Brenda Mihanjo, msomi mwenye Masters aliyejikita kwenye ufundi seremala

Brenda Mihanjo, msomi mwenye Masters aliyejikita kwenye ufundi seremala

Tuache fundishana mfecane war sijui Archimedes principle
InShot_20220112_153906812.jpg
 
Yule mwenye masterz ya marekani anaeuza makande vipi?
Nae hana tofauti na huyu.
Hakuna ubunifu pale ni mamantilie mwenye master.
Alichoongeza pale ni vyombo na mavazi mazuri kitu ambacho hata Shilole kakifanya kwenye mgahawa wake japo hana master.
Tunaendelea kuaminishana kuwa wenye master ni sahihi kuuza makande, kuendesha boda, kuuza mboga mboga, kuuza samski feli.
Binafsi sioni faida ya hizo master bali wamepoteza muda wsmao na pesa zao bure na kuishia kufanya vitu visivyohitaji master.
 
Huwa nawashangaa sana watu kuona VETA ndio suluhisho wakati hao wakufunzi wenyewe wa veta hawana jipya.
Chunguza assets zetu mitaani utagundua kuwa VETA hawana innovation zozote za maana wanashindwa na wachina wanaobumba assets kwa vumbi la mbao.
Tanzania kuna kila mti wa mbao lakini mafundi wameshindwa kubuni vitu vizuri kushindana na vya nje.
Upo sahihi kabisa.
Umuhimu veta ni certification mzee
Unaweza ukawa na skillz kibao ukaleta dizaini za kipekee

Ila unapofika time unataka tenda kwenye mashirika na makampuni wanataks uthibitisho wa kimaandishi na kazi za kuonekana utsjikus unakosa deals

Mimi mwenyewe nina bachelor ila nataka niende veta nikapate abc tu za ufundi fulani halafu nije kitaa nifanye manuva maana access ya mtaji ninayo
 
Hata keko wametoboa bila master.Issue sio kutoboa, issue ni kupoteza muda mashuleni halafu anaenda kufanya jambo dogo lisilohitaji hata diploma.
Tutumie vizuri muda.
Hio miaka kumi aliotumia kusoma angekuwa mbali zaidi.
Halafu sio peke yake anafanya ufundi wapo wengi tu, hivyo suala kutoboa ni kupambana wala sio kuwa na master, wanaweza kutonoa wasi na master ya shule bali wanauzoefu wa kutosha na kujua A-z za hio biashara.
Kuwepo kwenye game muda mrefu ni factor kubwa ya kuendelea kuliko makaratasi.
Endeleeni kujipa moyo ila muda mmeupoteza sana.
Wee nawee 🤔

Mambo ya interior designing ni taaluma za watu etii , tena ni biashara kubwa. Tatizo wewe unawaza padogo na exposure huna unaonekana, we unakomalia kumfananisha na mafundi wa keko tatizo.

Taaluma yake ya biashara itamsaidia kukuza biashara yake, kuleta ubunifu n.k

Kuna stage mfanyabiashara hata Kama ni darasa la Saba atahitaji elimu tu ili biashara yake ikue zaidi. Hata Kama hajasoma itabidi aajiri watu wenye taaluma zao.
Ndio maana familia za wakina bakheresa na dewji ziliwapeleka watoto wao shule na vyuo vya gharama ili waje wasimamie biashara. Sasa kwanini wao hawakupotezea elimu kwa watoto wao

Hizo biashara na kampuni kubwa unazoziona zimekuzwa na kusimamiwa na wasomi. Hata Kama mmiliki ni std seven Kuna stages za biashara inabidi utafute watu na utaalamu wao wakushauri n.k amabao ni wasomi pia, wewe std seven unabaki Kama mbeba maono na kuangalia mambo yanaendaje.

Wasomi kinachowafelisha ni uoga wa kuanzia chini na kutake risk tu sio kwamba hawana akili msiwadharau ndio maana std seven wanawategemea kusimamia na kuwaendeshea biashara na kampuni zao.
 
Ameandikwa kwa sababu amemaliza master vipi wale waliomaliza la7 na kwenda veta kujifunza huo ufundi, si watakuwa mbali zaidi kiufundi kuliko huyo mdada.
Huyo dada ameshindwa kuibadili digrii ya BBA kuwa pesa mpaka kaamua kurudi veta kozi ya la7.
Vocational skill anaweza kujifunza hata ambae hajasoma shule kabisa, sio mchongo wa maana.
Amesoma kozi za ujasilia mali ameshindwa kuwa mjasiliamali kaamua kuwa fundi hivyo wajanja watamtumia kupiga pesa.
Yeye alitakuwa afanye business sio ufundi hatotoboa.
Aliekuambia veta ya darasa la Saba Ni nani ? Yeyote unaruhusiwa kwenda kuchukua ujuzi Fulani.
Yeye ameenda veta kusoma useremala kwasababu alitaka kufanya biashara ya furniture Kuna ubaya gani ?
Au Ulitaka akanunue Vipodozi na nguo China ndio uone biashara ya kisomi ?

Watu Kama nyie ndio mnaofanya wasomi washindwe kujiajiri kutokea chini kwa kuogopa kusemwa na kuchekwa
 
Imewasaidia wangapi kujipanua ? We unafikiri yeye ndio wakwanza kuwa fundi msomi ? Wasomi wapo kila mahala wala sio issue kubwa.
Wengine wanauza Azam juisi za ukwaju wamebeba bonge la begi na kuvaa likofia likubwa.
Huyo dada hajaelimika men!
Ameshindwa hata kuanzisha kampuni la mfukoni ? walau kuwa consultant wa biadhara.
Kuna firsa nyingi sana kama una digrii ya BBA.
Acheni kupongezana vitu vya hovyo.
Alisha feli na master yake wala hanishawishi.
Hahaha wewe akili yako bhana ... kwahiyo unataka aishi kimisheni town na kampuni za mfukoni ?

Yeye kapenda na kavutiwa na idea ya biashara ya kutengeneza na kuuza furniture . Wewe Kama unapenda idea ya consultation fanya wewe , usikariri . Kuna ideas chungu mzima ni wewe tu na umeona fursa gani

Masters yake ya biashara itamsaidia Kwenye biashara yake hiyo
 
Wee nawee [emoji848]

Mambo ya interior designing ni taaluma za watu etii , tena ni biashara kubwa. Tatizo wewe unawaza padogo na exposure huna unaonekana, we unakomalia kumfananisha na mafundi wa keko tatizo.

Taaluma yake ya biashara itamsaidia kukuza biashara yake, kuleta ubunifu n.k

Kuna stage mfanyabiashara hata Kama ni darasa la Saba atahitaji elimu tu ili biashara yake ikue zaidi. Hata Kama hajasoma itabidi aajiri watu wenye taaluma zao.
Ndio maana familia za wakina bakheresa na dewji ziliwapeleka watoto wao shule na vyuo vya gharama ili waje wasimamie biashara. Sasa kwanini wao hawakupotezea elimu kwa watoto wao

Hizo biashara na kampuni kubwa unazoziona zimekuzwa na kusimamiwa na wasomi. Hata Kama mmiliki ni std seven Kuna stages za biashara inabidi utafute watu na utaalamu wao wakushauri n.k amabao ni wasomi pia, wewe std seven unabaki Kama mbeba maono na kuangalia mambo yanaendaje.

Wasomi kinachowafelisha ni uoga wa kuanzia chini na kutake risk tu sio kwamba hawana akili msiwadharau ndio maana std seven wanawategemea kusimamia na kuwaendeshea biashara na kampuni zao.
We muache aendelee kumcheka m, siku akiskia anauza fenicha zake wizarani na balozi mbalimbali ndio atatia akili.
 
Hahaha wewe akili yako bhana ... kwahiyo unataka aishi kimisheni town na kampuni za mfukoni ?

Yeye kapenda na kavutiwa na idea ya biashara ya kutengeneza na kuuza furniture . Wewe Kama unapenda idea ya consultation fanya wewe , usikariri . Kuna ideas chungu mzima ni wewe tu na umeona fursa gani

Masters yake ya biashara itamsaidia Kwenye biashara yake hiyo
Itamsaidia nini wakati imeshindwa kumsaidia sasa hivi. Wakati uliopo imeshindwa ila in future tense itamsaidia! anamkataba na mungu.
Hakuna chochote hapo ataishi kama mafundi wa keko kina piere liquid. Hio hela ya kununua mitambo ya kiwanda kashindwa kuipata kisha utegemee eti ata win.
In future tense hata mimi nitakuwa raisi, hata wewe utakuwa waziri mkuu but to make the dream become true kuna mziki.
Yani mna gurantee atawin kwani wale mafunfi wadio na master hawatawini?
Suala kubwa hapo ni hio master ni useless, huo ndio ikweli japo mnalemba lemba. Ukute hata kuandika business plan keshasahau.
 
We muache aendelee kumcheka m, siku akiskia anauza fenicha zake wizarani na balozi mbalimbali ndio atatia akili.
Akiuza hata wale mafundi wasio na master watauza. Naomba unielewe kwamba master yake mpaka sasa ipo kwenye sifuri kwani haijamsaidia chochote yani mpaka sasa inasoma negative.
Kuwin kila mtu atawini hata muuza nyanya huko mbele ata win.
Kuwini au kutokuwin hakuna uhusuano na master, jambo la msingi tusipoteze muda kusoma vitu tusivyovipenda huyu dada ni funzo kwa vijana, waangalie passion zao wajitupe huko.
Angeanza miaka 10 iliopita angekuwa mbali kwani amepoteza muda mwingi sana kumbe yeye si wa fani ile ya BBA.
Tjifunze kwa wanamziki na wachezaji wanazikimbilia ndoto zao mapema sana na kufaidi matunda ya kazi zao wakuwa vijana.
Kumbuka umri haukusubiri.
 
Hahaha wewe akili yako bhana ... kwahiyo unataka aishi kimisheni town na kampuni za mfukoni ?

Yeye kapenda na kavutiwa na idea ya biashara ya kutengeneza na kuuza furniture . Wewe Kama unapenda idea ya consultation fanya wewe , usikariri . Kuna ideas chungu mzima ni wewe tu na umeona fursa gani

Masters yake ya biashara itamsaidia Kwenye biashara yake hiyo
Mkuu hivi unaweza kupewa tenda kubwa ya kusambaza assets ukiwa huna kampuni ?
 
Akiuza hata wale mafundi wasio na master watauza. Naomba unielewe kwamba master yake mpaka sasa ipo kwenye sifuri kwani haijamsaidia chochote yani mpaka sasa inasoma negative.
Kuwin kila mtu atawini hata muuza nyanya huko mbele ata win.
Kuwini au kutokuwin hakuna uhusuano na master, jambo la msingi tusipoteze muda kusoma vitu tusivyovipenda huyu dada ni funzo kwa vijana, waangalie passion zao wajitupe huko.
Angeanza miaka 10 iliopita angekuwa mbali kwani amepoteza muda mwingi sana kumbe yeye si wa fani ile ya BBA.
Tjifunze kwa wanamziki na wachezaji wanazikimbilia ndoto zao mapema sana na kufaidi matunda ya kazi zao wakuwa vijana.
Kumbuka umri haukusubiri.
Yaani wewe umekaa kinegative negative .....hebu fungua ubongo huoo. Fungukaaa

Unasema angefuata passion yake si ndio huo useremala Sasa anafanya , au neno ufundi seremala limekuchanganya tuseme basi interior designing au sijui furniture making kwa kizungu . Pengine baada ya kujitafuta akagundua mapenzi yake yapo Kwenye useremala ndio ameamua kufanya.

Na kuhusu elimu yake aliyosoma Wala hajapoteza kitu itamsaidia kuendesha na kusimamia kiwanda chake . Au ndio Ulitaka akaajiriwe BOT ndio uone kaitendea haki elimu yake ??
Mawazo yako Ni ya kimasikini na kizamani kwa Nyakati hizi.

Mwenzio kaanzisha karakana na ana mpango wa kuongeza mashine kubwa zaidi ,kaajiri vijana na anakuambia wateja anapata kwa wingi ,sasa si ndio kiwanda hicho. Na anasema amehudumia kampuni kadhaa. Sasa unataka nini hapo ?
Elimu yake imepoteaje Wakati anaitumia kuendesha kiwanda chake

Wewe neno fundi seremala limekuvuruga tu , huyo ni mmiliki wa kiwanda huyo anafanya biashara ya furnitures. Ni namna tu ya lugha sababu ameanzia mwenyewe kutengeneza kwa mikono yake
Ni sawa sawa na mmiliki wa restaurants za KFC tutamuita mpishi japo ni mmiliki wa migahawa si alianza kwa kupika mwenyewe kuku zake.

Sasa wewe sijui Ulitaka afanye biashara gani unayosema iendane na Masters yake aliyosoma ??? Hebu niambiee
 
Wazazi wakiwa na pesa halafu mtoto ana akili, basi ni rahisi sana mtoto kufanya anachotaka.

Yaani mtoto anaenda chuo kuelimika tu, na akimaliza kusoma anarudi kwa wazazi wanamuuliza anataka afanye nini, wanampa mtaji.

Ukiwa mtoto wa tajiri hautakiwi kuhangaika na ajira za chini, unajiajiri tu kwa sababu mtaji na back up ipo. Labda upate kazi za mishahara mikubwa!
 
Brenda, msomi mwenye 'masters' aliyejikita kwenye ufundi seremala

Kote duniani vijana walio wengi wamepata elimu, lakini changamoto kubwa imekuwa ni suala la ajira, hivyo wanaamua kuutumia ujuzi wao kama muarobaini kukabiliana na changamoto hiyo.

Dar es Salaam. “Vijana wengi tukimaliza kusoma tunasubiri ajira, lakini hatuhangaiki kutafuta fursa za kazi, kazi zipo nyingi sana Tanzania, ni vijana kuchakarika kuziona hizo fursa na kuanza kuzitumia,” alisema Rais Samia Suluhu Hassan, Januari 07, 2022 katika maadhimisho ya kilele cha matembezi ya miaka 58 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Suala la kusubiri ajira baada ya kumaliza masomo kama alivyosema Rais Samia, ni tofauti kwa Brenda Mihanjo (33). Licha ya kuwa na elimu ya Shahada ya Uzamili ya usimamizi wa masuala ya biashara (Masters), aliiweka kando na kuanza kujihusisha na ufundi seremala.

Mwananchi ilifanya mahojiano na Brenda ili kujua nini kilisababisha ajiingize kwenye kazi hiyo, iliyozoeleka kufanywa na wanaume na pia ni msomi wa elimu ya juu.

Anasema kitu kilichomshawishi kufanya shughuli hiyo ni kupenda bidhaa za mbao asilia.

Anasema kuwa mwaka juzi ndio alijiunga rasmi kwenye ufundi seremala, akijifunza nyumbani na baadaye akaenda Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya ufundi Stadi (Veta) kusomea ufundi seremala kozi fupi ya miezi mitatu.

Anabainisha kuwa alikuwa anavutiwa na jinsi mbao zinavyoweza kudizainiwa bidhaa mbalimbali, hivyo akatamani kufahamu namna vinavyotengenezwa

“Napenda sana bidhaa za mbao asilia, navutiwa na mitindo ya bidhaa mbalimbali watu wanazotengeneza kutokana na mbao na mwonekano wake,” anasema.

Anafafanua: “Kwa kweli nilipata changamoto sana ya kwenye vipimo na ndio kilichonipeleka Veta...Maana kutojua vipimo kulinipa shida ya kuagiza mbao, kuna wakati nilikuwa ninazidisha au kupunguza kwa sababu ya kutokujua vipimo kamili. Kwa kweli sitasahau hili jambo,” anasema.

Hata hivyo, Brenda anasema mwanzoni alikuwa anakutana na changamoto ya watu kutokumuamini kwa sababu ni mwanamke, lakini sasa hivi wameanza kumuamini.

“Hii kazi inachukuliwa ni ya kiume, pia watu wanaofanya useremala wanadharauliwa na kuonekana ni maskini.

“Kwa hiyo wakati naanza watu walikuwa hawaniamini kabisa, mtu anaona akinipa kazi yake nitamharibia, lakini sasa hivi namshukuru Mungu wameanza kuniamini, hivyo napata oda nyingi,” anasema.

Anasema, wapo watu ambao wanamcheka na kumdharau kwa sababu ana elimu kubwa lakini ameamua kuwa fundi seremala, lakini yeye hawajali watu hao.

“Hii ndiyo kazi yangu na ninaichukulia kama nyingine, najua ningeamua kuwa na mgahawa au duka la mavazi hakuna ambaye angeshangaa. Lakini niliamua kuchagua useremala nikiwa na nia ya kuwa na biashara kubwa Tanzania yenye kuzalisha samani na bidhaa nyingine za mbao za kuuza ndani na nje ya nchi.

“Na najua kuwa ni sekta inayolipa kama ikifanywa kwa usahihi. Kwa hiyo kwa ujuzi, elimu na maono niliyonayo kuhusu hii kazi najua naweza kufika sehemu nzuri,” anasema.

Kuhusu mafanikio anabainisha kuwa amefungua karakana yake maeneo ya Chang’ombe mkoani Dar es Salaam pamoja na kuajiri vijana zaidi ya wanne wa kumsaidia kazi.

Mbali na hayo, anasema ameweza kutengeneza samani kwa kampuni mbalimbali pamoja na wazungu.

“Mafanikio sio makubwa, lakini nimefanikiwa kuwa na karakana yangu na pia kuajiri vijana ili wanipe nguvu ya kuzalisha bidhaa nyingi zaidi.

“Lakini pia napata oda nyingi sana kwa sasa tofauti na nilivyoanza na nyingi nazipata kutoka katika mitandao ya kijamii, hususan Instagram,” anasema.

Anaeleza kuwa haikuwa kazi rahisi, lakini alisimamia kile alichokipenda na kuamua kukifanya.

Anasema kuwa alipokuwa anataka kufanya kazi hiyo watu wengi walimkatisha tamaa, lakini yeye alipambania kwa kuwa alikuwa na nia.

“Najivunia sana, kwani nilivyoanza mwanzo na sasa ni tofauti, yaani sio Brenda yule aliyekuwa na vyeti vya elimu ya juu bila cheti cha ufundi seremala.”

Brenda anawashauri wanawake wasikate tamaa na wasimamie mawazo wanayoyaamini kwa sababu hakuna kazi ya mwanamke au mwanamume, vyote vinawezekana, kikubwa ni nia tu pamoja na kujiamini.

Anaongeza kuwa malengo yake ya baadaye ni kuja kufungua kiwanda kikubwa cha kuzalisha samani mbalimbali.

“Niamini mimi hii ndoto ya kuanzisha hiki kiwanda itafanikiwa, tofauti na watu wanavyodhani, kazi ya kuchonga samani ukiwa na soko la uhakika inalipa sana.

“Na nikifanikiwa najua nitatatua tatizo la ajira kwa vijana wengi, hususan wasomi kama mimi ambao wanaamini zaidi kupitia ajira,” anasema.

Hata hivyo, anasema changamoto anayokutana nayo kwa sasa ni mashine ndogo aliyonayo ya kupasulia mbao, hivyo kumlazimu kutoa gharama kupeleka mbao kwenye mashine kubwa.

Brenda anasema kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kupanua karakana yake ili iendane na vigezo vinavyohitajika.

“Nilipumzika kwa muda wa miezi miwili ili kufanya tathmini, kuangalia wapi nilikosea, ili ninapouanza mwaka nianze na kasi na mabadiliko zaidi, na hii itanisaidia kufikia malengo yangu haraka,” anasema Brenda.

Historia yake kwa ufupi

Brenda ambaye ni mama wa mtoto mmoja amezaliwa mwaka 1988 mkoani Dar es Salaam. Alianza elimu ya msingi mwaka 1995 katika Shule ya Msingi Kurasini na baadaye alijiunga na Shule ya Sekondari Zanaki ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha nne.

Anaeleza kuwa baada ya kuhitimu kidato cha nne alifaulu na kujiunga kidato cha tano katika Shule ya Sekondari Tambaza.

Anaongeza kuwa alipomaliza kidato cha sita, mwaka 2010 alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) akisomea shahada ya awali ya biashara na masoko, na mwaka 2012 alisoma stashahada ya uzamili katika diplomasia ya uchumi.

“Mwaka 2019 nilisoma Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Biashara (MBA), niliyoisoma katika chuo cha Eastern and Southern Afrika Management Institute (ESAMI),” anasema.

Gazeti la mwananchi 10/01/2022
[emoji122]
 
Nae hana tofauti na huyu.
Hakuna ubunifu pale ni mamantilie mwenye master.
Alichoongeza pale ni vyombo na mavazi mazuri kitu ambacho hata Shilole kakifanya kwenye mgahawa wake japo hana master.
Tunaendelea kuaminishana kuwa wenye master ni sahihi kuuza makande, kuendesha boda, kuuza mboga mboga, kuuza samski feli.
Binafsi sioni faida ya hizo master bali wamepoteza muda wsmao na pesa zao bure na kuishia kufanya vitu visivyohitaji master.
Yule wa makande ni ujinga wa kiwango cha lami. Unaenda kusoma marakeni nchi ya kibepari ambapo kuna kila biashara ambazo huku Tanzania bado hata kufikiriwa unarudi unauza makande kweli!!!!
 
Back
Top Bottom