alipomkana BWANA alikufa kiroho? Tatu Kama Roho wa MUNGU ndio pumzi je roho ya kibinadamu ni ipi?
Mimi kwa uwela wangu kuna Mambo haya Mwili wa binadamu unaobeba Nafsi ambayo ndio roho ya kibinadamu kwa maana nyingine ni Dhamira au nia. 2.ROHO wa MUNGU ambayo mtu hupata kwa kumtii MUNGU na kumwomba MUNGU na kuwa mtakatifu, na 3.Ni roho ya shetani ambayo huingia kwa mtu ambaye hana roho wa MUNGU pia humshawish mtu kutenda mabaya.
Ndo kusema roho ya kibinadamu hafanya kazi kwa 1.utashi wake 2.Kwa kumsikiliza ROHO WA MUNGU au neno la MUNGU na sauti yake au Mwisho Roho ya shetani,mapepo,majini n.k.
Roho ya kibinadamu hufanya kazi kwa kusikia kuona kuisi n.k Roho ya kibinadamu ndo nafsi hapo sasa kwenye kufa kwa dhambi ni Ipi kati ya Tatu hizo hufa yaani Dhamiri njema a.k.a ROHO WA MUNGU au Dhamiri ya kawaida a.k.a nia a.k.a utu a.ka Roho ya kibinadamu au Roho mbaya a.k.a Roho ya shetani nijibu ni ipi hufa? Kwa kutenda dhambi?
NafsiUnaposema miguu yangu inauma, ni nani huyo anayesema? Miguu ni ya nani?
Boss hiyo hadith yq biblia ilikua hadithi tu, yakujaribu kijenga mantik ya uumbaji na kukosa utii kwa mwanadamu.Bado nawaza kwa sauti, kwa nini hilo tunda la mti wa mema na mabaya liliumbwa.
Shukrani Sana mkuu umefikiria mbali kidogo zaidi ya pale nilipofikiria.Hapa kuna kitu nimekiona,
Mwili, Nafsi (damu kwa maelezo yako) & Roho
Tukianza na nafsi,
Umeichambua juu juu kama damu (kimiminika), kwa mtizamo wangu msingi wa nafsi ambayo ni damu ndicho kiwakilishi cha mabaya, (ego), namaanisha dhana ya dhambi. Nafsi ndio kiini cha mtu kutenda jambo kwa kujali upande wake au kujilinda ( njaa, hasira, wasi wasi chuki na tamaa).
Nafsi ndio dhana ya ubaya ktk mti ule,
Nafsi ndio chanzo cha dhambi,
Asilimia 90 ya wanadamu wanaongozwa na nafsi,
NAFSI NI GIZA.
Tukija ktk dhana ya roho,
Roho ni mema,
ROHO NI NURU (mwanga)
Roho ni kinyume cha nafsi.
Muunganyiko wa NAFSI na ROHO,,
Ndio mti wa mema na mabaya unaozungumziwa,
Katika mti huu ndipo penye lile tunda linalozungumziwa,
Ambalo kipo ktk tawi la nafsi,
Roho na nafsi zinaishi pamoja,
Lakini nafsi inanguvu zaidi ktk kumpumbaza mwanadamu,
Kwa sababu nafsi ndio mchakato wa kujitegemea na dhana ya kutajirika au umaarufu,
Kuishinda nafsi ni kazi kubwa sana,
Aliyeweza ni yesu peke yake.
Kumbuka zile nafsi zilizo shangilia zilizo mtesa yesu akiwa msalabani zilifanya maamuzi kwa kuangalia nafsi zao,
BINADAMU NI MATEKA WA NAFSI,
Lakini yesu alisema (kumbuka wakati huo anamisumari mkononi na miguuni pamoja na taji la miimba kichwani lakini hakuyajali maumivu hayo na kejeli hizo kwa sababu alikuwa anajua hivyo vitu ni nafsi) eee baba mwenyezi mungu wasamehe watu hawa maana hawajui walitendalo,
Pia rejea yule jamaa wa kulia na kushoto pale msalabani, yule wa kushoto alimwambia yesu kama kweli wewe ni mwana wa mungu jiokoe, kujiokoa hiyo ni nafsi.
KUISHINDA NAFSI UNAHITAJI KUTAMBUA UWEPO WA ROHO NA KUISHI KIROHO,
Ndio maana tunaambiwa watakao shinda dhambi (nafsi), wataishi milele huko mbinguni.
DHANA YA UBATIZO,
Kwamba mtu abatizwe kwa maji (sio maji kama unavyofikiria),
Hapo maji yame tumika kama kiwakilishi cha roho ambacho ni damu kwa muujibu wa maelezo yako(roho).
Kwahiyo mtu kuzaliwa upya kiroho kumwagiwa maji kichwani bali NI UTAMBUZI WA NGUVU YA ROHO ILI KUISHINDA NAFSI,
ndipo upate lile vazi alilokuwa nalo adamu na hawa kwa muujibu wa DIVINE.
Hayo ni maoni yangu tu.
Siku utakayo kula matunda hakika utakufa utakufa,
Ahadi ya Mungu ilikuwa ni kuishi milele katik hii dunia.
Na Mungu kila jioni alikuwa anaenda kuwatembelea,
Walipokula ndicho kilicho tokea kufa ni adhabu, Mungu hakuweka kifo mwanzoni kifo kilitokana na adhabu ilitokana na kukiuka maagizo ya Mungu katika bustani ya Edeni
Ukisoma mwanzo vizuri utaona adhabu iliyo tolewa na laana ilitolewa
Katika adhabu hizo kifo ni kimojawapo
Pia hakuna sehemu aliyosema atakufa baadae baada ya kumega tunda na kimwana, hii nayo vipi mkuu?Sioni wapi Mungu amesema utakufa siku hiyo hiyo,neno linasema utakufa hakika,ikiwa na maana kuwa kuanzia pale kutakuwa na kufa na sio kuishi milele,ndio maana baada ya hiyo miaka 139 Adam alikufa...
Mkuu umenena vyema lakini vipi kuhusu kitabu cha Petro kinachosena miaka elfu moja kwa mwanadamu ni sawa na siku moja kwa MunguUzi ni mtamu sana na unafikirisha kweli kweli.
Lakini kuna hoja nitazipangua hapa.
Kwanza mwanadamu ni roho inayoishi katika nyumba inaoitwa mwili...
Kwa maana hiyo ni kwamba mwanadamu anatakiwa kuangaliwa kwa kigezo cha kiroho na sio nyumba yake anayoishi kwayo, na ndio maana hata hukumu ya mwisho haitakuwa kwa mwili ila kwa roho yake.
Kuna kitu kimoja cha muhimu sana ambacho watu huwa tunachanganya.
Biblia inasema hukumu za Mungu huwa zinatoka lakini kwa rehema zake Mungu huwa zinacheleweshwa kutekelezwa mara moja.
Mfano ni kipindi cha mnara wa Babeli, Mungu alipunguza urefu wa miaka ya mwanadamu kuishi kutoka miaka 900 na ushehe mpaka miaka 120, lakini punguzo hilo halikutokea ndani ya siku moja.
Watu waliendelea kuishi kwa miaka mingi mfano Ibrahimu na Yakobo waliishi miaka zaidi ya 170.
Na punguzo lile liianza rasmi kutekelezeka mpaka kipindi cha Musa.
Ukisoma kwenye Zaburi Daudi mwenyewe anasema kuwa miaka ya kuishi mwanadamu ni miaka 70 mpaka 80, lakini Daudi huyo huyo akaishi miaka 120.
Kwa hiyo nyingi ya hukumu za Kimungu huwa hazitekelezeki kwa kwa timeframe ya kibinadamu katika time limit yetu, ila katika timeframe ya kiroho.
Ni kweli kabisa kuwa siku Adamu alipokula tunda alikufa, lakini kifo kile kilikuwa ni cha kiroho, kilikuja kudhihirika mwilini baadaye kabisa, na ndio maana Biblia inasema "Mlikuwa wafu kwa sababu ya dhambi na makosa yenu".
Kwa hiyo mtu anapotenda dhambi anakuwa mfu pale pale kiroho, Japo anakuwa anatembea na maisha yake yananawiri kama kawaida.
Mfano mzuri ni antivirus ya computer, ukiikatisha kuingia mtandaoni kuji-update inakuwa imekufa maana umeiblock kuingia kwenye source ya life yake, haifanyi kazi, ila kwenye computer itaendelea kuwepo japo haitakuwa inakamata virus.
Kwa hiyo si kwamba Adam siku alipotenda dhambi roho ilichomoka akabaki na nafsi na mwili, ila ni kweli kiroho alikufa.
Na kifo cha kiroho haina maana ya kuzimika kiroho na kukakamaa, hapana.
Kumbuka hata Jehunum ya moto Mungu anaiita kifo cha pili.
Ni kweli watu wataendelea kupumua na kuwa hai, lakini kiroho ile ni mauti.
Nikupenyezee ubuyu tu kuwa Adamu tangu amekufa mpaka wakati Yesu anakufa, hakuna mtu aiyewahi kwenda mbinguni, wote waliishia kuzimu, ni mpaka Yesu alipotoa ruhusa ya nani aende na ani abaki, maana yeye ndiye aliyeishinda mauti.
Na kweli mara baada ya kufa tu msalabani, alishuka huko chini kufanya kazi part tu, ambayo ni kuzihubiria roho za wafu na zilizomkubali zikapata kibali cha kuondoka naye.
Ni kama Yesu aliposema kuwa tubuni kwa kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia, watu wakajua kiama kimekaribia, lakini mpaka leo miaka buku mbili imepita bado tunadunda.
Umenitoa tongotongo mkuuMwili umewekwa tayar kubeba nafsi na roho
Mwili ni kibebeo tu
Nataka niwaze kwa upana, walipo kula hilo tunda la mti wa ujuz wa mema na mabaya
Nawaza hivi kwanini walijiona uchi?
Kwan mwanzo hawakuwa uchi?
Ina maana kuna vazi ambalo Mungu aliwaficha nalo liliondoka muda ule
Ni kama mtu aliyefunikwa baadaye akaondolewa ktk mfuniko huo ndio akajua yupo uchi
Na hicho ndicho kitu shetan alitaka akipate
Asingeweza kuwagusa katika lile vazi ambalo Mungu aliwavisha na shetan asingeweza kuwadhuru hadi wawe uchi
Kama wakiwa hawana nguo ndio ilimpa shetan uhalali wa kuwagusa sasa
Ndio maana Mungu akaamua kutekeleza adhabu aliyo waambia kuwa hakika mtakufa
Nawaza katika Roho kuwa
Kuna uwepo ambao Mungu aliwafunika nao kias kwamba alikuwa na uwezo wa kuja jioni kuwatembelea
Kuwa kwao uchi walipoteza kibali, nafasi na nguo ambayo Mungu aliwapa
Nawaza kuwa lilikuwa vazi special ktk Roho
Vazi ambalo ukilipoteza kulipata ni gharama kubwa sana kuirudisha
Ndio maana utakuja kukuta Yesu alikufa ili atukomboe
Mtu kufa kwaajil ya wengi nawaza ni kipi Adamu alichopoteza Eden hadi Mungu kuamua kumachilia mtoto wa pekee afe
Kilikuwa kitu kikubwa mno, ulinzi mkubwa mno, tena cha thamani ambacho kinacost Damu imwagike
Hivyo Adamu alibak na mwil nafsi na roho alichopoteza ni kitu kama hicho juu
Ushirika na Mungu uliondoka, uhusiano na Mungu ulipotea, urafiki na Mungu ulipotea
Yesu atupe kujua thamani Yetu rohoni
Amen
Umedadavua vyema hongeraUzi mzuri. Japo nimesoma kwa kuscan.
Tuanzie kwenye uliyoyasema kwenye uzi wako. Hivyo ili kugupisha, "kusummarise" sitarefer qoutes maana ushazionyesha na mimi nazitudia tu.
Kwenye hadithi ya piliya uumbaji( hadithi ambayo binadamu kaubwa kwa udongo). Hadithi imetanabaisha jinsi binadamu alivyo asili ya ardhi(mwili) na Mungu(roho).
Mungu akamfinyanga binafamu kwa vumbi la nchi, kisha akampulizia pumzi yake puani. Na binadamu akawa nafsi hai.
Binadamu alimbwa kwa udongo. Japo haielezewa kwenye biblia. Ila binadamu alimbwa kwa udongo akawa kiumbe hai.
Hivyo baada tu ya kufinyangwa kwa udongo, tayari alikua na nafsi.
Hata hivyo hakua na roho.
Ama kwa maana nyingine nafsi yake haikua hai.
Ila baada ya kupuliziwa Pumzi ya Mungu. Nafsi yale ilihuishwa.
Hivyo kiroho, nafsi ya binadamu ni zao la "reaction kati ya pumzi ya Mungu(roho) na mwili wa binadamu.
Hivyo ndan yetu binadamu, mna roho ya Mungu ilipaswa na inapaswa iwe hivyo.
Pia ndani mwetu mna roho zetu. Roho zetu zi hai. Pale tu ambapo roho ya Mungu i ndani mwetu.
Mda roho ya Mungu inatoka ndani mwetu. Roho zetu zimekufa. Ni hadi zitakapo huishwa tena kwa Roho wa Mungu kurudi ndani mwetu, ndipo zinapo pata na kufanya kazi inavyo paswa.