TANZIA Bondia Hassan Mgaya afariki Dunia baada ya kupigwa kwa TKO

Nina uhakika huyu bondia hajipima Afya.

Pia nina uhakika huyu ni wale bondia hutumia vitu Fulani kabla ya kulivamia jukwaa.

Pole Sana FAMILIA naona udhaifu mkubwa juu ya hili swala la boxing
Kuanzia maandalizi , lishe na n.k .
 
Huo mchezo ni hatari sana
Sio hata mchezo hatari kama wakizingatia mambo ya muhimu katika Boxing

Kuna Mtu alipigwa ngumi nyingi kama Evander Hollyfield au Muhammad Ally?

TATIZO, Hizi ngumi za uswahilini unakuta Bondia hapimwi vizuri afya na specialists au hazingatii mlo kamili unaoendana na shughuli ya Ubondia
 
Ndondi kwasasa imekuwa ni mchezo wa vijana wengi wenye hali duni, wanajitafuta, ni vizuri mtaalamu wa lishe awepo kila pambano awakague kabla ya kupanda ulingoni, anaoona hawana lishe wazuiwe, bila hivyo tutapoteza mabondia wengi.
RIP
 
Hatari sana, kama bondia atategemea hela ya Pambano ndo ale!
 
Tunatakiwa kuambiwa uzito aliokua nao. Aliopimwa kabla ya pambano, vipimo vya afya alivyofanyiwa kabla ya pambano kisha ndiyo waanze kujigamba kwamba watasimamia mazishi mwanzo hadi mwisho
 
Boxing siyo mchezo, kina gypsy king tu alipigwa Moja na usyk ile first match wenge aliloona siyo mchezo kabisa. Huu mchezo unahitaji maandalizi sana hasa ya kimwili na kiakili, huwezi kuniambia unakula mo energy na chapati au mihogo Kila asubuhi, mchana ukila vizuri sana ni dagaa au visamaki viwili, usiku chipsi au chapati mbili na maharage then unapigiwa simu tu from nowhere ukapigane kesho, this is insane. Poleni sana.
 
Tatizo la Boxing huwa hakuna kutegea waamuzi wa Ndondi Bongo wawe wanaangalia dalili za kabla ya mtu kupatwa na Brain damage.
Wanazijua basi hata dalili zake?

Ukizingatia hata huduma alizopewa zilikuwa duni mno,ilibidi mwamuzi atoe taarifa kwa kamisheni ya pambano bondia asipelekwe Sinza apelekwe moja kwa moja M/nyamala then M/nyamala wamrufae Muhimbili.
 
R.I.Pkamanda amefariki akiwa anapambania nyota
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…