Botswana imefanyaje kufikia hatua hii?

Botswana imefanyaje kufikia hatua hii?

Nilienda nikaingia hozpitali ya jeshi kasane nikapata huduma ya afya kutoka kwa kamanda na akanipa dawa za kutosha nilikuwa nasumbuliwa na mafua makali nikapewa hadi vidonge vya vitamin c , bureee nikachapa lapa
Upo right mkuu mimi nilisaidiwa sana pale Pandamatenga Barracks,matengenezo ya gari ya bure,coffee safi na kuwa adviced kuwa sio vema to drive usiku na wanyama wengi mbugani,nikapewa godoro main gate!asubuhi nikaanza ila nili drop name,offcourse Nyerere!!
 
Democary haiwezi kufanya kazi kweny watu wengi
Tanzania hapa tunatakiwa mambo yote yaratibiwe na Tume ya mipango ndio wapange vipaombele,namna ya kuviteleza,mda na tuwe na assessment ya mrejesho.

Pia tugawe Mikoa ipi ifanye kipi na tuchague sekta za kipaombele ila hii tabia ya kwenda jumla Jumla Hatuwezi kufika ,itakuwa ni mark time tuu.
 
Botswana siyo ndogo. Imeizidi Zimbabwe kwa ukubwa, inakaribia kulingana na zambia, Rwanda inaingia karibu mara ishirini kwa Botswana. Uganda ni mara mbili kwa ukubwa na Botswana.

Wana Tembo wengi hadi imekuwa kero wanataka kuwapunguza kwa kuwaua hadi wanaharakati wamewajia ulaya wamewajia juu. Majuzi wamewapa Angola Tembo 8000 na msumbiji Tembo mia 5.
wanaharakati samtaim mapimbi sana. ni kama ukimani kuzimu bongo tembo kila leo wanaleta madhara makubwa. walipaswa kudhibitiwa uzalianaji wao
 
They have one of the Best Mining Contract with Investors..., At least comparing with the likes of Us; And believe you me..., it will get worse as the contracts we are currently agreeing makes the Late Mangungo of Msovero look like a genius....
 
Botswana na Namibia wana unafuu wa maisha kwasababu wamedhibiti rushwa na ufisadi. Wee fikiria kama CCM isingekuwa inaiba tungesave zaidi ya trillion 50 kwa mwaka. Tungelipa na kupunguza deni la taifa na kuwekeza kwenye maendeleo. Ni ufisadi rushwa na utawala mbovu tu ndo chanzo cha nchi nyingi kuwa maskini.
CCM usipokuwa mwizi unatengwa au kufukuzwa kabisa.
 
Wabongo kuna watu wamejichagua wawe wanaiba chochote kinachoingia kwenye hazina
Yaani hawafiki hata 1m ila ndio kama familia ya majizi
Hakuna anaefungwa zaidi anapewa ndugu mwingine

Hatupo serious na maisha kabisa
Wenzetu mpaka Kenyans wameenda huko na kuanza Ranches za mifugo
Unapewa ardhi na unalindwa
24hrs patrol
Huwezi kuhamisha mifugo sehemu mpaka sehemu bila kuijulisha serikali ili upate kibali, hiyo ni kwa usalama wako na mifugo

Simu moja tu police wako na wewe hakuna cha ooh hatuna gari au tuwekee mafuta tuma hela kwenye Mpesa
Ukiacha hicho mnachoita wizi ila binafsi ukiniuliza Kwa nini tuna maendeleo ya kusuasua nitakwambia tuna shida ya kuchagua vipaombele na pia kufanya mambo kiujumla Jumla.

Mfano mdogo ni kwenye Barabara.Tunahitaji Barabara zaidi kuifungua Nchi kuliko miundombinu mingine ya usafiri.

Lakini hapo hapo kwenye Barabara tunatapanya Rasilimali bila kuwa na Barabara za vipaombele utakuta Kila Mkoa tunajenga vibarabara vya km 10,6,6,15,30,8,50 nk wakati tungekuwa na Barabara kadhaa za vipaombele zingeisha Kwa wakati zinaendelea Kuzalisha na tunahamia kwingine.

Angalia hapa yaani Waziri anaenda kuweka Jiwe la msingi Barabara ya km 6 out of 60 zinazoktakiwa Sasa hizi ni akili au ujinga wa Watanzania?

View: https://twitter.com/WizarayaUJ/status/1776596912470139079?t=WAehp_fLCnWhiGbT7Xhi8Q&s=19

Nchi haiwezi kuendelea Kwa utaratibu wa kutapanya Rasilimali Kwa maslahi ya Kisiasa Kwa sababu ya watu wajinga.
 
Mkuuu fafanua tafadhali
Huyo Mr ni bwa seretse Khama na Mrs hapo Ruth Khama... Huyo bwana alikuwa raisi wa Botswana alipelekwa ulaya kusoma alivyomaliza chuo akrudi nyumbani na Binti wa kizungu ambaye ni mkewe na kisha kuanza harakati za kisiasa na bibiye huyo wa kizungu na hatimaye kuwa raisi wa nchi na bibiye huyu wa kizungu kuwa first lady wa miongoni mwa nchi tajiri kwa madini afrika..... Kipindi cha uongozi wa huyo bwana Khama ndipo kulitokea mapinduzi ya kiuchumi ya halo ya juu sanaaaa!!!......... Ila kwa kufupisha badae mwanae pia alikuja kuwa raisi wa nchi..... Zaidi ingia maktaba au kama huwezi au huna maktaba google tu... Utapata...
 
Hivi huu ujasiri wa kusema ni nchi ndogo mara watu wachache, huwa mnautoa wapi? Ninyi wenye watu wengi patengenezeni basi hata Njombe au Makambako pawe pa kuvutia ili iwe mfano!?
Tunaweza ila tuu kama tutapata akili za kufanya hivyo.

Mimi ningekuwa Rais wenu ningefanya mambo mengi sana mazuri maana Nina akili za kiuchumi na najua kuwashirikosha wenye akili pia.

Kama umewahi msikiliza Mbunge Kunambi,basi Mimi ningefanya kazi na watu kama yeye.

Mwisho mambo mazuri Huwa yanahitaji mda na sucrifice unaweza wahishwa Kwa God maana hapa Bongo ni shida sana.
 
Rwanda ingekuwa kama Botswana chini ya Kagame ingekuwa kama Taiwan. Kagame licha ya ukatili wake anaweza kufanya Rwanda kuwa na unafuu licha ya limited resources. Angalia tu kama kwenye utalii yani sokwe mountain gorilla wachache amefanya utalii wa hatarii huku kwetu Tanapa wanaiba balaa.
Ukitaka kufahamu Tanzania ni masikini sana ukilinganisha na Botwana angalia GDP per capita.

Tanzania $1200

Botswana $7000

Jibu rahisi kwanini Botswana ipo vizuri ni rahisi tu ku. Pesa inaenda inapotakiwa iende. Rushwa na uzembe unaenda jela.

Hapa Tanzania kiongozi akikamatwa kwa rushwa anaseme "Tumbo halina siasa".

Hakuna anayejali mzee. Uzembe, uvivu, uchawa ndiyo mambo yanayosifiwa.

Hakuna wakulaumu zaidi ya sisi wananchi wajinga.
 
Ukiacha hicho mnachoita wizi ila binafsi ukiniuliza Kwa nini tuna maendeleo ya kusuasua nitakwambia tuna shida ya kuchagua vipaombele na pia kufanya mambo kiujumla Jumla.

Mfano mdogo ni kwenye Barabara.Tunahitaji Barabara zaidi kuifungua Nchi kuliko miundombinu mingine ya usafiri.

Lakini hapo hapo kwenye Barabara tunatapanya Rasilimali bila kuwa na Barabara za vipaombele utakuta Kila Mkoa tunajenga vibarabara vya km 10,6,6,15,30,8,50 nk wakati tungekuwa na Barabara kadhaa za vipaombele zingeisha Kwa wakati zinaendelea Kuzalisha na tunahamia kwingine.

Angalia hapa yaani Waziri anaenda kuweka Jiwe la msingi Barabara ya km 6 out of 60 zinazoktakiwa Sasa hizi ni akili au ujinga wa Watanzania?

View: https://twitter.com/WizarayaUJ/status/1776596912470139079?t=WAehp_fLCnWhiGbT7Xhi8Q&s=19

Nchi haiwezi kuendelea Kwa utaratibu wa kutapanya Rasilimali Kwa maslahi ya Kisiasa Kwa sababu ya watu wajinga.

Mkuu umesema kweli kabisa kuna wakati nilikuwa naendea malori Horohoro ndio border ila njia ya kuunganisha karibu na nchi jirani ilikuwa hovyo sana

Kuhusu kuchezea hela ndio hivyo tena wanaenda kufungua Choo gari 50 zinafuatana
Mimi sio mpenzi wa mwenge na ninapinga sana ubadhirifu ila kwa hayo umeongea kuntu
 
Back
Top Bottom