BRELA: Kalynda ilipewa leseni ya kuuza vifaa vya kielektroniki

BRELA: Kalynda ilipewa leseni ya kuuza vifaa vya kielektroniki

Directors ni kina nani? Wameshatapeli wasio na akili, Serikali inaelewa kabisa kuwa ina raia wa aina gani sijui kwann haiwalindi? Au wahusika wapo ndani ya serikali?
 
Hata matangazo ya ITV , ya hao Kalynda - yalikuwa hayaonekani kwa BRELA ?

Yawezekana ni mradi wa kigogo serikalini , kwa sababu kampuni ina leseni zaidi ya 3 , zote zimetoka serikalini na zinaoneshwa public na pili matangazo ya yalikuwa wimbo ITV
Na je wakitoa leseni hakuna ufuatiliaji kuona kama biashara iliyoombewa leseni ndiyo inayofanyika?

Serikali inayoongozwa na rais anayelipwa mshahara na wananchi, usalama wa mali za wananchi umewekwa rehani na hajali.

Bado mnanishauri tu kkuna serikali na TISS yake nchi hii?
 
Tambua itv n kampun ya biashara wao Kaz yao n kupokea matangazo yaliyolipiwa

Jukumu la kujua biashara n halali au siyo halali si lao zpo mamlaka zenye jukumu Hilo

Nadhan watanzania uelewa wetu n mdogo Sana kuhusu majukumu ya vyombo mbalimbali vya serikal na binafsi

Lakin pia alert ilitolewa humu watu hawakuelewa kitu

Mambugila nchi hii hawawez kuisha

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Unaongea simple coz hujaliwa😅
 
Tujikumbushe kidoogo ID
1665593533578.jpg
 
Tambua itv n kampun ya biashara wao Kaz yao n kupokea matangazo yaliyolipiwa

Jukumu la kujua biashara n halali au siyo halali si lao zpo mamlaka zenye jukumu Hilo

Nadhan watanzania uelewa wetu n mdogo Sana kuhusu majukumu ya vyombo mbalimbali vya serikal na binafsi

Lakin pia alert ilitolewa humu watu hawakuelewa kitu

Mambugila nchi hii hawawez kuisha

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Ni mamlaka gani inajua biashara ni halali na sio halali?

Kwa nini BRELA anatoa leseni?
 
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imesema leseni ya kampuni iitwayo Kalynda E-Commerce Limited iliyotolewa Juni 21, 2022 ni kwa ajili ya uuzaji wa jumla wa vifaa vya kielektroniki na mawasiliano pamoja na ufanyaji wa biashara ya kiteknolojia ya kimataifa mtandaoni.

BRELA imesema kumekuwa na taarifa zinazoleta taharuki kuhusu kampuni hiyo kufanya biashara ya upatu ya kukusanya fedha kutoka kwa wananchi kwa ahadi ya kupata faida ndani ya muda flani kinyume na bidhaa au huduma iliyoombewa leseni.

Taarifa ya BRELA imesema leseni ya biashara ya Kalynda E-Commerce Limited inamruhusu kufanya biashara ya masoko na mauzo ya bidhaa kwa njia ya mtandao pekee, hivyo ufanyaji wa biashara kinyume na leseni iliyotolewa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 19 cha sheria ya leseni za biashara, Sura Na. 208.

Aidha, Wakala imetoa angalizo kwa umma kuwa kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya kibiashara na kampuni yoyote ni vema kupata uthibitisho wa uhalali na uwepo wa kampuni hiyo pamoja na biashara husika kutoka BRELA na mamlaka nyingine za Serikali.

View attachment 2384974


Swahili Times.
Namsikitikia yule dada whatsapp nilimwambia kalynda ni pyramid scheme akaniambia atakufa ndani ya kalynda, 😄😄😄😄😄leo hii nahisi anakufa na presha
 
Brela wanaibuka kusema hayo baada ya watu kulizwa. BRELA walikuwa wapi siku zote wakati Kalynda wakipiga promo na watu wakijiunga?

Wote huo ni ujinga wa watu wacha waliwe tu! Wewe uliona wapi hela zinajazwa mfukoni mwako zisizo na jasho? Hata wanaoshinda pesa za betting wanatoa jasho la kuliwa kwanza! Mimi hii nimeipenda sana, wacha wajinga na wapumbavu wakomeshwe ili liwe fundisho kwa siku zijazo! Kalyanda hoyeeee! Kanyaga twende Kalyanda!
 
Kwa hio naweza kwenda kutangaza biashara za.magendo ITV kisa wanafanya biashara za matangazo?

Kama una ubavu nenda mradi kama umelipia watakutangazia tu, moto utakaoupata siyo wa ITV babu!
 
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imesema leseni ya kampuni iitwayo Kalynda E-Commerce Limited iliyotolewa Juni 21, 2022 ni kwa ajili ya uuzaji wa jumla wa vifaa vya kielektroniki na mawasiliano pamoja na ufanyaji wa biashara ya kiteknolojia ya kimataifa mtandaoni.

BRELA imesema kumekuwa na taarifa zinazoleta taharuki kuhusu kampuni hiyo kufanya biashara ya upatu ya kukusanya fedha kutoka kwa wananchi kwa ahadi ya kupata faida ndani ya muda flani kinyume na bidhaa au huduma iliyoombewa leseni.

Taarifa ya BRELA imesema leseni ya biashara ya Kalynda E-Commerce Limited inamruhusu kufanya biashara ya masoko na mauzo ya bidhaa kwa njia ya mtandao pekee, hivyo ufanyaji wa biashara kinyume na leseni iliyotolewa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 19 cha sheria ya leseni za biashara, Sura Na. 208.

Aidha, Wakala imetoa angalizo kwa umma kuwa kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya kibiashara na kampuni yoyote ni vema kupata uthibitisho wa uhalali na uwepo wa kampuni hiyo pamoja na biashara husika kutoka BRELA na mamlaka nyingine za Serikali.

View attachment 2384974


Swahili Times.
Haya tuimbe woteee....
IMG_20220713_130259_0.jpg
 
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imesema leseni ya kampuni iitwayo Kalynda E-Commerce Limited iliyotolewa Juni 21, 2022 ni kwa ajili ya uuzaji wa jumla wa vifaa vya kielektroniki na mawasiliano pamoja na ufanyaji wa biashara ya kiteknolojia ya kimataifa mtandaoni.

BRELA imesema kumekuwa na taarifa zinazoleta taharuki kuhusu kampuni hiyo kufanya biashara ya upatu ya kukusanya fedha kutoka kwa wananchi kwa ahadi ya kupata faida ndani ya muda flani kinyume na bidhaa au huduma iliyoombewa leseni.

Taarifa ya BRELA imesema leseni ya biashara ya Kalynda E-Commerce Limited inamruhusu kufanya biashara ya masoko na mauzo ya bidhaa kwa njia ya mtandao pekee, hivyo ufanyaji wa biashara kinyume na leseni iliyotolewa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 19 cha sheria ya leseni za biashara, Sura Na. 208.

Aidha, Wakala imetoa angalizo kwa umma kuwa kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya kibiashara na kampuni yoyote ni vema kupata uthibitisho wa uhalali na uwepo wa kampuni hiyo pamoja na biashara husika kutoka BRELA na mamlaka nyingine za Serikali.

View attachment 2384974


Swahili Times.
Watzn wanapenda kitonga,acha wapigwe hadi akili zikae sawa.
 
Back
Top Bottom