Boris Johnson akalia kuti kavu, mawaziri wawili waandamizi wajiuzulu. Ni Waziri wa Fedha Rishi Sunak na Waziri wa Afya Sajid Javid

Boris Johnson akalia kuti kavu, mawaziri wawili waandamizi wajiuzulu. Ni Waziri wa Fedha Rishi Sunak na Waziri wa Afya Sajid Javid

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
1657051217043.png

Boris Johnson akiwa na Rishi Sunak na Sajid Javid Bungeni, Picha na PA.

Mawaziri wawili waandamizi wa serikali ya Uingereza jioni hii wamejuzulu nafasi zao.

Mawaziri hao ni waziri wa fedha Rishi Sunak na waziri wa afya Sajid Javid.

Katika barua zao za kujiuzulu mawaziri hao waandamizi wameelezea sababu za kujiuzulu zikiwemo kutokuwa na imani na waziri mkuu Boris Johnson na kushuka kwa viwango vya uendeshaji wa Serikali.

Pamoja na mawaziri hao pia viongozi wengine waandamizi wamejiuzulu nafasi zao akiwemo makamu mwenyekiti wa chama cha wahafidhina bwana Bim Afolami, katibu wa bunge bibie Saqib Bhatti, balozi wa Uingereza nchini Morocco Andrew Murrison wa masuala ya biashara na Jonathan Gullis ambae ni mwakilishi wa Serikali kwa upande wa Ireland ya kaskazini.

Kujiuzulu kwa viongozi hao kunafuatia habari kwamba waziri mkuu Boris Johnson alikuwa anafahamu kuhusu tuhuma za ubazazi zilokuwa zikimkabili aliekuwa kiongozi wa wabunge bwana Chris Pincher kabla ya kumpa nafasi hiyo lakini akapuuzia.

Bwana Chris Pincher amekuwa na tabia ya kulewa na kisha kuanza kuwashika wanaume wenzie awapo katika klabu ya wanaume ya chama cha wahafidhina iliyopo katikati ya jiji la London.

Lakini wiki ilopita alipolewa alianza kuwashikashika (groping) wanaume wenzie zaidi ya wawili ambao baadae walitoa malalamiko kupitia watu mbalimbali, malalamiko kufikia kwenye vyombo vya habari.

Waziri mkuu alipojulishwa juu ya jambo hilo alipuuzia na kusema binadamu hukosea lakini akasahau kwamba mwezi Februari alijulishwa juu ya malalamiko juu ya tabia za bwana Pincher na akapuuzia na kumteua katika nafasi nyeti serikalini.

Lakini sababu zingine za kujiuzulu kwa viongozi hao zasemwa kuwa ni kuogopa kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao ambapo hadi sasa chama cha wahafidhina kimepoteza imani kwa wananchi kwa kutodhughulikia uzuri masuala ya mfumuko wa bei, kupanda kwa hgharama za maisha na kupanda kwa bei ya bidhaa mbalimbali yakiwemo mafuta ya petroli na dizeli.

Bwana Johnson jioni hii aliendelea kuketi na mawaziri kadhaa huku akiwa na muda mrefu na waziri wa elimu bwana Nadhin Zahawi ambae huenda akawa waziri wa fedha.

Zahawi ni mmoja wa mawaziri waandamizi walobakia lakini mwenye kupewa nafasi kubwa ya kuwa waziri wa fedha ambapo ofisi yake yaitwa namba 11.

Zahawi alihamia nchini Uingereza mwaka 1976 akiwa na miaka 9 yeye na familia yake walokimbia madhila ya aliekuwa raisi wa Iraq Sadam Hussein.

Hiyo kumaanisha kuwa Uingereza itakuwa na waziri wa fedha ambae hakuzaliwa Uingereza lakini amekulia hapo na kupata elimu yake nchini humo.
 
Ndiyo maana Joe Biden na Boris Johnson--Waziri Mkuu wake--wameng'ang'ania kufurukusha matatizo nje ya nchi zao ili wajisahaulishe yaliyomo kwao. Poor souls!

Hands-off Ukraine! Acheni kumshikia Zelensky akili, Mrusi atambutua ammalize. Haya, jifanyeni vichwa ngumu!
 
Mawaziri wawili wamejiuzulu wakisema hawawezi kuendelea kuifanyika kazi Serikali inayokabiliwa na kashfa. Uamuzi wao ni pigo kubwa kwa Waziri Mkuu, Boris Johnson ambaye Mwezi Juni alipigiwa Kura ya Imani

Rishi Sunak amesema Umma unatarajia Serikali kuendeshwa vizuri na kwa umakini, akieleza kuwa anajiuzulu kwasababu anaamini viwango hivyo vinapaswa kupiganiwa

Sajid Javid amesema Kura ya Imani kwa Waziri Mkuu ilikuwa wakati wa mwelekeo mpya, lakini ni dhahiri hali haitobadilika chini ya Uongozi wake

========

British Prime Minister Boris Johnson was dealt a huge blow on Tuesday when two of his top ministers announced their resignations, saying they could no longer work for a government mired in scandal.

Chancellor Rishi Sunak and Health Secretary Sajid Javid both announced they were quitting in letters posted to Twitter within minutes of each other on Tuesday evening.

"The public rightly expect government to be conducted properly, competently and seriously," Sunak said in his resignation letter. "I recognise this may be my last ministerial job, but I believe these standards are worth fighting for and that is why I am resigning."

"In preparation for our proposed joint speech on the economy next week, it has become clear to me that our approaches are fundamentally too different," Sunak added in the letter. "I am sad to be leaving Government but I have reluctantly come to the conclusion that we cannot continue like this."

Javid wrote that "it has been an enormous privilege to serve in this role, but I regret that I can no longer continue in good conscience." Javid added that the vote of confidence in the prime minister last month "was a moment for humility, grip and new direction."

"I regret to say, however, that it is clear to me that this situation will not change under your leadership -- and you have therefore lost my confidence too," Javid wrote.

Scandal after scandal​

The most immediate controversy facing Johnson is Downing Street's handling of last week's resignation of deputy chief whip Chris Pincher, who stepped down from his post last Thursday amid allegations he had groped two guests at a private dinner the night before.

While he did not admit the allegations directly, Pincher said in a letter to Johnson that "last night I drank far too much" and "embarrassed myself and other people."

Downing Street has struggled to explain why Pincher was in government in the first place, amid a wave of revelations about his previous alleged conduct, denying Johnson knew anything specific about the allegations.

On Tuesday, it emerged that a complaint had been made against Pincher in the Foreign Office about three years ago and that Johnson was briefed on what happened.

Minutes before Sunak and Javid announced their resignations, Johnson acknowledged it "was a mistake" to appoint Pincher to his government.

"I got this complaint. It was something that was only raised with me very cursory, but I wish that we had acted on it and that he had not continued in government because he then went on, I'm afraid, to behave, as far as we can see -- according to the allegations that we have -- very, very badly," Johnson said in a broadcast interview.

UK opposition leader Keir Starmer said it was "clear" that the government was "collapsing."

"Tory cabinet ministers have known all along who this Prime Minister is. They have been his cheerleaders throughout this sorry saga. Backing him when he broke the law. Backing him when he lied repeatedly. Backing him when he mocked the sacrifices of the British people," the Labour Party leader said in a statement released after the two resignations.

For months Johnson has been facing a barrage of criticism over his conduct and that of his government, including illegal, lockdown-breaking parties thrown in his Downing Street offices for which he and others were fined.

Johnson has faced numerous other scandals that have hit his standing in the polls -- despite his 80-seat landslide victory just two-and-a-half years ago. These include accusations of using donor money inappropriately to pay for a refurbishment of his Downing Street home and whipping MPs to protect a colleague who had breached lobbying rules.

Source: CNN
 
Hata huku kwetu watano wamejiudhuru kwa sababu hizohizo, wanasema kutoka nchini kwetu hadi vinezuela ni kilometa tano tu kwa mpaka wa majini lakini serikali ilisafirisha wajumbe watatu kwa bilioni 5 nauli
 
Hata huku kwetu watano wamejiudhuru kwa sababu hizohizo, wanasema kutoka nchini kwetu hadi vinezuela ni kilometa tano tu kwa mpaka wa majini lakini serikali ilisafirisha wajumbe watatu kwa bilioni 5 nauli
Walitumia usafir wa aina gani?
 
Kati ya nyakati ambazo waingereza wamekosea kuchagua waziri mkuu,basi ni huyu bwana Borris Johnson.
Muonekano wake pamoja na matamshi hayaendani na wadhifa wake.

Lakini yote kwa yote Putin anaiangusha Ulaya kwa ujinga wa hawa wanasiasa wao.
Naskia anakula nyeupe
 
Back
Top Bottom