Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Hamna aliyesema serikali idairekt movie au ifanye recruitment ya actors. Kwanini wasanii wakitaka msaada wa serikali mnashangaa?, kwani wao hawahitaji usimamizi kwenye kazi zao?

Ishu ni kuwa hujawahi kuwa kwenye kiwanda cha filamu. Swali dogo tu tumetengeneza movie hiyo tumeita sponsors n.k JE BONGO.... FILAMU INAUZWA VIPI? HATUNA SINEMAZ. WEWE UNAWEZA KUSTREAM FILAMU NETFLIX? na bando lako buku jero mkuu?

Its not about quality au waigizaji au sponsors ao wapo tu. Kwani sponsors hawapo? Faida inarudi vipi? Mna sinemaz? Mna stream?

Mkuu naomba ukasome how film industry works ndo tuje kuendelea na mjadala.
Nimefanya kazi za documentary kama msimamizi na pia za matangazo, naelewa nini nachozungumza, nilitengeneza script ya tangazo ambalo lilionekana bora kuliko waliosomea.
Point yako haina msingi hata kama sijawahi kutengeneza movie mwisho wa siku ukitengeneza unaotegemea kununua kazi zako sio walio na ujuzi wa movie industry lakini kitakachovutia kazi zako kununiliwa ni ubora wa kazi yako si kinginecho.
Kwa jinsi ulivyonijibu ndivyo inavyoonyesha upeo wenu ulivyo.
Nataka nikupe somo wewe na wenzako, Hollywood kuna watu wanaitwa criticism ambao movie ikitoka wao wanaangalia kabla haijaenda sokoni, wengi ni waandishi wa magazeti au watangazaji wa tv maoni yao ndio yanaiganya movie iuzwe au ikose soko na kazi yao kubwa ni kukosoa lakini nyinyi mkiambiwa ukweli mnabaki kubisha ndio maana movie zenu za hapahapa hazina mbele wala.nyuma.
 
Waziri kama shangingi[emoji23][emoji23], hata mimi nilishangaa, Tatizo hawafanyi research maisha ya waziri yanakuaje akiwa nyumbani , the way wanavyoongea Yan utadhan mmama anayeuza wanawake malaya
Hahahaha yaani nimecheeeka, sio utadhani shangingi ni lishangingi flan hivi kama sio la Magomeni basi la Kigogo linalomiliki danguro eti ndio waziri aiseee!
 
Nimefanya kazi za documentary kama msimamizi na pia za matangazo, naelewa nini nachozungumza, nilitengeneza script ya tangazo ambalo lilionekana bora kuliko waliosomea.
Point yako haina msingi hata kama sijawahi kutengeneza movie mwisho wa siku ukitengeneza unaotegemea kununua kazi zako sio walio na ujuzi wa movie industry lakini kitakachovutia kazi zako kununiliwa ni ubora wa kazi yako si kinginecho.
Kwa jinsi ulivyonijibu ndivyo inavyoonyesha upeo wenu ulivyo.
Nataka nikupe somo wewe na wenzako, Hollywood kuna watu wanaitwa criticism ambao movie ikitoka wao wanaangalia kabla haijaenda sokoni, wengi ni waandishi wa magazeti au watangazaji wa tv maoni yao ndio yanaiganya movie iuzwe au ikose soko na kazi yao kubwa ni kukosoa lakini nyinyi mkiambiwa ukweli mnabaki kubisha ndio maana movie zenu za hapahapa hazina mbele wala.nyuma.
Kwa jinsi wanavyoshupaza shingo wakikosolewa ndivyo wanavyozidi kwenda kuharibu, yaani wanaambiwa kuhusu story zao kukosa ubunifu na msisimko wanasema bajeti, Wanaambiwa waoneshe uhalisia wa hayo maigizo yao wanasema bajeti, wanaambiwa watafute location nzuri hapa hapa Tanzania tuna vivutio teleeee wanasema bajeti,

Basi watupishe wenye bajeti zetu tufanye kazi napo wanasema Bajeti, hehehehehe kazi kweli kweli.
 
BONGO MOVIE WENGI NI VILAZA, SIO AJABU WAMEILAZA SANAA YA UIGIZAJI.

Anaandika, Robert Heriel.

Hapana shaka sanaa ya Uigizaji kwa sasa imelala Usingizi wa Pono, imelala fofofo na waigizaji wake wanakoroma. Wapo kwenye ndoto za majinamizi wabaya wanaowakimbiza kwenye mitaro huko usingizini. Tangu kifo cha Marehemu Kanumba miaka zaidi ya tisa iliyopita Tasnia ya Bongo Movie imelala fofofo.

Hakuna Tasnia inayoongozwa na Vilaza isilale, sijawahi kuona popote pale duniani. Bongo Movie imejaa wasanii vilaza kwa kiwango kikubwa sana, watu waliokimbia shule ndio wamekimbilia huko kwenye tasnia ya filamu. Embu fikiria mtu amekimbia shule kwa kushindwa somo hata la kiswahili unafikiri atatuambia nini kwenye suala la kuelimisha jamii kupitia fani ya uigizaji.

Kilaza ni kilaza tuu, uwezo wake wa kufikiri ni mdogo alafu anakuwa Director wa filamu, unafikiri filamu yake itakuwaje kama sio Utopolo. Kilaza hufikiri mambo chini ya kiwango, ukiwaangalia wasanii wengi wa bongo movie wakiigiza kwanza hawawezi kuuvaa uhusika, wanachojua ni kutoa macho, kukenua, kubinua makalio, kuvaa nguo fupi, wakati kwa upande wa wasanii wa kiume wanachjua ni kupaka piko sijui waves nywele zao, kutoboa masikio au kubandika stiker masikioni, na kulamba lamba midomo kama sio kusuka nywele. Kwa mambo haya wamefuzu kwani mambo haya hufanywa kwa sehemu kubwa na vilaza, kwani hata mtu asiye msanii anaweza kufanya mambo hayo. Vilaza hufanya mambo ambayo mtu yeyote anaweza kufanya.

i/ Muongoza Filamu alifeli shule, akaunga unga wee akapata cheti, huyo akajiingiza kwenye Tasnia ya Filamu, haya embu niambie atatupa kipi cha maana hapo?
ii/ Mtayarishaji alifeli shule, akaunga unga wee, embu niambie ataleta jambo gani katika ulimwengu huu wa elimu, sayansi na teknolojia?
iii/Mchukua Kamera alipata sifuri au four ya mwisho kabisa, hivi unategemea atakuwa na ubunifu gani kwenye masuala ya kurekodi picha na video na kamera?
iv/ Mtia sauti, aliishia kidato cha nne, embu niambie anauelewa gani na mambo ya sauti, muziki na ala? Sio ajabu sauti nyingi zinazoingizwa kwenye movies nyingi ni zile zile haziendani na uhalisia,
v/ Mtu wa Makeup aliishia darasa la pili, hivi anajua nini kuhusu urembo? Kama utabisha angalia filamu zetu kisha angalia za wenzetu kama wanaijeria utaelewa.
vi/ Mtu wa simulizi, aliishia darasa la saba, hivi unafikiri uwezo wake wa kufikiri, na uelewa wa mambo ataandika script ipi yenye kufanya kizazi cha sasa kukubali kisa chake

Shida kubwa ya Wasanii wa Bongo Movie ni elimu ni ndogo sana kwa wengi wao, wengi ni Slow Learner, wachache sana wanauwezo mkubwa wa kiakili, kufikiri na kuchambua mambo. Wengi wao ni bora liende nao wawemo.

Ukitaka kujua kuwa Wasanii wetu wengi wao ni Vilaza basi angalia Role Model wao waliopo ughaibuni kama Marekani, bado ni wale wale waliokimbia shule, watu wenye Skendo, wavaa uchi, watumiaji wa madawa ya kulevya, na wahuni walioshindikana.

Bongo Movie ikataka iinuke iache kuchukua Vilaza, slow Learner watu waliokimbia shule ambao kimsingi lazima wawe na akili finyu na kazi zao lazima ziwe duni.

Waigizaji wengi wa Nigeria, Ghana, South Afrika wana elimu Degree moja kuendelea, yaani ambao hawajasoma ni wachache sana ukilinganisha na wenye shahada. Ndio maana wanajua kile wafanyacho. Embu angalia filamu na tamthilia za Kikorea ambazo kwa sasa zinateka soko hapa nchini, waigizaji karibu wote wa Kikorea ni Wasomi wa elimu ya juu kabisa kuanzia Degree tena nyingine ni zile za moto. Njoo kwa Wahindi, wafilipino, na kule Amerika ya kusini, waigizaji karibu wote ni wasome wa elimu ya juu kabisa.

Mtu mwenye elimu ya uhakika sio ile elimu ya kuunga unga kwenye vyuo visivyoeleweka hawezi kutoa kazi mbovu.

Naipongeza serikali kwa kuanzisha michepuo mipya itakayoendana na mambo ya sanaa na Lugha ili kufufua Tasnia ya Filamu hapa nchini.

Mtu kaishia Darasa la saba au kidato cha nne, atajuaje na kuigizaje mambo ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi yaani ataanzia wapi?
Mtu madarasa hayamtoshi, ataweza kuigiza filamu za kisiasa, ugaidi, na masuala ya demokrasia? Atawezaje ikiwa hajui hata historia ya hiyo demokrasia yenyewe zaidi ya maneno ya mtaani na vijiweni.
Mtu kaishia kidato cha nne atawezaje kufikiria kuandaa scripts ya mambo ya Mpango wa dunia wa milleniam, atawezaje kuigiza Umuhimu wa vyama vingi vya siasa ndani ya nchi?
Mtu kaishia kidato cha nne kwa kulazimishwa, atawezaje kuigiza filamu ya masuala ya sheria na haki za binadamu, hajui hata katiba ya nchi yake, mtu kama huyo huoni ni jipu?

Mtu kaishia kidato cha nne, atawezaje kuandaa filamu ya athari ya udikteta na ukosefu wa uhuru wa kujieleza ndani ya jamii,lini atawaza hayo, yeye kama sio kuwaza mapenzi tuu muda wote?

Mtu kaishia darasa la saba au kidato cha nne, atawezaje kufikiri hata kuigiza filamu inayopromoti utalii wa nchi yetu, utashangaa licha ya nchi yetu kuwa na Mbuga na vivutio vingi lakini tangu tupate uhuru hakuna filamu ya wanyama iliyochezwa na wabongo, utashangaa. Ndio shida ya vilaza hiyo. Wenyewe watakuambia uchumi mgumu.

Mtu anaelimu ya kuunga unga, atawezaje kuigiza inayozungumzia masuala ya fani za kitaalamu kama vile Ualimu wenyewe sio ule wa kuigiza kama wanaoigiza watoto kibaba baba na kimama mama. Au udaktari, au sheria, au injinia, utawezaje igiza kitu hukijui na huna akili ya ku-master kwa upesi.

Mimi nawashauri wenye nafasi na wanaotaka Bongo Movie iamke basi wafanye haya;
Wasajili watu wenye vipaji Fresh from the School, waende shule zenye vipaji huko, Vyuo vikuu vinavyotambulika wachukue watu huko.
Wasaniii wawekewe sheria kuwa ili uwe mwigizaji basi yakubidi uwe na elimu isiyochini ya Diploma. Na uwe umefaulu vizuri kidato cha nne

Tasnia inapoongozwa na Kilaza kamwe haiwezi kuzaa matunda chanya kwenye jamii.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Sumbawanga

Umesema vizuri sana

Niliwahi kufikiria kuwekeza huko Bongo Movies ili nimtafute director na mwandishi mzuri anayejua theater arts sawasawa kusudi awe anachagua waigizaji na kupanga maudhi siyo hawa wanaodhani movie ni urembo na kuigiza raha raha tu. Nilitaka tuanze kwa kuwa tunatengeneza movie zinazohusu uharifu na usimamizi wa sheria: kuwe na waharifu wazuri, polisi wazuri, wapelelezi wazuri, waendesha mashtaka wazuri, mawakili wazuri na mahakimu wazuri katika setting ambayo mtazamaji atadhani ni kweli kabisa. Nilipata miguu ya baridi baada ya kutoelewana na mtu ambaye nilitegemea awe msimamizi wa mradi huo.

Ni wazi kuwa Bongo movies hamna kitu kabisa ingawa Kanumba (RIP) alikuwa anajitahidi kidogo lakini naye alikuwa hajaiva sawasawa; movie zao ni za mambo ya kitoto, hazibuniwi vizuri na zina ujinga mwingi sana. Kuna muvi niliangalia zamani kidogo eti jambazi anavamia nyumba ya kifahari lakini alipofika mlangoni akuvua viatu kwanza kabla ya kuingia ndani. Huwezi kutengeneza movi nzuri kwa wiki moja tu!!
 
Bongo movie noma eti movie ya maisha ya hayati rais Magufuli tayari imekamilika. Kwa Maisha ya rais Magufuli eti movie yake ikamilike ndani ya wiki tatu hawa bongo movie hamna kitu hata kama hiyo movie sijaiona ila itakuwa utopolo tu.
 
Labda useme ujuzi ndo watakuelewa ukisema Elimu what comes in their mind is bachelor degrees. Unaweza tu kujifunza mambo ya film kupitia platform mbali mbali kuongeza ujuzi, tasnia ya uigizaji inahitaji akili zisizo za kawaida

Mkuu yeye huyo mleta mada ndie anaemaanisha Bachelor Degrees, mimi nimezungumza wazi kuwa taaluma ni muhimu na taaluma unajifunza kwa njia nyingi tu, nilichopinga mimi ni hii moja kwa moja kuamini Bachelor degree kitu ambacho hakina uhalisia kwenye masuala ya kuigiza. Yeye yupo kutolea povu watu walioishia darasa la 10.
 
NI HITIMISHE KWA KUSEMA,
WAIGIZAJI VILAZA WANA ANDAA MUVI KWA AJILI YA VILAZA WENZAO. NI VIGUMU WASOMI KUINGIA HUKO KWANI WATALAZIMISHWA KUSHABIKIA CHAMA CHAO

View attachment 1746116

Kwahili nikae kimya tu, ila hila tatizo sio kwa hawa tu hata wale Bongo fleva ambao mnawasifia nao ndio haya haya
 
Nimefanya kazi za documentary kama msimamizi na pia za matangazo, naelewa nini nachozungumza, nilitengeneza script ya tangazo ambalo lilionekana bora kuliko waliosomea.
Point yako haina msingi hata kama sijawahi kutengeneza movie mwisho wa siku ukitengeneza unaotegemea kununua kazi zako sio walio na ujuzi wa movie industry lakini kitakachovutia kazi zako kununiliwa ni ubora wa kazi yako si kinginecho.
Kwa jinsi ulivyonijibu ndivyo inavyoonyesha upeo wenu ulivyo.
Nataka nikupe somo wewe na wenzako, Hollywood kuna watu wanaitwa criticism ambao movie ikitoka wao wanaangalia kabla haijaenda sokoni, wengi ni waandishi wa magazeti au watangazaji wa tv maoni yao ndio yanaiganya movie iuzwe au ikose soko na kazi yao kubwa ni kukosoa lakini nyinyi mkiambiwa ukweli mnabaki kubisha ndio maana movie zenu za hapahapa hazina mbele wala.nyuma.

Critics daima hawajawahi kuamua hatma ya biashara za filamu, nayaelewa vizuri haya mambo.
 
Kwa jinsi wanavyoshupaza shingo wakikosolewa ndivyo wanavyozidi kwenda kuharibu, yaani wanaambiwa kuhusu story zao kukosa ubunifu na msisimko wanasema bajeti, Wanaambiwa waoneshe uhalisia wa hayo maigizo yao wanasema bajeti, wanaambiwa watafute location nzuri hapa hapa Tanzania tuna vivutio teleeee wanasema bajeti,

Basi watupishe wenye bajeti zetu tufanye kazi napo wanasema Bajeti, hehehehehe kazi kweli kweli.

Kwani umekatazwa si ukatengeneze?
 
Wewe ndio huelewi, filamu zenu mnakurupuka hamfanyi tafiti zozote, hamjui kuhusu masoko ya sinema zenu ndio maana mnatoa sababu zisizo na kichwa wala miguu

Kwanza mkuu mimi sihusiki na masuala ya Movie industry, na wala sio mshabiki wao. Naongea hapa ninachokielewa tu.

Kuendelea kuwashutumu waigizaji wakati hao waigizaji hawazidi hata asilimia 20% ya tatizo ni kuwaonea tu. Tatizo la bongo movie ni pana sana.
 
Critics daima hawajawahi kuamua hatma ya biashara za filamu, nayaelewa vizuri haya mambo.

Hawafahamu hayo mambo mkuu. Kuna movies zina very small ratings rotten tomatoes na metacritic lakini zimefanya vizuri kwenye soko na box office.

Hawafahamu haya mambo mkuu
 
Back
Top Bottom