Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

movie zetu kuna ule utamaduni sijui nani kawakalilisha, watu wapo kwenye mazungumzo alafu kuna mdundo unapiga yan adi kero ata watu wenyewe hauwasikii unasikia beat tu.. mbona movie za ulaya zipo silence watu wanapoongea yaan unayasikia maneno murua kabisa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119]
 
Kuna siku nliona Daktari wa bongo movie akisema "presha iko sawa, maleria pia iko sawa...." Nikatoka nje make nlikua kwa watu ningekua kwangu ningezima tv.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].. Dahh
 
Kuna siku nliona Daktari wa bongo movie akisema "presha iko sawa, maleria pia iko sawa...." Nikatoka nje make nlikua kwa watu ningekua kwangu ningezima tv.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] hhh
 
BONGO MOVIE WENGI NI VILAZA, SIO AJABU WAMEILAZA SANAA YA UIGIZAJI.

Anaandika, Robert Heriel.

Hapana shaka sanaa ya Uigizaji kwa sasa imelala Usingizi wa Pono, imelala fofofo na waigizaji wake wanakoroma. Wapo kwenye ndoto za majinamizi wabaya wanaowakimbiza kwenye mitaro huko usingizini. Tangu kifo cha Marehemu Kanumba miaka zaidi ya tisa iliyopita Tasnia ya Bongo Movie imelala fofofo.

Hakuna Tasnia inayoongozwa na Vilaza isilale, sijawahi kuona popote pale duniani. Bongo Movie imejaa wasanii vilaza kwa kiwango kikubwa sana, watu waliokimbia shule ndio wamekimbilia huko kwenye tasnia ya filamu. Embu fikiria mtu amekimbia shule kwa kushindwa somo hata la kiswahili unafikiri atatuambia nini kwenye suala la kuelimisha jamii kupitia fani ya uigizaji.

Kilaza ni kilaza tuu, uwezo wake wa kufikiri ni mdogo alafu anakuwa Director wa filamu, unafikiri filamu yake itakuwaje kama sio Utopolo. Kilaza hufikiri mambo chini ya kiwango, ukiwaangalia wasanii wengi wa bongo movie wakiigiza kwanza hawawezi kuuvaa uhusika, wanachojua ni kutoa macho, kukenua, kubinua makalio, kuvaa nguo fupi, wakati kwa upande wa wasanii wa kiume wanachjua ni kupaka piko sijui waves nywele zao, kutoboa masikio au kubandika stiker masikioni, na kulamba lamba midomo kama sio kusuka nywele. Kwa mambo haya wamefuzu kwani mambo haya hufanywa kwa sehemu kubwa na vilaza, kwani hata mtu asiye msanii anaweza kufanya mambo hayo. Vilaza hufanya mambo ambayo mtu yeyote anaweza kufanya.

i/ Muongoza Filamu alifeli shule, akaunga unga wee akapata cheti, huyo akajiingiza kwenye Tasnia ya Filamu, haya embu niambie atatupa kipi cha maana hapo?
ii/ Mtayarishaji alifeli shule, akaunga unga wee, embu niambie ataleta jambo gani katika ulimwengu huu wa elimu, sayansi na teknolojia?
iii/Mchukua Kamera alipata sifuri au four ya mwisho kabisa, hivi unategemea atakuwa na ubunifu gani kwenye masuala ya kurekodi picha na video na kamera?
iv/ Mtia sauti, aliishia kidato cha nne, embu niambie anauelewa gani na mambo ya sauti, muziki na ala? Sio ajabu sauti nyingi zinazoingizwa kwenye movies nyingi ni zile zile haziendani na uhalisia,
v/ Mtu wa Makeup aliishia darasa la pili, hivi anajua nini kuhusu urembo? Kama utabisha angalia filamu zetu kisha angalia za wenzetu kama wanaijeria utaelewa.
vi/ Mtu wa simulizi, aliishia darasa la saba, hivi unafikiri uwezo wake wa kufikiri, na uelewa wa mambo ataandika script ipi yenye kufanya kizazi cha sasa kukubali kisa chake

Shida kubwa ya Wasanii wa Bongo Movie ni elimu ni ndogo sana kwa wengi wao, wengi ni Slow Learner, wachache sana wanauwezo mkubwa wa kiakili, kufikiri na kuchambua mambo. Wengi wao ni bora liende nao wawemo.

Ukitaka kujua kuwa Wasanii wetu wengi wao ni Vilaza basi angalia Role Model wao waliopo ughaibuni kama Marekani, bado ni wale wale waliokimbia shule, watu wenye Skendo, wavaa uchi, watumiaji wa madawa ya kulevya, na wahuni walioshindikana.

Bongo Movie ikataka iinuke iache kuchukua Vilaza, slow Learner watu waliokimbia shule ambao kimsingi lazima wawe na akili finyu na kazi zao lazima ziwe duni.

Waigizaji wengi wa Nigeria, Ghana, South Afrika wana elimu Degree moja kuendelea, yaani ambao hawajasoma ni wachache sana ukilinganisha na wenye shahada. Ndio maana wanajua kile wafanyacho. Embu angalia filamu na tamthilia za Kikorea ambazo kwa sasa zinateka soko hapa nchini, waigizaji karibu wote wa Kikorea ni Wasomi wa elimu ya juu kabisa kuanzia Degree tena nyingine ni zile za moto. Njoo kwa Wahindi, wafilipino, na kule Amerika ya kusini, waigizaji karibu wote ni wasome wa elimu ya juu kabisa.

Mtu mwenye elimu ya uhakika sio ile elimu ya kuunga unga kwenye vyuo visivyoeleweka hawezi kutoa kazi mbovu.

Naipongeza serikali kwa kuanzisha michepuo mipya itakayoendana na mambo ya sanaa na Lugha ili kufufua Tasnia ya Filamu hapa nchini.

Mtu kaishia Darasa la saba au kidato cha nne, atajuaje na kuigizaje mambo ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi yaani ataanzia wapi?
Mtu madarasa hayamtoshi, ataweza kuigiza filamu za kisiasa, ugaidi, na masuala ya demokrasia? Atawezaje ikiwa hajui hata historia ya hiyo demokrasia yenyewe zaidi ya maneno ya mtaani na vijiweni.
Mtu kaishia kidato cha nne atawezaje kufikiria kuandaa scripts ya mambo ya Mpango wa dunia wa milleniam, atawezaje kuigiza Umuhimu wa vyama vingi vya siasa ndani ya nchi?
Mtu kaishia kidato cha nne kwa kulazimishwa, atawezaje kuigiza filamu ya masuala ya sheria na haki za binadamu, hajui hata katiba ya nchi yake, mtu kama huyo huoni ni jipu?

Mtu kaishia kidato cha nne, atawezaje kuandaa filamu ya athari ya udikteta na ukosefu wa uhuru wa kujieleza ndani ya jamii,lini atawaza hayo, yeye kama sio kuwaza mapenzi tuu muda wote?

Mtu kaishia darasa la saba au kidato cha nne, atawezaje kufikiri hata kuigiza filamu inayopromoti utalii wa nchi yetu, utashangaa licha ya nchi yetu kuwa na Mbuga na vivutio vingi lakini tangu tupate uhuru hakuna filamu ya wanyama iliyochezwa na wabongo, utashangaa. Ndio shida ya vilaza hiyo. Wenyewe watakuambia uchumi mgumu.

Mtu anaelimu ya kuunga unga, atawezaje kuigiza inayozungumzia masuala ya fani za kitaalamu kama vile Ualimu wenyewe sio ule wa kuigiza kama wanaoigiza watoto kibaba baba na kimama mama. Au udaktari, au sheria, au injinia, utawezaje igiza kitu hukijui na huna akili ya ku-master kwa upesi.

Mimi nawashauri wenye nafasi na wanaotaka Bongo Movie iamke basi wafanye haya;
Wasajili watu wenye vipaji Fresh from the School, waende shule zenye vipaji huko, Vyuo vikuu vinavyotambulika wachukue watu huko.
Wasaniii wawekewe sheria kuwa ili uwe mwigizaji basi yakubidi uwe na elimu isiyochini ya Diploma. Na uwe umefaulu vizuri kidato cha nne

Tasnia inapoongozwa na Kilaza kamwe haiwezi kuzaa matunda chanya kwenye jamii.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Sumbawanga
Mkuu umetisha sana, tena SANA ..
Point tupu toka mwanzo mpaka mwisho..
Btw naweza nkasema sio muangaliaji sana wa hizi movies unless sina usingizi au bored sna,
Best movies nlizozikubali ni ile girlfriend ya kina t.i.d,
Kuna action movie moja hivi mpaka wanapgana juu ya train (jina sjui) na nyingine ni action pia villain ni castrol Dickson mtangazji km sjakosea,humo ndani yumo uwoya na jeshi la police liliplay part nzuri.
Wanaojua majina ya hizi movies ntashukuru mkitaja
 
Jambazi likiwa linanyata utasikia ngingiiiiiiiii ngingiiiiiii..... Mtu Yuko beach anawaza nusu saa nzima , kichekesho kwenye sauti aisee inabidi remote yako iwe standby ....
Bongo movie Mungu anawaona aisee
 
Pamoja na kwamba nakubaliana na mleta UZI kwa sehemu but mengine kayakuza sana. Nitajie elimu za kina Bruce Lee, Chuck Norris, Anold Schwezneeger, Bill Blanks nk. Weka elimu zao wakati wakiwa wanatingisha sana soko la filamu those years; ukimaliza njo kwa wana music almost wote duniani kuanzia kwa kina Michael Jackson, Steve Wonder hadi hawa wa sasa. Binafsi bado natazama sana filamu zetu, ni shabiki wa kina JB, Rich Mtambalike, kina Nandy (utasema Nandy ni msomi) yule mama wa kingoni ambaye kacheza kama mama mkwe kwa igizo la HUBA kule DSTV, Bi Sikitu nk

Sijaona makosa makubwa kwa kina JB, Richie nk, yapo makosa ya kawaida sana ambayo hata hizo filamu za hao uliowataja hua yapo. Tasnia yetu Bongo sidhani kama shida ni elimu, waigizaji wanaweza wasiwe na shule kubwa sana but waongozaji labda script editors hao yes shule inatakiwa. Nitajie ubora wa Kanumba enzi hizo halafu nitajie udhaif wa kina JB leo; industry ya filamu bado ni changa as i said, kadiri siku zinavyo kwenda unaona kabisa wanavyo improve, to me wasani wanakua na sanaa yao inakua sana.
 
Mkuu naomba unitajie jina la hiyo muvi ambayo koplo anampigia saluti koplo au ni mwigizaji gani aliigiza kwa hiyo movie ili niitafute.

Tusije tukawa tunaongelea vitu ambavyo havipo ili tu tufurahishe umma
Labda misukosuko ya jayplus
 
Nafikiri hoja yako sijui kama ina maana la zaidi ni post ya udhalilishaji. Kuna vitu ni talent. Kuwa akili ya kujibu physics hakukupi talent ya kuwa muigizaji nzuri. Nafikiri unashindwa kuheshimu kwamba uigizaji unahitaji kipaji na sio kila mtu.
Najuhudi mkuu mf ukiangalia series ya KELELE iliyoandaliwa na Hayati Ruge ni dhahiri jamaa angepewa saport hakika angeiinua Bongo mvie
 
Mkuu ni kwamba hujui au free market works? Ushasema walibanwa kodi sasa ulitegemea wangeendelea kufanya biashara?

Okay fine walikuja na mechanism gani kuhakikisha the movie industry inapata distributor mwengine?

Serikali yenu imeshindwa hata kuita kampuni kama SILVER BIRD ya nigeria itengeneze sinemas watu wauze movie? JB angepata faida si ndo angeendelea kutengeneza movie nzuri zaidi?.

Sasa JB atatengenezaje movie nzuri kama hana hata sehemu ya kuuzia movie zake
Pia kuna kampuni ilikuwepo ilikua inaitwa Wananchi video productions store ambayo ilikuwa inasambaza film za Jumanne kihangala na Mussa Banzi nayo ilisitisha usambazaji kipindi cha kikwete na 7bu ilikua ni uigizaji mmbovu wa wasanii
 
Kizuri hujiuza ndo maana wakina Vandame wanaweza kuwa hawajui hata kuna nchi inaitwa TANZANIA ila huku ana ma role model kibao ukiacha mashabiki.TUACHENI VISINGIZIO SASA WE LI MTU(JENGUA)LINAIGIZA LINAPENDWA KICHIZI MPAKA DEMU ANAJIUA UKIANGALIA SURA YA JENGUA KAMA PALAMAGAMBA KABUDI JUMLISHA NA MIJICHO YAO we unaona watu wa TASNIA YA BONGO MOVIES WAPO SERIOUS
Mkuu mtake radhi mzee Jengua ni marehemu kwasasa
 
Pamoja na kwamba nakubaliana na mleta UZI kwa sehemu but mengine kayakuza sana. Nitajie elimu za kina Bruce Lee, Chuck Norris, Anold Schwezneeger, Bill Blanks nk. Weka elimu zao wakati wakiwa wanatingisha sana soko la filamu those years; ukimaliza njo kwa wana music almost wote duniani kuanzia kwa kina Michael Jackson, Steve Wonder hadi hawa wa sasa. Binafsi bado natazama sana filamu zetu, ni shabiki wa kina JB, Rich Mtambalike, kina Nandy (utasema Nandy ni msomi) yule mama wa kingoni ambaye kacheza kama mama mkwe kwa igizo la HUBA kule DSTV, Bi Sikitu nk

Sijaona makosa makubwa kwa kina JB, Richie nk, yapo makosa ya kawaida sana ambayo hata hizo filamu za hao uliowataja hua yapo. Tasnia yetu Bongo sidhani kama shida ni elimu, waigizaji wanaweza wasiwe na shule kubwa sana but waongozaji labda script editors hao yes shule inatakiwa. Nitajie ubora wa Kanumba enzi hizo halafu nitajie udhaif wa kina JB leo; industry ya filamu bado ni changa as i said, kadiri siku zinavyo kwenda unaona kabisa wanavyo improve, to me wasani wanakua na sanaa yao inakua sana.

Unataja watu waliowika enzi za giza dunia ikiwa gizani,

waambie sasa hivi waigize Movie uone kama hutaona vituko.

Hata hawa Bongo Movie wangeigiza hizi movie miaka ya 90 huko zingeonekana ni nzuri kutokana na akili za wakati huo.

Huna shule itaigiza nini kama sio utumbo tuu
 
Hapo ndipo kwenye point wakuu, matatizo ya filamu za bongo yapo kwenye utengenezaji, Directors na crew wao. kuwashutumu ma actors ni kutafuta kichaka cha kutoa matusi tu ila wao ni sehemu ndogo tu ya tatizo.
Mleta mada alikuja na hoja za kuwatolea povu ma actors kuwa hawana elimu hawajafika chou hapo ndipo nilipoanza kumpinga mimi.
Wewe umeongea bonge la POINT kweli ma director ndio kiini cha UBORA au UTOPOLO wa movies
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kaka tuhurumie mbavu zetu ah ah ah ah[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Tuwakele kidogo ili wakae kikao wajifikilie tena
 
Pamoja na kwamba nakubaliana na mleta UZI kwa sehemu but mengine kayakuza sana. Nitajie elimu za kina Bruce Lee, Chuck Norris, Anold Schwezneeger, Bill Blanks nk. Weka elimu zao wakati wakiwa wanatingisha sana soko la filamu those years; ukimaliza njo kwa wana music almost wote duniani kuanzia kwa kina Michael Jackson, Steve Wonder hadi hawa wa sasa. Binafsi bado natazama sana filamu zetu, ni shabiki wa kina JB, Rich Mtambalike, kina Nandy (utasema Nandy ni msomi) yule mama wa kingoni ambaye kacheza kama mama mkwe kwa igizo la HUBA kule DSTV, Bi Sikitu nk

Sijaona makosa makubwa kwa kina JB, Richie nk, yapo makosa ya kawaida sana ambayo hata hizo filamu za hao uliowataja hua yapo. Tasnia yetu Bongo sidhani kama shida ni elimu, waigizaji wanaweza wasiwe na shule kubwa sana but waongozaji labda script editors hao yes shule inatakiwa. Nitajie ubora wa Kanumba enzi hizo halafu nitajie udhaif wa kina JB leo; industry ya filamu bado ni changa as i said, kadiri siku zinavyo kwenda unaona kabisa wanavyo improve, to me wasani wanakua na sanaa yao inakua sana.
William Wayne Blanks is an American fitness guru, martial artist, actor, and the creator of the Tae Bo exercise program. In 1981 won men's karate medal representing USA.

Carlos Ray "Chuck" Norris is an American martial artist, actor, film producer, and screenwriter. After serving in the United States Air Force, Norris won many martial arts championships and later founded his own discipline Chun Kuk Do. Norris is a black belt in Tang Soo Do, Brazilian jiu jitsu and judo.

Bruce Lee was introduced to the film industry by his father and appeared in several films as a child actor. His early martial arts experience included Wing Chun, tai chi, street fighting, and boxing, winning the Hong Kong schools boxing tournament; he also learnt cha-cha dancing, winning the Hong Kong cha-cha championship. Lee moved to the United States at the age of 18 to receive his higher education at the University of Washington in Seattle; it was during this time that he began teaching martial arts, later drawing significant attention at the 1964 Long Beach International Karate Championships.

Schwarzenegger served in the Austrian Army in 1965 to fulfill the one year of service required at the time of all 18-year-old Austrian males. During his army service, he won the Junior Mr. Europe contest. He went AWOL during basic training so he could take part in the competition and then spent a week in military prison.

Nafkiri umeona vigezo vyao hao wote, wote wametoka mbali, wana experience kibao tangu wakiwa watoto ndio maana hata movie zenyewe walizicheza kama ukweli vile, walijua walichokuwa wanakifanya na pia kupitia mentors wao wakaendelea kufaulu.
Haya mambo ya kuokotana vijiweni ati msela ashakua actor/actress wakati hata hakuna chembe ya experience ako nayo be it academically or life ones ni utopolo unaoangusha filamu za Bongo na nchi zingine tu😂
✌️
 
William Wayne Blanks is an American fitness guru, martial artist, actor, and the creator of the Tae Bo exercise program. In 1981 won men's karate medal representing USA.

Carlos Ray "Chuck" Norris is an American martial artist, actor, film producer, and screenwriter. After serving in the United States Air Force, Norris won many martial arts championships and later founded his own discipline Chun Kuk Do. Norris is a black belt in Tang Soo Do, Brazilian jiu jitsu and judo.

Bruce Lee was introduced to the film industry by his father and appeared in several films as a child actor. His early martial arts experience included Wing Chun, tai chi, street fighting, and boxing, winning the Hong Kong schools boxing tournament; he also learnt cha-cha dancing, winning the Hong Kong cha-cha championship. Lee moved to the United States at the age of 18 to receive his higher education at the University of Washington in Seattle;[5] it was during this time that he began teaching martial arts, later drawing significant attention at the 1964 Long Beach International Karate Championships.

Schwarzenegger served in the Austrian Army in 1965 to fulfill the one year of service required at the time of all 18-year-old Austrian males. During his army service, he won the Junior Mr. Europe contest. He went AWOL during basic training so he could take part in the competition and then spent a week in military prison.

Nafkiri umeona vigezo vyao hao wote, wote wametoka mbali, wana experience kibao tangu wakiwa watoto ndio maana hata movie zenyewe wanazicheza kama ukweli vile, wanajua wanachokifanya na pia kupitia mentors wao wakaendelea kufaulu.
Haya mambo ya kuokotana vijiweni ati msela ashakua actor/actress wakati hata hakuna chembe ya experience ako nayo be it academically or life ones ni utopolo unaoangusha filamu za Bongo.
✌️

Huyo hujui anachokitetea Mkuu

Ili uigize pasipo elimu yakupasa uigize movie aina za kina Bushman yaani vituko vituko, lakini movie za akili hutoweza asilani.

Hata hivyo movie zenye maudhui ya kati ya masuala ya kawaida ya kijamii zinaweza igizwa hata na watu wenye elimu ya kawaida kama vile TAMTHILIA YA SIRI YA MTU. lakini Director wake ni wamoto kielimu Mr Jordan
 
Sidhani kama elimu ya waigizaji ndo tatizo maana kile ni kipaji. Tatizo ni directors na watunga hadithi. Unless mwigizaji ndo awe director.
Tatizo mnadhani elimu ni degrees au Diploma, Elimu kwa maana ya kujifunza vitu vipya, kurekebisha ya zamani, ndio maana kuna shule za mambo ya uigizaji, kipaji bila kuongezea udambwi dambwi ni kazi bure, kila siku utatoa kitu kile kile na hadhira itakuchoka,
 
Wewe umeongea bonge la POINT kweli ma director ndio kiini cha UBORA au UTOPOLO wa movies

Kwa ma directors wa Bongo movies, hata umtoe Robert Di Nero Hollywood ukimuingiza ndani ya bongo movie na pia utamuona utopolo tu
 
Tatizo mnadhani elimu ni degrees au Diploma, Elimu kwa maana ya kujifunza vitu vipya, kurekebisha ya zamani, ndio maana kuna shule za mambo ya uigizaji, kipaji bila kuongezea udambwi dambwi ni kazi bure, kila siku utatoa kitu kile kile na hadhira itakuchoka,
Anayeigiza sasa hapo kosa lake lipi? Si director ndo anajua nani anafaa hapa nani hafai? Kama muigizaji hana udambwi dambwi si ni kazi ya director kutokumpa nafasi? We sema mifilamu yenu muigizaji huyo huyo director.
 
In his early days, Lawrence did comedy shows in the Washington, D.C., area and supported himself through odd jobs. Comedian Ritch Snyder saw his act and suggested Lawrence make connections in New York.[6] Lawrence ended up moving to New York City and found his way to the legendary The Improv. Shortly after appearing at The Improv, Lawrence won a performance spot on Star Search.[1] He did well on the show and made it to the final round, but did not win. However, executives at Columbia Pictures Television saw Martin's performance and offered him the role of Maurice Warfield

Katika siku zake za mwanzo, Lawrence alifanya maonesho ya ucheshi katika eneo la Washington, D.C. na akajisaidia kupitia kazi ndogondogo za mitaani. Mchekeshaji Ritch Snyder aliona kipaji chake na akapendekeza Lawrence aunganishwe New York. [6] Lawrence aliishia kuhamia New York City na akapata shavu kwenye kazi za The Improv. Muda mfupi baada ya kuonekana katika The Improv, Lawrence alishinda nafasi ya ushiriki kwenye Star Search. [1] Alifanya vizuri kwenye onesho hilo na kufika hadi raundi ya mwisho, ingawa hakushinda. Wakuu wa Columbia Pictures Television waliona uwezo wa Martin na wakampa nafasi ya kucheza kama Maurice Warfield.

Nimejaribu kuweka hayo maelezo ya mmoja wa Waigizaji wa Hollywood, Martin Lawrence waliotokea mtaani tu...ambao kama Eddy Murphy na wengine kipaji kilitangulia.

Nikisoma bandiko la Mleta uzi ninaona zaidi ni kama ameamua kuzimwaga hasira zake kwa hawa Wana tasnia ya Filamu labda kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe.

Ni kweli inahitajika Elimu ili kufanya jambo lolote kwa ufanisi lakini sio kila Mwenye Elimu hufanya mambo kwa ufanisi au aliyekosa Elimu anaharibu kila anachokifanya.

Na tunapoongelea Filamu tukumbuke kuwa hii ni zao la kazi ya TIMU....na timu inahusisha Watu wa aina tofauti, hivyo wapo wanaohitaji Elimu ya kina,wapo wanaohitaji Elimu kiasi, wapo wanaohitaji kipaji (talent) zaidi...haswa Waigizaji.

Ni kweli unaweza kumfundisha Mtu kuigiza lakini utapata matokeo mazuri zaidi iwapo utamfundisha Mtu ambaye tayari ana kipaji cha kuigiza.

Changamoto tunayokumbana nayo hapa kwetu ni namna wanavyopatikana hao Wenye Vipaji vya Uigizaji. Hapa kwetu ukilinganisha na Nchi nyingine haswa zilizoendelea Mtu Kujihisi ana uwezo wa kuigiza na Mfumo kumkubali kuwa ana uwezo huo ni tofauti na huku kwetu ambapo wengi huingia huko kama tu kujaribu bahati zao na kwa isivyo bahati mfumo dhaifu uliopo unawapokea tu vivyo hivyo.

Kwa upande mwingine ukiangalia hata wanaosimamia , ambao labda walitarajiwa kutoa msaada (support) nao ni kama wanafuata mkumbo tu....ndio maana ukiangalia kwa makini utaona kila wanapoongelea kuinua tasnia basi nguvu zote na akilia wanaelekeza kwa Wasanii moja kwa moja....na kwa kuwa Wasanii nao ni "Wasanii" basi wanawapokea na mwisho wa siku hakuna matokeo yoyote chanya yanayopatikana.

Wanachopaswa kufahamu ni kuwa Msanii/Muigizaji ni sehemu tu ya timu, Filamu nzuri ni matokeo ya Screenplay nzuri, Upigaji picha mzuri na Uigizaji mzuri...mengine ni ziada lakini kama yanapatikana ni sawa.

Na kama kweli wanataka kukuza tasnia basi ni lazima nguvu iwekwe kwa Watayarishaji na sio Wasanii..kama ni kuwasaisia Wasanii basi wao ni kuwatafutia kozi za kuboresha uigizaji wao...Filamu bora zitatokana na Wazalishaji (Producers) Imara na wenye weledi...chini ya Mwamvuli wa Wazalishaji tutapata Waelekezi (Directors), Wapiga Picha(Cinematographer) n.k....Wasanii huajiriwa tu kwenye Filamu....sasa hapa kwetu ukisikia mikakati ya kuinua tasnia watawatafuta kina JB, Ray n.k....na kwa kiasi kikubwa huwa ni mikakati ya kisiasa zaidi kuliko kiuhalisia.

Nchi ikiwa na Vipaji vya kutosha swala la Elimu rasmi ya darasani sio tatizo kubwa ki hivyo kiasi kukwamisha mambo...ingawa tofauti ya ajabu niionayo ni kwa Mbongo akikwambia hajaenda shule ni tofauti na Chris Rock akikwambia hajaenda shule..Chris Rock au Dave Chapelle akisimama jukwaani kuongea hata unahisi labda angeenda hizo shule kivile angepoteza uwezo ule alionao.

Ushauri ninaodhani unaweza kubadilisha mtazamo wa tasnia ni kupokea damu changa zenye mawazo tofauti, damu changa zenye walau abcd za haswa nini maana ya kuwa Muigizaji...Damu changa waingie wakijua umuhimu na maana ya Screenplay/Script kwenye Filamu. Wakongwe tulionao wengi wanategemea uigizaji wa kuongea/kubwabwaja tu kama silaha yao kuu ya kuigiza ambamo ndani yake ndimo huficha udhaifu wao wa kuigiza...tutafute damu changa wenye vipaji waheshimu na wajue nidhamu ya Screenplay/Script..Filamu ni sanaa ya maonesho na sio ya kuelezea kwa maongezi tu.
 
Back
Top Bottom