TANZIA Bondia Hassan Mgaya afariki Dunia baada ya kupigwa kwa TKO

TANZIA Bondia Hassan Mgaya afariki Dunia baada ya kupigwa kwa TKO

Bondia Hassan Mgaya amefariki dunia, siku moja baada ya kupigwa TKO katika pambano la raundi sita lililofanyika Tandale kwa Mtogole, Dar es Salaam katika ukumbi wa Dunia Ndogo, na kupoteza fahamu dakika chache baadaye.

Mgaya alicheza pambano hilo lililofanyika Desemba 28, yaani usiku wa kuamkia leo, jijini Dar es Salaam. Pambano hilo, ambalo halikuwa la ubingwa, lilimkutanisha na mpinzani wake, Paulo Elias.

Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika Mgaya alidondoka ulingoni na mwamuzi akamhesabia na kumpa mpinzani wake ushindi wa TKO. “Mgaya alipigwa na kwenda chini, mwamuzi akamhesabia, na ikawa TKO kwa sababu marehemu alishindwa kuendelea. Baada ya mwamuzi kumaliza kuhesabu, alitembea hatua kadhaa hapo hapo ulingoni kisha akaanguka na kuzimia,” amesema shuhuda.

Ameongeza; “Baada ya kuzimia, Mgaya alipewa huduma ya kwanza kutoka kwa madaktari waliokuwepo kwenye pambano na akazinduka, kisha akapelekwa Hospitali ya Sinza kwa ajili ya matibabu,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kufikishwa Hospitali ya Sinza, kutokana na hali yake alipatiwa rufaa ya kupelekwa Hospitali ya Mwananyamala ambako umauti umemkuta leo. Pambano hilo liliandaliwa na Golden Gloves wakishirikiana na Ngoswe Uwezo.

Kwa upande wake, bondia Cosmas Cheka, ambaye ni Mweka Hazina wa Chama cha Mabondia nchini Tanzania, amesema suala la msiba wa marehemu Mgaya wanalishughulikia wao kama mabondia kuanzia mwanzo hadi mazishi.

Pia, Cheka amesema chama cha mabondia wapo mbioni kuandaa utaratibu wa kumsimamisha mwandaaji wa pambano hilo, Haji Ngoswe. “Nimemshauri Mwenyekiti wetu wa Chama cha Mabondia Tanzania, Japhet Kaseba, kuandika barua ya kupeleka TPBRC ya kumsimamisha Promota Haji Ngoswe kwa kutoonyesha ushirikiano kwa bondia aliyefariki dunia,” amesema Cosmas Cheka akionesha masikitiko.
View attachment 3188183
Ulaji wenyewe ugogolo halafu wenda kupigana. Siyo kila bondia ni bondia wanangu mchungu sana njaa zenu.
 
Hivi kwenye hali hiyo mgonjwa akikimbizwa Muhimbili hawezi kutibiwa?

Yule mama wa Huba aliishia hapo hapo, haipendezi.

Poleni wote.
 
Mshana Jr hivi hakuna mambo ya uganga hapo? Nahisi zile ngumk zao zinakuwa na uganga labda alizidiwa. Ila pia hapo hospital nahisi atakuwa alikosa huduma kabisa maana hospital zetu bila kufahamiana na kuwa na hela yaani unakufa huku wanakuangalia
 
Mshana Jr hivi hakuna mambo ya uganga hapo? Nahisi zile ngumk zao zinakuwa na uganga labda alizidiwa. Ila pia hapo hospital nahisi atakuwa alikosa huduma kabisa maana hospital zetu bila kufahamiana na kuwa na hela yaani unakufa huku wanakuangalia
Wabaroga sana lakini sometimes hali za maisha zinachangia
Kipato duni
Lishe mbovu
Afya dhoofu
Stress za familia, madeni nk
Usaidizi hafifu toka kwa promoter
Na baya zaidi kukamiana. Badala ya kucheza professional boxing wao ni kukamiana kuumizana
 
Waandaji wakamatwe. Wameua bila kukusudia.

Sioni bondia humo , namuona kijana wa mtaani mwenye lishe duni. Anapandaje ulingoni.!?
Jamaa anaonekana alikua na lishe duni sana
Bongo 95% ya mabondia wana lishe duni, mapambano mengi mno unakuta wanalipwa laki mpaka laki mbili unadhani utajimudu lishe nzuri, mana ng'ombe hanenepi siku ya mnada unakuta wiki kabla ndo mtu anaanza kuzingatia mlo wakati ilitakiwa iwe ndo desturi yake kuzingatia mlo.
 
Mshana Jr hivi hakuna mambo ya uganga hapo? Nahisi zile ngumk zao zinakuwa na uganga labda alizidiwa. Ila pia hapo hospital nahisi atakuwa alikosa huduma kabisa maana hospital zetu bila kufahamiana na kuwa na hela yaani unakufa huku wanakuangalia
Kuna kitu inaitwa muku ndo wengi nachanjia uyu akikupiga ngumi moja kabisa ya kuwania lazima uende chini na ukate moto muku ni 🔥
 
Binafsi wanaosema kuhusu lishe nawaunga mkono kabisa haiwezekani bondia kila siku ugali kachumbari kabadili sana kaenda mbagala kununua ming'oko sasa si kutafuta kifo huko ile kazi ngumu
 
Sipati picha huyu bondia aliyesababisha kifo Cha mwenzie yupoje kisaikolojia,ni ujiko kusababisha kifo ulingoni?atakosa mapambano mengine kwamba ngumi zake Zina mikosi?
 
Back
Top Bottom