Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

In his early days, Lawrence did comedy shows in the Washington, D.C., area and supported himself through odd jobs. Comedian Ritch Snyder saw his act and suggested Lawrence make connections in New York.[6] Lawrence ended up moving to New York City and found his way to the legendary The Improv. Shortly after appearing at The Improv, Lawrence won a performance spot on Star Search.[1] He did well on the show and made it to the final round, but did not win. However, executives at Columbia Pictures Television saw Martin's performance and offered him the role of Maurice Warfield

Katika siku zake za mwanzo, Lawrence alifanya maonyesho ya ucheshi katika eneo la Washington, D.C. na akajisaidia kupitia kazi isiyo ya kawaida. Mchekeshaji Ritch Snyder aliona kitendo chake na akapendekeza Lawrence aunganishe New York. [6] Lawrence aliishia kuhamia New York City na akapata njia ya hadithi ya The Improv. Muda mfupi baada ya kuonekana katika The Improv, Lawrence alishinda nafasi ya utendaji kwenye Star Search. [1] Alifanya vizuri kwenye onyesho na akafanya raundi ya mwisho, lakini hakushinda. Walakini, watendaji katika Televisheni ya Picha ya Columbia waliona utendaji wa Martin na wakampa jukumu la Maurice Warfield

Nimejaribu kuweka hayo maelezo ya mmoja wa Waigizaji wa Hollywood, Martin Lawrence waliotokea mtaani tu...ambao kama Eddy Murphy na wengine kipaji kilitangulia.

Nikisoma bandiko la Mleta uzi ninaona zaidi ni kama ameamua kuzimwaga hasira zake kwa hawa Wana tasnia ya Filamu labda kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe.

Ni kweli inahitajika Elimu ili kufanya jambo lolote kwa ufanisi lakini sio kila Mwenye Elimu hufanya mambo kwa ufanisi au aliyekosa Elimu anaharibu kila anachokifanya.

Na tunapoongelea Filamu tukumbuke kuwa hii ni zao la kazi ya TIMU....na timu inahusisha Watu wa aina tofauti, hivyo wapo wanaohitaji Elimu ya kina,wapo wanaohitaji Elimu kiasi, wapo wanaohitaji kipaji (talent) zaidi...haswa Waigizaji.

Ni kweli unaweza kumfundisha Mtu kuigiza lakini utapata matokeo mazuri zaidi iwapo utamfundisha Mtu ambaye tayari ana kipaji cha kuigiza.

Changamoto tunayokumbana nayo hapa kwetu ni namna wanavyopatikana hao Wenye Vipaji vya Uigizaji hapa kwetu ukilinganisha na Nchi nyingine haswa zilizoendelea....kwa Wenzetu Mtu Kujihisi ana uwezo wa kuigiza na Mfumo kumkubali kuwa ana uwezo huo ni tofauti na huku kwetu ambapo wengi huingia huko kama tu kujaribu bahati zao na kwa isivyo bahati mfumo dhaifu uliopo unawapokea tu vivyo hivyo.

Kwa upande mwingine ukiangalia hata wanaosimamia , ambao labda walitarajiwa kutoa msaada (support) nao ni kama wanafuata mkumbo tu....ndio maana ukiangalia kwa makini utaona kila wanapoongelea kuinua tasnia basi nguvu zote na akilia wanaelekeza kwa Wasanii....na kwa kuwa Wasanii nao ni "Wasanii" basi wanawapokea na mwisho wa siku hakuna matokeo yoyote chanya yanayopatikana.

Wanachopaswa kufahamu ni kuwa Msanii/Muigizaji ni sehemu tu ya timu, Filamu nzuri ni matokeo ya Screenplay nzuri, Upigaji picha mzuri na Uigizaji mzuri...mengine ni ziada lakini kama yanapatikana ni sawa.

Na kama kweli wanataka kukuza tasnia basi ni lazima nguvu iwekwe kwa Watayarishaji na sio Wasanii..kama ni kuwasaisia Wasanii basi wao ni kuwatafutia kozi za kuboresha uigizaji wao...Filamu bora zitatokana na Wazalishaji (Producers) Imara na wenye weledi...chini ya Mwamvuli wa Wazalishaji tutapata Waelekezi (Directors), Wapiga Picha(Cinematographer) n.k....Wasanii huajiriwa tu kwenye Filamu....sasa hapa kwetu ukisikia mikakati ya kuinua tasnia watawatafuta kina JB, Ray n.k....na kwa kiasi kikubwa huwa ni mikakati ya kisiasa zaidi kuliko kiuhalisia.

Nchi ikiwa na Vipaji vya kutosha swala la Elimu rasmi ya darasani sio tatizo kubwa ki hivyo kiasi kukwamisha mambo...ingawa tofauti ya ajabu niionayo ni kwa Mbongo akikwambia hajaenda shule ni tofauti na Chris Rock akikwambia hajaenda shule..Chris Rock au Dave Chapelle akisimama jukwaani kuongea hata unahisi labda angeenda hizo shule kivile angepoteza uwezo ule alionao.

Ushauri ninaodhani unaweza kubadilisha mtazamo wa tasnia ni kupokea damu changa zenye mawazo tofauti, damu changa zenye walau abcd za haswa nini maana ya kuwa Muigizaji...Damu changa waingie wakijua umuhimu na maana ya Screenplay/Script kwenye Filamu. Wakongwe tulionao wengi wanategemea uigizaji wa kuongea/kubwabwaja tu kama silaha yao kuu ya kuigiza ambamo ndani yake ndimo huficha udhaifu wao wa kuigiza...tutafute damu changa wenye vipaji waheshimu na wajue nidhamu ya Screenplay/Script..Filamu ni sanaa ya maonesho na sio ya kuelezea kwa maongezi tu.
Umemaliza kila kitu mkuu ikibidi fungua uzi wako wasanii wajue nini cha kufanya, pia kitu kingine kinachouwa tasni ni mashabi ama hadhila kwa ujumla kukalilishwa kuwa bila msanii fulani hiyo film haiwezi kuwa mzuri
 
BONGO MOVIE WENGI NI VILAZA, SIO AJABU WAMEILAZA SANAA YA UIGIZAJI.

Anaandika, Robert Heriel.

Hapana shaka sanaa ya Uigizaji kwa sasa imelala Usingizi wa Pono, imelala fofofo na waigizaji wake wanakoroma. Wapo kwenye ndoto za majinamizi wabaya wanaowakimbiza kwenye mitaro huko usingizini. Tangu kifo cha Marehemu Kanumba miaka zaidi ya tisa iliyopita Tasnia ya Bongo Movie imelala fofofo.

Hakuna Tasnia inayoongozwa na Vilaza isilale, sijawahi kuona popote pale duniani. Bongo Movie imejaa wasanii vilaza kwa kiwango kikubwa sana, watu waliokimbia shule ndio wamekimbilia huko kwenye tasnia ya filamu. Embu fikiria mtu amekimbia shule kwa kushindwa somo hata la kiswahili unafikiri atatuambia nini kwenye suala la kuelimisha jamii kupitia fani ya uigizaji.

Kilaza ni kilaza tuu, uwezo wake wa kufikiri ni mdogo alafu anakuwa Director wa filamu, unafikiri filamu yake itakuwaje kama sio Utopolo. Kilaza hufikiri mambo chini ya kiwango, ukiwaangalia wasanii wengi wa bongo movie wakiigiza kwanza hawawezi kuuvaa uhusika, wanachojua ni kutoa macho, kukenua, kubinua makalio, kuvaa nguo fupi, wakati kwa upande wa wasanii wa kiume wanachjua ni kupaka piko sijui waves nywele zao, kutoboa masikio au kubandika stiker masikioni, na kulamba lamba midomo kama sio kusuka nywele. Kwa mambo haya wamefuzu kwani mambo haya hufanywa kwa sehemu kubwa na vilaza, kwani hata mtu asiye msanii anaweza kufanya mambo hayo. Vilaza hufanya mambo ambayo mtu yeyote anaweza kufanya.

i/ Muongoza Filamu alifeli shule, akaunga unga wee akapata cheti, huyo akajiingiza kwenye Tasnia ya Filamu, haya embu niambie atatupa kipi cha maana hapo?
ii/ Mtayarishaji alifeli shule, akaunga unga wee, embu niambie ataleta jambo gani katika ulimwengu huu wa elimu, sayansi na teknolojia?
iii/Mchukua Kamera alipata sifuri au four ya mwisho kabisa, hivi unategemea atakuwa na ubunifu gani kwenye masuala ya kurekodi picha na video na kamera?
iv/ Mtia sauti, aliishia kidato cha nne, embu niambie anauelewa gani na mambo ya sauti, muziki na ala? Sio ajabu sauti nyingi zinazoingizwa kwenye movies nyingi ni zile zile haziendani na uhalisia,
v/ Mtu wa Makeup aliishia darasa la pili, hivi anajua nini kuhusu urembo? Kama utabisha angalia filamu zetu kisha angalia za wenzetu kama wanaijeria utaelewa.
vi/ Mtu wa simulizi, aliishia darasa la saba, hivi unafikiri uwezo wake wa kufikiri, na uelewa wa mambo ataandika script ipi yenye kufanya kizazi cha sasa kukubali kisa chake

Shida kubwa ya Wasanii wa Bongo Movie ni elimu ni ndogo sana kwa wengi wao, wengi ni Slow Learner, wachache sana wanauwezo mkubwa wa kiakili, kufikiri na kuchambua mambo. Wengi wao ni bora liende nao wawemo.

Ukitaka kujua kuwa Wasanii wetu wengi wao ni Vilaza basi angalia Role Model wao waliopo ughaibuni kama Marekani, bado ni wale wale waliokimbia shule, watu wenye Skendo, wavaa uchi, watumiaji wa madawa ya kulevya, na wahuni walioshindikana.

Bongo Movie ikataka iinuke iache kuchukua Vilaza, slow Learner watu waliokimbia shule ambao kimsingi lazima wawe na akili finyu na kazi zao lazima ziwe duni.

Waigizaji wengi wa Nigeria, Ghana, South Afrika wana elimu Degree moja kuendelea, yaani ambao hawajasoma ni wachache sana ukilinganisha na wenye shahada. Ndio maana wanajua kile wafanyacho. Embu angalia filamu na tamthilia za Kikorea ambazo kwa sasa zinateka soko hapa nchini, waigizaji karibu wote wa Kikorea ni Wasomi wa elimu ya juu kabisa kuanzia Degree tena nyingine ni zile za moto. Njoo kwa Wahindi, wafilipino, na kule Amerika ya kusini, waigizaji karibu wote ni wasome wa elimu ya juu kabisa.

Mtu mwenye elimu ya uhakika sio ile elimu ya kuunga unga kwenye vyuo visivyoeleweka hawezi kutoa kazi mbovu.

Naipongeza serikali kwa kuanzisha michepuo mipya itakayoendana na mambo ya sanaa na Lugha ili kufufua Tasnia ya Filamu hapa nchini.

Mtu kaishia Darasa la saba au kidato cha nne, atajuaje na kuigizaje mambo ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi yaani ataanzia wapi?
Mtu madarasa hayamtoshi, ataweza kuigiza filamu za kisiasa, ugaidi, na masuala ya demokrasia? Atawezaje ikiwa hajui hata historia ya hiyo demokrasia yenyewe zaidi ya maneno ya mtaani na vijiweni.
Mtu kaishia kidato cha nne atawezaje kufikiria kuandaa scripts ya mambo ya Mpango wa dunia wa milleniam, atawezaje kuigiza Umuhimu wa vyama vingi vya siasa ndani ya nchi?
Mtu kaishia kidato cha nne kwa kulazimishwa, atawezaje kuigiza filamu ya masuala ya sheria na haki za binadamu, hajui hata katiba ya nchi yake, mtu kama huyo huoni ni jipu?

Mtu kaishia kidato cha nne, atawezaje kuandaa filamu ya athari ya udikteta na ukosefu wa uhuru wa kujieleza ndani ya jamii,lini atawaza hayo, yeye kama sio kuwaza mapenzi tuu muda wote?

Mtu kaishia darasa la saba au kidato cha nne, atawezaje kufikiri hata kuigiza filamu inayopromoti utalii wa nchi yetu, utashangaa licha ya nchi yetu kuwa na Mbuga na vivutio vingi lakini tangu tupate uhuru hakuna filamu ya wanyama iliyochezwa na wabongo, utashangaa. Ndio shida ya vilaza hiyo. Wenyewe watakuambia uchumi mgumu.

Mtu anaelimu ya kuunga unga, atawezaje kuigiza inayozungumzia masuala ya fani za kitaalamu kama vile Ualimu wenyewe sio ule wa kuigiza kama wanaoigiza watoto kibaba baba na kimama mama. Au udaktari, au sheria, au injinia, utawezaje igiza kitu hukijui na huna akili ya ku-master kwa upesi.

Mimi nawashauri wenye nafasi na wanaotaka Bongo Movie iamke basi wafanye haya;
Wasajili watu wenye vipaji Fresh from the School, waende shule zenye vipaji huko, Vyuo vikuu vinavyotambulika wachukue watu huko.
Wasaniii wawekewe sheria kuwa ili uwe mwigizaji basi yakubidi uwe na elimu isiyochini ya Diploma. Na uwe umefaulu vizuri kidato cha nne

Tasnia inapoongozwa na Kilaza kamwe haiwezi kuzaa matunda chanya kwenye jamii.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Sumbawanga
Mkuu na kwenye Bongo Flava wamo wengi tuu...
 
William Wayne Blanks is an American fitness guru, martial artist, actor, and the creator of the Tae Bo exercise program. In 1981 won men's karate medal representing USA.

Carlos Ray "Chuck" Norris is an American martial artist, actor, film producer, and screenwriter. After serving in the United States Air Force, Norris won many martial arts championships and later founded his own discipline Chun Kuk Do. Norris is a black belt in Tang Soo Do, Brazilian jiu jitsu and judo.

Bruce Lee was introduced to the film industry by his father and appeared in several films as a child actor. His early martial arts experience included Wing Chun, tai chi, street fighting, and boxing, winning the Hong Kong schools boxing tournament; he also learnt cha-cha dancing, winning the Hong Kong cha-cha championship. Lee moved to the United States at the age of 18 to receive his higher education at the University of Washington in Seattle; it was during this time that he began teaching martial arts, later drawing significant attention at the 1964 Long Beach International Karate Championships.

Schwarzenegger served in the Austrian Army in 1965 to fulfill the one year of service required at the time of all 18-year-old Austrian males. During his army service, he won the Junior Mr. Europe contest. He went AWOL during basic training so he could take part in the competition and then spent a week in military prison.

Nafkiri umeona vigezo vyao hao wote, wote wametoka mbali, wana experience kibao tangu wakiwa watoto ndio maana hata movie zenyewe walizicheza kama ukweli vile, walijua walichokuwa wanakifanya na pia kupitia mentors wao wakaendelea kufaulu.
Haya mambo ya kuokotana vijiweni ati msela ashakua actor/actress wakati hata hakuna chembe ya experience ako nayo be it academically or life ones ni utopolo unaoangusha filamu za Bongo na nchi zingine tu😂
✌️
Sijaona shule zao hapo mkuu; nimeona mambo ya kijeshi na Bruce kua introduced na baba yake huko kwenye martial artists. Uzi unazungumza habari za shule za wasanii, nami nimeleta kama changamoto ya hao wachache kwamba nitajiwe elimu zao; labda sielewi kingereza, kuna sehemu Chuck Norris imeoneshwa kasoma hadi level gani ya elimu hapo?
 
Unataja watu waliowika enzi za giza dunia ikiwa gizani,

waambie sasa hivi waigize Movie uone kama hutaona vituko.

Hata hawa Bongo Movie wangeigiza hizi movie miaka ya 90 huko zingeonekana ni nzuri kutokana na akili za wakati huo.

Huna shule itaigiza nini kama sio utumbo tuu
Mkuu, unajua bado hao unaosema waliigiza enzi za giza bado movies zao zinabamba youtubes kwa zama hizi za mwanga? But again but watu wana nunua CD zao madukani until now, picha zina zaidi ya miaka 50 lakini hadi leo bado zipo madukani.
 
Sijaona shule zao hapo mkuu; nimeona mambo ya kijeshi na Bruce kua introduced na baba yake huko kwenye martial artists. Uzi unazungumza habari za shule za wasanii, nami nimeleta kama changamoto ya hao wachache kwamba nitajiwe elimu zao; labda sielewi kingereza, kuna sehemu Chuck Norris imeoneshwa kasoma hadi level gani ya elimu hapo?
Mkuu, hao jamaa experience zao ni shule tosha, na pia katika maisha yao wamepishana na wacheza film na ma director wakubwa ndio maana wakaonekana uwezo wao huo. Sio lazma uwe na Degree wala nini, kama huna experience yoyote ya kimaisha kama za hao jamaa hata ukipewa scene uicheze itakuzingua. Kwa wale wako shule za uigizaji, atleast hao huwa na knowledge kiasi ya kuigiza lakini sio kila mtu anayemuona unataka kumpatia Chance ya kuigiza, ndio hayo maneno ya movie za utopolo sasa.
 
Mkuu, hao jamaa experience zao ni shule tosha, na pia katika maisha yao wamepishana na wacheza film na ma director wakubwa ndio maana wakaonekana uwezo wao huo. Sio lazma uwe na Degree wala nini, kama huna experience yoyote ya kimaisha kama za hao jamaa hata ukipewa scene uicheze itakuzingua. Kwa wale wako shule za uigizaji, atleast hao huwa na knowledge kiasi ya kuigiza lakini sio kila mtu anayemuona unataka kumpatia Chance ya kuigiza, ndio hayo maneno ya movie za utopolo sasa.
Kama umenifatilia kuanzia mwanzo kabisa utagundua lugha unayo ongea ndio ninayo ongea as well; nilimalizia kwa kusema, "bongo movie inakua kadiri siku zinavyo kwenda" kwa hiyo statement,ndio experience yenyewe unayoisema wewe, kua na shule kubwa sio kigezo. Mdau kazungumzia degree za hao Wanageria, tuweni wakweli, nani ananunua CD za picha za Nigeria za miaka 10-20 iliopita? Au nani ana dowload youtube ile picha ya Nigeria ya pastor Ken sasa hivi? Jibu ni either hakuna, kama wapo basi may be ni less than 1000, kwa Bongo hapa ndio sidhani kabisa so tusiwakatishe tamaa wasanii wetu wa ndani kwa kigezo cha degree, by the way hata hao Wakorea ambao jamaa kawatolea mfano, huenda tuki search CV zao utagundua hata wenyewe wenye degree huenda ni wachache sana.
 
Kama umenifatilia kuanzia mwanzo kabisa utagundua lugha unayo ongea ndio ninayo ongea as well; nilimalizia kwa kusema, "bongo movie inakua kadiri siku zinavyo kwenda" kwa hiyo statement,ndio experience yenyewe unayoisema wewe, kua na shule kubwa sio kigezo. Mdau kazungumzia degree za hao Wanageria, tuweni wakweli, nani ananunua CD za picha za Nigeria za miaka 10-20 iliopita? Au nani ana dowload youtube ile picha ya Nigeria ya pastor Ken sasa hivi? Jibu ni either hakuna, kama wapo basi may be ni less than 1000, kwa Bongo hapa ndio sidhani kabisa so tusiwakatishe tamaa wasanii wetu wa ndani kwa kigezo cha degree, by the way hata hao Wakorea ambao jamaa kawatolea mfano, huenda tuki search CV zao utagundua hata wenyewe wenye degree huenda ni wachache sana.
Kweli hapo, ila utaalamu wa kuigiza pia unahitajika na kuna vyuo vinavyotoa tauluma hiyo. Huwezi linganisha aliyepitia chuo cha uigizaji na aliyechukuliwa tu mtaani sababu ati alikuwa akiigiza vizuri shule za msingi, haiwezekani. Akili zao ni tofauti na hapo ndipo ubora wa filamu unapoingilia.
 
Kweli hapo, ila utaalamu wa kuigiza pia unahitajika na kuna vyuo vinavyotoa tauluma hiyo. Huwezi linganisha aliyepitia chuo cha uigizaji na aliyechukuliwa tu mtaani sababu ati alikuwa akiigiza vizuri shule za msingi, haiwezekani. Akili zao ni tofauti na hapo ndipo ubora wa filamu unapoingilia.

Kutumia nguvu nyingi kuwa criticize waigizaji ni wazi kuwa tunashindwa kufahamu tatizo halisi la tasnia yenyewe. Waigizaji ni sehemu ndogo tu ya tatizo.
 
Elimu ya Darasani sio msing ila inasaidia,hata ukiangalia huko Hollywood kuna big directors lkn hawana hizo elimu za degree za film kuna big actors lkn hawana elimu

Tatizo la Bongo movie linasababishwa na hao wadau wabongo movie wenyewe.kuhusu bajeti hilo sio tatizo maana ukiangalia hizo tamthilia wanazoigiza watu wamepiga makeup nzuri,nguo Kali,wamekodi majumba makali,location za gharama kabisa, gari za gharama, kamera zina quality unaona kabisa bajeti sio shida.
Shida hawa watu wnafanya kimazoea mazoea.
Nlibahatika kufanya kaz na star wa bongo movie mkubwa tu mwaka Jana kma intern bwana tukawa tumeenda location ikatokea lights na equipment zake hazijafika kwa sababu mwenye nazo alikuwa kapata gig nyingne, sasa huyo star mwenyew ambay ni director,producer na main actor pia akasema tushoot hivyo hivyo bila lights dah nlishangaa sana,na movie within two days ilikuwa tayari
 
Bongo movie INA safari ndefu sana maana.mm naamin wakiwa serious na wakafanya kazi nzur wawekezaji watakuja weng na wakutosha,nenda kaangalie wasouth na wanaija huko Netflix.
Kuna series mmoja huko Netflix y kisauzi jina lake sikumbuki ila inahusu msichna mmoja anaenda shule ya matajiri kumtafuta pacha wake,ni series ya kawaida hata aina budget kubwa ila n nzuri
 
Umetolea mfano wa simba kwani simba inapewa pesa na serikali.
Mtu anataka kuweka pesa akiangalia wasanii ndio hawa, story ndio hizi mapenzi, mapenzi hebu angalia hizi series za uko datv(maisha magic), na azam tv nyingi ni visa ni mapenzi na vinafanana lakini kiuhalisia mkuu mtaani story ni nying hususani hapa Tz kuna visa vingi tu mtu anaejielewa anaweza kutungia story. Achana na za mapigano hizo uwezo wetu bado hizi hizi za kijamii kwani marehemu kanumba ye story alikua anatoa wapi.

Kwasababu filamu zake zilikua na mapenzi kama part tu ya kukuza migogoro(lazma iwepo kwenye filamu) lakini sio hizi wadada series yote wamevaa nusu utupu wakati kibongo bongo sio uhalisia huo
Serikali isipotia mkono hata huo ujinga unaofanywa na vijana hautaisha. Hiyo sanaa iliyopo inafanywa sababu kuu ikiwa kuganga njaa na sio vipaji. Serikali haina la kujitetea katika hili
 
Serikali isipotia mkono hata huo ujinga unaofanywa na vijana hautaisha. Hiyo sanaa iliyopo inafanywa sababu kuu ikiwa kuganga njaa na sio vipaji. Serikali haina la kujitetea katika hili
Kwa wasanii wa muziki serikali ilitia mkono gani mpaka leo tunaona kina diamond wanapaa?? Tusiilaumu tu serikali ilhali watu hawana jitihada binafsi.

Hukohuko bongomovie, enzi za kanumba hadi kupaa namna ile serikali ilitia mkono gani katika yale mafanikio, ni jitihada tu mkuu.
 
Kwa wasanii wa muziki serikali ilitia mkono gani mpaka leo tunaona kina diamond wanapaa?? Tusiilaumu tu serikali ilhali watu hawana jitihada binafsi.

Hukohuko bongomovie, enzi za kanumba hadi kupaa namna ile serikali ilitia mkono gani katika yale mafanikio, ni jitihada tu mkuu.

Huwezi kufananisha muziki na film industry, filamu industry ni tasnia inayohitaji uekezaji mkubwa pamoja na taaluma kubwa.
 
Huwezi kufananisha muziki na film industry, filamu industry ni tasnia inayohitaji uekezaji mkubwa pamoja na taaluma kubwa.
Hata muziki unahitaji uwekezaji na taaluma vilevile. Huwezi kufanya vitu hovyo ukategemea kufanikiwa mkuu, wasanii wa muziki wanaenda kushoot video zao nje ya nchi kwa gharama, wanawatumia directors kwa gharama kubwa halafu unasema huwezi kufananisha mkuu una maana gani hapo?? Wasanii wa muziki wengine wanakwambia video zao wametumia zaidi ya 50M mpaka kukamilisha. Kuna siku nilimskia msanii anasema wametumia 14M kukamilisha movie, hebu linganisha hapo wimbo una dakika 4 tu 50M imetumika lakini filamu masaa zaidi ya 2 na location tofaut tofaut na mambo kibao eti 14M tu. Wakati huo filamu nyingine hazitumii hata 1M.

Wajitathmini mkuu.
 
Hata muziki unahitaji uwekezaji na taaluma vilevile. Huwezi kufanya vitu hovyo ukategemea kufanikiwa mkuu, wasanii wa muziki wanaenda kushoot video zao nje ya nchi kwa gharama, wanawatumia directors kwa gharama kubwa halafu unasema huwezi kufananisha mkuu una maana gani hapo?? Wasanii wa muziki wengine wanakwambia video zao wametumia zaidi ya 50M mpaka kukamilisha. Kuna siku nilimskia msanii anasema wametumia 14M kukamilisha movie, hebu linganisha hapo wimbo una dakika 4 tu 50M imetumika lakini filamu masaa zaidi ya 2 na location tofaut tofaut na mambo kibao eti 14M tu. Wakati huo filamu nyingine hazitumii hata 1M.

Wajitathmini mkuu.

hiyo filamu iliyotumika kukamilika kwa milion 14 ndio hayo matatizo yenyewe ya filamu zetu. Filamu zinatakiwa kwa kuanzia tu zianzie alau milion 200 kwenda mbele.
Lakini nani atawekeza pesa zake nyingi bila ya kutarajia return?
Filamu zinategemea mauzo makubwa kwa kupitia cinemas, bongo hatuna kabisa tamaduni za kwenda cinema.
Filamu zinategemea kupata hela kwa kupitia streaming webs, bongo hatuna kabisa tamaduni za kujiunga na kulipia hizo streaming webs.

Mzunguko wa uingizaji pesa muziki ni mwepesi sana ndio mana wanaweza kurisk hizo 50 m, Ila kwa filamu ni ngumu ku risk hele ndefu hata ukatungiwe story na mtunzi kutoka Hollywood.
 
hiyo filamu iliyotumika kukamilika kwa milion 14 ndio hayo matatizo yenyewe ya filamu zetu. Filamu zinatakiwa kwa kuanzia tu zianzie alau milion 200 kwenda mbele.
Lakini nani atawekeza pesa zake nyingi bila ya kutarajia return?
Filamu zinategemea mauzo makubwa kwa kupitia cinemas, bongo hatuna kabisa tamaduni za kwenda cinema.
Filamu zinategemea kupata hela kwa kupitia streaming webs, bongo hatuna kabisa tamaduni za kujiunga na kulipia hizo streaming webs.

Mzunguko wa uingizaji pesa muziki ni mwepesi sana ndio mana wanaweza kurisk hizo 50 m, Ila kwa filamu ni ngumu ku risk hele ndefu hata ukatungiwe story na mtunzi kutoka Hollywood.
Mimi bado nakupinga mkuu ni vile tu hatujajizatiti huko naungana na mtoa uzi 100%. Tasnia imejaa wasioelimika kuhusu hiyo kazi yao. Japo uchumi ni changamoto lakini unaona kabisa jinsi hata hiyo pesa kidogo wanavotumia kutuonesha madudu kwenye filamu zao nyingi zenye story moja yenye kisa kinachofanana (MAPENZI).

Wasanii wa muziki miaka ya zamani hawakua watu wa kwenda kushoot video zao nje na kushirikisha saana wasanii toka nje ya nchi. Lakini hivi karibuni baada ya kuona wenzao wanaenda sana kushoot nje na wanashirikisha wasanii wakubwa wa nje nao wameiga icho kitu na kinawapa matokeo chanya. Ona jinsi tasnia ya muziki inavopaa, mfano ni hawa wasanii kina maroo,mboso na wanaofanana na hao.

Haya tuje kwenye filamu zamani ilikua inafanya poa sana na iliteka sana soko la bongo ikichuana na nigeria, hizi za kikorea zimekuja hivi karibuni tu labda za kihindi na kizungu ndio zilitamba sana enzi hizo nazo ilikua ni vibanda umiza majumbani ilikua bongo movies. Akaja kanumba nae akaipaisha mno, Ray nae hakua nyuma. Je hawa wasanii waliobaki walicopy nini toka kipindi kile sanaa iko juu, enzi za kanumba & Ray, yaan hakuna la kujifunza kabisa kwa hivyo vyote kama wenzao wa muziki wanavyonata na soko lao.
 
Mimi bado nakupinga mkuu ni vile tu hatujajizatiti huko naungana na mtoa uzi 100%. Tasnia imejaa wasioelimika kuhusu hiyo kazi yao. Japo uchumi ni changamoto lakini unaona kabisa jinsi hata hiyo pesa kidogo wanavotumia kutuonesha madudu kwenye filamu zao nyingi zenye story moja yenye kisa kinachofanana (MAPENZI).

Wasanii wa muziki miaka ya zamani hawakua watu wa kwenda kushoot video zao nje na kushirikisha saana wasanii toka nje ya nchi. Lakini hivi karibuni baada ya kuona wenzao wanaenda sana kushoot nje na wanashirikisha wasanii wakubwa wa nje nao wameiga icho kitu na kinawapa matokeo chanya. Ona jinsi tasnia ya muziki inavopaa, mfano ni hawa wasanii kina maroo,mboso na wanaofanana na hao.

Haya tuje kwenye filamu zamani ilikua inafanya poa sana na iliteka sana soko la bongo ikichuana na nigeria, hizi za kikorea zimekuja hivi karibuni tu labda za kihindi na kizungu ndio zilitamba sana enzi hizo nazo ilikua ni vibanda umiza majumbani ilikua bongo movies. Akaja kanumba nae akaipaisha mno, Ray nae hakua nyuma. Je hawa wasanii waliobaki walicopy nini toka kipindi kile sanaa iko juu, enzi za kanumba & Ray, yaan hakuna la kujifunza kabisa kwa hivyo vyote kama wenzao wa muziki wanavyonata na soko lao.
Ila mkuu ukienda mkoani huko Film za kibongo zinakiki
 
Ila mkuu ukienda mkoani huko Film za kibongo zinakiki
Sijajua mikoa mingine ila kwa michache niliyotembelea naona ni hizi series za kikorea zilizotafsiliwa. Na wengine ndo izo movies na series za nje, nyuzi zilizopo humu kuhusu masuala ya filamu pendwa zinathibitisha hilo. Hawajadili movie za bongo ni za nje tu.
 
Back
Top Bottom